Category Archives: General

Dr. Milton Makongoro Mahanga azikwa leo!

Marehemu Dr. Milton Makongoro Mahanga enzi za uhai wake!

Aliyekua Mwenyekiti wa Chadema mkoa wa kichama Ilala Dr Milton Makongoro Mahanga amezikwa leo majira ya mchana saa za Africa Mashariki katika makaburi ya Tabata-Segerea. Marehemu alizaliwa April 03, 1955 na kufariki dunia siku ya Jumatatu tarehe 23 mwezi huu, mwaka 2020 katika hospital ya Muhimbili alipokua anapatiwa matibabu. Marehemu ameacha mke, watoto, na wajukuu.

Kwaniaba ya familia ya mzee Otieno Olung’a Igogo naomba kutoa salamu za pole za dhati kabisa kwa familia ya marehemu, ndugu, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), majirani, pamoja na watu wote walioguswa na msiba huu.

Kama wewe ni mfuatiliaji mzuri wa alphaIgogo.com basi utakua ulishawahi soma huko nyuma post ambayo nilieleza uhusiano wa kidugu uliopo kati ya familia yetu na marehemu. Ilikua ni wakati wa msiba wa marehemu Dr. Didas Massaburi ????(https://www.alphaigogo.com/r-p-dr-didas-massaburi/) Kwa ufupi marehemu alikua anamuita baba yangu ‘kaka’ kwani mama zao ni madada. Marehemu Dr. Massaburi, marehemu Dr. Mahanga, pamoja na baba yangu mzazi hawa ni cousin-brothers mama zao ni ndugu wa damu. Basi kwa walio wengi wanamuangalia marehemu kama Mwanasiasa lakini kwa upande wetu ni mwana familia.

Na kwa wale mnao toka Rorya najua wengine nmnaweza jiuliza udugu wetu na marehemu Dr. Phenias Ziki Makoyo?! Dr. Makoyo naye pia ni cousin-brother wa baba yangu. Marehemu baba yake Dr. Makoyo, mama mzazi wa Dr. Massaburi, mama mzazi wa Dr. Mahanga, pamoja na mama mzazi wa baba yangu hawa ni ndugu wa damu!

Hivyo basi, baada ya kusema hayo, naomba ieleweke vizuri kabisa kua sijaweka hii post kuwakilisha chama chochote kile cha siasa hapa dunia! Hii post nimeweka hapa kwasababu marehemu ni sehemu ya familia yetu, pia hawa ndugu walikuwa marafiki wazuri sana. Natamani upendo waliokuaga nao wazazi wetu tungekua nao sisi watoto pia, lakini hichi kizazi cha Dot.com kina mambo mengi hivyo tuchukuliane tu hivyo hivyo ??

Pichani juu ni baadhi ya viongozi na makada wa CCM wakiongozwa na Katibu wa Itikadi na Uenezi Mr. Humphrey Polepole. Mr. Polepole alitoa salamu za rambi rambi kuwakilisha chama cha CCM ambapo marehemu ndipo alipo anzia mapambo yake ya kisiasa.

Ni vyema kuona mifano kama hii kwa viongozi wetu wa siasa a.k.a ‘wanasiasa’ ili Watanzania waweze kujifunza kutofautisha maswala ya kisiasa na mahusiano binafsi, itikadi za dini, na mambo mengine yote ambayo sio ya kisiasa. Siasa isimame kama siasa na isichanganywe na mambo mengine kama baadhi ya wanasiasa na “wanaharakati” wanavyotaka kuigawa taifa na familia za watu, tena wengine kwa makusudi tu na chuki zao binafsi!

Marehemu amefariki akiwa mwanachama wa Chadema lakini ikumbukwe kuwa alikuwa mwana CCM kwa muda mrefu, na huko alikuwa na marafiki, ndugu, na jamaa ambao bado ni wana CCM. Hivyo inapofika swala ambalo sio la kisiasa kama hili basi ni vyema wana siasa KUVUA KOFIA YA SIASA na kuweka swala la msingi mbele! Ni hatari sana kwa taifa kama wananchi wake wataweka siasa kwenye kila jambo. Kuna watu ambao hawapendi kujihusisha na vyama vya siasa ambao ni sehemu ya familia zetu na marafiki zetu basi ni busara, haki, na pia ni lazima maamuzi yao yaheshimiwe na kila mtu, msipende kulazimisha mambo eti kila mtu lazima awe mwanachama wa chama fulani cha siasa. Nope! Kila mtu ana hiyari ya kufanya maamuzi yake na hiyo ndio DEMOKRASIA.

“4 nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo. 5 Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako. 6 Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. 7 Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; 8 baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.” 2Timothy 1: 4-8

  • Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe milele zote. ????

Kumradhi!

Jana niliandika kua marehemu amezikwa jana 03/25/2020 jambo ambalo halikua sahihi. Marehemu amezikwa leo 03/26/2020 katika makaburi ya Tabata-Segerea.

Naomba radhi kwa kosa hilo ambalo nilitenda bila kukusudia, ni misunderstanding ya muda ndio ilitokea. ??

Ni muda muafaka wa kuelimisha Watanzania juu ya ugonjwa wa Alzheimer na Dementia!

Reposted from @millardayo Kama tunavyofahamu Mkuu wa Mkoa wa Iringa Ally Hapi @ally_hapi ameendelea kupiga kazi kwa kuzunguka sehemu mbalimbali za Iringa kukutana uso kwa uso na Wananchi kumaliza kero zao kwenye ziara anayoiita ‘Mahakama ya Wananchi’.•Kwenye hii video ni wakati alipokwenda Ipogolo, akajitokeza huyu Bibi na kusema Mtoto wake na Mjukuu wake hawataki kuishi nae, wamemfukuza na wamemuibia laki tatu zake.•Pamoja na kwamba Bibi alikua anaelezea matatizo yake, Watu waliohudhuria walijikuta wakicheka kwa jinsi Bibi alivyokua anahadithia. (? @ayotv_ ) – #regrann

Nimekua nikiona video hizi ambazo watu wanakua wanacheka au kuwazomea au kuwaita wachawi wazee ambao wanakua kama wanatatizo la kujielezea vizuri! Hili swala naona hata viongozi wetu wanahusika sana katika kuendeleza hii tabia ya unyanyasaji juu ya wazee! sina huwakika kama wanajua kuwa huwenda kunatatizo kwenye ubongo ambalo linawasababishia kuwa katika hali hiyo? au huwa hawafahamu? Au wanafahamu lakini ujinga (ignorance) imetawala akili zao! Yani unatazama kiongozi anaongea na mtu mzima mwenzake au saa nyingine amemzidi umri lakini jinsi anavyo ongea naye unabaki mdomo wazi na hasira juu!

Yani mara nyingi utakuta hawa viongozi wanapenda kuongea na watu kwa hasira (sauti za kufoka) kana kwamba wanaongea na mtoto wa miaka 2! yani hawana sauti (tone) ya kuonyesha compassion and respect kwa watu wengine! Utafikiri kwenye seminar / training zao za uongozi hivyo ndivyo walivyo fundishwa kua kiongozi ni mtu wa kufoka foka kama pombe ya “wanzuki”, kukunja uso na kutoa maneno ya dharau! ?? Lakini napo ninesikia wengi wakisema Watanzania walio wengi bila kumgombeza na kutoa maneno makali hakuna linalo fanyika ??‍♀️??‍♀️ na hii tabia wanaileta hata wanapokua kwenye mahusiano yani ni full ubabe tu! ?? Ukitaka kujua tabia ya jamii husika angalia viongozi wake utapata jibu.

Marehemu bibi yangu mzaa mama, Mrs Valeria Cornel Awiti alifariki March 12th 2014, akiwa na umri miaka 88

Turudi kwenye mada yetu, naamini ni muda muafaka sasa kwa serikali chini ya wizara husika inayo shughulikia mambo ya wazee pamoja na ustawi wa jamii kuchukua jukumu la kuanza kuelimisha Watanzania juu ya magonjwa au mabadiliko ya ya akili yanayotokana na uzee au msongo wa mawazo (severe depression). Kuna magonjwa kama ALZHEIMER na DEMENTIA ambayo mara nyingi yanawakuta wazee japo sio wote ! Nimesema mara nyingi kwani kuna wazee ambao hawakumbani na haya matatizo na pia kuma watu ambao wana umri wakawaida (average age) na wamepatikana na Alzheimer na Dementia. Binafsi nimeshuhudia mtu wa 55 na 51. Hivyo hatuwezi sema kuwa kwa 100% ni magonjwa yanayo wapata wazee! Mimi si Doctor hivyo siwezi kuelezea katika lugha ya kitaalamu zaidi ili watu waelimike. Ila nimeshawahi kufanya kazi na watu wenye matatizo kama hayo nikiwa kama muhudumu wa afya (Nurse Aide) katika Nursing home pamoja na sehemu ya kuwaangalia wazee; kwa maana hiyo nina ufahamu kiasi juu ya Alzheimer na Dementia.

Kwa lugha rahisi naweza sema Alzheimer ni tatizo linalohusiana na kupoteza kumbu kumbu kwenye ubongo ( brain memory loss), ambayo huja kwa stage au aina tofauti tofauti. Kuna wenye tatizo la kupoteza kumbu kumbu ya mambo yaliyo pita kwa miaka kadhaa. Kuna wenye tatizo la kupoteza kumbu kumbu ya kitu chochote kilicho tokea jana au ndani ya siku kadhaa (past 24 hrs or within72 ), kuna wenye tatizo la kupoteza kumbu kumbu ya kitu ambacho kimepita hata dakika moja! Hizi zote zina stage yake sidhani kama kuna mtu anaanza kwa kupoteza kumbu kumbu zote kwa mara moja, ila huwa ugonjwa unaanza taratibu huku ukizidi kuongezeka kwa kuwa na uwezo mdogo sana wa kutunza kumbu kumbu za matukio au jambo lolote lile.

Wakati Dementia ni ugonjwa unaohusisha kupoteza kumbu kumbu pamoja na uwezo wakuishi kama binadamu mwenye akili timamu. Yani mtu mwenye Dementia lazima ana Alzheimer lakini mtu mwenye Alzheimer peke yake basi hawezi kuwa na Dementia. Japo hatua za mwisho (last stage) ya Alzheimer huwa wanakutwa na Dementia. Hapa ndipo unakuta mtu hawezi kuongea vizuri, hawezi kufanya vile vitu ambavyo kwa kawaida angeweza kufanya mwenyewe kama kula, kuoga, kwenda chooni, n.k Mtu mwenye Dementia anakua hawezi kujua jema wala baya (can’t reasoning and make judgment). Yani anaweza akachukua chupi nakuvaa kichwani, anaweza sio tu kusahau majina ya watoto zake bali anaweza akawakana kabisa kuwa yeye hana watoto.

Sasa vitu kama hivi ni muhimu kwa jamii kuelimishwa ili kuweza kutambua, na kuwa teyari kukabiliana nayo. Hii hali ya Alzheimer na Dementia huwa ni very terrifying kwa watoto haswa pale unapoona mama yako au baba yako sio tu hakumbuki jina lako bali anakukana kabisa kuwa wewe sio mtoto wake na yeye hajawahi kuwa na watoto.

Kama hawa wenzetu ambao elimu ya haya magonjwa wanapewa na kuandaliwa (financially, psysociologically, emotionally, socially, na spiritually) pindi mzazi au ndugu anapoonyesha dalili za Alzheimer lakini bado unakuta inakua ni ngumu sana kwao sio tu kukabiliana na ugonjwa bali kukubali hali halisi kuwa huyo sasa ndio mzazi wake ambaye yeye alikua akimtazama kama hero / shero yupo kwenye hali hiyo ambayo hawezi kutofautiana chooni na jikoni! Anaweza jisaidia mahali popote pale. Tafadhali serikali ya Tanzania chukuweni jukumu la kulewa wazee kwa uzito na mapana zaidi.

Mimi nikiwa mgongoni mwa bibi yangu. Ilikuwa ni mwaka 2010, nikiwa kijijini Kowak ambapo mama yangu mzazi amezaliwa na kukulia hapo. Hiyo nyumba unayo iona ndio nyumba mama yangu amekulia na mahali yake hapo ndipo ilipotolewa. Nilikuwa nimekwenda likizo Tanzania nakama ilivyokuwa kawaida yangu ni lazima kwenda kutembelea bibi na babu zangu pamoja na shangazi zangu. Yani siwezi kurudi Marekani bila kwenda kuwasalimu; halafu watu wakiona unapewa upendeleo na Mungu wanakuchukia ?? jamani wengine tumetemewa yale mate yenye harufu ya kuku wa kienyeji yana bimaraka yale asikwambie mtu ?? Hapa bibi yangu alikua ameanza kuonyesha early stage ya Alzheimer. Saa nyingine alikua anasahau hata njia ya kurudi kwake akitoka kanisani. Bibi yangu na babu yangu mzaa mama wao walikuwa hardcore Catholic church believers.

Huyu ni babu yangu mzaa mama, marehemu mzee Cornel Awiti. Yeye alifariki 2011 akiwa na umri wa miaka 92. Hizi picha ndizo picha tulipiga mara ya mwisho kuonana (February, 2010). Kama nilivyo sema hapo mwanzo kuwa sio wazee wote wanapata Alzheimer basi ndivyo ilivyokuwa kwa marehemu babu yangu. Yeye mpaka anafikia hatua za kukata roho alikua na akili zake timamu na kumbu kumbu zake zote! Yani at age of 91 aikua ananitajia dawa zote anazo tumia tena kwa kingereza. Yeye alibahatika kupata elimu ya utabibu enzi za mkoloni, hivyo alikuwa na ufahamu juu ya magonjwa yake na dawa anazo tumia. Babu yangu alikuwa na tatizo la moyo kuwa mkubwa na BP ambayo yalipelekea kifo chake R.I.P. babu yangu missing you dearly ??

Pichani ni marehemu bibi yangu mzaa baba, Rhoda-Nyakanga Olwengo Igogo, akiwa na binti yangu Mercy mwaka 1996. Mwanangu jina lake lingine ni Teddy (Theresia) alipewa na babu yake kumkumbuka dada yake wa pekee. Baba yangu kwao walikua wanaume 3 na msichana mmoja. Shangazi alikua mtoto wa kwanza na binti pekee kwa tumbo la bibi yangu, japo nina mashangazi wengi kwani babu yangu alikua na wake wengi.

Kama ilivyokuwa kwa babu yangu mzaa mama basi ndivyo ilivyokuwa kwa bibi yangu mzaa baba. Yeye naye hakuwai kupatwa na tatizo la kupoteza kumbu kumbu, tena alikua anakumbuka mambo mengi ya zamani mpaka baba anamshangaa! Nafikiri mimi nimepata hicho kipaji toka kwake na kwa babu mzaa mama. My brain memory is good I mean ridiculously good ?? Yeye naye moyo wake ulianza kuwa mkubwa in the early 80s. Alifariki akikadiriwa kuwa na umri wa miaka 88. Bibi yangu asili yake ni Kenya.

Juu ni wadogo zangu Janeth na Magreth pamoja na bibi. Hizi picha tulipiga July 2013, na ndio ilikua mara ya mwisho kumuona bibi yangu akiwa hai. Mwaka uliofuata alifariki (March, 2014). Wakati huu tulipokwenda msalimia ilikua tofauti na 2010. Hapa alikua ana Alzheimer na Dementia. Yani Alikua hawezi hata kukaa mwenyewe bila mtu kumshika au kuweka mto kwa nyuma kumzuia asidondoke. Alikua hawezi kula mwenyewe wala kujihudumia kwa kitu chochote kile, hivyo kulikua na mfanyakazi pamoja na mama zangu walipeana zamu za kwenda kumuona. Nashukuru Mungu sana na siku zote nasikia faraja kuwa katika watu wote pamoja na watoto zake bibi yangu hakuweza kunisahau, yani alikuwa ananikumbuka jina langu ila nikimuuliza juu ya mama yangu anasema ‘Cecilia alikufa siku njingi’ halafu anaanza kumlilia ?? na mtoto wa Cecilia ambaye anamjua ni mimi tu ?? Nakumbuka alivyosema eti safari hii ukiondoka niachie hiyo suruali yako nataka na mimi nivae ??

Kwangu mimi ilikua rahisi sana ku adjust na hali aliyokuwa nayo bibi kwasababu nilisha ona hizo dalili toka anaanza kupoteza kumbu kumbu, na nikawa na jaribu kumuelimisha mama how to handle her na kukubaliana na hali halisi. Kitu ambacho mama hakukubali ni kununua depends / disposable underwears (zile diapers za wakubwa) kwa ajili ya bibi. Yani nilikua na mwambia itarahisisha usafi wa bibi lakini hakuweza kukubaliana nalo kwani kwake aliona kama nina m-degrade mama yake. Sikukasirika kwani nilijua yupo kwenye denial ya kuwa mama yake hayupo tena kwenye hali ya utuuzima (mama) japo ni mama yake.

Anyway, mimi huo ndio wito wangu kwa serikali na jamii kwa ujumla. Tuwajali na kuwatunza wazee wetu kwa kutambua mabadiliko ya kiafya ya mwili na akili wanayopitia. Tuelimishane na watu waache kugombeza wazee tunapo waona wapo katika hali isiyo eleweka. Tambua lazima kunashida mahala na tafuta msaada kwa madaktari. Tuache hii tabia ya kufokea watu wazima.

***Video shukrani kwa AyoTV***

Kulikuwa na ulazima gani?! Kwanini leo?!

Leo naona watu wengi wamempongeza Diamond kwa kitendo cha kuonyesha kuunga mkono kazi za Harmonolize a.k.a KondeBoy. Diamond ameandika ujumbe mzuri sana ambao wengi wameamini unatoka moyoni! Hata mimi naamini umetoka moyoni mwake ?? embu usome ????


Kweli hata mimi nampongeza Diamond kwa kuweka his “ego down” na kuonyesha upendo kwa mwanamuziki ambaye yeye mwenyewe alisaidia makuzi yake wakati yupo WCB! Nikitendo kizuri sana na chakufurahisha, lakini nimeshindwa ku-ignore the odds! Au wengine wanaweza sema the ‘hidden agenda’ au ‘the motive behind’!

Kama utakua ulisoma post yangu nilio andika mwanzoni mwa wiki hii inayo isha yenye kichwa cha habari kisemacho “Wema Sepetu ni mwanamke dhahifu sana” basi utakua ulisoma kile kipengele ambacho nilisema Diamond anapenda sana ‘attention’ na hiyo ilikua moja ya sababu hakuweza kumualika Wema Sepetu kwenye sherehe za miaka 10 ya muziki wake. Sasa basi, tumia maneno yangu hayo kutafakari alichofanya Diamond siku ya leo!

Yes, Diamond amefanya vizuri kuandika juu ya kum-support Harmonize! Lakini ilikua lazima afanye leo hii ambapo Harmonize amepamba kurasa za magazeti na social media?! Absolutely Not! Again, kama ilivyokuwa kwa Wema Sepetu asingependa kuona anapata attention zaidi yake basi ndivyo ilivyokuwa kwa Harmonize leo! Diamond baada ya kuona it’s all about Harmonize akaona njia pekee ya kuivunja nguvu hii ya attention anayopewa Harmonize ni kufanya kitendo ambacho kitagusa hisia ya kila mtu na kuelekeza attention yote kwake katika njia iliyo salama bila watu kugundua his agenda! The only way to steal Harmonize’s moment was to take his ego down! And yes, he won! Nilikwambieni Diamond ni manipulator and narcissist, mtu mwenye hulka kama hizi ni wakuogopa sana kwasababu yupo teyari kufanya kitu chochote kile ili abaki kuwa on top!

Kama kweli Diamond angekua muungwana, na kweli nia yake ilikua ni njema basi angesubiri hii momentum iwe all about Harmonize! Angesubiri ipite angala hata kwa siku moja halafu akaonyesha ukarimu wake! Lakini kwasababu hilo alikua lengo lake ndio maana hakuweza kuvumilia! Na hii naona ni style ya Management yake! Mnakumbuka walivyo fanya kwenye ufunguzi wa EP ya Tanasha?! Walikua wanajua kabisa Diamond hato kaa kwenye ile event lakini wakawa wanacheza na hisia za Tanasha bila yeye kujua na watu kufikiria kama kuna kitu nyuma ya pazia! Yaliyotokea wote mnayajua, wakatengeneza tukio la “dharura” na kulitangaza dakika za mwisho kabisa akijua watu wameweka macho yao wakisubiria kumuona Diamond na timu yake inaingia ukumbini! Hii yote ilikua ni kuvunja nguvu ya attention kwa tukio la Tanasha na kuhamia kwake! Hii ni typical behavior ya mtu anayependa ku control watu kama property yake binafsi! Hii nikuonyesha kua I’m still in control of you and everything!

Anafanya hivi kupata attention na trust kwenye macho ya jamii (haswa kwa watu wasiopenda kufanya tafakari ya kina) wakati anajua kabisa kitendo hicho kitamkwanza au muumiza hisia za muhusika! Yani hapo huwenda Harmonize anasema seriously bro?! This was my moment why steal it from me?! Kweli kabisa Harmonize anaweza hasiseme hadharani jinsi Diamond alivyo mkwaza na kitendo hicho lakini nina huwakika kwa wale watu wake wakaribu anao waamini lazima atakua anasema hata wao watakua wameumizwa sana! Harmonize nakushauri be a bigger person! Usimuonyeshe kua umechukia, wewe mshukuru tu halafu endelea na maisha yako! Kwasababu usipo sema neno la kumshukuru utakua unampa more attention na kuharibu image yako mbele za watu! Huna haja ya kuandika kwenye social medias, mtumie private msg. Na watu wakikuuliza sema nimeshukuru basi! Waswahili wanasema “funika kombe mwanaharamu apite”!

Nawashangaa sana watu wanaosema eti hii inaonyesha jinsi Diamond alivyo komaa?! ?? You people must be out of your mind! Diamond, he is a very insecure person! Ndio maana hawezi ku consider hisia za mtu mwingine! Diamond his self esteem ni sawa na ZERO!! Ndio maana “kiki” is the only way for him to boost his esteem!! Mtu asiyejiamini ndio huwa saa zote yupo kwenye mood ya mashindano yasio na tija, wabongo wanasema “anapenda ligi”. Mimi katika masomo yangu ya Ethics kuna somo nilisoma linaitwa “Human being behavior” hivyo najua mtu mwenye kujiamini anafananaje! Diamond ni entertainer mzuri sana lakini ni manipulator na narcissist, mwenye very-very low self esteem!.

Anyway, mie yangu ni hayo tu! Nawatakieni wote mafanikio mema na wazidi kuipeperusha bendera yetu vizuri! Na hongera sana Harmonize kwa event nzuri.

Housegirl kaalikwa ubalozi wa Marekani!

Tukiwa bado tunasherekea mwezi wa Superwomen duniani, basi siku ya juzi nikakutana na post ya Superwoman Joyce Kiria kama isomavyo ????

Reposted from @joycekiriasuperwoman Basi leo nilipata Fursa ya kualikwa na Ubalozi wa Marekeni kwenda kushea Safari yangu ya maisha katika kuendeleza Sherehe za Siku ya Wanawake Duniani 2020..Nilikuwa na Masupa Wuman wenzangu hawa hapa, Mercy Kitomari mwenye IceCream zake mjini, MD wa Lake Fm Noreen, Neema Md wa Penuel Investment, ..Aisee Nimegundua safari yangu ya maisha inasisimua na inahamasisha sana kupambana bila kuchoma, safari yangu ni nguvu ya Mwanamke hasa binti ambae anaanza kutafuta maisha…. nitaisimulia tena na tena coz I am a Super Woman ???? Stay tuned ??? Nitagie hawa masupa woman ???..Asante sana Ubalozi wa Marekani ??? – #regrann

Joyce Kiria akiwa na Superwomen wenzake walio alikwa ubalozi wa Marekani, Tanzania

Kwanza kabisa nianze kwa kusema hongera sana Joyce Kiria kwa mualiko huu! Kama nilivyo sema kwenye kurasa yako kuwa “what a milestone”! Unastahili!

Pili, naomba Watanzania mjifunze kutoka kwa wenzenu ambao wametoka katika nchi zilizo endelea. Mnaona jinsi gani wanavyo heshimu wapambanaji wa aina zote bila kujali elimu zao! Sidhani kama hizi nchi zingeendela kwa kubagua mtu au kitu chochote kile ambacho kina uhai, ndio maana huku kuna mifumo ya kusaidia na kuelimisha hata watu wenye utindio wa ubongo (matahaira), huku kuna haki za wanyama hadi Paka! Ndio maana wazungu waligundua Kia iki wapige hatua na kuendelea kuwa na nguvu ya kutawala dunia lazima ubaguzi na biashara za watumwa zikome! Maana walijua hatoweza kuendelea kwa kubagua fungu la watu fulani ambao wako ndani ya ardhi yao!

Mara nyingi unakuta baadhi ya Watanzania wanapenda kuona mtu ambaye ana “Masters” au “PhD” au anayejua kuongea Kingereza ndio mwenye akili ya kufanya vitu vizuri na vikubwa ambavyo watamuangalia kama “Role model”! Yani wanaona mtu aliye fanikiwa kwakupitia “structured” system basi huyo ndio anatakiwa kuwa role model na inspiration person wao! Watu kama akina Joyce Kiria ambao wamepata elimu na kupambania ndoto zao katika mifumo isiyokua rasmi wao wanakua hawana maana mbele ya hawa watu wanaojiita “wasomi”! Hata serikali yetu haiwatambu na kuwapa uzito watu wenye history ya maisha kama ya Joyce Kiria. Yani ni mentality fulani ya kuhuzunisha sana. Embu ona Kim Kardashian West anavyothaminiwa hapa Marekani, anauwezo wa kuweka appointment na kuonana na Rais kuongea juu ya maswala muhimu yanayohusu nchi yao. Everyone has something to offer, we need to learn to respect one another!

Wakiambiwa leo hii watoke hadharani watu wangapi ambao wanajiita “wasomi” nawamuangalia Joyce Kiria kama “Role model” wao?! Sidhani kama kuna hata mmoja atajitokeza! Siyo kwamba hawamjui au hawatizami kipindi chake hapana! Nikwasababu tu nakwenda shule kwenye mpangilio uliopangwa na serikali (jamii), mafanikio yake hayakutokana na ‘elimu’ hivyo wanamuona kwamba ni mtu fulani asiye na thamani ya (she is beneath) kua miongoni mwao! Hapo ndipo utasikia aah! Mie namuda wa kumuangalia housegirl? ?? nahivi sio member wa Chadema basi ndio tobaaa ?? Wakati ukweli ndani ya mioyo yao wanatamani wangekua na courage kama ya Joyce! Kwanza kumbuka huyu sasa watu wanasema “ALIKUWA Housegirl” keynote hapao ni ALIKUWA, she no longer exist in that title! hiyo ni history tu sasa! It defines where she came from but not her destiny! Haya housegirl huyo ndani ya American Embassy tena kwa mualiko maalum! #Respect people’s hustles! Kama ingekua Mungu anaangalia history ya mambo ya watu basi tusingekua na BiBle! Maana vitabu vingi ndani ya Bible vimeandikwa na watu ambao walikua wadhambi kweli kweli!

Joyce Kiria

Mimi Joyce ni mmoja ya watu wanao ni inspire, kwakweli ni mwanamke shujaa! Japo siwezi muita “role model” wangu, kwani binafsi huwa nasema na huu ni mtazamo wangu mimi Alpha; Katika dunia hii sina mtu yoyote yule ninaye muita “role model” wangu zaidi ya Yesu Kristo! Nina watu wengi wana ni inspire katika mambo mbali mbali na wakwanza kabisa ni wazazi wangu! I never call anybody in this planet my “role model”, kwani huyo ni mtu unayetamani kua kama yeye, nami kama kuna mtu natamani nifanane kama yeye basi si mwingine bali Yesu mwana wa Mungu! I want to be like Jesus!

Nilichogundua Watanzania wengi wenye elimu haswa hawa wakizazi hichi cha kwetu wapo very ignorance na wanachuki sana na watu ambao wamefanikiwa bila kupitia mfumo rasmi ya elimu (structured education). Haswa hawa watoto walikua, kusoma, na kutanua maisha kwa kutumia kodi za wananchi! Utakuta wazazi au mzazi wao alikua Mbunge / waziri / au senior Government officer basi wakiona mtu kama Joyce ambaye baba yake hukuwahi kua hata katibu kata amefanikiwa basi roho zinawauma wanakua na chuki kibao ?? Sikiliza wewe msomi, wewe unakipaji kwasababu kuna mtu katumia muda wake kukujaza madini kichwani mwako! Ingekua hauna hiyo elimu uliyopata darasani huwenda ungekua ni Zero brain! Mtu kama Joyce amejaliwa kipaji na uwezo mdogo wa elimu ambacho kimemfikisha hapo alipo ambapo wewe mwenye elimu umeshindwa kufika! Embu fikiria kama Joyce akiamua kuongeza elimu kidogo tu, itakuaje?! Unafikiri kuna msomi yoyote atakaye mbabaisha! Respect people’s hustles siyo elimu! Hata Bill Gates hakumaliza shule itakuwa Housegirl! Elimu ya darasani ni nzuri sana na ni muhimu lakini elimu ya ubinadamu (UTU) ni muhimu zaidi!

Marehemu Ruge Mutahaba akielezea kwa uchungu jinsi wasomi wa Tanzania walivyo small-minded, they think so shallow! Na hili tatizo huwa linanishangaza sana! Anyway, R I. P Legend, tutakukumbuka daima!

Kila tatizo lina chanzo chake kama ilivyo kwa jambo jema. Viongozi ambao mnatizamwa kama kioo cha jamii mnatakiwa muanze kuonyesha mfano wa UTU wa kuthamini kila mtu bila kubagua uwezo wake wa kuelimisha! Huku kwa walio endelea, utakuta viongozi wa juu hata Rais anatembelea shule yenye watoto wenye utindio wa ubongo, ili akiwa anafanya maamuzi au kuongea awe anaongea kitu anacho kijua na sio kusimuliwa na mtu, ambapo utakuta hata huyo mtu aliyekwambia naye kasimuliwa tu! Senator anaopopeleka mswada wa kuomba kuongeza pesa za kuelimisha watoto ambao ni Autist, anakua teyari anaelimu tosha juu ya Autism na umewaona kwa macho yake kua Autist anaweza kufundishwa kwa level ya uwelewa waka na akafundishika kabisa na kuwa independent! #Tubadilike

Kwa mara nyingine tena hongera sana Joyce, safari ndio kwanza umeanza, nakutakia mema yote!

Wema ni mwanamke dhaifu sana!

Siku ya jana ilikua ni siku ya wanawake dunia kote, kama ilivyokua kwa wengine basi naye Diamond alipost picha kuonyesha wanawake ambao ni muhimu kwake kama picha inavyo onekana hapo juu ???? na ujumbe wake! Hii nitofauti sana na tabia ya Diamond ambayo kwa miaka mingi amekua akiweka picha ya mama yake au saa nyingine anaweka na za dada zake.

Hakuna ubaya wa mtu yoyote kupost picha ya ‘X’ au ya “Ma_eX” zako kama bado upo single na unauhusiano mzuri nao. Lakini kwa hii ya Diamond inakua tofauti kwani inazidi kuonyesha jinsi gani Diamond anatabia za Unyanyasaji wa hisia (emotional abuse) kwa wanawake! Inazidi kuonyesha kua Diamond ni manipulator na narcissistic! Ukitizama wanawake ambao Diamond amekuanao kwenye mahusiano iwe kwa mapenzi yao wawili au bahati mbaya lazima utagundua na kukubaliana na mimi kua wote walijikuta wana poteza muelekeo wa maisha yao kusahau wao ni akina nani na nini wanataka kua katika hii dunia (they lost focus of who they are, their dreams, and what is their main purpose of existence in this planet world)!

Kaa chini angalia vizuri, utagundua kua karibia wote wanakua wakifanya vitu ambavyo vinampa Diamond ‘kiki’ ya kuongelewa na ku-boost muziki wake huku wao wakizidi didimia na kupauka! Anawatumia kutengeneza pesa lakini hawapi pesa za kufanya vitu vya maendeleo! halafu wao wenyewe wanakua hawashtuki mpaka watu wanapoanza kuwaonea huruma then wanadangwa na ‘maigizo’ ya kununuliwa gari na nyumba fake! Mtu ambaye alikua anaakili zaidi ya Diamond na alikua na uwezo wa kumshawishi Diamond kufanya vitu kwa maendeleo yake huku akijua kua 100% atanufaika na hayo maamuzi ni Zari the Bosslady peke yake na ndio maana familia haikumpenda. Na hii chuki ilianza baada ya kuweza kumshawishi Diamond anunue nyumba South Africa baada ya kuzaa naye Tiffah! Sidhani hata Tanasha kama ameondoka nalile gari la ‘maigizo’ ambalo alinunuliwa wakati wa birthday yake! Someone can prove me wrong, lakini naamini kwa asilimia zote limebaki Dar na sidhani kama lilikua kwa jina lake yeye Tanasha.

Kwanini nimesema Wema ni mwanamke dhaifu sana; wewe angalia katika huu ujumbe hakuna hata mwanamke moja ambaye ni Ex wa Diamond “kaushabikia” wala kujibu! Hila bidada hapa tobaaa! Embu soma comment yake hapo juu ???? Wema ngoja nikuulize, hivi kwalipi jema ambalo Diamond amekutendea mpaka awe na “special place” in your heart just for him?! Wanawake wengine wanajaribu kusahau hata majina ya “babydaddy” zao itakua Diamond?!

Huyu si ndio alikutumia wakati ukiwa upo juu, alipo ona thamani yako imeshuka akaenda zake? Kama hakukujali wakati ule upo mbichi leo hii umejizeekea kama akina Alpha hapa ndio atakuthamini?! Huyu Diamond juzi kati sialifanya sherehe ya miaka kumi tangu kuanza muziki, akawashukuru watu wote isipokuwa wewe! Wote walialikwa lakini wewe ukaachwa kama paka yatima! Sasa huyu mtu unawezaje ku reserve a special place in your heart just for him?!! Diamond anapenda attention na alifahamu fika kua kwenye hiyo sherehe angekuleta wewe attention yote ingehamia kwako, na hilo lisingewafurahisha ndio maana hukualikwa! Sasa inakuja issue ya Tanasha, Diamond alikua anajua hana mpango wowote na Tanasha ila hakujua kama Tanasha anaweza fanya maamuzi haraka hivyo imekuja kama surprise. Alijua angemchezea kama wewe! (Alisahau Tanasha ana damu ya Kijaluo, we are very intelligent! Tunajua kusoma alama za nyakati ????) Sasa anataka kukutumia wewe kama ‘scapegoat’ kumuumiza Tanasha na kupata attention zaidi.

Wema, labda nikuulize kwanini unakubali kutumika kuumiza mwanamke mwingi?! Are you that insecure and miserable?! Kwasababu Only weak women ndio wana hiyo eager and energy ya kuumiza mwanamke mwenzio. Mwanamke anaye jiamini kamwe hawezi kukubali upuuzi kama huo! Mwanamke anaye jiamini kamwe huwezi mkuta anafanya vitu petty ili mradi apate attention! Mtu yoyote ambaye ana furaha yakweli toka moyoni kamwe hana muda wala nguvu ya kukera wengine.

Juzi kati nilikuona upo kwenye event ya Idriss Sultan nauliulizwa kama utakuja kufanya nae kazi ukasema ‘ndio’! sasa kwa mtaji huu unafikiri Idriss atataka kuinvest his money on you?! Who wants to take that “liability” girl?! Na hapa inawezekana hata Diamond amesikia dalili za Idriss kutaka kukunyanyua tena; hivyo katumia akili ndogo tu kukuzibia fursa! Kweli marehemu Mugabe alikuwa sahihi aliposema “If you a woman with beauty and no brains it’s your private part suffers most”!!

Mimi nafikiri unatatizo fulani psychologically, unahitaji msaada wa wataalamu! Na hakuna ubaya wowote kuomba msaada wa wataalamu kwani kila mtu anamatatizo yake na tunawaona hao wataalamu wanatusaidi. Kitu kikubwa na chakwanza kabisa ni wewe mwenyewe ukubali kua kweli ninatatizo, na wewe mwenyewe ukubali kua unahitaji msaada wa wataalamu wa Psychology hapo ndipo utakua umeamua kweli. Lakini bila kufanya hivyo utashangaa utakavyo zidi kuchezewa na hawa wanaume!

Diamond is an emotional and energy sucker person. Wabongo huwa wanapenda kuwaita “wanyonya damu”! Mtu kama Diamond ambaye ana tabia za kuweza manipulate hisia za watu na ni narcissist basi anakua na uweze wa ku drain your brain and your emotions mpaka unakuwa highly depressed, hapo ndipo atakupelekesha kama “msukule” vile. Kuwa makini sana na watu kama hawa, bila Mungu huwezi mshinda! Diamond akija kuoa ataoa for ‘cover-up’ lakini huyo mwanamke atakua anaishi kwenye ndoa yeye peke yake (married but no different with single women out there)! Yani anaweza akanunuliwa gari zuri, mafuta full tank 24 / 7 lakini harusiwi kwenda popote bila ruhusa ya Diamond. Kila kitu atakua anafanya just to shut people’s mouth na sio kwa mapenzi.

Anyway, hayo ndio yangu sina la zaidi. Nakutakia mafanikio mema!

Kheri ya siku ya wanawake kwa wanawake wote ulimwenguni!

Alpha (Blogger) pamoja na mama yake mzazi
Mama Samia Suluhu, first female Vice President in Tanzania, an icon of women in leadership
Mama Janeth Magufuli, First Lady wa Tanzania awamu ya tano!
Veronica Sarungi, Mathematics genius at The Aga Khan University
Shilole, mama wa Shishi-food, Actress, Singer,
Jacqueline Mengi, Mwenyekiti wa Dr Ntuyabaliwe Foundation , owner of Amorrete furniture
Faiza Ally, mmachinga wa kishua
Jokate Mwegelo, Kisarawe District Commissioner, phenomenal woman behind Tokomeza Zero Kisarawe
Zarina Hassan, The one and only one East Africa Bosslady, owner of Brooklyn City Collage
Phenomenal women behind Women Matters talk show
Modester Opiyo (PhD), Lawyer, Judge of High court of Tanzania
Zamaradi Mketema, owner of Zamaradi TV, the woman behind Wonder woman event
Emelda Mwamanga, the mastermind behind the Bang! Magazine
Dinna Marious, Radio Personality, the ‘engine’ behind Women Kitchen Party Gala
Joyce Kiria, powerful phenominal woman behind Wanawake Live talk show
Hoyce Temu, TV presenter, amazing woman behind Mimi na Tanzania show

Kheri ya siku ya wanawake kwenu nyote na wanawake wengine wote duniani! Mwanamke ni msingi na nguzo ya kila jambo! Mungu azidi kutubariki kwa mema yote tutendayo!

Happy Women’s day!

Happy 67th birthday Sir O.O Igogo

Sir O.O Igogo

“YESTERDAY MY 66th YEAR ENDED & TODAY MY 67th YEAR BEGINNING ???? My days are counting down towards the Eve day, I am as healthy as a new born, blessed with wonderfull family members, a work that I enjoy doing every day, a business that affords us the daily needs and beyond, true friends who have been holding my hands for years, a peacefull mind ever that accepts failure as a challange to overcome, a big heart that never look down on others, a forgiveness habit that one can not doubt, a charitable giving hands that meets with the needy’s ever since. Allah have done wonders to me and through me to others. I father numerous children, born to me, adopted, dependants, able and disabled ones. I am blessed with amazing grand Childrens. God made my dreams to become real to establish business ventures which employs over seven hundred individuals on parmanent basis!! I vow to work for Allah Silently, in the back ground of believers, as a symbol of his kindness the population on earth, through my deeds, humbleness, humanly honest, hard work manship and a true God fearing man all my life time on earth. I thank all of you who have wished me a happy birth day and for the gifts I have recieved from some of you. Asanteni sana, Erokamano uru, Thank you so much. Otieno Olung’a Igogo. 07/03/2020.”

Birthday wishes from daughter Magreth Igogo-Massawe
Birthday wishes from daughter Janeth Igogo-Nyagilo
Daughter Blessing Gwethrhoda Igogo (given middle name after our paternal grandmother Rhoda) enjoying 67th birthday of her son ?
Birthday wishes from son William Ernest Mjee Oucho

On behalf of family members, friends, employees, and business partners I say Happy 67th birthday Sir O.O Igogo. Many more blessings to you! ?❤

Ukijua umekosea basi huna budi kuomba msamaha!

Katika vitu ambavyo ni tabia yangu hata wale ambao wananifahamu vizuri na niwatu wa kuongea ukweli basi wanaweza kushuhudia hili. Mimi ni mtu ambaye nikijua nimekosea au hata kuumiza hisia za mtu mwingine basi huwa sioni haibu kuomba msamaha, kwani huo ndio ubinadamu! Kama mtu alinikwanza kiasi cha kunifanya niongee vitu ambavyo katika hali ya kawaida siwezi kuongea basi nitamwambia naomba msamaha kwa lugha niliyo tumia lakini kwamwe sito omba msamaha kwa REACTION yangu! Kwasababu REACTION yangu ipo au ilikua sahihi japo lugha yangu haikuwa sahihi! Sikumbuki kama nilisha wahi muomba mtu msamaha kwa REACTION yangu kwani mie huwa sina hulka ya kumchokoza mtu au kufanya jambo ili tu nimkwaze fulani! Pettiness is not in my vocabulary! Because I strongly believe pettiness is a ground for evil! Mtu yoyote ambaye anaweza kufanya vitu fulani vyakipumbavu kwa makusudi mimi naamini mtu huyo ana viashilia vya uchawi na anaweza hata kuua mtu!

Kitakacho nidisturb sana kwenye hii kesi ama ambacho kina nidisturb kupita vitu vyote kwenye hii kesi ni jinsi jina la mume wangu linavyo kashifiiwa“- Jacqueline Mengi

Baada ya kusikiliza haya mahojiano ya Jacqueline na Millard Ayo naomba nikubali kua nilikosea sana kutoa maoni yangu bila kusikia upande wa Jacqueline! Nilisikia upande mmoja wa hii issue na kuongea na Jacqueline kwa hisia zote na kusahau kabisa kuwa siku zote kuna sehemu tatu ya jambo lolote lisemwalo! Hivyo ninakila sababu ya kusema Jacky naomba unisamehe nimekukosea sana! I’m a woman enough to admit I was wrong thus I am sincerely apologizing for the language used and negative image that I imposed on you! Naomba ieleweke siombi msamaha kwa REACTION yangu juu ya hii issue kwani 100% I stand by Dr. Reginald Mengi’s legacy! Msamaha wangu ni kwa jinsi nilikua harsh / so hard kwa Jacqueline!

Nilichogundua hapa watu tunaweza hukumu mtu asiye na hatia kabisa kwasababu ya watu waongo ambao wengine wanaaaminika katika jamii kua ni watu wema! Mimi nachukukia sana mtu muongo na mnafiki! Yani bora niishi na mchawi au mwizi huku nikijua kabisa huyu ni mchawi na yule ni mwizi hivyo natafuta njia salama ya kuishi nao! Lakini mtu muongo na mnafiki ni mtu mbaya sana, ni wakuogopwa zaidi ya ukoma! Hawa ndio wale wanaweza kukuua halafu anakuja msibani kwako kutoa hushuhuda jinsi gani mlikua mmeshibana!

Nimeongelea uongo na unafiki kwasababu angalia hawa watu walivyo kua wakidanganya watu kua Jackie anahusika na kifo cha mzee Mengi! Ndio maana kila nikitaka kuamni hisia zangu zinakataa kabisaaa! Hivyo hizi habari za kua Jacky ameweka pingamizi mahakamani nikasema basi huyu Jacky ni mkorofi anataka kuharibu Legacy ya Dr Mengi! Kumbe mtoto wa watu anapigania kuendeleza legacy ya mumewe! Dah! I’m deeply sorry Jacky. Unafiki huu, kama huyu mdogo mtu alikua na shida na kaka yake mbona hakusema wakati akiwa hai? Ameishi na marehemu miaka tisa (9 yrs) baada ya kumuoa Jacky mbona hakusema kitu?! na kwenye harusi alikuwepo?!! Inamaana wakati ule alitumia nafasi ile kumuumiza mtalaka wa marehemu (mama Mercy Mengi) kwa faida zake binafsi na sasa anatumia kifo cha kaka yake kumuumiza Jacky na watoto wa marehemu kwa manufaa yake!

Huyu baba mdogo inaelekea hata marehemu alishamuona ni “kasheshe” hivyo machale yakamcheza akataka azikwe kwenye mji wake na sio makaburi ya familia?! Kama kweli yanayosemwa na Jacky ni ya kweli basi huyu baba mdogo ndio mvuruga familia! Na kama Regina na Abdiel watamsikiliza huyu baba mdogo wakifikiria wako salama basi wanajidanganya sana! Akimalizana na Jacky atawaingilia wao atahakikisha Regina na Abdiel wanagombana huku yeye akijifanya ndio mpatanishi! Hii dhambi mnayo itenda haita waacha salama! Naona anahasira hakuandikwa kwenye Wosia, sasa sijui anafikiria kua naye ni mtoto wa marehemu?! Halafu, Regina na Abdiel how dare are you?? Mtu anaandika mambo ya kumdhihaki baba yenu halafu mnaungana naye? Eti mkidhani mnamkomoa Jacky? Si ndio mnaionyesha umma nyie ni watu wa namna gani!

Najaribu kutafakari baba yenu aliwatendea dhambi gani ambayo mnaona anastahili kukashifiwa wakati hawezi kujitetea?! Mnataka kutuambia vile vilio vya kujiinamisha mbele ya jeneza ilikua ni maigizo?! Regina mtoto wa kike muogope Mungu wewe! Hivi kumbe hautaki Legacy ya baba yenu iendele? Au kwasababu nyie hamna watoto hivyo mnafikiri mnamkomoa Jacky? Sorry, I may sound rude but I am only trying to understand what’s this “war over”?! Mbona huo WOSIA sounds right to me! Nyie mmechukua khamsini 50% na wale watoto wamepewa 50% na Jacky wala hausiki kwenye mali ambazo marehemu alichuma na mke wa kwanza? What’s this all about? We the people of Republic of Social Media we desperately want to know!! Mzee wetu alikua mtu wa Social Media he got huge family kwenye ardhi na huku mawinguni (mitandaoni) hivyo mtueleweshe huu ugomvi wa nini! Nyie wenyewe mmesha broke “family code” kwa kwenda mahakamani sasa tunataka kusikia sauti zenu mtuambie kama Jacky anadanganya au la!!

Chakushangaza Jacky hakuingilia ndoa wala kuvunja ndoa ya mama yetu Mercy Mengi kama tulivyo aminishwa hapo mwazo! Hana nawala hataki mali yoyote ambayo ilichumwa kabla yeye hajaolewa! Sasa hizi hasira zote zanini? Kwanini mnamuonea huyu dada?! Angalia anavyo ongea kwa busara na upendo kwenye hiyo interview, anawaita “hawa wote wanangu”, “watoto wetu wakubwa” mpaka marehemu mama yenu anamuita mama?!! Jamani, if that is not LOVE then what is it!! Hivi mnajua watu wangapi wanatamani wangekua na step mama mwenye roho kama ya Jacky!! Hivi mnajua kuna step mother wangapi ambao wako busy kubomoa legacy za waume zao tena wakiwa bado hai?! Seriously, you guys had the best of best and yet naona mna ZERO appreciation! Wee Abdiel, how can you let this happen? Hivi mnaachaje baba mdogo anavuruga legacy ya baba yenu namna hii?! Nasema tena hii dhambi haita waacha salama!

Jacqueline Mengi akihojiwa na Millard Ayo!

Jacky sasa tumekupata na kukuelewa! Unakila haki na sababu ya kuongea, tena zidi kuongea ili kumbu kumbu ziwekwe! Kama unasema uongo basi wajitokeze na evidence wakanushe ulichosema! Na kwamtaji huu you deserve to sit on that throne because you have Dr Mengi’s interest in your heart! Kwanza hauja mdhulumu mtu! Nakama hawato kubali kutengua hizo kauli na maneno yao waliyo andika huko mahakamani basi kataa kupatanishwa nao kabisa! Nakuanzia sasa kitu chochote kikimkuta Jacky wao ndio watakua watuhumiwa namba moja! Halafu wataona nguvu ya familia ya mzee Mengi (The Republican of Social Media ??) kama itawaacha salama! Mimi nasema Dr Mengi’s Legacy Must Live On! Dr Mengi’s Legacy For Life!

Once again, I’m so sorry! Nitakuweka kwenye maombi yangu kuanzia sasa. ?❤❤

***Shukrani za dhati kwa Millard Ayo TV kwa interview nzuri sana***

“Acha Alama nzuri mioyoni mwa wale wanaostahili”***** Zamaradi Mketema

Reposted from @zamaradimketema Leo nilikutana na watu walikuwa wanajadili jambo japo katika hali ya masihara lakini nikagundua makosa makubwa ambayo huwa tunafanya sisi binaadamu

Zamaradi Mketema na binti yake Shubi Ruge Mutahaba

Watu wengi husema ukipendwa Ringa, mi nasema hapana, Ukipendwa THAMINI, na ikiwezekana mkomeshe kwa kumpenda zaidi, wenye mapenzi ya kweli ni wachache mno Duniani, Make Sure ukimpata kuwa KILEVI chake, mfanye awe ADDICTED na wewe, mzoeshe ama weka utaratibu ambao hata itokee mmekosana ashindwe kukaa siku moja mbili kakaza, sababu kuna kitu tu anakosa, kuna watu wanahisi pozi ndio Ujanja, Pozi ni ushamba!! Especially kwa mtu anaekupenda, kama wanavyosema Dawa ya Moto ni Moto kwenye mabaya basi hata mazuri ni hivyohivyo, mtu akikupenda mpende zaidi, haupotezi unawekeza, hata kesho akiwa mbali, kitakachomuumiza ni hiko, lakini kama wewe ni mtu wa headache kilasiku hakuna atachokumbuka

Beautiful Zamaradi Mketema

Na hii haiapply kwa mume/mke ama mpenzi peke yake, ila hata rafiki na watu wema tunaokutana nao, Acha Alama nzuri mioyoni mwa wale wanaostahili kiasi kesho na kesho kutwa hiyo ndio silaha yako pale mtakapokuwa mbalimbali, ukijiangalia una chochote ulichowekeza kwa wale wakupendao!!? Unahisi wewe ni kilevi chao ama headache!!? Kuna Alama umeshaweka ama ndio Upepo utakapopita umepita!? Tafakari halafu chukua hatua

Nimejisikia tu kuongea hiki, Muwe na Usiku Mwema!! – #regrann

Usiogope kuanza upya!

? Huo ni ujumbe wa Jacqueline Mengi siku ya leo!

Siku ya leo Jackie aliandika post mbili ya kwanza iliwakumbusha watu kua katika dunia hii ambayo unaweza ukawa kitu chochote kile basi chagua kua muungwana / mkarimu! “in a world you can be anything be kind”! Ni maneno machache lakini mazito sana! Sasa ujumbe wake wa pili ndio huo ? halo juu, ambo wenyewe unawasihi watu waaiogope kuanza upya kwani hiyo ni njia ya FURSA mpya kwao na kufanya kile kitu ambacho roho yako ilikua siku zote inatamani!

Nikweli kabisa, usiogope kuanza upya eti kwasababu ulishindwa mara ya kwanza au maamuzi ya mara ya kwanza hayakuzaa matokeo uliyo tarajia! Niliupenda ujumbe bila kuwa na swali lolote kichwani mpaka pale nilipo kutana na post ya Faraja Nyalandu Murugenzi wa ‘Shule Direct’ mke wa Mh. Lazaro Nyalandu. Yeye aliandika ujumbe huu ????

Mrs Faraja Kota Nyalandu

Reposted from @farajanyalandu May this new month remind you, you have all it takes to start and start again. That greatness awaits, that your little steps will lead you home. May you have eyes that see opportunities, a mind that seeks to build and hands that never destroy. May you overcome all that is holding you back. May you overcome you, if need be. May you find the peace to come back to the center of what truly matters. And find the Purpose that is above all. Happy New Month! – #regrann

Faraja ni kama alikua ametilia mkazo zaidi ujumbe wa Jacky! Naweza sema kama Jacky aliweka mbegu basi Faraja yeye akaweka mbolea na kumwagilia maji ili zao liote vizuri! Kwa kifupi Farajaja amesema tunapo anza huu mwezi mpya basi na uweze kukumbusha kuwa unacho kila kitu ambacho kinahitajika kuanza upya! Kwamba mambo makuu yanakungojea, hatua zako hizo ambazo ni ndogo ndogo zitakufikisha kwenye nchi ya ahadi! Basi na ukajaliwe macho yakuona FURSA mpya, fikra za kujenga na mikono ambayo kamwe haita bomoa! Na ukajaliwe ujasiri wa kushinda yale yote yanayo kukwamisha, na uishinde nafsi yako kama itahitajika kuishinda! Pia ukajaliwe amani ya kukuwezesha kutullia katika kile ambacho ni muhimu sana kwako na kuliko vyote!

Huo ujumbe wa Faraja Nyalandu ukaniwekea maswali kichwani mwangu! Je, Jacqueline Mengi anataka kuanza maisha upya?! Au hii ilitokea tu ujumbe zikagongana?! Wenye lugha zao wanasema “coincident”! Sina uhakika na maswali yote japo nimependa sana jumbe zote mbili kwani zina ujumbe mzuri sana wa kutia moyo!

Nachoweza kusema ni kua Jacky anaweza kufanya kitu chochote kile ambacho anatamani kufanya. Umri wake bado unamruhusu kufuta na kuanza upya! She’s too young kuvaa kofia ya “mjane”! Yes, mzee wetu kafariki lakini Jacky bado mbichi sana kukaa single! She needs a shoulder to lean on jamani! Anaweza omboleza mpaka pale atakapo jisikia yupo teyari kuanza familia mpya na mtu mwingine! Hilo halina ubaya kabisaaa! Ni baada ya muda gani; hiyo ni juu yake yeye kwani yeye ndio aliye vaa hivyo viatu anajua vinapo mbana! Ndio maana nikasema hawezi kukalia kiti cha mzee Mengi!

Jackie, wewe ukimpata Billionaire mwingine wewe tualike tu kwenye harusi sisi tutakuja bila shida ?? na picha zako mie nitapost ?? Au ukijipatia mzungu fulani wewe tupe tu mualiko tutakuja! You are very free, and don’t let people victimize you kuvaa kofia ya ujane sijui kwa miaka kumi?! Nope! This is your “prime time” use it correctly!

Kikubwa wewe unabiashara zako nyingi tu zisimamie my dear ili siku watoto wako waje kuwa proud na wewe. Those little Billionaires (the twins) wana haki zote kwenye kila kitu ambacho kina jina la marehemu baba yao! Huu ni mtihani kwa Regina na Abdiel tuone kama watawatunza wadogo zao au la! Hao watoto ni jukumu lao kuwatunza kwa kila kitu! Yes, wewe mama yao upo lakini kama wataamua kuvaa viatu vya baba yao basi hao watoto ni jukumu lao kwa asilimia 100%! Mpaka watakapofika miaka 18 basi wapewe haki zao zote! Wao ndio wataamua nini cha kufanya! Na wakumbuke kuwa hao watoto wamezaliwa baba yao akiwa Billionaire teyari, hivyo hayo maisha ndio walio zaliwa na kuyakuta na ndio maisha wanayo yajua, hivyo hiyo ndio level ya style ya maisha tunayotegemea kuona wakiishi! Sisi wapembeni tutakua tunatizama kama kweli wana kee-up the standard! Huu utakua muda muafaka wa public kuwajua vizuri Regina na Abdiel ni watu wa namna gani kwa kutizama jinsi watakavyo wajali wadogo zao!

Kwakumalizia nasema, ndio unaweza kuanza upya nasi washangiliaji tutakua hapa kukushangilia! Unakila kitu cha kuanzia na kila sababu ya kuanza upya! Huwezi kuwa mjane forever! You are too young for that!

“Wanaume wenzangu! To spare maneno tusiongee kila kitu. Kwa wake zetu” *** Harris Kapiga

Reposted from @harriskapiga Huu ni waraka kwa Wanaume! Walio kwenye ndoa! Wasio kwenye ndoa! Na walio na wachumba!

Familia ya Harris Kapiga katika picha

Si kila kitu cha kuonge na mkeo / mchumba wako, hasa mapungufu ya wazazi wako! Walezi wako, jamaa zako wakaribu ndugu zako, Boss wako! Kazini / kwenye biashara yako! Wanaume wengi huwa tunadhani tunanogesha penzi kumbe tunaharibu.

Unaanza mama yangu bana omba omba sana, una mwambia mkeo hapo au mchumba! Dada zangu bana waongeaji sana! Wana madeni kila kona. Boss wangu bana ananionea wivu anafanya fitina nifukuzwe kazi. Sisi bana, tumezaliwa kila mtu na baba yake! Mama aliachaga shule kakimbilia kwa bwana! Bi Mkubwa bana wanamsemaga mchawi! Kuongea kila Kitu hasa mapungufu ya wazazi na jamaa zako wakaribu unaharibu mahusiano kati ya mkeo na hao unaowasema vibaya kwake!

Lazima tukubaliane kila mtu anamapungufu , hata wewe unaeongea unayo yakwako! Baada ya kuongea nakudhani unanogesha Penzi! Kumbuka mwanamke kiukweli wale sio ndugu zake! Hana feelings nao kiviile kama wewe! Sababu ni wazazi wako, na umemjaza sumu mkeo / mchumba wako, anajiweka mbali sasa! Unageuka mwanaume unataka mke apeleke watoto kwa bibi yao! Akawasalimie na wewe ulimjaza masumu Bi Mkubwa mchawi! Bi Mkubwa ana mdomo; Bi Mkubwa ni mama yako unataka uonekane mwema, umpelekee wajukuu! Mke kagoma sababu ulimjaza masumu na mapungufu ya kwenu! Mgogoro unaanza, ooo mke jeuri, hapendi mama, haendi kwa mama! Kumbe wewe ndo ulikuwa mbaya ukamharibu (mazungumzo mabaya huharibu tabia njema)

Wanaume tumeumbwa na koromeo ina maana kuna vitu tuvihifadhi pale! Nieleweke hasa mapungufu ya jamaa zako, wazazi, boss wako na ndugu wakaribu!

1Petro 3;7…… Kadhalika ninyi waume kaeni na wake zenu kwa Akili. Kwa akili ni pamoja na kuchagua mambo yakuongea kuendeleza familia kwa Amani; Mwandishi ka endelea kusema Na kumpa mke Heshima; mtu unaemheshimu huezi mwambia kila kitu utachagua vya kuongea!

Wanaume wenzangu! To spare maneno tusiongee kila kitu. Kwa wake zetu! Vingine tunaharibu! Sasa pale umejiachia umemwambia mkeo sisi tumezaliwa kila mtu na baba yake!Halafu akakufuma na sms ya mapenz! Akakasirika ukasikia! Malaya kama mama yako! Aliewazaa kila mtu na baba yake! Usirushe ngumi! Uliongea kila kitu – #regrann

Ujumbe mzuri sana! Hii tabia ipo sana hata kwa wanawake! Unakuta mwanamke anaongelea vibaya sana ndugu zake tena watumbo moja akifikiri kwamba mwanaume atamuona yeye ni watofauti sana kumbe hajui anajichimbia kaburi lake mwenyewe! Mimi huwa naamini mtu ambaye anaongelea mtu katika njia ya kutaka kumfanya yule mwingine aonekane hana thamani au ni mtu wa ovyo mara nyingi hua kuna mapungufu mengi ndani yao hivyo wanajaribu kuondoa attention kutoka kwao kwa kuamini kwa njia hiyo watu hawato ona mapungufu yao na kutokujiamini kwao. (trying to diverge attention from their weaknesses / insecurities by pointing other people weaknesses and flaws). Hivyo hiyo ni njia yao ya kujihami! Ni guilty ya kutokujiamini ndio inawasumbua. Japo wengine ni mashetani na mapepo ndio yamewajaaa.

Mwenyekiti wa Dr. Ntuyabaliwe foundation asaidia kugawa vitabu mashuleni!

Mwenyekiti wa Mfuko wa Dr Ntuyabaliwe Mrs Jacqueline Mengi

Reposted from @j_n_mengi Yesterday I as the chairperson of @drntuyabaliwe_foundation had the pleasure of attending the launch of books for English Medium schools as well as Braille books for blind children organized by Tanzania Institute of Education. It’s a great step for the betterment of the education of our children and we @drntuyabaliwe_foundation congratulate Tanzania Institute for Education @taasisiyaelimu and our Government for this very significant achievement. – #regrann

Hongera sana Jacqueline kwa kufanya kazi za jamii! Sasa hapa ndio mahala pako pa.

kujinadi na kuonyesha “woman power”! This is your “THRONE” babe! Go girl and make your family proud! Kule kwa IPP na Bonite na mazaga zaga yao yote waachie wenyewe. Wewe kua sehemu yao lakini let them be the front runners! Kuwa sehemu yao kwani ni part of the Mengis’ but at the same time you are not the Mengis’ ?? (nafikiri unanipata my dear). Wewe uliolewa na mzee wetu Dr Mengi na una watoto ambao ni damu ya mzee Mengi lakini kutokana na mazingira ya mambo usijiweke mbele.

Kazi nzuri na hongera sana!

NIMECHOKA, SITAKUBALI KUENDELEA KUONA WANANGU WAKISONONEKA NA SITAKAA KIMYA.” *** JACQUELINE MENGI-2

Jacqueline mpendwa, naomba uwelewe kua hakuna anayepinga maamuzi yako ya kuolewa na marehemu mzee Mengi, nawala hakuna anaeweza kuleta ubishi kwenye hilo kwani ni maamuzi ambayo marehemu aliyaafiki na kuweka wazi akiwa katika utashi wa akili zake timamu! Hilo halina mjadala! Naamini hata watoto wa marehemu walikubaliana na hiyo hali, ndio maana kuna siku ulituwekea video mkiwa Hyatt Regency Kilimanjaro hotel mkila brunch wote kama family! Hata mimi nilikua shabiki mkubwa wa “the Billionaire family” ? Honestly, I miss those moments nikiwapost humu!

Late Dr Reginald Mengi

Sasa basi, tatizo ninalo liona hapa nikitendo cha wewe kutaka to sit on the “throne” representing the “face” of Mengi’s family tena kwa dharau na kiburi! Woman! You must have lost your mind!! Who made you the ‘Queen of the castle’ to begin with?! Kwakweli, hapo UMEKOSEA SANA TENA SANA!! Hivi unajua hakuna familia iliyo simama bila MAMA!! nafahamu ili mji wa mtu fulani usimame na kuhesabiwa lazima kuna mwanamke jembe fulani nyuma yake??! Wewe umekuta mji huo umesimama, kuna maziwa na nasali, dhahabu na lulu; hivi unafikiri viliokotwa tu bara barani?! Unafikiri vilipatikana kwa kupaka makeup masaa 24 na kuweka kucha bandia?! Kuna watu waliosota kwenye huo mji ili kuakikisha hiyo empire inasimama! Kuna watu walifunga na kuomba dua kwa Mungu ili huo mji usimame! Kuna walio lia kwa changamoto mbali mbali walizopitia! Hivyo wewe kushupaza shingo lako na kutaka kukaa kwenye ‘throne’ ni uwendawazimu uliopitiliza!!

Haiwezekani, narudia kusema tena haiwezekani kuongelea Legacy ya mzee Mengi bila kumtamka mke wake mkubwa mama Mercy Mengi! Kama kweli ulimpenda marehemu kwa dhati basi lazima uheshimu jina la huyu mama! Tunafahamu kwasasa hayupo, lakini ana wawakilishi wake ambao ni Regina na Abdiel! You have obligation to respect watoto wa mke mkubwa kwani sio tu wanamuwakilisha mama yao bali na baba yao pia. Hao watoto ni chimbuko na kiini cha Dr. Mengi’s legacy! Waheshimu!

Makaburi ya ukoo wa marehemu mzee Mengi

Jacqueline, haiwezekani kamwe ukaongelea legacy ya mzee Mengi bila kutaja ndugu zake watumbo moja! Haiwezekani! Hawa ndungu ni watu ambao marehemu aliwapenda, aliwajali, na kuwaheshimu mpaka mauti ilipo mfika! Sisi tulio bahatika kusoma kitabu chake tumeona jinsi gani marehemu alivyo ongelea mchango wa ndugu zake katika mafanikio yake toka akiwa shule ya msingi! Yeye hakuwatenga wala kuwadharau sasa inakuaje wewe unaenda kinyume?

Post ya Jacqueline leo

Mmh! Sasa wewe ulitegemea nini ulipo iwekea pingamizi familia?! Haya makaburi yapo ndani ya family property hivyo wanahaki ya kukufukuza! Hata mimi ningekufukuza! Jacqueline, ngoja nikwambie, at this point you have proven to be nothing but one of the 21st century classic “homewreckers”!! And as usual Homewreckers wanatumia watoto kama kigezo cha uhalifu wao! Hawana uchungu na kuvuruga familia za watu kwani they care less for the people who “paved” the way! Nia yao huwa ni moja tu; kuchuma na kuvuruga familia za watu!! Homewrecker huwa haonagi shida kuvunja legacy ya mtu kwani hawajui vilianzaje na hata wakijua hawajali ili mradi wamepata wanachotaka! Ndio maana ni rahisi sana kwako wewe Jacqueline kuongelea huu mtafaruku kwenye mitandao kuliko watoto wa marehemu!

Nilikua nakupenda nabado nakupenda ila kwa hili?! Gal! You are deadly wrong! Halafu, acha kabisa kutumia watoto kuichafua hii family! Hao watoto wanauwezo wa kwenda kwao na kuona hayo makaburi muda wowote ule, usitumie watoto kwa hila zako! Hizi “bongo movie” zako hazita kusaidia kabisa! Usifikiri watu hawaoni mambo unayofanya! People are paying attention and they are puzzled!!

Ushauri wangu kwako, tafuta upatanisho na watoto wa marehemu pamoja na ndugu zake wa damu! Hauwezi kukalia kiti cha mzee Mengi eti unawakilisha familia ya Mengi na ukoo wake wakati ulikuta kuna mji umesimama! Hiyo itakuwa dharau kubwa sana na kuwavunjia heshima si tu watoto wa marehemu bali ukoo wote! Learn to humble yourself!

The Mengis’

“Nimechoka, sitakubali kuendelea kuona wanangu wakisononeka na sitakaa kimya.” *** Jacqueline Mengi

Naam! Hayo ni maneno yake mwenyewe Jacqueline Mengi aliyekua mke wa marehemu Billionaire Dr Reginald Mengi. Ujumbe huo aliandika kupitia account yake ya Tweeter na pia ku-share kwenye Insta-story yake! Kuna wengi wamemsapoti na kuhuzunika naye kitu ambacho kinaonekana kimemfariji Jacqueline hata kuandika tena ujumbe mwingine wa kushukuru leo hii kwa kutumia Insta-story yake (soma ????),

Ujumbe wa Jacqueline leo hii kwa Insta-story yake

leo hakupeleka Tweeter ?? najiuliza kwanini huu ujumbe wa shukrani haupo Tweeter leo? ?? nafikiri jibu lako halitakua na tofauti sana na lakwangu! ??

Jacqueline mpendwa, unajua kuishi na Wamarekani kumenifundisha mambo mengi sana na moja ya vitu ambacho nimejifunza na nimeamua kukitumia katika maisha yangu ya kila siku ni kua ‘kama kweli unampenda mtu kwa dhati basi lazima utamwambia ukweli mchungu’! Umwambii mtu ukweli ili kumnyanyapaa la asha! Ni ili umfungue macho na akili aone vitu kwa mapana na katika uhalisia! Wenye lugha zao wanasema “help them to see outside the box”!

Sasa mpendwa Jacqueline, mama wawili, Ooh! How I miss calling you muke ya Billionaire ?? naomba nikwambie ukweli but you have to understand it comes from a very place of nothing but PURE LOVE! Najua naweza nikawa nalugha isiyo kupendeza, unisamehe tu kwani somehow I’m taking it very personal kwa kuvaa viatu vya watoto wa marehemu Dr. Mengi na ndugu zake! Na pia hii mikasa inatokea kwenye familia nyingi za Kiafrika hivyo kwa upande mmoja au mwingine inanigusa!

Unasema umenyamaza kimya kwa mengi sana?! Ni mengi yapi hayo? Maana huku social media sisi ambao tunakufatilia hatujawahi kuona ukilalamika kuhusu jambo lolote juu ya watoto wa marehemu wala ndugu zake, hivyo kuandika ujumbe kama huu bila kuelezea japo kwa kifupi tu ili watu wajue kama wanakusapoti wanakusapoti kwa misingi hipi?! Unasema umechoka, hutokubali na hutokaa kimya?! ?? mmh! Hivi watoto wa marehemu mzee Mengi nao wakisema hayo maneno na wakaamua kuvunja ukimya wao hivi itakuaje??! Hivi utaweka sura yako wapi?!

Marehemu Dr Mengi akiwa na watoto wake Regina na Abdiel wakati wa msiba wa mke wake marehemu Mercy Mengi!

Labda nikuulize, hivi unajua watoto wa marehemu wamenyamaza kimya kwa muda gani sasa?! Toka wazazi wao walipo farakana nakutenga mpaka mauti ilipo watenganisha kama ahadi ya kiapo walichokula mbele za Mungu, na hatimaye sasa ni yatima, hao watoto umesha sikia wanaongea wapi kwenye hizi media?! Unafikiri wanamangapi mioyoni mwao ambayo yanawaumiza kimwili, kiroho, kiakili hata kisaikolojia lakini wamenyamaza nayo wanalia nayo huko ndani ya nyumba zao wakati taa zikiwa zimezimwa, madirisha yamefungwa, na pazia likiwa limeshushwa?! Na hayo yote wanavumilia kwasababu wanalinda heshima ya familia yao pamoja na Legacy ya baba yao ambayo wao wenyewe walimsaidia baba yao kuijenga!!

Marehemu Dr Mengi namke wake wa kwanza marehemu Mercy Mengi

Hivi, unajua Regina na Abdiel wanamaumivu kiasi gani ndani ya mioyo yao, kutoka kuzaliwa na kukua katika familia walioaminishwa kua inafuraha na amani mpaka wazazi kutengana, mara baba kuishi “single life” na hatimaye kuoa msichana ambaye ana umri sawa na “Mjukuu” wake?! Unataka kweli nao waseme wamechoka na ni muda sasa wa wao kuvunja ukimya?!! Jacqueline take that chip off your shoulder and learn to humble yourself!! Hao watoto wamenyamaza na mengi sana ndani ya mioyo yao, wanamaumivu makali sana only people with EXTRAORDINARY kind heart will understand maumivu yao! So, don’t play a victim card because it doesn’t give you any justice!!

***Itaendelea***

MAMA SALMA KIKWETE UMEKOSEA SANA! HIYO INAITWA INSTITUTIONALIZED DISCRIMINATION!-2

Hon. Jakaya Mrisho Kikwete and his daughters!

Mama yangu, ninacho jaribu kukwambia ni kwamba fungua macho yako utazame hii hoja yenu kwa macho mapana utaona jinsi gani imejaa ubaguzi na unyanyapaaji wa hali ya juu kwa mabinti wanao pata mimba wakiwa shuleni! Kama mmeamua kufukuza shule wanafunzi basi mfukuze wote wanaofanya ngono wakike na wakiume kwa ujumla wao na siyo kubagua wanaopata mimba tu! Hivi mama Salma, kweli unataka kusimama hapa na kuiambia dunia, mbele za Mungu kuwa huyu binti yako mwenye gauni jeusi bado ni bikira?! Au kwasababu hajapata mimba kwahiyo unamuona mtakatifu?!!

Kumbuka kabla ya kutunyooshea kidole sisi hakikisha kucha zako ni safi! Maana lazima tutazikagua!! Hizi sheria mnazoziweka bila kutafakari madhara yake katika jamii ipo siku damu zenu zitazilipa tu! Yawezekana leo hii haitamkuta binti yako lakini huenda kesho yakamkuta mjukuu wako! Oh! Nimekumbuka nyie ni “high profile” people, you do “high profile crimes” bila sisi walalahoi kujua, mama kumbuka Mungu anawaona!!Kumnyima mtoto yoyote haki ya ku-access education ni kinyume na haki za binadamu. Kwani kupata elimu ni haki ya msingi ya binadamu wote! Wanafunzi wanaopata mimba wanatakiwa waachwe waendelee na masomo yao kama kawaida bila kubaguliwa na mtu yoyote yule. Kama hiyo ni ngumu basi wapewe “sick leave” wakisha jifungua waendelee na masomo yao.  Au kama hizo mimba zinawakera sana basi wafungulieni Abortion clinics ili wawe wanakwenda kuzi-abort huko, labda roho zenu zitafurahia!!

Kumbuka kuwa unapomnyima mama moja  haki ya kuelimika inamaana unatengeneza jamii / community ya watu wasio na muelekeo wa maisha na kuendeleza mila ambazo hazina tija kwa taifa! Mama ndio nguzo za familia nyingi haswa Africa. Hakuna njia mbadala katika hili swala zaidi ya kuwaacha waendelee na masomo yao bila ubaguzi wowote ule kwa faida zao binafsi, vizazi vyao, na taifa kwa ujumla!Ngoja nimalizie kwa kusema kuwa, tatizo wazazi wengi wa Africa wanataka waonekane kuwa wao ni malaika hawajawahi fanya mistakes yoyote ile maishani mwao! Ndio maana wako guilty na busy kuwahukumu watoto kwa kuwapa adhabu za ajabu ajabu badala ya kuwaelekeza juu ya maisha. Unajua yale mambo ya kila mzazi anajifanya alipata ‘A’ darasani, alikuwa wakwanza siku zote, na kila mwanamke aliolewa akiwa bikira! Just a bunch of nonsense (Excuse my language)!. Uongo mwingi kwa watoto zenu bila sababu yoyote ya msingi!  Btw, hii ni karne ya 21, mama yangu where have you been?! Unaona statistics za dunia zinavyo kwambia yani karne hii wazazi nmnatakiwa kuongea na watoto / wajukuu zenu juu ya sex / elimu ya kujamiiana kabla ya miaka 10! Kwani watoto wa miaka 10 siku hizi wako sexually active na wengine wanabeba mimba! How? I don’t know usiniulize mimi lakini hiyo ndio hali halisi ya sasa, just get with the program mama!!

***FBF*** Hii story yangu niliandika May 17th, 2017 wakati Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza mjadala juu ya hitimisho la elimu kwa watoto wakike wanao pata ujauzito wakiwa shuleni!****

MAMA SALMA KIKWETE UMEKOSEA SANA! HIYO INAITWA INSTITUTIONALIZED DISCRIMINATION!

Hivi ule usemi wako wa “mtoto wa mwenzio ni wako” uliufuta baada ya kuvua kofia ya u-FirstLady!! Bado najaribu kukutafakari nia yako haswa ni nini?! Wahenga walisema “uchungu wa mwana aujuae ni mzazi” lakini mimi saa nyingine napingana na huu usemi kwani kuna watu hawajawahi onja machungu ya uzazi wala malezi lakini wanaumizwa na kuguswa na watoto wa wengine kuliko baadhi ya wanawake walio zaa! Hapa simuongelei  mwingine bali ni aliyekuwa mkuu wangu ya shule ya Kowak Girls Secondary school Sister Magdalena (R.I.P). 

Miaka 23 iliyopita, nilipopata ujauzito nilikuwa form 2 pale Kowak Girls Secondary school Wilaya ya Rorya, mkoa wa Mara. Shule ilikuwa inaongozwa na wamishonari wa Catholic na huyu Sister Magdalena ndio alikuwa Headmistress (yeye alikuwa Mmarekani) na msaidizi wake alikuwa Sister Nyambosa  ambaye alikuwa Mtanzania. Sasa Sister Nyambosa kulingana na the so called “mila na desturi, sheria za Tanzania na dini” alitaka nifukuzwe shule!! Eti hiyo ndio adhabu yangu nikajifunze! But guess what?!! Sister Magdalena akasema NO! Hato hidhinisha hiyo barua ya mimi kufukuzwa shule kwani haoni logic ya hizo mila na desturi, pamoja na sheria za Tanzania. Yeye aliamini kuwa kitendo cha mimi kuwa mama kwa umri ule ni adhabu tosha! Pia nilikuwa mmoja ya wanafunzi wazuri pale shuleni hivyo hakuona kwanini aniharibie future yangu kwa kunifukuza shule ambayo technically angekuwa anaharibu future ya watoto wawili (mimi na kiumbe kilichokuwa tumboni mwanangu wakati ule).

Kufupisha story hii, wakafikia makubaliano yakunipa sick leave mpaka nitakapokua tayari kurudi shule basi wao walikuwa tayari kunipokea au kunipa uwamisho kwenda shule nyingine! Miezi sita baada ya kujifungua nilitafuta shule nikahamia, uhamisho wangu ulitumwa bila tatizo!! Shule niliyo hamia ilikuwa ni Nurulyakini Secondary school pale Mwembe Yanga, Temeke. Nilirudia form 2 kwani nilikuwa sijafanya mtihani wa form 2 nilipokuwa nimetoka Kowak. Wanaonijua vizuri wanaweza kushuhudia kuwa hata siku moja sijawahi kuwa ashamed kusema kuwa mimi nina mtoto. Kwani miezi mchache tu hapo shuleni nilianza kuwaambia wanafunzi wenzangu na hatimaye story zikafika hadi kwa walimu wote wa shule! Guess what?! Hakuna aliye jali wala kunifanya nijisikie vibaya kuwa mimi ni mama katika umri ule!! Walichojali ni academic records zangu! Tulipoingia form 3, nikachaguliwa kuwa Assistance HeadGirl, na nipofika form 4 wakanichagua kuwa HeadGirl na hiyo yote ni kwasababu ya jinsi nilivyo kuwa hapo shuleni walimu walipenda sana na kuniona as a blessing to their school.

Nakumbuka siku moja dada aliyekuwa ananiangalizia mtoto alikuwa anaumwa hivyo hakuweza kukaa na mtoto siku hiyo. Ilikuwa ni wiki ambayo tunafanya final exams review kwa ajili ya kuanza final exams za form 4!! Nilikuwa na 2 choices; ama nisiende shule nibaki nyumbani nimuangalie mwanangu au nimbebe mwanangu niende naye shule! Sikiliza mama, jinsi walimu wangu na wanafunzi wenzangu walivyo nifanya nijisikie wakawaida kama wao, yani wala sikufikiria mara mbili!! Nikamuogesha mwanangu nikajiandaa nikaendanae shuleni. Nipo darasani nasoma na mwanangu yupo pembeni yangu! Hakuna aliyeniona waajabu wala nini!  kila mtu alikuwa anamfurahiya mwanangu!! And for the records nilifaulu vizuri sana form 4!

Hon. Salma Kikwete

Mama yangu sikiliza, tatizo lolote lile hata liwe kubwa kiasi gani ilikutafutiwa suluhisho la kudumu inategemea na attitude ya jamii husika na viongozi wake! Embu tafakari kama Sister Magdalena asingeweka msisitizo kuwa hato hidhinisha hiyo barua ya kunifukuza shule mimi ningekuwa wapi leo?!! Vipi kama walimu na wanafunzi wa Nurulyakini wangenibagua na kunitenga je mimi ningeweza endelea na masomo yangu?! Je, maisha yangu na ya mwanangu yangekuaje kama nisingepatiwa nafasi ya pili ya kufanya matengenezo?! Maana hivyo vyeti vyangu I mean my academic records ndio vilivyonileta hapa nilipo leo hii!! Labda nikwambie tu kuwa Nurulyakini ni shule ya Waislamu!

Hii tabia ya kutokutoa nafasi ya pili kwa “wakosaji” ndio inaleta matitizo mengi ndani ya Tanzania kama mambo ya vyeti feki, na forgeries nyingine! Viongozi wenye mtazamo kama wako ndio wanao changia matatizo kama hayo niliyo yataja katika jamii yetu!

By no means, siungi mkono maswala ya wanafunzi wa kike kupata mimba wakiwa mashuleni. Hata mwanangu analijua hilo kwani niliongenae mapema mno nilipo ona anaakili za kutosha kuelewa kile nitakacho mueleza. Lakini naomba uwelewe kuwa tatizo si kupata mimba, tatizo ni familia, jamii, na serikali imeshindwa kuelewa kuwa kuna uhitaji mkubwa wa kuelimisha familia pamoja na jamii nzima kuhusu swala la kujamiiana na changamoto zake haswa kwa watoto wakike! Leo hii unasema waliopata mimba wasiruhusiwe kuendelea na shule, ok! Fine! Vipi wanao adhirika na magonjwa Kama HIV, gonorrhea, genital herpes, syphilis, n.k  hao mnawafanyaje?! Kwani hayo pia siyanatokana na ngono??! Hauoni kama kuna haja ya kuwataka madaktari wawataharifu shule mara tu wampatapo mwanafunzi anaugonjwa wowote wa zinaa ili nao wafukuzwe shule?? Mbona mnawaonea wanaopata mimba peke yao?! Ooh! Au mnaonaje muanzishe sheria ya watoto wakike kukagualiwa kama wako sexually active au bado kabla ya kuingia shule katika kila muhula?! Labda hiyo ingetoa fursa sawa kwa mabinti wote! Na wanaume je mgewafanyaje?!!! Acha ubaguzi na unyanyapaaji mama yangu?!

***ITAENDELEA……… ***

***FBF*** Hii story yangu niliandika May 17th, 2017 wakati Bunge la Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania umeanza mjadala juu ya hitimisho la elimu kwa watoto wakike wanao pata ujauzito wakiwa shuleni!****

Simulizi za maisha ya mzee Igogo kwa maneno yake mwenyewe!

MATUKIO YA LEO 19.02.2020 KWA MFADHILI:- 1. Bi Mole Akungo, mjane wa marehemu Akungo fundi magari, aliyekuwa Mwajiri wa Mkurugenzi John Orwanda. Anaumwa kisukari na kasikia tuna dawa ya Jufeel, pamoja na kukosa uwezo wa kujikimu.

2. Dada yangu wa kihindi Bi. Dirishan mlemavu wa Kibiongo aliniita kumtembelea kwake, ndiye aliyekuwa mwenye ofisi ya mtaa wa mshihiri na eneo la kurasini, nilipoanzia kampuni ya Utegi. Walinisaidia mno nilipokuwa naanza kampuni.

3. Rafiki yangu Bi. Zainabu Mbuguni, mlemavu wa macho (KIPOFU KABISAA), Aliniletea zawadi ya kazi ya mkono wake, kikapu cha ukiri, aliyoitengeneza mwenyewe kuanzia kusuka ukiri na kushona kapu hilo, ili nimpelekee mama Igogo kwendea sokoni, pia kaniletea zawadi ya miwa anazolima shambani kwake huko Kibamba.

Pichani yupo na Mwanasheria Asha Nassoro Mwanasheria wangu, na Maria Patrick Kagose, Mfadhili wangu nilitumia tiketi yake ya Bus na treni akiwa mdogo, kuijia jijini Dar, kwa upendo wa Mama yake, Dada Theresia Olung’a Igogo, aka Mama Maria.

***Imeandikwa na Sir O.O Igogo na kuleta hapa na Alpha Igogo (Blogger)***

Simulizi za maisha ya mzee O.O Igogo kwa maneno yake mwenyewe!

Za asubuhi marafiki wapendwa. Natumai soote tumeamka salama na hao wadogo wasiyoweza kuwasiliana kwenye group. Jana ilikuwa siku yangu ya kumbukizi ya mambo ya ujanani, kama alivyosema Mama ni kweli niliwahi kushiriki kanywaji kati ya mwaka 1972 hadi 1979. Nilishuhudia matukio mengi ya kuchekesha na kuhuzunisha ndani ya kipindi hicho. Nakubaliana fika na Rais Mstaafu wa Nchi ya Merekani OBAMA, alichokiandika kwenye kitabu chake kilichompa Umaarufu kiitwacho THE DREAM FROM MY FATHER. Aliota njozi toka Baba yake, na wala siyo ndoto!!!Nami mwaka wa 1979, nikiwa kazini wilaya ya Geita enzi hizo, kwenye machimbo ya dhahabu Nyarugusu, nikiwa Msimamizi wa Ujenzi wa mitambo hapo mgodini na Shirika la NECO Ltd. Nilienda kijiji cha jirani kumtembelea Mama yangu mdogo, aitwaye Leokadia Ombwa Olwengo, mdogo wake Rhoda Nyolwengo. Yeye na Vijana wake walikuwa wachimbaji wadogo wadogo. Nilikuwa na gari la Shirika na ikawa shangwe ya hali ya juu nilipofika hapo kwake. Kuku wawili walipoteza uhai ghafla kuwa kitoweo rasmi. Mama alikuwa mtengenezaji maarufu wa pombe ya kienyeji iitwayo APELO, yaani CHANG’AA?? Ile furaha ya kukutana na ndugu zangu, nao kuniona nimekuwa Bosi naendeshwa na gari la Shirika, ikazua unywaji wa kilevi Apelo bila kipimo. Nilivyorudi kambini na kuingia chumbani sikujuwa. Ila usiku huo wa tarehe 7/6/1979, nilijiwa njozini na Marehemu Baba yangu Mzee William Olung’a Igogo. Aliniita kwa sauti ya juu sana nami nikamuitikia, nilikuwa napepesuka kwa ulevi, manano aliyoniambia ni:- MBONA UNAHARIBIKA KWA POMBE?? ACHA ULEVI, UNAPOTEA!! ACHA KABISA?

Asubuhi yake nilipoamka, nilikuwa hovyo, hovyo kweli, kweli!!! Nilijikuta nimelala kwenye matapishi yangu yanayonuka kama taka teke teke ya chooni. Mchovu kupindukia, kichwa kinawanga na kugonga kama nyundo!! Ilinilazimu kujifanyia usafi huku nikiitafakari hayo maneno ya njozini, niliyohaswa na Marehemu Baba!! Sikuweza kwenda kazini siku hiyo, ilipofika mchana nilipata mlo kwenye kantini ya hapo Camp, na hatimaye nikaamwambia dereva anipeleke Geita mjini, nilikwenda moja kwa moja kwenye duka la Vitabu, na kununua kijitabu kidogo cha Agano Jipya. Nikaanza kuisoma msitari kwa msitari, kurasa hadi kurasa ifuatayo hadi mwisho, na nikairudia mara kadhaa.Ni kweli tangia siku hiyo hadi leo hii, zaidi ya miaka arobaini sijaweka kinywaji cha aina yoyote kinywani mwangu. Naamini bila mashaka ya aina yeyote kwamba Maandiko matakatifu isemavyo kwamba Baba na Mama yako ndiyo Mungu wako wa Duniani, ni kweli haswaa.

Mzee Igogo na mjukuu wake Cecilia Chaulo

***imeandikwa na mzee O.O Igogo (muhusika) na kunukuliwa hapa na Alpha O.O Igogo (blogger)***

“Life can be a rollercoaster and you will never know where you’ll end UP.” >>> Zari the Bosslady

Life can be a rollercoaster and you will never know where you’ll end up

From studying my Cosmetology course in the UK ( which hasn’t helped me) while doing house girl work to pay my accommodation (yes I’ve been a maid before) to running through buses to get to my next stop woodgreen where I worked as a Cashier and sometimes as an Isle packer in Sainsbury. Friend, I started out early wasn’t even sure why me. But the inner voice in me wanted better.

My dad had left, my mom was doing tailor jobs day and night I couldnt stand seeing her struggle I couldn’t stand her pain. I was living with my aunt in the UK who treated me like a step child. Gooosh?
Been through boutiques, long economy flights to china in between building a school and having babies. My music and tv career is a story for another day. Phew? All I’m saying, consistency is key. Doesnt matter where you are or what you do. Just do it.

I am the author of my life, my story, don’t rewrite it for me.! Let me be the one to tell it.
Throwbacks are good, reminds us of where we’ve come from and I think that kinda keeps you grounded.

William Ernest Mjee Oucho: Ndoto yangu ya kua Engineer

William Ernest Mjee Oucho
Napenda nishee na nyie story ya safari yangu ya kutafuta kuwa muhandisi tangu nimekua na mpaka sasa nilipofika. Twende sambamba utajifunza kitu hapa.

Mwaka 1993, Jumatano moja ya tarehe 09 mwezi wa Sita, mama angu alinizaa na kunileta duniani, na kunibarikia jina la William, ambaye alikua ni marehem baba yangu mkubwa. Nikaishi na wazazi wangu wote baba na mama, kaka yangu (JUMA SELA), dada yangu (Zainabu), na mdogo wangu Benadetha(R.I.P) katika kijiji cha Utegi, wilaya ya RORYA (kama mnavyoniita), mkoani Mara.

Familia ilikua ya hali ya kawaida sana. Ilipofika mwaka 2000, nilijiunga na shule ya msingi Utegi, iliyopo kwa kukadiria ni kama Km 4 kutoka home. Nikasoma na kuhitimu 2007. Nilianza kuonekana kama taa, baada ya kuwa nafaulu vizuri katika masomo yangu, na kupelekea kujulikana kwa waalimu na baadhi ya watu. Mwaka 2003, nikapewa uongozi (Kiranja) kwenye darasa la watu (188). Nikawakilisha vyema shule yangu katika uandishi wa Insha uliohusisha wilaya nzima ambao uliuletea shule yangu ya Utegi sifa nzuri. Walimu walianza kuniona mbali tangu hapo na kuniombea sanaa ndoto zangu zitimie.

Ilipofika December 10, mwaka 2004, baba yangu alifariki nikiwa darasa la tano. Akatuacha na mama na familia ya baba mkubwa (Olambo Oucho) kama baba yetu mlezi! Tulisikitika na kuhuzunika sana ila tuliyasahau na kumuona baba yetu mkubwa kama baba yetu mzazi. Mwaka 2006, nilihitimu shule pale pale utegi Primary school. Chakushangaza ni kwamba hata kufaulu sikufaulu, mbali na kujitahidi sana darasani (sijui nini kilitokea), ila mwaka huo (awamu ya kwanza) walifaulu wanafunzi 12! Nilikasirika sana, nikasema nitarudia shule na nitafaulu kwa alama za juu sana. January 8, 2007 nikarudi shule kurudia darasa la saba nijaribu bahati yangu tena. Haikuchukua muda sana March 01, 2007 matokeo ya awamu ya pili yakatoka nikawa nimo kati ya watahiniwa waliofaulu kwa alama za chini 159/250? na kuchaguliwa kujiunga na shule ya sekondari PASTOR RAPHAEL ODUNGA, ilioko kijiji cha Buturi, umbali wa Km kama 18 kutoka nyumbani.

Sikua na namna nilitamani sana kusoma na wenzangu form One, nikamwambia mama yangu akatafuta njia kwa kushirikiana na baba mkubwa wakanihamishia NYANDUGA Secondary iliyoko kwenye Kata yetu. Jumatatu ya tarehe 07 March, nilianza shule nikiwa nimebeba jembe, ndoo ya maji, kwanja, rim paper (double A) na shilingi 26,000/= nikaanza masomo. Wiki iliyofuata Jumatatu ya tarehe 12/03/2007 tulianza mitihani ya mid-term test nikiwa na siku tano tuu shuleni, nilipata alama za kushangaza watu sanaa ndio ukawa mwanzo mzuri! Nilipenda sana Maths, Physics, Chemistry na Biology ndipo nikaona mimi naweza kuwa Engineer baadaye maana masomo hayo nayaweza vizuri.

Mbali na kwamba baba angu mkubwa alisomea uhandisi (Engineering) nlipomgusia kuhusu nia yangu mimi ya kusomaea fani hiyo pia alinitia moyo sana, na kuniambia nikazane kwani kuna chuo kipo Dar kinaitwa DAR TECH, wanachukua watu wanaopasua sana masomo kama hayo! Akanipa dondoo za raha ya chuo hicho; wanavyokula, chuo kipo katikati ya jiji la Dar, wanalipwa hela, hakuna kufanya usafi, ? basi nikaona huko ndo patanifaa, nikasema wacha nikomaeee na shule kwanzaa.

MAISHA YA NYANDUGA SEKONDARI:
Nilijitahidi sana kusoma na kukazania masomo ya sayansi nikijua nikimaliza naenda chuo cha Dar Tech. Baba mkubwa alituwekea hazina ya vitabu vya kujisomea, nikapambana hadi mwaka 2010 ilipo maliza form four hapo Nyanduga Secondary, matokeo yalitoka yakiwa mazuri kwangu, na kwa rafiki zangu wengine. Tuliofaulu na kuchaguliwa technical school tulikuwa watatu; David Kajode alipelekwa Arusha Tech, David Kimira alipelekwa Ubungo Maji na William Ernest Mjee Oucho.

Hutaamini, nilichaguliwa moja kwa moja kujiunga na CHUO CHA SAYANSI NA TEKNOLOJIA Dar es salaam (Dar Tech), kusomea Shahada ya Uhandisi mitambo kwa miaka mitatu.????? ndoto ikawa imetimia kwa namna moja. Nilifurahi sanaa! Mama na kila mtu aliyejua walifurahia sanaa. Namshukuru hata Mbunge wangu wa jimbo (MH. LAMECK O. AIRO, Lakairo) aliniona kwa jicho lingine na kunitia moyo na kuniahidi kushikamana nami bega kwa bega mpaka nitakapofika.

SAFARI YA KUJA DAR:
Ilifika siku ya kutoka nyumbani kuanza safari ya kuja chuo, nikiwa mwenyewe kwa mara ya kwanza ? nilipofika tuu Tarime Km 14 kutoka home nikaibiwa pesa zangu zote, na nikarudi home tena kutafuta pesa nyingine. Nikapata pesa nikaanza safari kwa mara nyingine na kuja mpaka Dar. Nilipofika Dar nilipokelewa na mama mkubwa (Mrs. Cecilia Igogo), kisha kunipeleka nyumbani kupumzika. Kesho yake asubuhi mama alinisindikiza chuoni kufanya usajili na baadaye kuhamia chuoni kwani nilikua natakiwa nikae chuoni. Mama mkubwa ni mama mwema sana, alikua akipita kunisalimia na kuniombea kwa Mungu, alinambia niamini katika ninachofanya nitafanikiwa. Nilitii na nikamuahidi sitamuangusha. Nilisoma na hatimaye 2014, nikahitimu.

William na mama yake mzazi wakati wa sherehe za kumaliza chuo, Dar Tech

Ikawa furaha nyingine kubwa kwangu, kwa mama yangu, baba yangu mkubwa na kila mtu aliyetamani kuniona nafika hapo.
Nilitamani kuunganisha kuendelea kusoma ila kuna somo moja lilinifanya nisiweze kuunganisha, kwani matokeo yetu yalicheleweshwa kupelekwa NACTE, ikanibidi nikae mtaani kwa miaka miwili. Katika kipindi hicho cha miaka miwili nilitumia kupata uzoefu wa kile nilichosomea, ambapo baba yangu mkubwa (Mr. Otieno O. Igogo) aliniona na kunipeleka kiwanda kimoja cha kutegeneza juice cha (U-fresh food), Tegeta. Nilifanya kazi pale kama fundi mchundo wa mashine hizo. Baadaye milango ya kazi ilifunguka na kujiunga na moja ya kampuni kubwa hapa nchini ya Kuzalisha Umeme na Kusambaza gesi (Songas Power Plant), iliyopo Ubungo. Nilifanya kazi pale huku nikiwa najitegemea sasa, naishi kwenye chumba changu cha kupanga.

Ilipofika mwaka 2016, nikasema lazima nijiunge kumalizia masomo yangu ya Shahada ya kwanza. Nilifanikiwa kufanya hivyo, nikapata chuo kile kile, fani ile ile, na nikaanza masomo rasmi ya kuitwa Engineer. Nilianza masomo yangu ya shahada ya kwanza mwaka 2016, na nikadumu kwa miaka mitatu, hadi kufikia june 10, 2019 nilipohitimu rasmi na kuweza kufaulu na kupata nlichokua nakitafuta kwa muda mreeefu! New Mechanical Engineer in Town.

Changamoto kila mtu anazo ndio maana hata sijaziongelea hapa, msije mkadhani nilikua nasona kwa raha raha, weee! ???? Ila natumia fursa hii kwanza kumshukuru Mwenyezi Mungu wa Mbinguni, muumba wa Mbingu na nchi kwa upendo na uhai alionikirimia. Pia napenda kushukuru kila mmoja kwa nafasi yake alivyoshirikiana na mimi kuniwezesha mimi kuwa hapa. Wanadarasa wenzangu, kuanzia darasa la kwanza hadi chuo Kikuu, ?!

? Mama yangu mzazi kapambana sana na mimi, kuhakikisha sikati tamaa, hata kama Inakuja gharika gani.

?Baba yangu mkubwa, Kwa kunionyesha njia na kutupatia elimu hakika, aliweza kutupa vitabu na sasa tunaona raha yake.

?familia ya Mr &Mrs Otieno Olung’a Igogo, mbarikiwe mpaka shetani aje awaulize mmewezaje wezaje???

? Lameck O. Airo, Erasto Airo bro asanteni kwa kila kitu kwa kipindi chote nilivokuwapo skuli.?Mbogi yangu ya Rorya, Robhin Edson, Edina Ziporah, Kajode, Mary, Triza, Omara, Vicky, Triza Wuod nam, Emma Lucas, na wengineo wengi ambao sitamaliza kuwataja hapa tumeshikana vyema na tuendelee hivi hivi?

Niwakaribishe katika mahafali ya kuhitimu shahada yangu ya kwanza ya uhandisi Mitambo, tarehe 28/11/2019 katika viwanja vya chuo chetu, tufurahie kwa pamoja maana nikishinda nanyi mmeshinda…NB: wanaosoma au una mpango wa kusoma, tia bidii sanaa utafanikiwa tuu, Mungu ni mwema na ni wa kwetu sote.NAWAPENDA SANA WOTE. ? THE END?