Category Archives: Leadership

TUSIBEZE VITA HII (Sehemu ya I)- Peter Sarungi

 Tusibeze uthubutu wa mtu tena kijana wa kawaida ambaye bado hajawa nguli katika siasa wala uongozi. Tumpe muda maana hiyo vita aliyoichagua ni vita ngumu inayo hatarisha maisha yake. Huyu ndiye kiongozi pekee wa kumuombea tofauti na wengine. Huyu yupo kwenye vita ambavyo kama wewe ungepewa fursa ya kuwa mkuu wa mkoa huu basi inawezekana ungeshindwa kudeal hata na dagaa kama Makonda alivyoanza. Tumpe moyo mkuu na kumwombea kwa Mungu apigane vita vizuri, naamini hata kama hatashindwa kufikia mafanikio tunayoyataka lakini atakuwa amefanya sehemu flani ya kutatua uovu huu ambapo mwingine atakaye jitokeza katika vita hiyo ataanza alipo ishia Makonda. Hatuwezi kunyamaza kimya kwa tatizo kubwa kama hili na asitokee hata mtu mmoja wa kusema hata kidogo alafu tukajiona tupo samala, Laa hasha kukaa kimya ni kuhalalisha uwepo wa tatizo. Vijana wengi wana angamia na kupoteza nguvu kazi na vipaji kwa sababu ya kukaa kimya na hata kubeza jitiada hizi ndogo zinazo chukuliwa na Makonda. Tuungane na Makonda kutenda na kufikiri tofauti kwa kuchukua hatua za kutenda badala ya malalamiko na matamko yasiyo isha wala kusaidia jamii. Tuweke siasa pembeni kwenye majanga makubwa kama haya ili kuunga kila hatua zitakazo chukuliwa na yeyote katikakupambana na Tatizo hili. 

Na Peter Sarungi (Next Speaker)

Asanteni..

Sabato Njema wana wa Mungu.

WIZARA INA MIKAKATI GANI JUU YA WATU WENYE WALEMAVU TANZANIA?- Peter Sarungi

Na Peter Sarungi (Next Speaker)

Watu wenye ulemavu ni moja ya jamii iliyo katika makundi nyonge (kwa sasa tumefika milioni 4 kwa idadi). Makundi mengine ni kama wazee, watoto na wanawake, makundi haya yanaitwa ni makundi nyonge kwa sababu yana mahitaji maalumu ya kibinadamu na hayawezi kumudu ushindani ulio sawa katika jamii hivyo ni lazima jamii pamoja na serikali iyatizame kwa jicho la tatu lenye utu, huruma na upendo ili nao wajione wapo katika nchi yao na waweze kuonesha uwezo wao ambao Mungu amewakirimu pasipo kujali mapungufu waliyo nayo. 

Peter Sarungi akiwa na dada zake; Alpha Igogo (kushoto) na Magreth Igogo (kulia) nyumbani kwa Peter huko Chanika.

Mimi ni Mlemavu lakini hata wewe ni Mlemavu mtarajiwa maana kama bado unaishi duniani basi jua Mungu bado anaendeleza uumbaji wake kwako. Hivyo linapotokea jambo linalohusu ulemavu basi jihisi na wewe ni mhusika kwa namna moja ama nyingine.

Katika uchaguzi uliopita 2015, nilitoa tamko kupitia jumuiya za watu wenye ulemavu Tanzania ambao ulilenga kueleza changamoto za walemavu pamoja na mapendekezo yake. Changamto kuu nilizoziainisha kwa msisitizo ni ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu katika vyombo vya maamuzi pamoja na muundo wa kusimamia maswala ya watu wenye ulemavu. Niliamini kuwa ili kutibu changamoto hizi za elimu, ajira, afya, uchumi, siasa na huduma zingine ni vizuri tukashirikishwa katika kupika chakula na kukiandaa mezani.

Nilifarijika sana baada ya Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutangaza baraza la Mawaziri pamoja na muundo wa wizara zake, kwa kweli mhe. JPM alitutendea haki ambayo haikuwahi kutendwa na tawala tangu kupatikana kwa uhuru wa nchi. JPM alisikia kilio cha watu wenye ulemavu kwa kutenga wizara itakayo husika na maswala ya walemavu tena ikiwa chini ya ofisi ya waziri mkuu kama tulivyotoa kwenye tamko na pia akateua waziri mwenye asili ya ulemavu (dr. Abdallah posy) na makatibu wa wizara wawili wenye ulemavu akiwemo mwanasiasa Amon Mpanju ili kushiriki kupika chakula cha walemavu. Hakika baada ya uteuzi huu, jamii ya qatu wenye walemavu tulianza kuona nuru na kuona matumaini ya kula chakula tulichoshiriki kukipika na kukiandaa mezani. Nampongeza sana Raisi kwa moyo huu wa kujali makundi manyonge katika jamii(Mungu azidi kumpa afya tele na azidi kutetea wanyonge kama anavyofanya sasa)

TATIZO NI NINI?????

Kwa mtazamo wangu, bado naona hakuna mabadiliko chanya yanayoletwa na wizara hii hasa kutoka kwa waziri husika Mh.Posy. Bado mifumo ya unyonyaji imeendelea kuwepo kwenye vyama vya watu wenye ulemavu, bado uchumi umezidi kudorora kwa watu wenye ulemavu, bado Elimu imekua duni na garama kwa watu wenye ulemavu, Bado siasa haiwatambui watu wenye ulemavu kwa vitendo, Bado sheria No 10 ya watu wenye ulemavu imewekwa kando, Bado ajiri imekuwa ngumu na ya kubagua watu wenye ulemavu na bado huduma bora imekuwa ni kitendawili kwa watu wenye ulemavu.

Je ni nani wa kututetea? Ni nani wa kutusemea kama sio Mh. Posy na wenzake akina stella ikupa, Dr. Macha, Amina Mollel, Amon Mpanju na wengine walio katika kundi hili?. Ni nani wa kulaumiwa ikiwa JPM ametupa nafasi kupitia hawa wenzetu alafu wamekaa kimya? Ni nani wa kuonesha mfano na kuaminisha jamii juu ya uwezo wetu kama sio akina Posy, Mpanju, macha, stella na wenzake? Ni nani wa kupiga kelele juu ya mateso na manyanyaso wanayoyapata wafanyabiashara walemavu wa Tanzania kama sio akina Mh. Posy, Mpanju na wenzake waliopata fursa? Ni nani wa kutuunganisha watu wenye ulemavu na kupata fursa za uchumi na siasa kama sio hawa walio teuliwa na JPM? Mbona wamejisahau utafikiri hawajatoka katika kundi hili? Au wanadhani fursa waliyopata ni kwaajili yao peke yao? Au ndo kusema ni aibu na dhihaka kuwa mlemavu na kutetea jamiiyako? Mbona kasi ya JPM inawaacha mbali? Tatizo ni nini?

Tulikaa kimya na kuwapa ushirikiano ili kuona matunda ya kushirikishwa katika kupika chakula lakini inakaribia mwaka sasa hatuoni kama chakula mnachotupikia ni kizuri…

Tafakarini na chukueni Hatua…. 

Tafadhali, naomba ifahamike yakuwa hii article iliandikwa wiki mbili zilizopita wakati Dr. Posy akiwa bado ni Waziri. Lakini sasa nafasi yake ipo wazi!

“Sometimes I really wonder!”- Sandra Mushi

Sometimes I really wonder! How we can just wake up and pull ‘sherias’ out of our hats. Sasa ati no spot lights, no fog lights and no tints …

How about you install street lights on ALL streets and actually have them ON and working; and how about having proper and working security measures including when I come report a theft, you actually attend to it and FOLLOW it up!  Instead of asking for ‘chai’ na ‘nauli’ kila kukichwa.

Those lights are our safety so I don’t have to worry about driving into a bridge on a dark night.  They are my safety so I can see clearly on a rainy day.  They are my safety so I can see that drunkard staggering from a far even before I get to that corner.

Those tints are our safety so I don’t have my windows broken as I am sitting in a meeting simply because the street boy saw my gym bag on the back seat.  They are my safety so when they want to follow me home they are not sure who is in the car.  They are my safety so that conniving motor cyclist does not see that its a lone woman driving.

Hembu do your due diligence basi and assure us of our safety before you mercilessly start imposing this ‘out of the hat’ sheria on us.

You do your part and we will humbly oblige and do ours.

Wametugusa sana; watakumbukwa daima!

Rais Obama anaweza asiwe the best President in American history. Lakini ni ukweli usio pingika kuwa they were the best 1st family ever!!……..Wamegusa miyoyo yetu, wamebadilisha mitizamo ya familia nyingi kwa kuonyesha jinsi gani family should look like! Mr and Mrs Obama wameonyesha mfano bora wa jinsi gani couple  should respect and support each other for the goodness of the family and your country! Wamekuwa mfano mwema wa wazazi jinsi ya kulea humble children pamoja na kuwa na access to everything they wanted! Wamegusa nafsi za watu wengi sana na kuacha their own legacy kwenye hii dunia! Tutawakumbuka siku zote, Mungu azidi wabariki!

Rwanda has started legislative process to Make Swahili one of the official languages!

Hon. ShyRose Bhanji

Presenting the Motion to congratulate Rwanda for Starting a legislative process to make Kiswahili one of the official languages in Rwanda. This is highly commendable move and should be strongly supported by all stakeholders who have EAC integration at heart. #Kiswahili #OnePeopleOneDestiny …. #Nikiwasilisha Hoja bungeni ya kuipongeza Rwanda kwa Kuanza mchakato wa kutunga sheria ya kukifanya Kiswahili kuwa moja ya lugha rasmi nchini Rwanda. Hatua hii inahitaji kuungwa mkono na wadau wote ambao ni waumini wa mtangamano wa Jumuiya ya Afrika Mashariki. #UmojaWetuNiNguzoYetu

#EalaInKampala

HUYU ANA MOYO MKUU…..by Peter Sarungi

Na Peter Sarungi (Next Speaker)Kwa sasa ni nadra sana kupata binadamu walio umbwa na Moyo Mkuu, moyo unao weza kuhimili shida, kejeli, dharau, matusi ma vikwazo mbalimbali vyenye lengo la kulainisha Moyo. Mh. Lowasa Edward alikumbwa na kashfa akiwa CCM tena Waziri Mkuu, akasemwa na kutukanwa na viongozi, wanachama na wapenzi wa chama kikuu cha upinzani Chadema Tanzania, huku akiitwa Fisadi nchi nzima… Alikaa kimya bila kujibu.

Alipo hama CCM kwenda CDM, CCM walimuona kama msaliti ingawa kwa CDM alibadilika na kuwa Malaika. Bado aliendelea kutukanwa, kudharauliwa na hata kuombewa mabaya na viongozi, wanachama na wapenzi wa chama tawala kipindi cha uchaguzi 2015… Alikaa kimya bila kujibu.

Pamoja na yote hayo, bado ameendelea kuwa na Moyo Mkuu kwa nchi yake. Huyu namfananisha na Mh. Raila Odinga wa Kenya na Mh. Kiiza Besige wa Uganda kutokana vikwazo wanavyopitia. Mungu awatimizie haja ya mioyo yao.

Tujifunze kitu hapo, unajifunza nini?

MH. LOWASSA ANAIJUA SIASA YA TANZANIA-Peter Sarungi

Peter Sarungi a.k.a Next Speaker a.k.a Baba Pilato

Siasa za Tanzania bado hazieleweki kwa wananchi wengi na mimi nikiwemo. Wengine wanaiita siasa maji taka, siasa za kujipendekeza, siasa za mafigisu, siasa za mamluki na usaliti, siasa za propaganda, siasa za nguvu ya umma na nguvu ya dola, siasa za uongo, siasa za kidiplomasia, siasa za matukio, siasa za maigizo, siasa za maonyesho na mimi kwa sasa naziita siasa za Mwendo Kasi.Kwa Tanzania, ni Mh. Lowasa Edward pekee anaye jua siasa za nchi, anayeweza kubadili njano kuwa nyekundu, anayeweza kupanga na kupangua, anayeweza kubadilika kutokana na mazingira, anayeweza kumpenda adui yake hata kwa unafiki, anayeweza kubadili msimamo wa mpinzani wake, anayeweza kumbadili mpinzani kuwa mfuasi wake, anayeweza kupiga ngoma kisha serikali ikacheza, anayeweza kuwa na chama ndani ya chama, anayeweza kusababisha mafuriko ama hata kuyatengeneza, anayeweza kusababisha taharuki mtaani anapo onekana nahata kuwapa hofu watawala.

Kumekuwepo na kauli nyingi za kukubali ama kukataa uwepo wa njaa na uhaba wa chakula kwa muda wa zaidi ya wiki bila kuwepo kwa solution. Lakini Mh. Lowassa alipokuja na kauli ya kuwa na nia ya kutafuta chakula kwa ajili ya wahanga kwa madai kuwa Mkuu kakataa kutoa chakula kwa wahanga ikiwa ni sehemu ya kuleta suluisho la tatizo, jana serikali ikajibu mapigo kwa kusema ita sambaza chakula na ina hifadhi tosha ya chakula.

Viongozi kama akina Mh. Lowassa ni muhimu sana kwa jamii yetu hata kama wasipo weza kutawala nchi lakini uwepo wao na uwezo wao katika siasa za nchi intosha kufanya mabadiliko nje ya ya mfumo rasmi na kuleta matokeo chanya ya maendeleo..

Tutafakari kwa matendo bila hisia za vyama.

Ubaguzi wa watu wenye ulemavu nani alaumiwe na nini kifanyike?!

Hongera sana shule direct kwa jitihada zenu za kuokoa maisha ya watoto katika nyanja ya elimu!……Binafsi najiuliza hivi nani wakulaumiwa na nini kifanyike juu ya watu wenye ulemavu?! Mimi nasema ni ubaguzi wa wazi wazi kwa watu hawa na jamii imelifumbia macho! …….Miaka ya nyuma tulisema kuwa watu hawana uwelewa na leo hii je tunasemaje?! Shule moja ya secondary ya viziwi tena ni private?! Majengo mengi yanajengwa bila kujali kuwa tunao walemavu katika jamii yetu!! Majengo na maeneo mengi hakuna parking za magari specific kwa walemavu! Makanisa mengi sana hayana wakalimani wa viziwi! n.k………Huu ubaguzi ni mpaka lini? Nani wakulaumiwa? Na nini kifanyike? ……..Tafakari na chukua hatua!

MATOKEO YA KELELE ZA #BringBackBenAlive NI YAPI NA YAMEISHIA WAPI?- Peter Sarungi

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Watu wa Makabila yanayo patikana mkoa wa Mara (Kwetu Pazuri) wana desturi ya kuwa jasiri, wakweli na wenye uwezo wa kusimamia jambo analo liamini. Lakini huku jijini Dar tulipokuja kutafuta maisha, mambo yake yanaendeshwa kwa usanii, unafiki, uoga, dilli, uongo na kutafuta kicky pasipo sababu ya msingi.

Uozo huu umeingia hadi kwenye siasa kiasi kwamba huwezi kutofautisha siasa za chama tawala na zile za Upinzani yaani wote wamekuwa wafuasi wa mambo hayo ya jijini.

Wahusika Tuelezeni, kwanini mpo kimya kwa swala mlilo lianzisha? na mtuambie matokeo chanya ya #Bring_Back_Ben_Alive ?

Msianzishe kampeni katika mitandao halafu mkaziacha katikati bila kujua hatima yake, What if Ben amedhurika? Kelele zenu na ukimya wa Ghafla utakuwa umemsaidia nini Ben? Tafakari, Chukua hatua… 

SIASA NA DEMOKRASIA YA KENYA….. TUNAJIFUNZA NINI KATIKA MIFUMO YAO??-Peter Sarungi

 

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Taarifa zinaonesha kuwa kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati, Jamhuri ya watu wa Kenya ndio nchi ambayo ina mifumo inayo tekeleza Siasa huru na Demokrasia ya kiwango kizuri ukilinganishs na nchi zingine katika ukanda huo. Pamoja na kuwepo kwa Siasa za Ukanda na Makabila kwa muda mrefu lakini bado siasa zao zimekuwa ni za mfano kupita zetu za Tanzania.

Je, tunajifunza nini? kuna lipi unalo lijua kuhusu mfumo wao ambacho kwetu hakipo? Je, wananchi wao na wana siasa wao wana tabia gani ambazo ni tofauti na kwetu Tanzania? Saidia kujadili ili tupate Ufahamu.

KILA MTU ABEBE MZIGO WAKE….. LASIVYO, MWAFA! -Peter Sarungi

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Naunga mkono kauli ya Mkuu wa Kaya kwa watani (Wajukuu) wangu wa mkoa wa kagera lakini naunga mkono kwa utani maana tulilia pamoja wakati wa msiba sasa ni lazima niwatanie kidogo kipindi hiki cha matanga.

Naamini hata Mkuu wa Kaya alikuwa anawatania ili kuwarudisha katika hali ya Kazi Tu ingawa bado sijafahamu kama Mkuu wa Kaya ni mtani wenu kikabila au kisiasa, naendelea kufanya utafiti kwa kina.

Huu ndio utani wa kisiasa, wanasiasa wana tabia ya kubadilika badilika kama walivyo wananchi wenyewe (No guarantee at all)Ni Utani tu kwa Wajukuu zangu, dont take seriousl

SABABU ZA UGIZA WA AFRIKA- Peter Sarungi

Ptr 1. DINI/IMANI YA WAAFRIKA NI IPI..?

Sababu ya kujiuliza maswali hayo ya juu ni kutokana na udhaifu, udumazi na ufinyu wa fikra zetu sisi watu weusi katika kuendeleza jamii zetu na bara letu. Kuna msemo inasema kuwa “Ukubwa wa matatizo ndio kipimo cha akili” na katika kutafakari kwangu nikakutana na falsafa ya mwimbaji hodari wa Tanzania Marehemu Remy Ongala (R.I.P) Alipoimba kilio cha samaki (Live perfomance). Wimbo wake umeniachia maswali mengi ya kutafuta majibu na kumepanua uwezo wa kufikiri zaidi tena tofauti ili tu nipate majibu.

Swali la kwanza: ni ipi Imani/ Dini ya watu weusi? Kabla ya kupata jibu hilo ni lazima tujue kuwa Imani ni hali ya kuwa na uhakika na vitu/ jambo lisilokuwa bayana yaani kuwa na uhakika na jambo usilolijua uwepo wake. Imani huponya, uhadhibu, huelekeza na hutatua matatizo katika jamii. Jamii ni lazima iwe na imani katika kujibu swali kuu la maisha baada ya kifo au kujibu matatizo yaliyoshindwa kuelezeka ama kutibika. Hivyo jamii nyingi zinataka kufanana katika imani ndani ya bara moja, mfano wazungu wanaamini katika kristo, wachina wana imani yao, wahindi wana imani yao, waarabu wana imani yao, wajamaica wana imani yao, wakorea wana imani yao na hata warusi wana imani yao. Na hizo ni imani zao ambazo hawaku iga kutoka katika jamii zingine bali zilibuniwa na wazee wa kale wa mwanzoni ili kujenga fikra za jamii zao kstika imani waliyoona inawafaa.

Je waafrika tulikuwa na imani ipi? maana imani ya ukristo na uislamu ni imani zilizoletwa kipindi cha ukoloni, ni imani tulizolazimishwa kupokea chini ya ukatili na utumwa wa kikoloni. kila mtu anajua athari za ukoloni, ukoloni ulisababisha tukawa wanyonge katika dunia, tukawa watumwa na wajenzi wa uchumi za wengine katika duni, tukalaani na kuacha mila&desturi na tamaduni zetu, tukapoteza imani zetu, tukadharau sayansi na teknologia zetu, tuacha mafundisho yetu, tukatupa fikra zetu na kununua elimu ya wakoloni, tukaacha majina yetu na kukumbatia majine ya wenzetu na tukaacha mitindo ya maisha yetu tukaegemea mitindi ya wakoloni. Ukoloni ulipoteza dira ya waafrika, ukapandikiza mbegu ya imani ngeni, mbegu ya elimu yao, mbegu ya kuiga kila kitu chao na kukiona ni kizuri, Mbegu ya kujidharau, kujinyenyekeza, kujipendekeza na kujishusha, Mbegu ya kushindwa kufikiri tofauti na mkoloni yaani waafrika tuna amini mkoloni ndio kila kitu hata maandiko ya imani zao zinatuaminisha kuwa wao ni wateule na lugha zao ndizo teule.

Waafrika tuliweza kumfukuza mkoloni na kupata uhuru kutokana na wazee wetu walio pambana kwa njia zote hadi za imani zetu kipindi hicho mfano vita ya majimaji. Pamoja na kumwondoa mkoloni lakini mkoloni aliweza kuacha mbegu zake za Imani, mafundisho na elimu katika lugha yao. Hizi mbegu ndizo ambazo zinasumbua sana kwa mtu mweusi kuwa huru katika kufikiri. Fikra zetu zimewekewa ukomo wa kufikiri katika kutatua matatizo ya jamii zetu. 

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

#MyTake

Waafrika hatupendani kwa sababu ya mbegu ya mkoloni, IQ za kufikiri ni ndogo kwa sababu ya mbegu ya mkoloni, tumekuwa wanafiki na waongo kwa wana nchi kwa sababu ya mbegu ya mkoloni, tumekuwa wabinafsi na wasaliti katika siasa zetu kwa sababu ya mbegu ya mkoloni, tumekosa dira na hata malengo thabiti ya miaka 30 ijayo kwa sababu ya mbegu ya mkoloni.

Tafakari na uchukue hatua

TANZANIA INAHITAJI MIFUMO IMARA KULIKO VIONGOZI IMARA- Peter Sarungi

Bara la Africa ni moja kati bara lililo wahi kutawaliwa na viongozi washupavu, majasiri na imara kwa muda mrefu bila mafanikio. Historia imeshuhudia viongozi jasiri na imara kama Mandela, Kwame Nkuruma, Gadafi, Idd Amini, Nyerere, Samwel Doo, Samora, Patrick Lumumba, Mugabe, Kawawa Simba wa vita, Mobutu Seseko, Savimbi, Karume, Kabila sr, Kenyatta sr, Obotte, Kagame, Satta na wengine wengi ambao walitikisa Afrika wakati wa utawala wao na wengine wapo mpaka sasa. Historia inaonesha kuwa watawala hawa walikuwa Imara ingawa wengine walitawala kwa mabavu, vita, mauaji ya alaiki na wengi walitawala nje ya mfumo wa demokrasia kupitia chama kimoja. Pamoja na uimara na ujasiri wa hawa viongozi bado Afrika imeendelea kulia na kuteseka na umasikini, maradhi na ujinga kwa viongozi na wananchi wao, Bado Afrika imeendelea kumwaga damu yao wenyewe kwa wenyewe, Bado Afrika imeendelea kuwa dhaifu kutokana na utengano dhidi ya mataifa ya magharibi na Asia, Bado Afrika imeendelea kuwa tegemezi katika afya, elimu, teknolojia, biashara, uchumi, utawala na mengi ambayo yanatoka nje ya afrika.

Tanzania tumebahatika kupata kiongozi imara, shupavu, jasiri na mwenye msimamo. Kiongozi anayeweza kufanya maamuzi na akasimamia maamuzi yake bila kutetereka hata kama yatakuwa na makosa, kiongozi anayethubutu kupita viongozi watatu waliopita. Huyu ni Dr John Pombe Magufuli (Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania), Mimi binafsi namkubali sana Mhe. JPM ingawa ana baadhi ya mapungufu kama binadamu lakini bado ameonesha kuwa yeye ni imara. JPM kwa sasa amekuwa ni gumzo kwa bara letu la Afrika na dunia kwa ujumla. Nimepata kuona taarifa nyingi sana kutoka nchi zingine Afrika na Duniani kuhusu uimara wa JPM na hata mwaka uliopita JPM amekuwa ni Raisi wa Afrika aliyejadiliwa na kupata umaarufu mkubwa kuliko maraisi wengine. Hii ni tunu na sifa nzuri kwa utawala wake.

Pamoja Uimara wa JPM, Bado Tanzania tumendelea kulia kilio cha uchumi duni, afya mbovu, elimu duni, demokrasia na udikteta, uhuru wa kujieleza, upatikanaji wa haki mahakamani, utawala bora, utumiaji wa nguvu na vitisho, wajibu wa bunge na wabunge, uelewa wa haki na wajibu wa raia, uchaguzi huru na wa haki, uzalendo na utaifa. Haya ni mambo yanayo endelea kurudisha nyuma maendelea ya taifa letu kwa kasi kubwa sana.

Hii ina sababishwa na Mifumo mibovu, kandamizi na yenye mianya ya kutenda maovu. Mifumo inatoa nguvu nyingi kwa kiongozi mmoja bila kuwa na njia za kudhibiti akikosea, mifumo inayo elekeza kiongozi kuwa juu ya sheria kwa kauli na matendo, mifumo inayo weza kuyumbishwa mda wowote bila kujali athari, mifumo inayo unganisha chama na serikali kuwa kitu kimoja, Mifumo tegemezi katika taasisi za nchi.

Hii mifumo mibovu ndio chanzo cha wana nchi kuendelea kulia vilia vilivyo zoeleka. Kwa aina ya mifumo hii, hata aje malaika kutoka mbinguni kuja kutawala bila kubadili ni sawa na kutwanga maji ndani ya kinu. Tunaweza kuwa viongozi imara kam JPM hata 50 lakini kwa mifumo yetu bado tutaendelea kuumia kila siku.

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

#MyTake

Bora kuwa na Mifumo imara itakayo weza kulinda maslahi ya nchi na wananchi wake hata kama kiongozi wa mfumo atakuwa legelege, bado mfumo utamnyoosha na kumlinda kuliko kuwa na kiongozi imara ndani ya mifumo dhaifu, maana siku kiongozi imara akibadilika basi nchi itarudi nyuma tena.

Mhe. JPM ni kiongozi Imara lakini mifumo ya serikali na taasisi zake bado zinaonesha udhaifu mkubwa na ndio maana utumbuaji ni mkubwa mno, Yaani kila kiongozi anayeguswa katika taasisi ni kama ameoza kwa rushwa, uzembe, uvivu na mengine mengi.

Tunahitaji mifumo imara kama ya jirani zetu Kenya na Zambia wanaoweza kusimamia matakwa ya wana nchi kisheria bila kutetereka.

HUU NI MWAKA WA KUONGEZA NA KUTENGENEZA MAHUSIANO MAZURI NA WANA WA NCHI WA TANZANIA- Peter Sarungi

Kila mwaka una lengo kuu endelevu linalotimizwa kuanzia mwanzo wa mwaka hadi mwisho wa mwaka. Kwa mimi Simba wa Utegi na Babu wa Kagera nimeamua kuweka mwaka huu 2017 kuwa mwaka wa kutengeneza mahusiano ya kijamii, kisiasa na kiuchumi na wananchi. Mahusiano yanatengenezwa kwa kupitia mawasiliano.

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Unaweza kunipata kupitia:

1. Public No & Watsup No. +255 713 037 798

2. Facebook ID : Peter sarungi

3. Instagram ID : peter.sarungi

4. E. Mail : [email protected]

5. Tweeter ID : @psarungi

6. Post Code : 9291- Dar es Salaam

7. Physical Adress : Chanika Village – Dar

Hizo ni baadhi ya njia unazoweza kunipata kupitia mawasiliano yangu rasmi kama Next Speaker mwaka 20…

Karibu tuwasiliane katika kujenga nchi ili hata watoto,wajukuu,vitukuu na vizazi vijavyo vije vipate kula matunda yetu

Imetolewa na:

Idara ya Habari na Maelezo ya Peter Sarungi

Raisi-Jukwaa la Walemavu Tz, Next Speaker. Asante sana kaka yangu mimi pia nitakuwa mmoja wa wafuasi wako!

2016 ULIKUWA NI MWAKA MGUMU SANA ULIOKUWA NA MABADILIKO YA GHAFLA YA JPM by Peter Sarungi

Ni desturi yangu kutathmini mwaka unapofikia mwisho. Nianze kwa kuimba wimbo wangu kwa Tanzania.

“Tanzania eeee, Nakupenda sana x2”

“Hata kama nikilala porini lakini ni ndani ya Tanzania bado nitajivunia”

“Najua wengi wanakutamani ingawa uchaguzi wako bado upo mashakani”

“Nakuaga mwaka kwa maumivu ingawa ni maumivu ya mpito”

“Naamini sasa ni muda wa kula matunda ndani ya mwaka unao anza”

Kwa kifupi mwaka 2016 ulikuwa ni mwaka mchungu na mgumu kwa watanzania masikini na wanyonge wasio jua leo yao itakwishaje na kesho itaanzaje baada ya kuletewa utaratibu wa kufanya kazi kabla ya kula ingawa kazi zenyewe hazipatikani na zingine zinezuiwa kupisha uchunguzi wa HEWA.

Ni mwaka uliokuwa mgumu kwa watumishi wa umma baada ya kulazimishwa mabadiliko makubwa ya utumishi wa serikali na hasa baada ya kuziba mianya mikubwa ya ubadhilifu wa pesa za umma pamoja na kuziba hadi vitundu vidogo vya posho kwaajili ua motisha ya watumishi.

Ni mwaka mgumu kwa wana siasa feki walio ingia kwenye siasa kwa maslahi ya kutajirika. kuna wabunge na madiwani walio tumia nguvu nyingi kupata uongozi, kwa sasa wanajuta ni kwanini walichagua siasa na wengine wana lia hadharani bila kuficha. Lakini pia ni Mwaka mgumu sana kwa wapenda mabadiliko, wana harakati na wapenda demokrasia baada ya kusitishwa kwa shuguli zao za siasa za majukwaa na harakati zingine kama maandamano.

Ni mwaka mgumu sana kwa uchumi wa taifa na wananchi hasa baada ya kutanda kwa UKATA wa hali ya juu sana. imefika mahala ambapo heshima ya ndoa imerejea, heshima ya mshahara imerejea, heshima ya mlo imerejea na hata heshima ya kazi imerejea. Ukuaji wa Uchumi wa nchi kwa mwaka huu nimeufananisha kuwa na kasi  kama ya konokono dhidi ya farasi. Naamini imekuwa hivyo kwa sababu JPM ametumia mwaka huu kuweka misingi sawa, tuangalie mwaka 2017

Umekuwa ni mwaka wa Matamko mbalimbali machungu kwa wanchi katika sekta mbalimbali. Tumepata matamko mengi ya wakuu wa mikoa mbalimbali hasa Dar, matamko ya wakuu katika Mfumo wa Elimu, Afya, Ardhi, Kodi, Usafirishaji, kilimo, Ufugaji, bomoa bomoa, Madini, Umeme na maeneo mengine yaliyo acha alama ya maumivu kwa wananchi.

Tumeshuhudia hadithi za mfalme Juha na simuzili za kusadikika kutoka kwa Polepole, Ben sa8, Yericko nyerere, Faru John, Magoiga, Menuka, Malisa na wengine wengi waliokuwa mstari wa mbele kutupigia hadithi nzuri kwa kila upande kwa mwaka mzima.

Ulikuwa ni mwaka mchungu sana kwa watumishi wa umma zaidi ya 300 walio tumbuliwa mwaka huu kutokana sababu mbalimbali kupitia kauli mbiu ya KUTUMBUA inayoongozwa na mkuu wa kaya akisaidiwa na wasaidizi wake kila idara.

Ulikuwa ni mwaka mchungu sana kwa wafanya biashara za utalii, mahoteli, mabasi, nguo, bar, ujenzi, usafirishaji wa mizigo, wamachinga, madalali, vyuo na mashule, biashara za mitaji na biashara za Bank. Maana tumeshuhudia taatifa za kufilisika kwa baadhi ya biashara hizo kwa sababu ya mdororo wa uchumi. Tusife moyo, mwaka ulikuwa ni wa mapito.  

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

#MyTake

Mwaka umekwisha na changamoto zake, ikiwa mwaka unao anza utakuwa na changamoto hizi basi tujue ni sisi wenyewe tutakuwa tumezitengeneza. Huu ulikuwa ni mwaka wa majaribio ya mabadiliko makubwa, naamini tutajipanga sasa kukubali na kukabiliana na magumu yanayotokana na Mabadiliko haya kutoka kwa Mkuu wa Kaya…….Mwaka 2017 ukiwa mchungu tena kwako basi jua ni kati ya wewe au serikali kuna mmoja atakuwa ni mzembe wa mabadiliko.

Kumbe na huyu ni shemeji..!

Kumbe na huyu kimbau mbau mwiko wa pilau ni shemeji yangu ?? Yani wewe Max ndio unasumbua kichwa ya baba yangu Dr Magufuli na #FreedomOfSpeech? Utafikiri unaijua vile ??? Kama  kweli wewe unapigania hiyo “huru ya kujielesa”  (in Luo’s voice)   mbona siku ile yule “mwanaharakati” nyenzio alianika wewe na familia yako aka bandika na picha ya mutoto yako kwa mtandao yake ulipiga magoti yako kwa nguvu sana ukaomba msamaha akutoe kwa blog yake nakuwa hauto rudia tena kumuongelea??? Kwani hile haikuwa #FreedomOfSpeech ??  Au nyie hii ya kwenu  ina “discrimination”?? ????? •••••• Anyway pole kwayalio kukuta binafsi sipendi kuongelea mambo ambayo yapo Mahakamani kwani tuache Mahakama zifanye kazi zake bila kuingiliwa na mtu yoyote kwa uhuru na uwazi! Lakini hata hivyo naamini haya yataisha na punde utakuwa huru! And you and your #FreedomOfSpeech can go away ???

 

“It’s time to change our political culture”

Sent as received. However, I still have so many questions and am yet to get answers. So many sayings come to my mind:
1. If it’s too good to be true probably it is not
2. There is no free lunch
3. Not every kiss represents love, think of Judas when he betrayed Jesus
4. Change begins with me
5. If I can dream it I can achieve it

The list of thoughts is endless. Looking forward to reading different perspectives and probably solutions

Every Patriot in Africa should read this article; penned by US-based Zambian media practitioner and author. He is a PhD candidate with a B.A. in Mass Communication and Journalism, and an M.A. in History.

They call the Third World the lazy man’s purview; the sluggishly slothful and languorous prefecture.

In this realm people are sleepy, dreamy, torpid, lethargic, and therefore indigent—totally penniless, needy, destitute, poverty-stricken, disfavored, and impoverished. In this demesne, as they call it, there are hardly any discoveries, inventions, and innovations.

Africa is the trailblazer. Some still call it “the dark continent” for the light that flickers under the tunnel is not that of hope, but an approaching train.

And because countless keep waiting in the way of the train, millions die and many more remain decapitated by the day.

“It’s amazing how you all sit there and watch yourselves die,” the man next to me said. “Get up and do something about it.

When I first discovered I was going to spend my New Year’s Eve next to him on a non-stop JetBlue flight from Los Angeles to Boston I was angst-ridden.
I associate marble-shaven Caucasians with iconoclastic skin-heads, most of who are racist.

“My name is Walter,” he extended his hand as soon as I settled in my seat.

I told him mine with a precautions smile.

“Where are you from?” he asked.

“Zambia.”

“Zambia!” he exclaimed, “Kaunda’s country.”

“Yes,” I said, “Now Sata’s.”

“But of course,” he responded. “You just elected King Cobra as your president.”

My face lit up at the mention of Sata’s moniker. Walter smiled, and in those cold eyes I saw an amenable fellow, one of those American highbrows who shuttle between Africa and the U.S.

“I spent three years in Zambia in the 1980s,” he continued. “I wined and dined with Luke Mwananshiku, Willa Mungomba, Dr. Siteke Mwale, and many other highly intelligent Zambians.” He lowered his voice. “I was part of the IMF group that came to rip you guys off.” He smirked. “Your government put me in a million dollar mansion overlooking a shanty called Kalingalinga.

From my patio I saw it all—the rich and the poor, the ailing, the dead, and the healthy.”
“Are you still with the IMF?” I asked.

“I have since moved to yet another group with similar intentions. In the next few months my colleagues and I will be in Kenya to hypnotize the Raisi

I work for the broker that has acquired a chunk of your debt. Your government owes not the World Bank, but us millions of dollars.

We’ll be in Lusaka to offer your president a couple of millions and fly back with a check twenty times greater.”

“No, you won’t,” I said. “King Cobra is incorruptible. He is …”

He was laughing. “Says who? Give me an African president, just one, who has not fallen for the carrot and stick.”

Quett Masire’s name popped up. “Oh, him, well, we never got to him because he turned down the IMF and the World Bank. It was perhaps the smartest thing for him to do.”

At midnight we were airborne. The captain wished us a happy 2015 and urged us to watch the fireworks across Los Angeles.

“Isn’t that beautiful,” Walter said looking down.

From my middle seat, I took a glance and nodded admirably.

“That’s white man’s country,” he said. “We came here on Mayflower and turned Indian land into a paradise and now the most powerful nation on earth.
We discovered the bulb, and built this aircraft to fly us to pleasure resorts like Lake Zambia or lake Kenya .
I grinned. “There is no Lake Zambia or lake Kenya
He curled his lips into a smug smile. “That’s what we call your countries . You guys are as stagnant as the water in the lake.

We come in with our large boats and fish your minerals and your wildlife and leave morsels—crumbs. That’s your staple food, crumbs.
That corn-meal you eat, that’s crumbs, the small Tilapia fish you call Kapenta / omena are crumbs.
We the Bwanas (whites) take the catfish.
I am the “Bwana” and you are the “mtu”.
I get what I want and you get what you deserve, crumbs. That’s what lazy people get—Zambians, Kenyans , other Africans, the entire Third World.”

The smile vanished from my face.
“I see you are getting pissed off,” Walter said and lowered his voice.

“You are thinking this Bwana is a racist.
That’s how most Zambians , Kenyans respond when I tell them the truth.
They go ballistic.
Okay. Let’s for a moment put our skin pigmentations, this black and white crap, aside.

Tell me, my friend, what is the difference between you and me?”

I said
“There’s no difference.”

“Absolutely none,” he exclaimed. “Scientists in the Human Genome Project have proved that. It took them thirteen years to determine the complete sequence of the three billion DNA subunits.
After they were all done it was clear that 99.9% nucleotide bases were exactly the same in you and me.
We are the same people. All white, Asian, Latino, and black people on this aircraft are the same.”

I gladly nodded.

“And yet I feel superior,” he smiled fatalistically. “Every white person on this plane feels superior to a black person.
The white guy who picks up garbage, the homeless white trash on drugs, feels superior to you no matter his status or education.
I can pick up a nincompoop from the New York streets, clean him up, and take him to Lusaka and you all be crowding around him chanting muzungu, muzungu and yet he’s a riffraff.
Tell me why my angry friend.”

For a moment I was wordless.

“Please don’t blame it on slavery like the African Americans do or colonialism, or some psychological impact or some kind of stigmatization.
And don’t give me the brainwash poppycock. Give me a better answer.”

I was thinking.

He continued. “Excuse what I am about to say. Please do not take offense.”
I felt a slap of blood rush to my head and prepared for the worst.

“You my friend flying with me and all your kind are lazy,” he said. “When you rest your head on the pillow you don’t dream big.

You and other so-called African intellectuals are damn lazy, each one of you only going for leadership; just to fill their own stomach and steal from poor.

It is you, and not those poor starving people, who is the reason Africa is in such a deplorable state.”

“That’s not a nice thing to say,” I protested.

He was implacable. “Oh yes it is and I will say it again, you are lazy in your minds.

Poor and uneducated Africans are the most hardworking people on earth. I saw them in the Lusaka markets and on the street of Nairobi selling merchandise. I saw them in villages toiling away.

I saw women on Kafue Road crushing stones for sell and I wept. I said to myself where are the Zambian intellectuals? And on kenya l saw women as bricklayers. Where are these intellectual men ?

Are the Zambian or Kenyans engineers so imperceptive they cannot invent a simple stone crusher, or a simple water filter to purify well water for those poor villagers? Or sort out the drainage system to make Biogas or rivers purification systems.

Are you telling me that after thirty-seven years or more of independence your university school of engineering has not produced a scientist or an engineer who can make simple small machines for mass use?

What is the school there for?”

I held my breath.

“Do you know where I found your intellectuals? They were in bars quaffing.
I saw with my own eyes a bunch of alcoholic graduates. Calling themselves policy makers

Zambian , Kenyans , other African intellectuals work from eight to five and spend the evening drinking. We don’t. We reserve the evening for brainstorming.”

He looked me in the eye.

“And you flying to Boston and all of you Africans in the Diaspora are just as lazy and apathetic to their country.

You don’t care about your country and yet your very own parents, brothers and sisters live there.
Many have died or are dying of neglect by you as democratic government .
They are dying of AIDS because you cannot come up with your own preventive measures. To much immoral .

You are here calling yourselves graduates, researchers and scientists and are fast at articulating your credentials once asked—oh, I have a PhD in this and that so what?
What next? Handouts from IMF ? Then repay?

I was deflated.
“Wake up you all!” he exclaimed, attracting the attention of nearby passengers. “You should be busy lifting ideas, formulae, recipes, and diagrams from American manufacturing factories and sending them to your own factories.

All those dissertation papers you compile should be your country’s treasure. Why do you think the Asians are a force to reckon with? They stole our ideas and turned them into their own. Look at Japan, China, India, just look at them.”

He paused. “The Bwana has spoken,” he said and grinned.

“As long as you are dependent on my plane, I shall feel superior and you my friend shall remain inferior, how about that?
The Chinese, Japanese, Indians, even Latinos are a notch better.
You Africans are at the bottom of the totem pole.”

He tempered his voice. “Get over this white skin syndrome and begin to feel confident.
Become innovative and make your own stuff for God’s sake.”

At 8 a.m. the plane touched down at Boston’s Logan International Airport. Walter reached for my hand.

“I know I was too strong, but I don’t give it a damn. I have been to Zambia , Kenya , other African countries and have seen too much poverty.”

He pulled out a piece of paper and scribbled something. “Here, read this. It was written by a friend.”

He had written only the title: “Lords of Poverty.”

Thunderstruck, I had a sinking feeling.

I watched Walter walk through the airport doors to a waiting car. He had left a huge dust devil twirling in my mind, stirring

I remembered some who have since passed—how they got the highest grades in mathematics and the sciences and attained the highest education on the planet.

They had been to Harvard, Oxford, Yale, Massachusetts Institute of Technology (MIT), only to leave us with not a single invention or discovery.

I knew some by name and drunk with them at the Lusaka Playhouse and intercontinental hotel, safari park Kenya and Central Sports in Lusaka

Walter is right. It is true that since independence we have failed to nurture creativity and collective orientations.

We as a nation lack a workhorse mentality and behave like 13 million civil servants dependent on a government pay cheque.

We believe that development is generated 8-to-5 behind a desk wearing a tie with our degrees hanging on the wall.

Such a working environment does not offer the opportunity for fellowship, the excitement of competition, and the spectacle of innovative rituals.

But the intelligentsia is not solely, or even mainly, to blame.

The larger failure is due to political circumstances.
Knowing well that King Cobra , Kenyatta, and others will not embody innovation at Walter’s level let’s begin to look for a technologically active-positive leader who can succeed them after a term or two.

That way we can make our own stone crushers, water filters, water pumps, razor blades, and harvesters. Or dig our own boreholes without IMF involve.

Let’s dream big and make tractors, cars, and planes,
or, like Walter said, forever remain inferior…

A fundamental transformation of our country from what is essentially non-innovative to a strategic superior African country requires a bold risk-taking educated leader with a triumphalist attitude and we have one in YOU.

Don’t be highly strung and feel insulted by Walter. It is like shooting the messenger.

Take a moment and think about our country.

Our journey from 1963 has been marked by tears. It has been an emotionally overwhelming experience.

Each one of us has lost a loved one to poverty, hunger, and disease.

The number of graves is catching up with the population.

It’s time to change our political culture. It’s time for Zambian , Kenyans and other Africans intellectuals to cultivate an active-positive progressive movement that will change our lives forever.

Don’t be afraid or dispirited, rise to the challenge and salvage the remaining….

Use Africa to substitute Zambia/Zambian in the article and it holds true for all Africa/Africans.

Fact or fiction?
Just ponder.

Hongera sana mama Mboni Masimba!

screenshot_2016-12-17-20-34-28-1screenshot_2016-12-17-20-33-40-1screenshot_2016-12-17-20-33-34-1

screenshot_2016-12-17-20-33-56-1Hongera sanaaaaaa mama Mboni kwa kuonyesha mfano mwema siyo tu kwa  watoto wako na jamii inayo kuzunguka bali kwa Tanzania nzima. Ni mfano mzuri sana unaotia moyo kwa wengi! Well done mama!  ???? #Inawezekana  #ItBeginsWithYou

HONGERA SANA ANTON H. NGOLI

fb_img_1482025152919Hongera nyingi zikufikie mdogo wangu na Kiongozi mwenzangu wa Jukwaa La Watu Wenye Ulemavu Tanzania kwa kuhitimu masomo yako yaliyochukua miaka mitatu ukiwa chuo cha ununuzi na ugavi IPS. Najivunia sana kwa wewe kuwa mmoja kati ya vijana wengi nilikuwa nashauriana nao kipindi nipo IPS. Juhudi zako na uvumilivu wako katika kufuata ndoto yako ndio imekufikisha hapo ulipo. Kila safari ina changamoto na mafanikio, hivyo zidisha juhudi na nia katika kila step utakayo piga kuelekea katika mafanikio yako. Jamii ya watu wenye ulemavu kupitia bodi ya Jukwaa la Watu Wenye Ulemavu Tanzania ina imani na elimu yako pamoja na juhudi zako na tuna imani uta acha alama nzuri katika jukwaa kupitia utendaji wako kama Katibu Mkuu wa Jukwaa.

Mungu akupe maisha marefu yenye furaha, amani na upendo kwa watu wote.Tuendelee kutafuta Maarifa ili kupanua ufahamu wetu tulio pewa na Mungu

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!
Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Ni mimi kaka yako
P.L. Sarungi
Raisi wa Jukwaa La Watu Wenye Ulemavu Tz.

****fb_img_1477414420906-1Nami naomba nimpe pongezi zangu za dhati! Naomba ukatumie elimu uliyopata siyo tu kwa faida zako binafsi bali jamii inayo kuzunguka na taifa kwa ujumla! Hongera sana!

Dr. Mwele ni hazina ya Tanzania!

screenshot_2016-12-17-02-40-34-1Ngoja niende moja kwa moja kwa mada husika! Sina hakika nalo lakini inasemekana kuwa Dr. Mwele hakufuata “protocol” na ndio maana ametenguliwa nafasi yake!……Nakubali hilo ni kosa lakini si kosa la JINAI hivyo naamini bado Dr. Mwele anafasi kubwa sana ya kutumia taifa kupitia serikali ya Dr. Magufuli kwani Dr Mwele IS ONE OF THE VERY FEW BEST ASSETS WE HAVE IN THE COUNTRY! Yani natamani nafasi ya Ummy Mwalimu itenguliwe apewe Dr. Mwele as she deserves it so very much! Watu huwa wanafanya makosa lakini kuna watu wachache sana wanaohitajika kupewa second chance na Dr. Mwele ni mmoja wao! Natumaini my baba Dr. Magufuli ataangalia hili swala kwa maslahi mapana ya taifa letu na dunia kwa ujumla!