Category Archives: Couples we like

Thank you from Mr and Mrs A. Banduka 

We would like to thank you for all the love and support you have given us over the course of our lives and for being in the midst of this exciting and memorable adventure. We appreciate each of you and recognize your participation. We’re honored that you came to celebrate and witnessed our love and vows to each other. To each and everyone of you, you mean so much to us and we’re beyond thankful to have you in our lives. Finally, to all of those who have given us their time and helping hands with planning this wedding, WE THANK YOU. From the bottom of our hearts we could not have done this without you.

The most attractive quality any man could have is integrity!

2017-Hottest And Best Couple Of The Year!

Mr and Mrs Joseph Musira ndio Hottest And Best Couple of the Year!……Sababu haswa ya kuichagua hii couple kwanza nimeamua kwa mwaka huu ni enzi wazee wetu. Pili miaka 53 ya ndoa si kitu kidogo lazima kiheshimiwe! Napia ni kwasababu wanastahili!!……Basi ifuatayo ni historia yao fupi ambayo nitaieleza kwa kutumia picha zao za sherehe ya miaka 50 ya ndoa yao (Golden Jubilee of their wedding) ambayo ilifanyika huko Musoma, Mara miaka 3 iliyopita! Sherehe hiyo ilianzia kanisani ambapo walibariki ndoa yao na kuvaa pete ya nadhiri ya miaka hamsini!…….Haya furahia picha and Happy Valentine’s Day to you all! Maombi na kiapo yakiendelea ……….. Mr Joseph Musira na Felister Awiti wao ni wazaliwa wa mkoa wa Mara. Walikutana kwa katika kijiji kimoja kijulikanacho kama Kowak katika wilaya ya Rorya mkoani Mara. Felister yeye ni mzaliwa wa kijiji hicho cha Kowak akiwa ni mtoto wa kwanza wa mzee Cornel Awiti. Wakivishana pete baada ya ndoa kubarikiwa!…….Mzee Joseph Musira yeye ni Mwalimu kwa taaluma; hivyo wakati alipokutana na Felister alikuwa ni Mwalimu wa Kowak Middle School ambayo ipo chini ya missionary ya Wakatoliki. Kwasasa shule hiyo imebadilishwa na kuwa secondary ya wasichana ijulikanao kama Kowak Girls Secondary School ambayo mimi nilikuwa ni miongoni mwa wanafunzi walio fungua shule hiyo kwa mara ya kwanza. Mdogo wangu anaye nifuata kuzaliwa naye alisoma hapo! Picha ya pamoja na viongozi wa Diocese ya Musoma ambapo mzee Musira amekuwa mtumishi wao mpaka leo hii! Alianza kwa kufundisha kama Mwalimu, baadaye alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa shule zote za mkoa wa Mara ambazo zinamilikiwa na kanisa Katoliki mkoani humo! Ali stahafu akiwa katika cheo hicho zaidi ya miaka 5 iliyopita, lakini kwa uwadilifu wake na maadili mema kazini walimuomba kuongoza charity organization ambayo ipo chini la kanisa hilo hapo Mwembeni street, Musoma. 

Cheti kiki kabidhiwa toka Vatican kwa Papa!….. Furaha iliyoje! Wakielekea ukumbini kwenye sherehe!…..Kama nilivyo waeleza hapo mwanzo kuwa Mzee Musira alikutana na bibi Felister katika kijiji cha Kowak akiwa Mwalimu. Basi naye bibi Felister alikuwa ni Registered Nurse katika hospitali ya Kowak Mission ambayo nayo ipo chini ya missionary ya Wakatoliki. Ambapo pia baba yake mzazi bibi Felister alikuwa akifanya kazi kama Clinical officer katika hospitali hiyo…….Miaka miwili baada ya wapenzi hawa kukutana waliamua kufunga ndoa, kula kiapo kitakatifu mbele za Mungu na uso wa dunia! Hapo ilikuwa tarehe 12 / September / 1964! Kama mnavyo jua kuwa maswala ya kuoa katika familia za Kiafrika si kitu cha mchezo kama wenzetu wa dunia ya Magharibi ambapo wapenzi wanaweza kuwataharifu wazazi wao kupitia Facebook, text msg, Tweeter, na Instagram kuwa wao wamepanga kuoana siku fulani na wazazi wakafurahia kabisa kwa furaha kuu! Hapana, ndoa ni agano takatifu lazima liheshiwe sana kwa kufata taratibu maalum za kimila na kidini! Basi ndivyo hivyo kama wafanyavyo wengine naye alifanya! Mzee Musira alifata mila za Waluo ili kuweza kumchumbia na kumuoa bibi Felister! Yeye aliambiwa atoe mahali ya ng’ombe 12 na pia amjengee mama nkwe nyumba ya mabati ya vyumba vitatu na sebule! Awwwh! Huu ukoo wa Awiti siyo watu wa sport sport ati 🙂 🙂 🙂  Si mnajua kuwa bibi Felister alikuwa msomi (Registered Nurse) wa nguvu 🙂 🙂 hivyo baba mtu hakutaka mchezo na binti yake! …….Ukisikia “mapenzi mubashara” basi haya ndo yenyewe kwani mzee Musira alitekeleza hayo masharti yote bila pingamizi! Hiyo nyumba ndio mama mkwe wake aliishi mpaka mauti ilipo mkuta mwaka 2014! Tutakiane mkono wa amani mpenzi wangu, tumetoka mbali sana. Asante sana kwa “mapenzi mubashara”…..,hayo yalikuwa maneno matamu kabisa kutoka kwa mzee Musira kwenda kwa la azizi wake bibi Felister ???   Champaign zikifunguliwa na watu wenye nyuso za furaha kabisa! Aliye vaa vazi la kitenge ni mdogo wake bibi Felister aitwaye Anna Cornel au Mrs Obure. Yeye ndiye anaye mfuatia Felister, ni Mwalimu mstahafu hapo Musoma. Baada ya kufunga ndoa bibi Felister ilibidi ahame kwenye nyumba aliyopewa kuishi kama nurse mkuu hapo mission na pia alibadili jina lake la mwisho kutoka Awiti kwenda Musira. Hapo ndipo walifanya maamuzi ya kuhamia Musoma, na miezi michache baadaye mzee Musira alipelekwa Germany kuongezea utaalamu zaidi katika fani yake! …….Waliishi Musoma kwa miaka kadhaa na baadaye mwaka wa 1970 waliamishiwa Moshi ambapo waliishi kwa zaidi ya miaka 10 kabla ya kurudishwa tena Musoma……. Mr na Mrs Musira wao wamebarikiwa kupata watoto 6. Watatu wa kiume (Musira, Gerald, na Peter) na watatu wakike (Eddina, Yasinter, na Neema). Eddina a.k.a Eddi yeye ndio mtoto wa kwanza na Neema ndio wa mwisho! Kwa bahati mbaya kijana wao aitwaye Peter yeye alisha lala usingizi wa mauti; hivyo hayupo nao tena! May his soul continue to rest in peace!Mungu pia amewajalia kupata wajukuu wanne! Wakiume watatu na wa kike mmoja!  Wakinyweshana kinywaji maalum cha siku hiyo Mahaba mahabani! Kama walivyo shikamana siku ya kwanza pale Kowak basi ndivyo watakavyo shikana mikono yao mpaka mauti itakapo watenganisha! Waki kata keki kwa upendo na furaha Nilishe nikulishe ndio ishara ya upendo Mungu ni pendo. Penye Mungu kuna upendo mwingi na furaha isiyo elezeka! Hapa siongelei tu ndoa za “maigizo”, zile ndoa za ku-show off picha kwenye mitandao ya kijamii wakati ndani ya nyumba zenu wengine hawahemi! hapana! Naongelea real marriage, real commitment, honoring your vowels!!………. Miaka 53 ya ndoa hakuna michepuko wala mtoto wa “bandia”! Jamani, inawezekana!! These are real people in our communities; nina huwakika wapo wengine wengi tu!………Ee Mwenyezi Mungu endelea kumimina baraka zako kwenye hii ndoa na familia yao, Amen!

Couples we like!

Je, upo tayari?! Couple yangu ya pili -2016

Are you ready!!! Hii ndio ilikuwa couple yangu ya pili kuichagua. Mpaka sasa sijajutia kuichagua. Yani couple zote bado zipo kwenye mahaba mazito sana!! Nawaombea Mungu ndoa zao zidumu milele na awatangulie katika kila jambo! Kama ulipitwa soma HottestAndBestCouple-2016 …….. Je, upo tayari kwa 2017?!! Stay tuned!

je, upo tayari?! Couple yangu ya kwanza -2015

Nilipo anza ku-blog ilikuwa ni mwezi wa Pili mwaka 2015. Na hii ndio ilikuwa couple yangu ya kwanza kabisa kuichagua kama Hottest and Best Couple of the yr kwa mwaka huo! Nikitu niliamua kufanya kila tarehe 14/2 ya mwaka (siku ya Valentine day) nitatangaza couple moja iliyonivutia ambayo pia naona kuwa ni mfano mzuri wa kuigwa katika jamii! Kama ulipitwa na tangazo hilo tazama hapa ? HottestAndBestCouple-2015

Je, upo tayari kwa mwaka huu?? Stay tuned!!

If you sign up for a “sex only” relationship in the beginning…..! Don’t ask him to wait if you can’t!

Ujumbe huu unajieleza wazi kabisa! Kama wewe nia yako ni kuwa na mume basi usitafute boyfriend kwani nia ya malengo yako hayata timia! Kama nia yako ni kuwa na mtu wa ku share naye mapenzi maisha yako yote basi usikubali tittle ya “my lover au mwanamke wangu” kwani hivyo ndivyo utakavyo ishia! Respect is earned not given!…………. Na usimwambie mwanaume ngoja mpaka tufunge ndoa wakati wewe si bikira! 😉 😉 ……….. Happy early Valentine to you all!

Couple we like!

Couple yangu. Best and Hottest couple ya  2016 ; sijutii kuichagua kwani sikufanya makosa! Wanastahili!

The Makondas’! Beautiful couple with amazing souls!

Da Tuma na barafu ya moyo wake! Wamependeza! 

LONG WALK TO SUPER CLASS by Sir O.O Igogo

Sir O.O Igogo
Sir O.O Igogo

In life from the poorest widower’s son at the age of 15. Having failed to join secondary education, ending up to be employed as Cattle rustler, a butchery labourer at my elder brother’s butcher; inherited from our late father, at a pay of either 50 cents a day or half a pound of beef to bring home. Then a dishes washer, waiter and mishikaki roster at the restaurant of my first cousin JC Igogo. It was until my sister Teddy came for my rescue and took me to Dar for job seeking. That was in 1969, I was 16. I worked in the factories while attending my evening classes to become a professional. I recall when I managed to have our own shelter in 1978.

fb_img_1457295925797
Mr and Mrs O.O Igogo back in the days

We were five in the family, fortunately you was the youngest after Elline and Vetto. That was the biggest achievement I had ever had in life. A four wall of cement and sand moulded blocks, with corrugated iron sheets covered our roof; never the less it had no fittings on the doors and window openings. With sandy floor without any cement sand screedning, walls were bare without any plastering, but at least Cecy and I owned a piece of land of our own, built that ugly and hut to live in that was better by far from what my mom had in the village. Though we shared common challenges of having no electricity and running water connection.

Mr and Mrs O.O Igogo
Mr and Mrs O.O Igogo

On and on, with endurance I furthered my education, and got a better salary  job as a Manager at NECO LTD. Then life changed to at least a more decent living, I could drive company vehicles and travelled a lot in the regions. That made me to earn more money as allowances. My hard workmanship, honesty, reliability and a big heart on helping others, got me where I am today after I toiled a lot in life. img-20161214-wa0000You were there when we moved into our first small hut, and fortunately you will be there when we move into our state of art Villa this month. Though that is not real success in life but I’m proud of you guys who have made me what I am today specifically my spouse, mama Alpha.fb_img_1438002378122Difficulties in life are ladders to bigger achievements in life; if you can allow them to come and go because HARD TIMES NEVER LAST BUT HARD PEOPLE DO. Be like baba, don’t hate your enemies, love them and God will raise you beyond their expectations.

The best pic of the week: Baba na Mama Wawili!

screenshot_2016-12-14-22-50-26-1Awiiiiii! We Jakilini Jakilini wee ee! ngoja niimbe kidogo ???? Wana meremeta wana waka-waka aa! ??  huo naona haunogi ngoja niimbe huu ? ndo  wenyewe wa ukweli ????

Wenye wivu wajinyonge tu kwakweli maana hamna namna ?? Na idumu milele hiyo asali ya moyo wako ???

Couples we love!

screenshot_2016-12-13-07-56-28-1fb_img_1481637239288fb_img_1481636977016My wifiiii! can’t wait kuserebuka ???