ADD Friends Campaign – Epsd 013: Mchango wa Imani kueneza fikra potofu juu ya Ulemavu.~~~~Peter Sarungi

ADD Frriends Campaign - Epsd 013
Mchango wa Imani kueneza fikra potofu juu ya Ulemavu.
Peter Sarungi (The Next Speaker)
Habari marafiki zetu, leo ni moja kati ya siku za kuabudu kwa baadhi ya imani tulizo nazo nchini. Nami naomba nitumie siku hii kutoa ujumbe unao endana na siku hii lakini ukigusa kampeni yetu ya kuondoa fikra potofu juu ya watu wenye ulemavu.

Tabia, desturi na utamaduni ni moja ya vitu vinavyo tengeneza mitindo ya kuishi kwa jamii. Hata hivyo Imani ndio chanzo kikuu cha kutengeneza tabia, desturi, mila na utamaduni kwa jamii. Leo hii katika jamii zetu kuna mitindo mingi ya kuishi inayo akisi imani tulizo nazo. Imani ya mtu huonekana kupitia fikra zake, kwani kile mtu anacho kiamini ndicho atakacho kitenda.

Fikra potofu za jamii juu ya ulemavu ni moja ya zao linalo tokana na imani zetu katika jamii. Sipo kwaajili ya kupinga imani za watu lakini ni wajibu wangu kukataa imani kandamizi kwa walemavu. Imani zetu zimekuwa ziki tuaminisha kwamba moja ya makundi yenye kuhitaji misaada na huruma kutoka kwa jamii ni watu wenye ulemavu. Waumini wengi wamekuwa wakiamini kwamba ukimsaidia mlemavu basi unapata baraka na thwawabu kwa Mungu. Wanaamini walemavu wameumbwa ili kuwa chanzo chao cha baraka na mafanikio iwapo wata saidia kundi hilo.

Imani hii imejenga fikra ya kuwaona walemavu kama sehemu ya mtihani wa imani kwa jamii, imeleta fikra ya kuwaona walemavu kama viumbe walsio weza na hata ikitokea mlemavu huyo ameweza basi wataamini sio yeye wala jitihada zake bali ni Mungu. Yaani ni kama kobe unapo mkuta amepanda juu ya mti, lazima utasema kapandishwa.

Hizi ni fikra potofu zinazo tokana na mafundisho ya imani zetu. Kuna haja ya viongozi wa dini kubadilika haraka maana wakati ni huu ambao ADD Friends Campaign imefunguliwa maono yaliyo jificha kwa muda mrefu.
Ikiwa wewe unapata thwawabu kwa kunipa msaada wa siku moja, je mimi napata wapi hiyo thwawabu??? Au mimi si wa Mungu?? Au mimi naingia mbinguni bure??

Karibu ADD Friends tufikiri tofauti kwa pamoja ili kutibu jamii juu ya fikra potofu kwa watu wenye ulemavu.

Leave a Reply