All posts by Alpha Igogo

Kheri ya siku ya kuzaliwa kwa dada yangu!

Leo ni siku ya kuzaliwa dada yetu, uzao wa pili wa familia yetu. Ni huyo mwenye nguo ya rangi ya Blue. Yeye kwa sasa anaishi Tabora lakini alikuja Dar kwa mambo fulani hivyo mdogo wangu akatumia nafasi hiyo ya pekee kumuandalia chakula cha mchana kufurahia maadhimisho ya siku hii. Tunamtakia kheri na baraka zote, Mungu atembee naye mwaka mwingine na milele zote ????

“Wamama na Wababa wa Wajukuu wetu, habarini za asubuhi njema ya leo. Leo nawasalimu kwa salaam ya kipekee, maalum ya kuhitimisha hiyo tafrija ya aina yake, yenye kunikumbusha miaka takriban 45 za Malezi yetu kwa huyo Mdada wenu na Mama wa wajukuu wetu wapendwa. Elline ana historia ya maisha yanayosadifiana na yangu, mie Baba yenu. Maisha yangu duniani yalianza kwa taabu ya afya dhaifu kwa kuwa niliwahi kutengana na lishe ya Mama tumboni mwake, nikazaliwa NJITI??‍♀️??Nakawa ngangari hadi leo hii bado nadunda japo udogoni nilikiona cha moto, kama Rafiki yangu, Binti yangu mpendwa Mama Min Ji. Alikuwa na afya mgogoro mno udogoni, naye kama nilihadithiwa na Mama kwamba bila huruma na upendo wa Baba yangu, yeye aliisha kata tamaa kwamba nitaishia utotoni tu, naye Nyategi kusema kweli nilimhangaikia vya kutosha utotoni, tukiwa na kipato kidogo mno, hadi hadi katengemaa na leo twasherekea siku yake ya 16,425 hapa duniani, Namuombea azidi kutengamaa na kupata tena siku kama hizo na kuzidi, hapa duniani. ????. Upendo wenu na mshikamano huu mliyonayo iwe ni mizizi inayo sambaa kwenye uzao wetu na kuendelea kwa vizazi na vizazi vijavyo. Nawatakia Sherehe njema, yenye Amani tele na kueneza Upendo wa JK milele.” * Baba mzaa chema -Sir O.O Igogo

Hapa wakiwa Tabora, ambapo mdogo wetu Janeth (aliyebeba mtoto) alikwenda kuwatembelea mwanzoni mwa mwaka huu!

Happy Anniversary to my parents!

Mr and Mrs Otieno Igogo @Seacliff hotel

??? Cecy anasema Otty mpaka kufa eeh, nami nasema Cecy wangu wakufa na kuzika eeeeh …. usitumie pesa aa kama fimbo kaka mambo ya pesa mpaka makubaluano hapo ndipo pesa huwa na thamani eeh ?? ??? Happy Anniversary to one of my favorite love birds! Mzidi barikiwa mpaka mshangae! ?❤

“Sometime back over four decades ago, I was visiting my old Mum in the village of Utegi, on a date same like today, 17th August.

I had a fully commited heart and desire to go out and look for the better half of me, so that we can pair and share our remaining part of the long walk to Heaven together.

Poor and young as I was, I did not have any other Choice than for that beautiful young girl I knew since 1970, whose home was in the village of Kowak.

During those days there were no telephones, nor did I have any means of transport neither did I have any money to afford bus fare to the ten kilometers distance away from my Village of Utegi. So I remained with only one means of mobility, if I had to make a suprise visit to my choice of life patners homestead, and that was walking on foot to and fro.

Ernegetical with full courage on assumption that she ought be at home, I set my feet on the ground pace after pace, at times I jogged to catch up with time, till I reached Kowak.

Counting on good luck and trust that she would not shame me, I reached the Kumbini shoping Centre of Kowak. I had look for a reliable person to send across to her home, for signaling of my presence and got one young man whom I sent over and eventualy made my mission a successful.

It was on that very same of 17th August over four decades ago when we traditionaly paired as couples to date with my better half named Cecilia.

Our beloved and Mercifull God has blessed our life together with very understanding, humble, highly deciplined and caring four daughters and a son, giving us a marvellous gift of seven grand children to date.

This is not a tell tell or a bed time story, but a true and live background of the Mzee Otieno Igogo and his Spouse Cecilia.”~~ Sir O.O Igogo

“Kijana wangu Boaz (UVCCM) na Mchumba wake walinitembelea jioni ya leo ofisini, na kutuletea Zawadi ya Kumbukizi ya siku yetu na Min Ji (mama). 17.08.2020” *** Sir O.O Igogo

Haya wenye chama chao wamewakilishwa ?? Asante Boaz na wifi yetu. Mbarikiwe sana.

Meet the Obama’s extended family members!

Let me introduce you to some amazing people whom also are apart of my family. Oh Yes! I’m related to the Obama’s, Lupita Nyongo, Raila and the the greats who originated from Uhuru Kenyatta’s land. ??

Ladies and gentlemen; its my honor to bring to you the Obama’s extended family members! Lupita Nyong’o cousin-brother, sister inlaw, nephew, and niece! The Raila Odinga’s son and daughter in-law and grandchildren! The Uhuru Kenyatta’s neighbors ?? The Duke and Duchess of Homabay County family! The Royal family of Mr and Mrs Tobby Nyagilo! The Kaganian village descendants! The Luos from great land of Kenya. Looking amazing! Bless His Holy name, the Maker of all! Mbarikiwe sana. ?❤❤

??????

Kheri ya siku ya kuzaliwa mama yangu kipenzi!

Leo ni siku aliyo zaliwa mama yangu mzazi, kipenzi cha roho yangu. Ila kwasababu birthday yake imeangukia siku ya kazi na wajukuu wanakwenda shule basi wadogo zangu siku ya jana (Jumapili) wakaamua kum-surprise na birthday cake kama video zinavyo onekana hapo juu ?? ?? …. ukiona mahala kuna upendo basi fahamu kuna Mungu kwani Mungu ni Pendo!

My mama! My MVP! The G.O.A.T! Always triple my blessings when comes to her! Happy birthday Nyarkowak, binti wa Cornel Awiti, muke ya Jategi ?? Mungu akujalie umri mrefu zaidi, maisha yenye furaha na amani zaidi ya jana! Nakupenda mama yangu! ?❤

Ubarikiwe miaka elfu! ??❤

Happy birthday to me!

“Bwana ni mwema sana alitupa mibaraka ya mtoto wa kike usiku wa Alfajiri ya tarehe 26/06/1977 umekuwa mibaraka kwetu, umenifanya kutembea Merikani kama Queen Mungu asingetupa wewe ni nani angenipeleka kwa Hellen G. White, ni nani angenipeleka Washington DC nikaona ikulu ya Trump, ni nani angenifikisha Califonia nikaona Los Angeles, ni nani angenifanya nikaona HOLLYWOOD, na Golden Gate, umenifikisha Chicago, Michigan, Indiana, Houston, nimeona kaburi la mama Hellen G. White (Battle creek, Michigan). Kuishi kwako Merikani Mungu kanifuta machozi nami ninaongea kati ya wanawake. Ubarikiwe 100 times ningekuwa na uwezo ningekutumia nguo ya kuvaa leo lakini endelea kutuombea siku moja nami nikubariki mwanangu. Tunakupenda sana.” I LOVE YOU MORE Mama! ?❤

Blessed beyond measure! Forever grateful ???? #LovingFarther
thank you darling daughter! ?❤

Namshukuru Mungu kwa yote! Nimeuona mwaka mwingine. Happy birthday to me!

Tanzia: Pumzika kwa amani baba yetu mzee Joseph Musira

Mr and Mrs Musira

Ni miaka 59 ya kujuana kwao na September 12, 2020 walitakiwa kufikisha miaka 56 tangu wale kiapo kitakatifu cha ndoa yakwamba “MPAKA KIFO KIWATENGANISHE”! Kiapo chao kitakatifu aliapa katika kanisa la Roman Catholic lillopo katika kijiji cha Kowak, wilaya ya Rorya mkoa wa Mara. Siku ya leo tarehe 06 / 05 / 2020 Mungu aliamua kuitimiliza ahadi walio iweka mbele zake. Mnamo majira ya saa kumi na moja alfajiri saa za Africa Mashariki baba yetu kipenzi mzee Joseph Musira alilala usingizi wa mauti katika hospital kuu Musoma alipokuwa akipatiwa matibabu!

Tunahuzunika kwasababu sisi ni wanadamu tulioumbwa kwa hisia. Tulikua bado tunampenda sana. Rafiki yake (Mke wake) bado alikua anamuhitaji sana. Lakini mapenzi ya Mungu yametimia nasi tunasema Amen!

Pumzika kwa amani ya Bwana baba yetu, ulitupenda nasi tunafarijika kujua yakwamba umelala ukitambua upendo wetu kwako. Maisha uliyo ishi ni mfano wa kuigwa kwa watu wengi sana. Umeishika imani na kuiishi kwa vitendo mpaka mwisho wa safari yako. Ulikuwa Mwalimu ulielimisha jamii nyingi sasa. Mchango wa elimu kama Mkurungenzi wa elimu wa mkoa katika Diocese ya Mkoa wa Mara kwa zaidi ya miaka 25+ kamwe hauta sahaulika. Hata baada ya kustahafu walikuhitaji wakati wote nawe hukusita kwenda kusaidia. Kazi zako za kujitolea katika mambo mbali mbali ya jamii zimeacha alama kubwa kwa vizazi vya sasa na hata vijavyo.

Asante kwa kuwa baba mlezi wa mama yangu wakati akisoma Secondary. Kazi ambayo hukusita kuifanya tena kwangu mimi nilipokuwa mwanafunzi pale Kowak Girls Secondary school. Umeishi maisha vyema nasi tutayasherekea kwani unastahili! Pumzika kwa amani, tukutane asubuhi njema. ????

“Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.” ** 2Timothy 4: 6-8

  • “Leo ngoja niandike kidogo. Mwl. Joseph Musira alikuwa baba kwangu, alikuwa Mwl. wangu wa hesabu na Jografia nikiwa nikiishi nao ni mshauri. Alinilea kwa upendo usio mfano akiniita “rafiki yangu” Halafu ananitania “Susilia” kisha anacheka wote familia ni kicheko. Jamani na umri niliyo nao nikimsalimia Mwl. kwenye simu napiga magoti hadi chini, watu hunicheka kwa kupiga magoti kwa mtu nisiyemuona lakini upendo wake ulinikaa katika akili mimi nashtukia nimeshapiga magoti nikisikia sauti yake. Mzee Musira, ameniinua kutoka msingi, amenifanya nimefikia hapa kwa kunisaidia na kunitia moyo nikiwa darasa la saba hadi nikafanya vizuri na kujiunga na Rugambwa Sekondari School enzi hizo. Mara ya mwisho nilikwenda kuwasalimia akiwa ameanza kuumwa nikampelekea Rozari nzuri kutoka Jerusalem akafurahi sana kwa maana Wimbo wake ulikuwa sala. Lakini safari imefika hatungeweza kuongeza dakika wala nukta. Amepiga vita vilivyo vizuri vya upendo akiwa ni mkwe wa kwanza kwa Baba yangu na mama yangu Marehemu Mzee Cornel Awiti Oyata na mama Valeria (Mareh.) Maishao yao ni hubiri tosha kiasi kwamba mabinti na wajukuu wa Mzee Awiti wangeiga mfano wao hakika kifo ndicho kingetutenganisha na wenzi wetu. Baba wa mfano na kila mara mimi na mzee wangu O.O Igogo tunawataja kwa maisha matulivu, furaha na amani waliyonayo. Familia hii ninawaombea faraja peke yake Bwana awatie nguvu ni maumivu makali lakini ni lazima tushukuru kwa kila japo. Bwana ametoa na Bwana ametwaa jina lake litukuzwe.” *** Shemeji wa marehemu Mama Igogo pichani juu ????

Till we meet again baba yangu, tutakukumbuka daima!

LifeWellLived #ManOfGod #ManOfIntegrity #HusbandOfOneWifeOnly #FamilyMan #GrandFatherToMany #Educator #Trustworthy #GoodCitizen #CommunityAsset #Patriot

Baadhi ya picha za msiba:

Nawatakieni kheri na baraka za mwezi June!

Wapendwa wasomaji wangu nimekua mvivu sana siku hizi kuandika humu! Natafuta pesa wapendwa, mambo ya kuandika magazeti humu wakati bank kunasomeka negative zero hata hainogi ?? Lakini kama mjuavyo huu si ni mwezi June!! Sasa nitaachaje uwanze bila kuandika kitu humu. Huu sindio mwezi tuliozaliwa viumbe wenye roho za kipekee, viumbe wenye upendo mwingi kuliko viumbe vyote duniani! Viumbe tusiojua kuangaika na mambo ya watu, viumbe wenye furaha na amani muda wote. Viumbe wenye akili za ziada na utashi (Intelligence) wa hali ya juu! Viumbe vinavyo penda kujitegemea zaidi, viumbe vinavyo chukia majungu na umbea ?? Viumbe vinavyo jali na kuheshimu hisia za watu. The Legends ??? Yani ni viumbe fulani amazing kinoma and I am proud of myself to be one of them!

Unaona hiyo picha hapo juu baba mzazi kashanipa baraka zake za kuanzia mwezi. Basi nami naomba niwatakie kheri na baraka zote za mwezi huu wa Sita. Wale tulio zaliwa ndani ya mwezi huu nawatakieni birthday njema, Mungu akawabariki sana ukawe mwaka wa kheri nyingi sana katika miezi iliyo bakia. Mbarikiwe wote. June born babies we truly Rock! ?❤❤

Wakili Jacob Sarungi kuagwa kesho!

*OBITUARY*

*ADVOCATE JACOB EMMANUEL SARUNGi

*Dear Member,It is with deep regret that we inform you of the untimely death of TLS member Advocate Jacob Emmanuel Sarungi , Roll Number 4666 who passed away on Friday 15th May 2020 in Morogoro *after being involved in car accident*

*Last respects* for the late Advocate Jacob Emmanuel Sarungi will be held on *Monday 18th May, 2020 from 1700hrs at his residence, Mbagala Majimatitu Saku street , Dar es Salaam* Thereafter the *burial services will take place at Rorya Utegi village, Mara region on Wednesday , 20th May, 2020*Members who wish to attend the last respects and burial in honor of our dearly departed friend and colleague, should dressed in bibs and robes.

*MAY THE ALMIGHTY GOD REST HIS SOUL IN ETERNAL PEACE* Regards, |Tanganyika Law Society Secretariat

  • Kwa taharifa kutoka ndani ya familia na kama ilivyo andikwa na jumuiya ya wanasheria wa Tanzania yakwa Wakili Jacob Sarungi ataagwa kesho mchana masaa ya Africa mashariki kisha mwili wake kusafirishwa kwenda kijijini Utegi, wilaya ya Rorya, mkoa wa Mara ambapo atalazwa katika nyumba yake ya milele katika makaburi ya familia. Nitaendelea kuweka kumbukumbu hizi kadri nitavyokuwa nazipata. Asanteni.

Tanzia: Pumzika kwa amani Advocate Jacob Sarungi!

Marehemu Jacob Emmanuel Sarungi enzi za uhai wake

Kwamasikitiko makubwa sana naomba kuweka kumbukumbu hii ya kifo cha kaka yangu (first cousin brother) Advocate Jacob Emmanuel Sarungi kilichotokea siku ya Ijumaa tarehe 15, May; 2020 kwa ajali ya gari maeneo ya kona ya Mikese, Morogoro, Tanzania. Marehemu alikua akielekea Dodoma kikazi ndipo mauti ilipo mkuta. Marehemu ameacha mke na watoto, wazazi, pamoja na kaka na dada zake.

Kuna vitu vya kuandika lakini sio kifo cha mtu yoyote yule! Ni ngumu sana, haswa unapoona kijana ambaye ana maono makubwa, nguzo imara ya familia, moja ya watu ambao anategemewe katika kuongoza ukoo fulani, na nguvu kazi ya taifa inaondoka wakati ndio kwanza ameanza mwendo, amewasha mshumaa wake teyari kuimulika dunia halafu ghafla unazimika! Unajikuta unamaswali mengi sana lakini kwakua tunaimani katika Mungu hivyo tunaamini kazi ya Mungu haina makosa!

Natoa pole zangu za dhati kabisa kwa mke wa farehemu, watoto, wazazi, ndugu, marafiki, wanasheria wenzake wote walioguswa na msiba huu haswa chama cha wanasheria (Tanganyika Law society), wafanyakazi wenzake, pamoja na ukoo wote wa Chief Sarungi Igogo.

2 Timoth 4: 7-8 …. “7Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; 8baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.”.

R.I.P brother! Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe milele zote ????

Watu wengi wameguswa na msiba huu, na zifuatazo ni baadhi tu ya jumbe zilizo andikwa na ndugu pamoja na mara fiki

  • ???? Huo ulikua ni ujumbe wa masikitiko toka Mwanasheria mwenzake, na dada yake Janeth Igogo ambao aliuandika kupitia account yake ya WhatsApp
  • Naye dada wa marehemu Maria Sarungi-Tsehai kwa kupitia account zake ya Instagram na Facebook aliandika ujumbe huo ? hapo akionyesha ishara ya kuguswa na kusikitishwa na msiba huu.
Kwa kweli, kwa masikitiko makubwa sana nimepokea taarifa ya kifo cha kaka, ndugu, jamaa, rafiki  na mwanasheria msomi mzuri kijana wetu damu ya Rorya Jacob Sarungi (Adv).Moyo wangu umeugua sana. Najikongoja kifikra kukubali kuwa Adv Jacob Sarungi ameaga dunia.Jacob alikuwa ni kijana mweye ndoto nzuri na pevu sana kwa ujenzi wa Rorya Mpya.Jacob ameacha familia changa sana nyuma yake na vijana waliomtegemea sana kujifunza katika tasnia ya sheria.Imeniuma sana. Jacob alitegemea njonzi yake ingekuwa angavu kwa maisha ya familia yake,  wanarorya, jumuiya ya wanasheria na watanzania kwa ujumla.Tumbo la dunia lihifadhi mwili wake kwa amani. Namuomba Mungu mwingi wa rehema aipokee roho yake ikisubiri parapanda ya mwisho.Bwana alitoa, Ndiye ametwaa.Jina lake lihimidiwe.  ??????                                                                                                                                 Maina Ang'iela Owino.©2020. 
  • REST IN PEACE BROTHER JACOB SARUNGI.Ni Mapema sana kuamini kwamba umerudi kwa Muumba wetu. Mungu akupe kauli thabiti huko uendako, nasi atupe uvumilivu wa kustahimili maumivu haya sisi tuliobaki.
  • Ujumbe huu ulitoka kwa mdogo wa marehemu Mwanasheria na mpatanishi wa serikali (government Arbitrator) Magreth Igogo ambao aliandika katika kupitia account yake ya WhatsApp

Kama ilivyo semwa na wengi kua ni ngumu kuamini lakini hatuna budi kukubali kuwa hiyo ndio hali halisi. Mungu awe nanyi wakati wote haswa katika kipindi hichi cha maombolezo.

Rest easy brother you are gone but you will never be forgotten ????

Happy birthday Mercy!

Leo ni siku ambayo mwanangu kipenzi cha roho yangu amezaliwa. Katika kuadhimisha siku hii nimeamua kuweka kumbu kumbu ya post zote za birthday wishes ambazo Niliwahi kuandika huko Facebook. Japo nikawaida yangu kupost siku za birthday yake lakini sijui bbn kwanini nimejikuta nimewaza kama Facebook ikafutika ghalafa hizi kumbu kumbu zote zitapotea. ?‍♀️?‍♀️?‍♀️ Nilipokuwa naziandika niliandika hisia zangu halisi, niliandika vitu ambavyo sio tu vilitoka moyoni bali ninaviamini, hivyo vinabeba uzito mkubwa sana kwangu. Na nilipokua nazisoma tena leo yani mwili unanisiaimka kwa furaha na tabasamu la amani moyoni. ?? Ninawatoto wengi lakini aliyekaa tumboni mwangu na kunifanya ni experience uchungu wa kuzaa ni huyu mmoja tu! Hivyo ana Extra special place in my heart and life!

Mimi huwa nikiandika kitu chochote ambacho kinagusa hisia zangu huwa sirudii kukisoma mpaka muda upite sanaaaa! Yani huwa napenda ku-present my raw feelings! Napenda mtu apate ujumbe kwa jinsi nilivyo jisikia mara ya kwanza. Ndio maana hata kama kuna makosa ya kiherufi (spelling error) huwa naacha hivyo hivyo mpaka nitakapo jiona nipo tayari kusoma hisia zangu katika maandishi ya uhalisia wake! Haya ngoja nitiririke kama ifuatavyo ??






https://www.alphaigogo.com/ni-kwa-neema-tu/

Haya yani hapa nimesha weka kumbu kumbu sawa za toka akiwa na miaka 18 mpaka leo ??? Yani hii hata siku Mungu akinijalia wajukuu basi watakuja ona jinsi nilivyo mpenda mama yao nao itabidi wampende hivyo hivyo, sitaki utani na mwanangu mie ??

Happy birthday Mercy, mjukuu number moja, ubarikiwe sana. Nakupenda leo, nitakupenda zaidi kesho, na milele nitazidi kukupenda.

“Watenda wema wa ukweli, hutenda wema kwasababu ni hulka yao na sio malipo kutokana na mtu wanayemtendea wema alivyo”***** Faraja Nyalandu

Prince Harry and his wife Meghan Markle

Reposted from @farajanyalandu Najua kipindi hiki cha #COVID19 tunaweza kusahau uwezo wa binadamu kupambania jambo lake. Kwa sasa hivi tunapambana na hiki kirusi cha corona. Kimetukumbusha wasiwasi ndio maarifa bila kupepesa macho.Hapo nyuma niliwafurahia sana Prince Harry na Meghan wake. Waliamua jambo lao, waliamua watapendana. Mapenzi ni rahisi kuliko upendo. Upendo huwa ni parefu jamani. Lakini hawa wameweza kutuonyesha vyote: mapenzi na upendo. Lakini zaidi wametuonesha thamani ya hivyo vitu wawili. Upande mmoja namuonea huruma Harry na upande mwingine namuona ni shujaa, kati ya hawa wawili, yeye amesacrifice sana. Amejua kumtetea huyu dada. Haijalishi dada anastahili au hastahili. Watenda wema wa ukweli, hutenda wema kwasababu ni hulka yao na sio malipo kutokana na mtu wanayemtendea wema alivyo. Hata hivyo ametukumbusha uwezo wa binadamu kupambania jambo analolipenda, analoliamini na analotaka. AKIAMUA. Ukiona vinginevyo tofauti na unavyotarajia ujue ni maamuzi pia.

Tuendelee kupambana na corona. Tuendelee kutetea tunaowathamini na tunavyovithamini. GOD is still ON THE THRONE! #BeSafe – #regrann

Dr. Milton Makongoro Mahanga azikwa leo!

Marehemu Dr. Milton Makongoro Mahanga enzi za uhai wake!

Aliyekua Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa kichama Ilala Dr Milton Makongoro Mahanga amezikwa leo majira ya mchana saa za Africa Mashariki katika makaburi ya Tabata-Segerea. Marehemu alizaliwa April 03, 1955 na kufariki dunia siku ya Jumatatu tarehe 23 mwezi huu, mwaka 2020 katika hospital ya Muhimbili alipokua anapatiwa matibabu. Marehemu ameacha mke, watoto, na wajukuu.

Kwaniaba ya familia ya mzee Otieno Olung’a Igogo naomba kutoa salamu za pole za dhati kabisa kwa familia ya marehemu, ndugu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), majirani, pamoja na watu wote walioguswa na msiba huu.

Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa alphaIgogo.com basi utakua ulishawahi soma huko nyuma post ambayo nilieleza uhusiano wa kidugu uliopo kati ya familia yetu na marehemu. Ilikua ni wakati wa msiba wa marehemu Dr. Didas Massaburi ????(https://www.alphaigogo.com/r-p-dr-didas-massaburi/) Kwa ufupi marehemu alikua anamuita baba yangu ‘kaka’ kwani mama zao ni madada. Marehemu Dr. Massaburi, marehemu Dr. Mahanga, pamoja na baba yangu mzazi hawa ni cousin-brothers mama zao ni ndugu wa damu. Basi kwa walio wengi wanamuangalia marehemu kama Mwanasiasa lakini kwa upande wetu ni mwana familia.

Na kwa wale mnao toka Rorya najua wengine nmnaweza jiuliza udugu wetu na marehemu Dr. Phenias Ziki Makoyo?! Dr. Makoyo naye pia ni cousin-brother wa baba yangu. Marehemu baba yake Dr. Makoyo, mama mzazi wa Dr. Massaburi, mama mzazi wa Dr. Mahanga, pamoja na mama mzazi wa baba yangu hawa ni ndugu wa damu!

Hivyo basi, baada ya kusema hayo, naomba ieleweke vizuri kabisa kua sijaweka hii post kuwakilisha chama chochote kile cha siasa hapa dunia! Hii post nimeweka hapa kwasababu marehemu ni sehemu ya familia yetu, pia hawa ndugu walikuwa marafiki wazuri sana. Natamani upendo waliokuaga nao wazazi wetu tungekua nao sisi watoto pia, lakini hichi kizazi cha Dot.com kina mambo mengi hivyo tuchukuliane tu hivyo hivyo ??

Pichani juu ni baadhi ya viongozi na makada wa CCM wakiongozwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Mr. Humphrey Polepole. Mr. Polepole alitoa salamu za rambi rambi kuwakilisha chama cha CCM ambapo marehemu ndipo alipo anzia mapambo yake ya kisiasa.

Ni vyema kuona mifano kama hii kwa viongozi wetu wa siasa a.k.a ‘wanasiasa’ ili Watanzania waweze kujifunza kutofautisha maswala ya kisiasa na mahusiano binafsi, itikadi za dini, na mambo mengine yote ambayo sio ya kisiasa. Siasa isimame kama siasa na isichanganywe na mambo mengine kama baadhi ya wanasiasa na “wanaharakati” wanavyotaka kuigawa taifa na familia za watu, tena wengine kwa makusudi tu na chuki zao binafsi!

Marehemu amefariki akiwa mwanachama wa Chadema lakini ikumbukwe kuwa alikuwa mwana CCM kwa muda mrefu, na huko alikuwa na marafiki, ndugu, na jamaa ambao bado ni wana CCM. Hivyo inapofika swala ambalo sio la kisiasa kama hili basi ni vyema wana siasa KUVUA KOFIA YA SIASA na kuweka swala la msingi mbele! Ni hatari sana kwa taifa kama wananchi wake wataweka siasa kwenye kila jambo. Kuna watu ambao hawapendi kujihusisha na vyama vya siasa ambao ni sehemu ya familia zetu na marafiki zetu basi ni busara, haki, na pia ni lazima maamuzi yao yaheshimiwe na kila mtu, msipende kulazimisha mambo eti kila mtu lazima awe mwanachama wa chama fulani cha siasa. Nope! Kila mtu ana hiyari ya kufanya maamuzi yake na hiyo ndio DEMOKRASIA.

“4 nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. 5 Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako. 6 Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. 7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; 8 baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.” 2Timothy 1: 4-8

  • Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe milele zote. ????

Kumradhi!

Jana niliandika kua marehemu amezikwa jana 03/25/2020 jambo ambalo halikua sahihi. Marehemu amezikwa leo 03/26/2020 katika makaburi ya Tabata-Segerea.

Naomba radhi kwa kosa hilo ambalo nilitenda bila kukusudia, ni misunderstanding ya muda ndio ilitokea. ??

Ni muda muafaka wa kuelimisha Watanzania juu ya ugonjwa wa Alzheimer na Dementia!

Reposted from @millardayo Kama tunavyofahamu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi @ally_hapi ameendelea kupiga kazi kwa kuzunguka sehemu mbalimbali za Iringa kukutana uso kwa uso na Wananchi kumaliza kero zao kwenye ziara anayoiita ‘Mahakama ya Wananchi’.•Kwenye hii video ni wakati alipokwenda Ipogolo, akajitokeza huyu Bibi na kusema Mtoto wake na Mjukuu wake hawataki kuishi nae, wamemfukuza na wamemuibia laki tatu zake.•Pamoja na kwamba Bibi alikua anaelezea matatizo yake, Watu waliohudhuria walijikuta wakicheka kwa jinsi Bibi alivyokua anahadithia. (? @ayotv_ ) – #regrann

Nimekua nikiona video hizi ambazo watu wanakua wanacheka au kuwazomea au kuwaita wachawi wazee ambao wanakua kama wanatatizo la kujielezea vizuri! Hili swala naona hata viongozi wetu wanahusika sana katika kuendeleza hii tabia ya unyanyasaji juu ya wazee! sina huwakika kama wanajua kuwa huwenda kunatatizo kwenye ubongo ambalo linawasababishia kuwa katika hali hiyo? au huwa hawafahamu? Au wanafahamu lakini ujinga (ignorance) imetawala akili zao! Yani unatazama kiongozi anaongea na mtu mzima mwenzake au saa nyingine amemzidi umri lakini jinsi anavyo ongea naye unabaki mdomo wazi na hasira juu!

Yani mara nyingi utakuta hawa viongozi wanapenda kuongea na watu kwa hasira (sauti za kufoka) kana kwamba wanaongea na mtoto wa miaka 2! yani hawana sauti (tone) ya kuonyesha compassion and respect kwa watu wengine! Utafikiri kwenye seminar / training zao za uongozi hivyo ndivyo walivyo fundishwa kua kiongozi ni mtu wa kufoka foka kama pombe ya “wanzuki”, kukunja uso na kutoa maneno ya dharau! ?? Lakini napo ninesikia wengi wakisema Watanzania walio wengi bila kumgombeza na kutoa maneno makali hakuna linalo fanyika ??‍♀️??‍♀️ na hii tabia wanaileta hata wanapokua kwenye mahusiano yani ni full ubabe tu! ?? Ukitaka kujua tabia ya jamii husika angalia viongozi wake utapata jibu.

Marehemu bibi yangu mzaa mama, Mrs Valeria Cornel Awiti alifariki March 12th 2014, akiwa na umri miaka 88

Turudi kwenye mada yetu, naamini ni muda muafaka sasa kwa serikali chini ya wizara husika inayo shughulikia mambo ya wazee pamoja na ustawi wa jamii kuchukua jukumu la kuanza kuelimisha Watanzania juu ya magonjwa au mabadiliko ya ya akili yanayotokana na uzee au msongo wa mawazo (severe depression). Kuna magonjwa kama ALZHEIMER na DEMENTIA ambayo mara nyingi yanawakuta wazee japo sio wote ! Nimesema mara nyingi kwani kuna wazee ambao hawakumbani na haya matatizo na pia kuma watu ambao wana umri wakawaida (average age) na wamepatikana na Alzheimer na Dementia. Binafsi nimeshuhudia mtu wa 55 na 51. Hivyo hatuwezi sema kuwa kwa 100% ni magonjwa yanayo wapata wazee! Mimi si Doctor hivyo siwezi kuelezea katika lugha ya kitaalamu zaidi ili watu waelimike. Ila nimeshawahi kufanya kazi na watu wenye matatizo kama hayo nikiwa kama muhudumu wa afya (Nurse Aide) katika Nursing home pamoja na sehemu ya kuwaangalia wazee; kwa maana hiyo nina ufahamu kiasi juu ya Alzheimer na Dementia.

Kwa lugha rahisi naweza sema Alzheimer ni tatizo linalohusiana na kupoteza kumbu kumbu kwenye ubongo ( brain memory loss), ambayo huja kwa stage au aina tofauti tofauti. Kuna wenye tatizo la kupoteza kumbu kumbu ya mambo yaliyo pita kwa miaka kadhaa. Kuna wenye tatizo la kupoteza kumbu kumbu ya kitu chochote kilicho tokea jana au ndani ya siku kadhaa (past 24 hrs or within72 ), kuna wenye tatizo la kupoteza kumbu kumbu ya kitu ambacho kimepita hata dakika moja! Hizi zote zina stage yake sidhani kama kuna mtu anaanza kwa kupoteza kumbu kumbu zote kwa mara moja, ila huwa ugonjwa unaanza taratibu huku ukizidi kuongezeka kwa kuwa na uwezo mdogo sana wa kutunza kumbu kumbu za matukio au jambo lolote lile.

Wakati Dementia ni ugonjwa unaohusisha kupoteza kumbu kumbu pamoja na uwezo wakuishi kama binadamu mwenye akili timamu. Yani mtu mwenye Dementia lazima ana Alzheimer lakini mtu mwenye Alzheimer peke yake basi hawezi kuwa na Dementia. Japo hatua za mwisho (last stage) ya Alzheimer huwa wanakutwa na Dementia. Hapa ndipo unakuta mtu hawezi kuongea vizuri, hawezi kufanya vile vitu ambavyo kwa kawaida angeweza kufanya mwenyewe kama kula, kuoga, kwenda chooni, n.k Mtu mwenye Dementia anakua hawezi kujua jema wala baya (can’t reasoning and make judgment). Yani anaweza akachukua chupi nakuvaa kichwani, anaweza sio tu kusahau majina ya watoto zake bali anaweza akawakana kabisa kuwa yeye hana watoto.

Sasa vitu kama hivi ni muhimu kwa jamii kuelimishwa ili kuweza kutambua, na kuwa teyari kukabiliana nayo. Hii hali ya Alzheimer na Dementia huwa ni very terrifying kwa watoto haswa pale unapoona mama yako au baba yako sio tu hakumbuki jina lako bali anakukana kabisa kuwa wewe sio mtoto wake na yeye hajawahi kuwa na watoto.

Kama hawa wenzetu ambao elimu ya haya magonjwa wanapewa na kuandaliwa (financially, psysociologically, emotionally, socially, na spiritually) pindi mzazi au ndugu anapoonyesha dalili za Alzheimer lakini bado unakuta inakua ni ngumu sana kwao sio tu kukabiliana na ugonjwa bali kukubali hali halisi kuwa huyo sasa ndio mzazi wake ambaye yeye alikua akimtazama kama hero / shero yupo kwenye hali hiyo ambayo hawezi kutofautiana chooni na jikoni! Anaweza jisaidia mahali popote pale. Tafadhali serikali ya Tanzania chukuweni jukumu la kulewa wazee kwa uzito na mapana zaidi.

Mimi nikiwa mgongoni mwa bibi yangu. Ilikuwa ni mwaka 2010, nikiwa kijijini Kowak ambapo mama yangu mzazi amezaliwa na kukulia hapo. Hiyo nyumba unayo iona ndio nyumba mama yangu amekulia na mahali yake hapo ndipo ilipotolewa. Nilikuwa nimekwenda likizo Tanzania nakama ilivyokuwa kawaida yangu ni lazima kwenda kutembelea bibi na babu zangu pamoja na shangazi zangu. Yani siwezi kurudi Marekani bila kwenda kuwasalimu; halafu watu wakiona unapewa upendeleo na Mungu wanakuchukia ?? jamani wengine tumetemewa yale mate yenye harufu ya kuku wa kienyeji yana bimaraka yale asikwambie mtu ?? Hapa bibi yangu alikua ameanza kuonyesha early stage ya Alzheimer. Saa nyingine alikua anasahau hata njia ya kurudi kwake akitoka kanisani. Bibi yangu na babu yangu mzaa mama wao walikuwa hardcore Catholic church believers.

Huyu ni babu yangu mzaa mama, marehemu mzee Cornel Awiti. Yeye alifariki 2011 akiwa na umri wa miaka 92. Hizi picha ndizo picha tulipiga mara ya mwisho kuonana (February, 2010). Kama nilivyo sema hapo mwanzo kuwa sio wazee wote wanapata Alzheimer basi ndivyo ilivyokuwa kwa marehemu babu yangu. Yeye mpaka anafikia hatua za kukata roho alikua na akili zake timamu na kumbu kumbu zake zote! Yani at age of 91 aikua ananitajia dawa zote anazo tumia tena kwa kingereza. Yeye alibahatika kupata elimu ya utabibu enzi za mkoloni, hivyo alikuwa na ufahamu juu ya magonjwa yake na dawa anazo tumia. Babu yangu alikuwa na tatizo la moyo kuwa mkubwa na BP ambayo yalipelekea kifo chake R.I.P. babu yangu missing you dearly ??

Pichani ni marehemu bibi yangu mzaa baba, Rhoda-Nyakanga Olwengo Igogo, akiwa na binti yangu Mercy mwaka 1996. Mwanangu jina lake lingine ni Teddy (Theresia) alipewa na babu yake kumkumbuka dada yake wa pekee. Baba yangu kwao walikua wanaume 3 na msichana mmoja. Shangazi alikua mtoto wa kwanza na binti pekee kwa tumbo la bibi yangu, japo nina mashangazi wengi kwani babu yangu alikua na wake wengi.

Kama ilivyokuwa kwa babu yangu mzaa mama basi ndivyo ilivyokuwa kwa bibi yangu mzaa baba. Yeye naye hakuwai kupatwa na tatizo la kupoteza kumbu kumbu, tena alikua anakumbuka mambo mengi ya zamani mpaka baba anamshangaa! Nafikiri mimi nimepata hicho kipaji toka kwake na kwa babu mzaa mama. My brain memory is good I mean ridiculously good ?? Yeye naye moyo wake ulianza kuwa mkubwa in the early 80s. Alifariki akikadiriwa kuwa na umri wa miaka 88. Bibi yangu asili yake ni Kenya.

Juu ni wadogo zangu Janeth na Magreth pamoja na bibi. Hizi picha tulipiga July 2013, na ndio ilikua mara ya mwisho kumuona bibi yangu akiwa hai. Mwaka uliofuata alifariki (March, 2014). Wakati huu tulipokwenda msalimia ilikua tofauti na 2010. Hapa alikua ana Alzheimer na Dementia. Yani Alikua hawezi hata kukaa mwenyewe bila mtu kumshika au kuweka mto kwa nyuma kumzuia asidondoke. Alikua hawezi kula mwenyewe wala kujihudumia kwa kitu chochote kile, hivyo kulikua na mfanyakazi pamoja na mama zangu walipeana zamu za kwenda kumuona. Nashukuru Mungu sana na siku zote nasikia faraja kuwa katika watu wote pamoja na watoto zake bibi yangu hakuweza kunisahau, yani alikuwa ananikumbuka jina langu ila nikimuuliza juu ya mama yangu anasema ‘Cecilia alikufa siku njingi’ halafu anaanza kumlilia ?? na mtoto wa Cecilia ambaye anamjua ni mimi tu ?? Nakumbuka alivyosema eti safari hii ukiondoka niachie hiyo suruali yako nataka na mimi nivae ??

Kwangu mimi ilikua rahisi sana ku adjust na hali aliyokuwa nayo bibi kwasababu nilisha ona hizo dalili toka anaanza kupoteza kumbu kumbu, na nikawa na jaribu kumuelimisha mama how to handle her na kukubaliana na hali halisi. Kitu ambacho mama hakukubali ni kununua depends / disposable underwears (zile diapers za wakubwa) kwa ajili ya bibi. Yani nilikua na mwambia itarahisisha usafi wa bibi lakini hakuweza kukubaliana nalo kwani kwake aliona kama nina m-degrade mama yake. Sikukasirika kwani nilijua yupo kwenye denial ya kuwa mama yake hayupo tena kwenye hali ya utuuzima (mama) japo ni mama yake.

Anyway, mimi huo ndio wito wangu kwa serikali na jamii kwa ujumla. Tuwajali na kuwatunza wazee wetu kwa kutambua mabadiliko ya kiafya ya mwili na akili wanayopitia. Tuelimishane na watu waache kugombeza wazee tunapo waona wapo katika hali isiyo eleweka. Tambua lazima kunashida mahala na tafuta msaada kwa madaktari. Tuache hii tabia ya kufokea watu wazima.

***Video shukrani kwa AyoTV***

Kulikuwa na ulazima gani?! Kwanini leo?!

Leo naona watu wengi wamempongeza Diamond kwa kitendo cha kuonyesha kuunga mkono kazi za Harmonolize a.k.a KondeBoy. Diamond ameandika ujumbe mzuri sana ambao wengi wameamini unatoka moyoni! Hata mimi naamini umetoka moyoni mwake ?? embu usome ????


Kweli hata mimi nampongeza Diamond kwa kuweka his “ego down” na kuonyesha upendo kwa mwanamuziki ambaye yeye mwenyewe alisaidia makuzi yake wakati yupo WCB! Nikitendo kizuri sana na chakufurahisha, lakini nimeshindwa ku-ignore the odds! Au wengine wanaweza sema the ‘hidden agenda’ au ‘the motive behind’!

Kama utakua ulisoma post yangu nilio andika mwanzoni mwa wiki hii inayo isha yenye kichwa cha habari kisemacho “Wema Sepetu ni mwanamke dhahifu sana” basi utakua ulisoma kile kipengele ambacho nilisema Diamond anapenda sana ‘attention’ na hiyo ilikua moja ya sababu hakuweza kumualika Wema Sepetu kwenye sherehe za miaka 10 ya muziki wake. Sasa basi, tumia maneno yangu hayo kutafakari alichofanya Diamond siku ya leo!

Yes, Diamond amefanya vizuri kuandika juu ya kum-support Harmonize! Lakini ilikua lazima afanye leo hii ambapo Harmonize amepamba kurasa za magazeti na social media?! Absolutely Not! Again, kama ilivyokuwa kwa Wema Sepetu asingependa kuona anapata attention zaidi yake basi ndivyo ilivyokuwa kwa Harmonize leo! Diamond baada ya kuona it’s all about Harmonize akaona njia pekee ya kuivunja nguvu hii ya attention anayopewa Harmonize ni kufanya kitendo ambacho kitagusa hisia ya kila mtu na kuelekeza attention yote kwake katika njia iliyo salama bila watu kugundua his agenda! The only way to steal Harmonize’s moment was to take his ego down! And yes, he won! Nilikwambieni Diamond ni manipulator and narcissist, mtu mwenye hulka kama hizi ni wakuogopa sana kwasababu yupo teyari kufanya kitu chochote kile ili abaki kuwa on top!

Kama kweli Diamond angekua muungwana, na kweli nia yake ilikua ni njema basi angesubiri hii momentum iwe all about Harmonize! Angesubiri ipite angala hata kwa siku moja halafu akaonyesha ukarimu wake! Lakini kwasababu hilo alikua lengo lake ndio maana hakuweza kuvumilia! Na hii naona ni style ya Management yake! Mnakumbuka walivyo fanya kwenye ufunguzi wa EP ya Tanasha?! Walikua wanajua kabisa Diamond hato kaa kwenye ile event lakini wakawa wanacheza na hisia za Tanasha bila yeye kujua na watu kufikiria kama kuna kitu nyuma ya pazia! Yaliyotokea wote mnayajua, wakatengeneza tukio la “dharura” na kulitangaza dakika za mwisho kabisa akijua watu wameweka macho yao wakisubiria kumuona Diamond na timu yake inaingia ukumbini! Hii yote ilikua ni kuvunja nguvu ya attention kwa tukio la Tanasha na kuhamia kwake! Hii ni typical behavior ya mtu anayependa ku control watu kama property yake binafsi! Hii nikuonyesha kua I’m still in control of you and everything!

Anafanya hivi kupata attention na trust kwenye macho ya jamii (haswa kwa watu wasiopenda kufanya tafakari ya kina) wakati anajua kabisa kitendo hicho kitamkwanza au muumiza hisia za muhusika! Yani hapo huwenda Harmonize anasema seriously bro?! This was my moment why steal it from me?! Kweli kabisa Harmonize anaweza hasiseme hadharani jinsi Diamond alivyo mkwaza na kitendo hicho lakini nina huwakika kwa wale watu wake wakaribu anao waamini lazima atakua anasema hata wao watakua wameumizwa sana! Harmonize nakushauri be a bigger person! Usimuonyeshe kua umechukia, wewe mshukuru tu halafu endelea na maisha yako! Kwasababu usipo sema neno la kumshukuru utakua unampa more attention na kuharibu image yako mbele za watu! Huna haja ya kuandika kwenye social medias, mtumie private msg. Na watu wakikuuliza sema nimeshukuru basi! Waswahili wanasema “funika kombe mwanaharamu apite”!

Nawashangaa sana watu wanaosema eti hii inaonyesha jinsi Diamond alivyo komaa?! ?? You people must be out of your mind! Diamond, he is a very insecure person! Ndio maana hawezi ku consider hisia za mtu mwingine! Diamond his self esteem ni sawa na ZERO!! Ndio maana “kiki” is the only way for him to boost his esteem!! Mtu asiyejiamini ndio huwa saa zote yupo kwenye mood ya mashindano yasio na tija, wabongo wanasema “anapenda ligi”. Mimi katika masomo yangu ya Ethics kuna somo nilisoma linaitwa “Human being behavior” hivyo najua mtu mwenye kujiamini anafananaje! Diamond ni entertainer mzuri sana lakini ni manipulator na narcissist, mwenye very-very low self esteem!.

Anyway, mie yangu ni hayo tu! Nawatakieni wote mafanikio mema na wazidi kuipeperusha bendera yetu vizuri! Na hongera sana Harmonize kwa event nzuri.

Housegirl kaalikwa ubalozi wa Marekani!

Tukiwa bado tunasherekea mwezi wa Superwomen duniani, basi siku ya juzi nikakutana na post ya Superwoman Joyce Kiria kama isomavyo ????

Reposted from @joycekiriasuperwoman Basi leo nilipata Fursa ya kualikwa na Ubalozi wa Marekeni kwenda kushea Safari yangu ya maisha katika kuendeleza Sherehe za Siku ya Wanawake Duniani 2020..Nilikuwa na Masupa Wuman wenzangu hawa hapa, Mercy Kitomari mwenye IceCream zake mjini, MD wa Lake Fm Noreen, Neema Md wa Penuel Investment, ..Aisee Nimegundua safari yangu ya maisha inasisimua na inahamasisha sana kupambana bila kuchoma, safari yangu ni nguvu ya Mwanamke hasa binti ambae anaanza kutafuta maisha…. nitaisimulia tena na tena coz I am a Super Woman ???? Stay tuned ??? Nitagie hawa masupa woman ???..Asante sana Ubalozi wa Marekani ??? – #regrann

Joyce Kiria akiwa na Superwomen wenzake walio alikwa ubalozi wa Marekani, Tanzania

Kwanza kabisa nianze kwa kusema hongera sana Joyce Kiria kwa mualiko huu! Kama nilivyo sema kwenye kurasa yako kuwa “what a milestone”! Unastahili!

Pili, naomba Watanzania mjifunze kutoka kwa wenzenu ambao wametoka katika nchi zilizo endelea. Mnaona jinsi gani wanavyo heshimu wapambanaji wa aina zote bila kujali elimu zao! Sidhani kama hizi nchi zingeendela kwa kubagua mtu au kitu chochote kile ambacho kina uhai, ndio maana huku kuna mifumo ya kusaidia na kuelimisha hata watu wenye utindio wa ubongo (matahaira), huku kuna haki za wanyama hadi Paka! Ndio maana wazungu waligundua Kia iki wapige hatua na kuendelea kuwa na nguvu ya kutawala dunia lazima ubaguzi na biashara za watumwa zikome! Maana walijua hatoweza kuendelea kwa kubagua fungu la watu fulani ambao wako ndani ya ardhi yao!

Mara nyingi unakuta baadhi ya Watanzania wanapenda kuona mtu ambaye ana “Masters” au “PhD” au anayejua kuongea Kingereza ndio mwenye akili ya kufanya vitu vizuri na vikubwa ambavyo watamuangalia kama “Role model”! Yani wanaona mtu aliye fanikiwa kwakupitia “structured” system basi huyo ndio anatakiwa kuwa role model na inspiration person wao! Watu kama akina Joyce Kiria ambao wamepata elimu na kupambania ndoto zao katika mifumo isiyokua rasmi wao wanakua hawana maana mbele ya hawa watu wanaojiita “wasomi”! Hata serikali yetu haiwatambu na kuwapa uzito watu wenye history ya maisha kama ya Joyce Kiria. Yani ni mentality fulani ya kuhuzunisha sana. Embu ona Kim Kardashian West anavyothaminiwa hapa Marekani, anauwezo wa kuweka appointment na kuonana na Rais kuongea juu ya maswala muhimu yanayohusu nchi yao. Everyone has something to offer, we need to learn to respect one another!

Wakiambiwa leo hii watoke hadharani watu wangapi ambao wanajiita “wasomi” nawamuangalia Joyce Kiria kama “Role model” wao?! Sidhani kama kuna hata mmoja atajitokeza! Siyo kwamba hawamjui au hawatizami kipindi chake hapana! Nikwasababu tu nakwenda shule kwenye mpangilio uliopangwa na serikali (jamii), mafanikio yake hayakutokana na ‘elimu’ hivyo wanamuona kwamba ni mtu fulani asiye na thamani ya (she is beneath) kua miongoni mwao! Hapo ndipo utasikia aah! Mie namuda wa kumuangalia housegirl? ?? nahivi sio member wa Chadema basi ndio tobaaa ?? Wakati ukweli ndani ya mioyo yao wanatamani wangekua na courage kama ya Joyce! Kwanza kumbuka huyu sasa watu wanasema “ALIKUWA Housegirl” keynote hapao ni ALIKUWA, she no longer exist in that title! hiyo ni history tu sasa! It defines where she came from but not her destiny! Haya housegirl huyo ndani ya American Embassy tena kwa mualiko maalum! #Respect people’s hustles! Kama ingekua Mungu anaangalia history ya mambo ya watu basi tusingekua na BiBle! Maana vitabu vingi ndani ya Bible vimeandikwa na watu ambao walikua wadhambi kweli kweli!

Joyce Kiria

Mimi Joyce ni mmoja ya watu wanao ni inspire, kwakweli ni mwanamke shujaa! Japo siwezi muita “role model” wangu, kwani binafsi huwa nasema na huu ni mtazamo wangu mimi Alpha; Katika dunia hii sina mtu yoyote yule ninaye muita “role model” wangu zaidi ya Yesu Kristo! Nina watu wengi wana ni inspire katika mambo mbali mbali na wakwanza kabisa ni wazazi wangu! I never call anybody in this planet my “role model”, kwani huyo ni mtu unayetamani kua kama yeye, nami kama kuna mtu natamani nifanane kama yeye basi si mwingine bali Yesu mwana wa Mungu! I want to be like Jesus!

Nilichogundua Watanzania wengi wenye elimu haswa hawa wakizazi hichi cha kwetu wapo very ignorance na wanachuki sana na watu ambao wamefanikiwa bila kupitia mfumo rasmi ya elimu (structured education). Haswa hawa watoto walikua, kusoma, na kutanua maisha kwa kutumia kodi za wananchi! Utakuta wazazi au mzazi wao alikua Mbunge / waziri / au senior Government officer basi wakiona mtu kama Joyce ambaye baba yake hukuwahi kua hata katibu kata amefanikiwa basi roho zinawauma wanakua na chuki kibao ?? Sikiliza wewe msomi, wewe unakipaji kwasababu kuna mtu katumia muda wake kukujaza madini kichwani mwako! Ingekua hauna hiyo elimu uliyopata darasani huwenda ungekua ni Zero brain! Mtu kama Joyce amejaliwa kipaji na uwezo mdogo wa elimu ambacho kimemfikisha hapo alipo ambapo wewe mwenye elimu umeshindwa kufika! Embu fikiria kama Joyce akiamua kuongeza elimu kidogo tu, itakuaje?! Unafikiri kuna msomi yoyote atakaye mbabaisha! Respect people’s hustles siyo elimu! Hata Bill Gates hakumaliza shule itakuwa Housegirl! Elimu ya darasani ni nzuri sana na ni muhimu lakini elimu ya ubinadamu (UTU) ni muhimu zaidi!

Marehemu Ruge Mutahaba akielezea kwa uchungu jinsi wasomi wa Tanzania walivyo small-minded, they think so shallow! Na hili tatizo huwa linanishangaza sana! Anyway, R I. P Legend, tutakukumbuka daima!

Kila tatizo lina chanzo chake kama ilivyo kwa jambo jema. Viongozi ambao mnatizamwa kama kioo cha jamii mnatakiwa muanze kuonyesha mfano wa UTU wa kuthamini kila mtu bila kubagua uwezo wake wa kuelimisha! Huku kwa walio endelea, utakuta viongozi wa juu hata Rais anatembelea shule yenye watoto wenye utindio wa ubongo, ili akiwa anafanya maamuzi au kuongea awe anaongea kitu anacho kijua na sio kusimuliwa na mtu, ambapo utakuta hata huyo mtu aliyekwambia naye kasimuliwa tu! Senator anaopopeleka mswada wa kuomba kuongeza pesa za kuelimisha watoto ambao ni Autist, anakua teyari anaelimu tosha juu ya Autism na umewaona kwa macho yake kua Autist anaweza kufundishwa kwa level ya uwelewa waka na akafundishika kabisa na kuwa independent! #Tubadilike

Kwa mara nyingine tena hongera sana Joyce, safari ndio kwanza umeanza, nakutakia mema yote!

Wema ni mwanamke dhaifu sana!

Siku ya jana ilikua ni siku ya wanawake dunia kote, kama ilivyokua kwa wengine basi naye Diamond alipost picha kuonyesha wanawake ambao ni muhimu kwake kama picha inavyo onekana hapo juu ???? na ujumbe wake! Hii nitofauti sana na tabia ya Diamond ambayo kwa miaka mingi amekua akiweka picha ya mama yake au saa nyingine anaweka na za dada zake.

Hakuna ubaya wa mtu yoyote kupost picha ya ‘X’ au ya “Ma_eX” zako kama bado upo single na unauhusiano mzuri nao. Lakini kwa hii ya Diamond inakua tofauti kwani inazidi kuonyesha jinsi gani Diamond anatabia za Unyanyasaji wa hisia (emotional abuse) kwa wanawake! Inazidi kuonyesha kua Diamond ni manipulator na narcissistic! Ukitizama wanawake ambao Diamond amekuanao kwenye mahusiano iwe kwa mapenzi yao wawili au bahati mbaya lazima utagundua na kukubaliana na mimi kua wote walijikuta wana poteza muelekeo wa maisha yao kusahau wao ni akina nani na nini wanataka kua katika hii dunia (they lost focus of who they are, their dreams, and what is their main purpose of existence in this planet world)!

Kaa chini angalia vizuri, utagundua kua karibia wote wanakua wakifanya vitu ambavyo vinampa Diamond ‘kiki’ ya kuongelewa na ku-boost muziki wake huku wao wakizidi didimia na kupauka! Anawatumia kutengeneza pesa lakini hawapi pesa za kufanya vitu vya maendeleo! halafu wao wenyewe wanakua hawashtuki mpaka watu wanapoanza kuwaonea huruma then wanadangwa na ‘maigizo’ ya kununuliwa gari na nyumba fake! Mtu ambaye alikua anaakili zaidi ya Diamond na alikua na uwezo wa kumshawishi Diamond kufanya vitu kwa maendeleo yake huku akijua kua 100% atanufaika na hayo maamuzi ni Zari the Bosslady peke yake na ndio maana familia haikumpenda. Na hii chuki ilianza baada ya kuweza kumshawishi Diamond anunue nyumba South Africa baada ya kuzaa naye Tiffah! Sidhani hata Tanasha kama ameondoka nalile gari la ‘maigizo’ ambalo alinunuliwa wakati wa birthday yake! Someone can prove me wrong, lakini naamini kwa asilimia zote limebaki Dar na sidhani kama lilikua kwa jina lake yeye Tanasha.

Kwanini nimesema Wema ni mwanamke dhaifu sana; wewe angalia katika huu ujumbe hakuna hata mwanamke moja ambaye ni Ex wa Diamond “kaushabikia” wala kujibu! Hila bidada hapa tobaaa! Embu soma comment yake hapo juu ???? Wema ngoja nikuulize, hivi kwalipi jema ambalo Diamond amekutendea mpaka awe na “special place” in your heart just for him?! Wanawake wengine wanajaribu kusahau hata majina ya “babydaddy” zao itakua Diamond?!

Huyu si ndio alikutumia wakati ukiwa upo juu, alipo ona thamani yako imeshuka akaenda zake? Kama hakukujali wakati ule upo mbichi leo hii umejizeekea kama akina Alpha hapa ndio atakuthamini?! Huyu Diamond juzi kati sialifanya sherehe ya miaka kumi tangu kuanza muziki, akawashukuru watu wote isipokuwa wewe! Wote walialikwa lakini wewe ukaachwa kama paka yatima! Sasa huyu mtu unawezaje ku reserve a special place in your heart just for him?!! Diamond anapenda attention na alifahamu fika kua kwenye hiyo sherehe angekuleta wewe attention yote ingehamia kwako, na hilo lisingewafurahisha ndio maana hukualikwa! Sasa inakuja issue ya Tanasha, Diamond alikua anajua hana mpango wowote na Tanasha ila hakujua kama Tanasha anaweza fanya maamuzi haraka hivyo imekuja kama surprise. Alijua angemchezea kama wewe! (Alisahau Tanasha ana damu ya Kijaluo, we are very intelligent! Tunajua kusoma alama za nyakati ????) Sasa anataka kukutumia wewe kama ‘scapegoat’ kumuumiza Tanasha na kupata attention zaidi.

Wema, labda nikuulize kwanini unakubali kutumika kuumiza mwanamke mwingi?! Are you that insecure and miserable?! Kwasababu Only weak women ndio wana hiyo eager and energy ya kuumiza mwanamke mwenzio. Mwanamke anaye jiamini kamwe hawezi kukubali upuuzi kama huo! Mwanamke anaye jiamini kamwe huwezi mkuta anafanya vitu petty ili mradi apate attention! Mtu yoyote ambaye ana furaha yakweli toka moyoni kamwe hana muda wala nguvu ya kukera wengine.

Juzi kati nilikuona upo kwenye event ya Idriss Sultan nauliulizwa kama utakuja kufanya nae kazi ukasema ‘ndio’! sasa kwa mtaji huu unafikiri Idriss atataka kuinvest his money on you?! Who wants to take that “liability” girl?! Na hapa inawezekana hata Diamond amesikia dalili za Idriss kutaka kukunyanyua tena; hivyo katumia akili ndogo tu kukuzibia fursa! Kweli marehemu Mugabe alikuwa sahihi aliposema “If you a woman with beauty and no brains it’s your private part suffers most”!!

Mimi nafikiri unatatizo fulani psychologically, unahitaji msaada wa wataalamu! Na hakuna ubaya wowote kuomba msaada wa wataalamu kwani kila mtu anamatatizo yake na tunawaona hao wataalamu wanatusaidi. Kitu kikubwa na chakwanza kabisa ni wewe mwenyewe ukubali kua kweli ninatatizo, na wewe mwenyewe ukubali kua unahitaji msaada wa wataalamu wa Psychology hapo ndipo utakua umeamua kweli. Lakini bila kufanya hivyo utashangaa utakavyo zidi kuchezewa na hawa wanaume!

Diamond is an emotional and energy sucker person. Wabongo huwa wanapenda kuwaita “wanyonya damu”! Mtu kama Diamond ambaye ana tabia za kuweza manipulate hisia za watu na ni narcissist basi anakua na uweze wa ku drain your brain and your emotions mpaka unakuwa highly depressed, hapo ndipo atakupelekesha kama “msukule” vile. Kuwa makini sana na watu kama hawa, bila Mungu huwezi mshinda! Diamond akija kuoa ataoa for ‘cover-up’ lakini huyo mwanamke atakua anaishi kwenye ndoa yeye peke yake (married but no different with single women out there)! Yani anaweza akanunuliwa gari zuri, mafuta full tank 24 / 7 lakini harusiwi kwenda popote bila ruhusa ya Diamond. Kila kitu atakua anafanya just to shut people’s mouth na sio kwa mapenzi.

Anyway, hayo ndio yangu sina la zaidi. Nakutakia mafanikio mema!

Kheri ya siku ya wanawake kwa wanawake wote ulimwenguni!

Alpha (Blogger) pamoja na mama yake mzazi
Mama Samia Suluhu, first female Vice President in Tanzania, an icon of women in leadership
Mama Janeth Magufuli, First Lady wa Tanzania awamu ya tano!
Veronica Sarungi, Mathematics genius at The Aga Khan University
Shilole, mama wa Shishi-food, Actress, Singer,
Jacqueline Mengi, Mwenyekiti wa Dr Ntuyabaliwe Foundation , owner of Amorrete furniture
Faiza Ally, mmachinga wa kishua
Jokate Mwegelo, Kisarawe District Commissioner, phenomenal woman behind Tokomeza Zero Kisarawe
Zarina Hassan, The one and only one East Africa Bosslady, owner of Brooklyn City Collage
Phenomenal women behind Women Matters talk show
Modester Opiyo (PhD), Lawyer, Judge of High court of Tanzania
Zamaradi Mketema, owner of Zamaradi TV, the woman behind Wonder woman event
Emelda Mwamanga, the mastermind behind the Bang! Magazine
Dinna Marious, Radio Personality, the ‘engine’ behind Women Kitchen Party Gala
Joyce Kiria, powerful phenominal woman behind Wanawake Live talk show
Hoyce Temu, TV presenter, amazing woman behind Mimi na Tanzania show

Kheri ya siku ya wanawake kwenu nyote na wanawake wengine wote duniani! Mwanamke ni msingi na nguzo ya kila jambo! Mungu azidi kutubariki kwa mema yote tutendayo!

Happy Women’s day!

Happy 67th birthday Sir O.O Igogo

Sir O.O Igogo

“YESTERDAY MY 66th YEAR ENDED & TODAY MY 67th YEAR BEGINNING ???? My days are counting down towards the Eve day, I am as healthy as a new born, blessed with wonderfull family members, a work that I enjoy doing every day, a business that affords us the daily needs and beyond, true friends who have been holding my hands for years, a peacefull mind ever that accepts failure as a challange to overcome, a big heart that never look down on others, a forgiveness habit that one can not doubt, a charitable giving hands that meets with the needy’s ever since. Allah have done wonders to me and through me to others. I father numerous children, born to me, adopted, dependants, able and disabled ones. I am blessed with amazing grand Childrens. God made my dreams to become real to establish business ventures which employs over seven hundred individuals on parmanent basis!! I vow to work for Allah Silently, in the back ground of believers, as a symbol of his kindness the population on earth, through my deeds, humbleness, humanly honest, hard work manship and a true God fearing man all my life time on earth. I thank all of you who have wished me a happy birth day and for the gifts I have recieved from some of you. Asanteni sana, Erokamano uru, Thank you so much. Otieno Olung’a Igogo. 07/03/2020.”

Birthday wishes from daughter Magreth Igogo-Massawe
Birthday wishes from daughter Janeth Igogo-Nyagilo
Daughter Blessing Gwethrhoda Igogo (given middle name after our paternal grandmother Rhoda) enjoying 67th birthday of her son ?
Birthday wishes from son William Ernest Mjee Oucho

On behalf of family members, friends, employees, and business partners I say Happy 67th birthday Sir O.O Igogo. Many more blessings to you! ?❤

Ukijua umekosea basi huna budi kuomba msamaha!

Katika vitu ambavyo ni tabia yangu hata wale ambao wananifahamu vizuri na niwatu wa kuongea ukweli basi wanaweza kushuhudia hili. Mimi ni mtu ambaye nikijua nimekosea au hata kuumiza hisia za mtu mwingine basi huwa sioni haibu kuomba msamaha, kwani huo ndio ubinadamu! Kama mtu alinikwanza kiasi cha kunifanya niongee vitu ambavyo katika hali ya kawaida siwezi kuongea basi nitamwambia naomba msamaha kwa lugha niliyo tumia lakini kwamwe sito omba msamaha kwa REACTION yangu! Kwasababu REACTION yangu ipo au ilikua sahihi japo lugha yangu haikuwa sahihi! Sikumbuki kama nilisha wahi muomba mtu msamaha kwa REACTION yangu kwani mie huwa sina hulka ya kumchokoza mtu au kufanya jambo ili tu nimkwaze fulani! Pettiness is not in my vocabulary! Because I strongly believe pettiness is a ground for evil! Mtu yoyote ambaye anaweza kufanya vitu fulani vyakipumbavu kwa makusudi mimi naamini mtu huyo ana viashilia vya uchawi na anaweza hata kuua mtu!

Kitakacho nidisturb sana kwenye hii kesi ama ambacho kina nidisturb kupita vitu vyote kwenye hii kesi ni jinsi jina la mume wangu linavyo kashifiiwa“- Jacqueline Mengi

Baada ya kusikiliza haya mahojiano ya Jacqueline na Millard Ayo naomba nikubali kua nilikosea sana kutoa maoni yangu bila kusikia upande wa Jacqueline! Nilisikia upande mmoja wa hii issue na kuongea na Jacqueline kwa hisia zote na kusahau kabisa kuwa siku zote kuna sehemu tatu ya jambo lolote lisemwalo! Hivyo ninakila sababu ya kusema Jacky naomba unisamehe nimekukosea sana! I’m a woman enough to admit I was wrong thus I am sincerely apologizing for the language used and negative image that I imposed on you! Naomba ieleweke siombi msamaha kwa REACTION yangu juu ya hii issue kwani 100% I stand by Dr. Reginald Mengi’s legacy! Msamaha wangu ni kwa jinsi nilikua harsh / so hard kwa Jacqueline!

Nilichogundua hapa watu tunaweza hukumu mtu asiye na hatia kabisa kwasababu ya watu waongo ambao wengine wanaaaminika katika jamii kua ni watu wema! Mimi nachukukia sana mtu muongo na mnafiki! Yani bora niishi na mchawi au mwizi huku nikijua kabisa huyu ni mchawi na yule ni mwizi hivyo natafuta njia salama ya kuishi nao! Lakini mtu muongo na mnafiki ni mtu mbaya sana, ni wakuogopwa zaidi ya ukoma! Hawa ndio wale wanaweza kukuua halafu anakuja msibani kwako kutoa hushuhuda jinsi gani mlikua mmeshibana!

Nimeongelea uongo na unafiki kwasababu angalia hawa watu walivyo kua wakidanganya watu kua Jackie anahusika na kifo cha mzee Mengi! Ndio maana kila nikitaka kuamni hisia zangu zinakataa kabisaaa! Hivyo hizi habari za kua Jacky ameweka pingamizi mahakamani nikasema basi huyu Jacky ni mkorofi anataka kuharibu Legacy ya Dr Mengi! Kumbe mtoto wa watu anapigania kuendeleza legacy ya mumewe! Dah! I’m deeply sorry Jacky. Unafiki huu, kama huyu mdogo mtu alikua na shida na kaka yake mbona hakusema wakati akiwa hai? Ameishi na marehemu miaka tisa (9 yrs) baada ya kumuoa Jacky mbona hakusema kitu?! na kwenye harusi alikuwepo?!! Inamaana wakati ule alitumia nafasi ile kumuumiza mtalaka wa marehemu (mama Mercy Mengi) kwa faida zake binafsi na sasa anatumia kifo cha kaka yake kumuumiza Jacky na watoto wa marehemu kwa manufaa yake!

Huyu baba mdogo inaelekea hata marehemu alishamuona ni “kasheshe” hivyo machale yakamcheza akataka azikwe kwenye mji wake na sio makaburi ya familia?! Kama kweli yanayosemwa na Jacky ni ya kweli basi huyu baba mdogo ndio mvuruga familia! Na kama Regina na Abdiel watamsikiliza huyu baba mdogo wakifikiria wako salama basi wanajidanganya sana! Akimalizana na Jacky atawaingilia wao atahakikisha Regina na Abdiel wanagombana huku yeye akijifanya ndio mpatanishi! Hii dhambi mnayo itenda haita waacha salama! Naona anahasira hakuandikwa kwenye Wosia, sasa sijui anafikiria kua naye ni mtoto wa marehemu?! Halafu, Regina na Abdiel how dare are you?? Mtu anaandika mambo ya kumdhihaki baba yenu halafu mnaungana naye? Eti mkidhani mnamkomoa Jacky? Si ndio mnaionyesha umma nyie ni watu wa namna gani!

Najaribu kutafakari baba yenu aliwatendea dhambi gani ambayo mnaona anastahili kukashifiwa wakati hawezi kujitetea?! Mnataka kutuambia vile vilio vya kujiinamisha mbele ya jeneza ilikua ni maigizo?! Regina mtoto wa kike muogope Mungu wewe! Hivi kumbe hautaki Legacy ya baba yenu iendele? Au kwasababu nyie hamna watoto hivyo mnafikiri mnamkomoa Jacky? Sorry, I may sound rude but I am only trying to understand what’s this “war over”?! Mbona huo WOSIA sounds right to me! Nyie mmechukua khamsini 50% na wale watoto wamepewa 50% na Jacky wala hausiki kwenye mali ambazo marehemu alichuma na mke wa kwanza? What’s this all about? We the people of Republic of Social Media we desperately want to know!! Mzee wetu alikua mtu wa Social Media he got huge family kwenye ardhi na huku mawinguni (mitandaoni) hivyo mtueleweshe huu ugomvi wa nini! Nyie wenyewe mmesha broke “family code” kwa kwenda mahakamani sasa tunataka kusikia sauti zenu mtuambie kama Jacky anadanganya au la!!

Chakushangaza Jacky hakuingilia ndoa wala kuvunja ndoa ya mama yetu Mercy Mengi kama tulivyo aminishwa hapo mwazo! Hana nawala hataki mali yoyote ambayo ilichumwa kabla yeye hajaolewa! Sasa hizi hasira zote zanini? Kwanini mnamuonea huyu dada?! Angalia anavyo ongea kwa busara na upendo kwenye hiyo interview, anawaita “hawa wote wanangu”, “watoto wetu wakubwa” mpaka marehemu mama yenu anamuita mama?!! Jamani, if that is not LOVE then what is it!! Hivi mnajua watu wangapi wanatamani wangekua na step mama mwenye roho kama ya Jacky!! Hivi mnajua kuna step mother wangapi ambao wako busy kubomoa legacy za waume zao tena wakiwa bado hai?! Seriously, you guys had the best of best and yet naona mna ZERO appreciation! Wee Abdiel, how can you let this happen? Hivi mnaachaje baba mdogo anavuruga legacy ya baba yenu namna hii?! Nasema tena hii dhambi haita waacha salama!

Jacqueline Mengi akihojiwa na Millard Ayo!

Jacky sasa tumekupata na kukuelewa! Unakila haki na sababu ya kuongea, tena zidi kuongea ili kumbu kumbu ziwekwe! Kama unasema uongo basi wajitokeze na evidence wakanushe ulichosema! Na kwamtaji huu you deserve to sit on that throne because you have Dr Mengi’s interest in your heart! Kwanza hauja mdhulumu mtu! Nakama hawato kubali kutengua hizo kauli na maneno yao waliyo andika huko mahakamani basi kataa kupatanishwa nao kabisa! Nakuanzia sasa kitu chochote kikimkuta Jacky wao ndio watakua watuhumiwa namba moja! Halafu wataona nguvu ya familia ya mzee Mengi (The Republican of Social Media ??) kama itawaacha salama! Mimi nasema Dr Mengi’s Legacy Must Live On! Dr Mengi’s Legacy For Life!

Once again, I’m so sorry! Nitakuweka kwenye maombi yangu kuanzia sasa. ?❤❤

***Shukrani za dhati kwa Millard Ayo TV kwa interview nzuri sana***

“Acha Alama nzuri mioyoni mwa wale wanaostahili”***** Zamaradi Mketema

Reposted from @zamaradimketema Leo nilikutana na watu walikuwa wanajadili jambo japo katika hali ya masihara lakini nikagundua makosa makubwa ambayo huwa tunafanya sisi binaadamu

Zamaradi Mketema na binti yake Shubi Ruge Mutahaba

Watu wengi husema ukipendwa Ringa, mi nasema hapana, Ukipendwa THAMINI, na ikiwezekana mkomeshe kwa kumpenda zaidi, wenye mapenzi ya kweli ni wachache mno Duniani, Make Sure ukimpata kuwa KILEVI chake, mfanye awe ADDICTED na wewe, mzoeshe ama weka utaratibu ambao hata itokee mmekosana ashindwe kukaa siku moja mbili kakaza, sababu kuna kitu tu anakosa, kuna watu wanahisi pozi ndio Ujanja, Pozi ni ushamba!! Especially kwa mtu anaekupenda, kama wanavyosema Dawa ya Moto ni Moto kwenye mabaya basi hata mazuri ni hivyohivyo, mtu akikupenda mpende zaidi, haupotezi unawekeza, hata kesho akiwa mbali, kitakachomuumiza ni hiko, lakini kama wewe ni mtu wa headache kilasiku hakuna atachokumbuka

Beautiful Zamaradi Mketema

Na hii haiapply kwa mume/mke ama mpenzi peke yake, ila hata rafiki na watu wema tunaokutana nao, Acha Alama nzuri mioyoni mwa wale wanaostahili kiasi kesho na kesho kutwa hiyo ndio silaha yako pale mtakapokuwa mbalimbali, ukijiangalia una chochote ulichowekeza kwa wale wakupendao!!? Unahisi wewe ni kilevi chao ama headache!!? Kuna Alama umeshaweka ama ndio Upepo utakapopita umepita!? Tafakari halafu chukua hatua

Nimejisikia tu kuongea hiki, Muwe na Usiku Mwema!! – #regrann