Category Archives: Giving back to the community

Temeke SDA Nursery and Primary School watoa shukrani kwa mama Igogo!

Mama Igogo akitazama kwa furaha picha iliyochorwa kwa taswira yake.

Wanao onekana kwenye video hapo juu ni baadhi ya wafanyakazi wa Temeke SDA Nursery and Primary School walifika nyumbani kwa mama Igogo mchana wa jana tarehe 09/27/2021, masaa ya Africa Mashariki, kwaajili ya kutoa shukrani zao za dhati kwa mchango wake wa hali na mali ambao aliutoa toka kuwaza yakwamba kanisa la Temeke SDA linahitaji kuwa na shule, kuisimamia kuanzishwa kwakwe toka elimu ya awali ya chekechea (Nursery school) mpaka kufikia kuwa na darasa la kwanza mpaka la saba.

Kuhakikisha kuna kuwa na boarding (hostel) kwa wanafunzi wanao kaa mbali haswa wanafunzi wa jinsia ya kike! Mama Igogo alikuwa full time Mkurugenzi mkuu (Director) ambaye hakuwai kulipwa mshahara hata mara moja kwa miaka 7! Alifanya kazi ya kujitolea kwa asilimia 100%! Na baada ya miaka 7 aliomba “kung’atuka” na kuwaachia vijana waikimbize. Yeye alibakia kuwa mshauri kwenye bodi ya shule. Mungu ni mwema shule ilisimama na inaendelea vizuri! Mwanangu ni mmoja wa wanafunzi wa mwanzo kabisa wa shule hii! Alianzia  Nursery hadi darasa la sita. Mungu azidi wabariki wote walimu, wanafunzi, pamoja na watu wote wanaojitoa kwaajili ya huduma hii muhimu sana kwa jamii. ????

Kwenye video ya pili ni Mama Igogo akitoa shukrani zake za dhati baada ya kupokea shukrani na zawadi ya picha kutoka kwa wafanyakazi wa Temeke SDA Nursery and Primary School. 

Na hapa, mama Igogo akitoa ufafanuzi wa zawadi ya picha iliyochorwa kutoka kwenye moja ya picha zake ambazo alipiga akiwa kwenye Makao Makuu ya Wasabato ulimwenguni yaliopo Silver Springs, Maryland/ Washington DC eneo la kumbukumbu za Ellen G. White (mmoja wa waasisi wa dhehebu la Wasabato). Mama yangu hajatembea dunia nzima, Mungu ni mwema amembariki kutembelea nchi kadhaa hapa dunia na ameona mengi; lakini safari ya kutembelea kijiji cha history ya Wasabato huko Battle Creek, Michigan na safari ya kutembelea Makao makuu ya Wasabato ulimwenguni kwakweli ni moja ya safari ambazo zimemgusa sana moyo wake na siku zote huwa anaziongelea kwa hisia sana! Namshukuru Mungu kuwa amenichagua mimi binti yake kuwa kiungo kikuu cha mbaraka huo. Si kwamba asingeweza kufika Marekani hapana! Naamini Mungu kama alimpangia kufika angefika tu bila ya mimi kuwepo kama hizo nchi zingine alizo tembelea bila mimi kuwepo! Lakini kufika sehemu kama hizo kwa urahisi na kwa furaha kupitia mwanae naamini nikitu kinampa faraja kubwa sana moyoni! ?? No mama ain’t done yet! Mungu atupe uhai utakula more good time very soon! ?????

Mzee O.O Igogo, Magreth Otieno Igogo, na mama Igogo

Hapa juu ni moja ya picha waliyopiga wakati walikuwa wamekwenda kutembelea kijiji cha historia ya Wasabato huko Battle Creek, Michigan mwaka 2014 mwezi wa 11. Picha A siku hii zipo nyingi lakini zipo kwenye Flashdisk, sijapata muda wa kuziangalia.

Kama ulipitwa na picha za mama Igogo kutembelea Washington DC basi bonyeza ???? Safari ya mama Washington DC , na Safari ya mama Washington DC

Twamshukuru Mungu kwa yote kwani ni kwa neema yake tu ndio maana haya yote yanatokea. Sifa na utukufu ni zake yeye tu milele na milele. ????

AMETIMIZA MOJA YA NDOTO ZAKE!

Mercy akiwa na Dr Kapesa

Siku ya leo tarehe 08/16/2021 majira ya mchana masaa ya Africa Mashariki, mwanangu katimiza moja ya shahuku yake kubwa au nawezasema moja ya ndoto yake!

Amekutana na mmoja wa madaktari walio nihudumia na kuhakikisha anaingia katika dunia hii akiwa salama! ?? Marehemu Dr Amood alikuwa ndio my primary Dr lakini alinikabidhi kwa Dr. Kapesa na Dr Kaisi kama mbadala wake pindi yeye anapokuwa na majukumu mengine. Siku ya kujifungua Dr Kaisi ndio aliyekuwepo zamu, Dr Amood aliitwa na alipofika Mercy alikuwa teyari kazaliwa! ??

Mungu azidi wabariki wote Dr Kapesa na Dr Kaisi! Bahatimbaya Dr Kaisi alipatwa na stroke (kiharusi) hivyo kwasasa amepumzika kufanya kazi za utabibu aliyosomea.

BTW, nilikuwa natibiwa Tanzania Maternity Service ambapo madaktari hawa wote walikuwa business partners!

Jacqueline Mengi: The day @drntuyabaliwe_foundation will be able to put up libraries in all regions and hopefully all districts of Tanzania will be the peak of my happiness

Regrann from @j_n_mengi - There’s so much joy in seeing a dream become a reality,and how that dream can change other peoples lives.I can’t even put in words how lucky and blessed I feel to be able to fulfill my dream of encouraging and enabling kids to develop the habit of reading. The day @drntuyabaliwe_foundation will be able to put up libraries in all regions and hopefully all districts of Tanzania will be the peak of my happiness. - #regrann 

Make someone smile today!

A poorest street beggar who had no teeth in her mouth, showing a smile of life time, soon after coming from a dental theatre, where she got all her 32 artificial teeth done, under sponsorship of a good Samaritan (name will not be mentioned). Happened earlier today in Dar es salaam, Tanzania….. The simple things that make a difference! Be kind today! Make someone smile today!

#God is good!

#MakeSomeoneSmileToday

#GivingBackToTheCommunity

#Picture taken at Utegi Tech office

Hongera sana Dr Ntuyabaliwe Foundation

Hongera sana Dr. Ntuyabaliwe Foundation kwa kazi nzuri sana ya kujali elimu kwa watoto wanaosoma katika mazingira duni. Hakuna kitu ambacho cha furaha ambacho hata Mungu anafurahia kama mtu anayetoa sehemu ya jasho lake na kuwapa watu ambao hawawezi kumlipa na bila kuhitaji fadhila yoyote ile toka kwao. Mrs Mengi SIYO mkazi wa  wilaya ya Temeke, wala SIYO mwanasiasa kusema labda ipo siku ataomba kura. Na wala haitakaa hata siku moja watoto wake wasome katika wilaya ya Temeke! Hello!! Can we talk? Am keeping it real! Hata kama wakifirisika leo sana sana wataishia kusoma labda South Africa au India ?? No shade people! Kwa mfano my feature babies nani alikwambia watasoma Bongoland?! Subutuuu! Watasoma hapa hapa kwa Trump Bongoland wataenda kutembea tu ?? anyway back to our story…. Ninachotaka kusema ni kwamba Jacqueline kwa kupitia mfuko wa Dr. Ntuyabaliwe Foundation hawakuwa na ulazima wa kukanyaga wilaya ya Temeke, hivyo kwa wao kuifikiria wilaya hiyo ambayo hawana faida nayo yoyote inaonyesha jinsi gani wanaguswa na maisha ya Mtanzania wa hali ya chini bila kujali wanatoka sehemu gani!! Kwamaana hiyo, watu wa Wilaya ya Temeke ambao mpo jirani na shule ya Muungano ikifika siku ya Ijumaa mjitokeze kwa wingi kuwashukuru na kuwaomba waendelee kuikumbuka wilaya hiyo! Wapi Juma Nature na wanaume TMK?! ? Please show some love to Dr. Ntuyabaliwe Foundation on Friday! “Today in celebrating Universal Children’s Day I had the pleasure of visiting Muungano Primary School as the chairman of @drntuyabaliwe_foundation and got a chance to talk with the children there. I was happy to see how confident and smart these kids were and can’t wait for Friday when we will launch a new library and donate books to them.” Jacqueline N. Mengi