Category Archives: General

Zari amekosea sana!

Kumpenda mtu siku zote utakuwa mkweli kwake hata kama yeye mwenyewe hapendi ukweli wako! As much as I Iove Zari, but I have to tell her this beater-truth! Kuwa Zari kwa hili umekosea sana!

Kwanza nianze kwa kusema simsapoti Diamond kwa udhalilishaji wake anao wafanyia wanawake kila siku! Hii ya Zari ni series ya matukio mengi ambayo amewafanyia wanawake ambao wamekuwa kwenye mahusiano naye.Amegeuza wanawake ndio mtaji wake wa kuongeza nguvu kwenye kazi zake! Which is very very wrong! However, despite all the evilness he has done, when comes to this issue ya kumdhalilisha Zari, personally I kinda understand where his pain is coming from! But again it doesn't justify what he did.

Kwanini nasema Zari amekosea? Ni kwasababu moja kuu ya kuamua kufanya udhilishaji kwa baba wa watoto wake bila kufikiria kuwa the real victims here are her own children! Tendo alilofanya Zari linamuweka level moja na Diamond, yani hakuna tofauti kati yao and two wrongs can't make it right! ..Kitendo cha Zari ku-move on na maisha yake ni kizuri sana! Tena sana! Nampongeza kwa hilo. Lakini kitendo cha yeye kuleta mwanaume mwingine kwenye nyumba ya mwanaume mwingine ni kukosa heshima sio tu kwa Diamond kama baba wa watoto wake bali pia kawakosea heshima watoto wake!
Zari, The Bosslady

Ule mji ulinunuliwa kama mji wa familia.That’s a place where her children as long as they live they will always remember and call it home! Home is small sanctuary, Zari has dishonored her children sanctuary! Hivi unajua ipo siku watakuwa wakubwa na sidhani kama watakuwa so impressed with their mom decisions! Haswa Tiffa, unajua jinsi watoto wakike walivyo na baba zao, Mungu atupe uzima kushuhudia yajayo!..Sijui kama Zari anajua anachofanya ni kosa au ndio maisha ya u-celebrity yamemuingia kwani hii sio mara ya kwanza kufanya hivyo. Tunaona hata alipo achana na marehemu Ivan Ssemwanga alikua anamleta Diamond kwenye nyumba ya watoto zake! Na marehemu hakufurahishwa na hili! ?? wanasema malipo ni hapa hapa duniani eeh! So Diamond got what he deserves!!.. Inajua mimi nashindwa kuelewa sijui ni Usabato wangu au ujaluo ndio unanifanya nishindwe kuelewa hii celebrity lifestyle!

Hivi wanawezaje kuleta mtu mpya kwenye nyumba au chumba ulichokuwa unatumia na your Ex-girlfriend / boyfriend? Nashindwa kuelewa haswa kwa wanawake! Majasho ulioweka kwenye makochi na mwanaume mwingine ndio hapo hapo unamleta mpenzi wako mpya ? Dah! Mie sielewi hii lifestyle! Labda ushamba umenizidi can’t think right ?‍♀️?‍♀️

Diamond ni mwanaume mshezi tu (sorry to say that) lakini hapa Zari kampa sababu na nguvu ya kumdhalilisha kwa kitendo cha kuleta mwanaume mwingine kwenye nyumba yao ambayo walinunua kwaajili ya familia. Ndio maana nimesema naelewa hasira za Diamond japo sifurahii alicho kifanya! Hii imekuwa ni desturi yake kudhilisha Exs wake toka wakina Penny, Wema n.k wote kawafanyia huu ushenzi! Ila amini usiamiani Tanasha anatmnyoosha Diamond wewe weka macho yako utayaona!

Mama Tiffah, the Bosslady

Kama kweli Zari anataka amani na kuishi maisha yake bila bugudhi yoyote basi Zari, you need to move to your own house, period! Let those men who desperately need you move to your house ili wakikuletea ujinga unamwomba aondoke kwenye mji wako. Lakini kitendo cha kuendelea kuishi kwenye mji wa wanao ambao baba yao kawanunulia haitakupa uhuru ambao unautaka! Just get your own place hata kama ni kubaya kama kwangu lakini ni kwako! Ni chakwako hakuna wakukwambia kitu! Please!

Halafu, I don’t know about you Zari maybe because you’re living that “celebrity lifestyle” but a man who dishonors his fellow man’s home like that?! Ain’t a man for me! Because it comes down to his morals and ethics! I hope he won’t turn around to be like the one you just dumped or even worse!..Hapa ndipo Tanasha kawazidi, unaona ametaka nyumba mpya kabisaaa ambayo hakuna Ex-girlfriend yoyote wa Diamond amewahi kulala wala kufika hapo! Msichana wa Kijaluo akili kwa kichwa ?? Nani anataka kulalia vitanda au kukalia makochi yenye majasho ya mikosi ya mtu mwingine? ?

Anyway, just prepare for the worst and hope for the best ?? I saw somewhere you said you are about to say ‘I do’, my advice to you is take your heart with you but don’t forget your brain!! And prayer is key to every battle! Otherwise wishing you the best in everything you do! ❤

Dina Marious: Je, marafiki walio tuzunguka ni wa aina gani?

Reposted from @dinamarious – Leo nimeamka kichwa kiko mbio maana zimebaki siku 4 tu niwe nawe katika Maisha Class Seminar.

Lakini nimemkumbuka rafiki yangu mmoja wa toka udogoni.Hatuonani sanaa ila tunaongea sana kwenye simu.Nikakumbuka namna walivyokuwa wakiishi maisha mazuri sana.Wao ni miongoni mwa watu wa kwanza wazazi kuporomosha mijengo huku Mbezi beach.Miaka ya 90 wana hadi boat ya kucruz kwenda visiwa hivyo vya bongoyo sijui mbudya ambavyo sie ndio twaenda leo.

Dina Marious; Mtangazaji, Mfumbuzi na Mkurugenzi Mkuu wa Dina Marious Coconut Oil, Founder of Mwanamke wa Shoka and Kitchen Party Gala

Mama yao aliwazaa mapema sana na baba yao akafariki mapema pia.So walilelewa zaidi na mama.Mama alikuwa na pesaa alikuwa mrembo sanaa na alikuwa na marafiki wengiii mno.Na pia alikuwa mzuri wa sura na wa roho kujitolea kwa marafiki na ndugu sanaa.Wadogo zake kama watatu aliwawezesha kwenda kuishi nje.Yeye safari za nje ya nchi kama sijui kitu gani.Party za babakyu na marafiki safari na marafiki za kula bata nyumbani kwake palikuwa hawakauki watu.
Yule mama alikuja akaanza kuishiwa akaanza pia kuumwa aliugua kwa muda kidogo na kwa wakati huo rafiki yangu na mimi tupo kidato cha pili.Ndugu walikula kona,marafiki ndio usiseme.Alibaki yeye na watoto wake tu na hadi anafariki alimfia mwanae huyo shoga angu mikononi hivi akimhudumia maana ndio wa kwanza.

Dina Marious; Mtangazaji, Mfumbuzi na Mkurugenzi Mkuu wa Dina Marious Coconut Oil, Founder of Mwanamke wa Shoka and Kitchen Party Gala

Kuna mengi yalitokea sanaa lakini hili jambo huwa silisahau.Maana mie ndio nilikuwa shoga ake namna ndugu zake walikuwa wakimfanyia nilishuhudia kwa macho.Na huwa namkumbuka sana huyo mama na sasa nimekuwa mtu mzima ishu hiyo huzunguka sana kichwani kwangu.

Je marafiki waliotuzunguka ni wa aina gani?una marafiki kweli au una wapambe?Ni wangapi katika mafanikio tunakuwa na marafiki wengiii ambao kiukweli wapo hapo kwa manufaa yao?Wapo na wewe sababu una nafasi fulani,wadhifa fulani kupitia wewe mambo yao yatanyooka?Kwa sababu una mkono wa kutoa labda utatatua shida zao,utasikiliza hofu na nyakati ngumu wanazopitia. Utawalisha,utawanywesha,utawapa pesa,nguo,viatu inshort unarahisisha maisha yao.Ngoja pesa ikate ndio wa kwanza kukusema umefulia na kukukimbia.
Ngoja cheo/nafasi uliyonayo ipotee ndio utawajua walimwengu au wali nyama!Sitasema sana ila Mungu atujaalie watu sahihi katika maisha yetu.

MaishaClass #NenoLangu – #regrann

**Imeandikwa na Dina Marious**

Unapokutana na mtu mwenye mafanikio usimuombe pesa. Muulize amefanyaje kufikia hapo alipo!

“When you meet a person with means, a person that is well-off you think is successful  that you always wanted to be; don’t go there asking  for money” Hayo ni maneno yake Comedian na TV host Steve Harvey kwenye Oprah Master Class. Master Class ni show ambayo watu wengi waliofanikiwa katika nyanja mbali mbali za maisha wanaelezea mafanikio yao kwa undani zaidi toka walivyokuwa wadogo mpaka walipo fikia. Changamoto zipi walipata, vipi waliweza kuvumilia, kumudu hizo changamoto, na hata kufanikiwa bila ya kukata tamaa. Unapopata nafasi ya kukutana na mtu au watu ambao unawaangalia kama  “role mode / icon”  katika maisha yako usiwaombe pesa waombe wakuelimishe nini walifanya kufikia hapo walipo. Watu wengi wapo wepesi wa kuomba pesa kwa mtu aliyejaliwa kuwa nazo kwa ajili ya kujikimu na hiyo shida aliyonayo. Nautakuta muda mwingi shida hiyo haiishi ni kaituliza tu kwa muda. Hii yote nikwasababu wengi tunapungukiwa hekima ya kujua kuwa ni kheri mtu akupe elimu ya maisha ya nini alikifanya mpaka kufika hapo ili uone kama na wewe unaweza tumia njia hiyo kufikia malengo yako au kujikwamua kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Au utakuta wengine tumepingukiwa hekima ya kuona mafanikio ya watu ni maovu mbele zetu nakuanza kutafuta njia ya kumuangusha bila kujua kuwa anguko lake ni maafa kwako pia. …….Hivyo tuwe waelevu kama nyoka na wenye hekima kama Solomon ili tuweze kujifunza kutoka kwa wengine haswa ambao tunaona wana tija katika maisha yetu. Pale watu wanapokukatisha tamaa wewe piga moyo konde usiwasikilize. Kwanza mimi kwa experience yangu binasfi watu wengi wenyekukatisha watu tamaa ni watu ambao hawajiamini na pia hawapendi kuonekana kuwa wao wameshindwa katika kufikia kile wakitakacho hivyo hamna la zaidi zaidi ya kupiga makelele ili uwe muoga. Wakati ukweli wanatamani wangekuwa na ujasiri kama wako. Utaona wanakuja na maneno mengi ya kejeli ikishindikana wataingilia personal attack “hajaolewa”, “mnene”, “hana nywele”, “mbeba mabox” yani ukishaona mtu anaenda kwa personal attacks jua maumivu yamemuhelemea ?? . . Nasiku hizi social media, basi watatafuta kila event au tukio lenye viongozi waende kupiga picha ili warushe kwa Facebook / Instagram basi tu ufikirie kuwa there really happy and making it, wakati rohoni wanatamani wawe na kipaji au nafasi kama yako. ?? Wanasaikolojia wanasema mara nyingi watu wanao ongelea wengine vibaya muda wote huwa kuna mambo ambayo hayopo sawa kwa upande wao sasa kwasababu hawataki watu wajue huo upande wao hauwapendezi, basi dawa inakuwa ni kugeuza attention kwa wengine! Na huo ndio ukweli! Wewe usikate tamaa na mapicha yao! Nawala usiache mashauzi yao yasio na kichwa wala miguu yakuumize au yakutoe kwenye malengo yako. Mimi nilivyoanza hii blog yangu nimetungiwa uzushi wa kila namna; ooh huyo muhuni anatafuta mwanaume, huyo FBI, huyo kada wa CCM (utafikiri walishaniona na kadi ya CCM au nimevaa gwanda la CCM ??), mara anatafuta umaaharufu, mara mkabila, mdini, yani maneno mengi mno wengine wakadiri hata kwenda kwetu kuchunguza maisha ya kwetu nakuja kuongea kwenye magroup yao. Mara kazi yake kudhalilisha watu. Eti huyo anagombania mali za wazazi wake ?? Wengine wakazunguka kuwaambia watu wasiweke picha zao kwa hii blog. Yani hayo yote walifikiri nitaacha kublog!! Lakini nipo hapa and I’m here to stay! Mimi najua ninachofanya na ninako kwenda hivyo sijali. Waliokua wanasema mimi kazi yangu ni ku copy and paste ndio hao hao wanakosa raha kwani wanatamani niwaweke humu kwa blog yangu nami hata habari nao sina ??  Ni maumuvi makali sana wanapata. Wewe songa tu, wakikwambia huwezi wambie wewe ni nani hata useme hivyo! Kitu kingine usiamini kila rafiki. Yani ukiona mtu ambaye ni rafiki yako anachukia maendeleo au mafanikio ya mwingine achana na huyo rafiki mara moja. Kwani inamaana wewe ni rafiki yake Kwasababu haujamzidi kimaendeleo lakini siku ukitaka kunyanyuka atakuwa wakwanza kukuangamiza! Niamini nimeyaona! Siku zote kuna mtu mmoja ambaye atakuelewa na ambaye atakuwa yupo teyari kukusaidia kufikia malengo yako. Mungu huwa hamtupi mja wake! Kama nipesa basi huyo mtu anaweza kusaidia, kama ni mawazo yanini ufanye ili ufanikiwe basi huyo mtu atakuwa yupo tayari kutoa ushauri. It means that person believes in you and truly cares about you! When it looks like nobody cares trust me someone is out there who really cares about you! Muda ukifika Mungu atamleta kwako. Usikate tamaa!

**Imeandikwa na Alpha Igogo** **#TBT #Sept.2017**