Category Archives: Leadership

JINSI YA KUJENGA JAMII DHAIFU NA BONGOLALA- Peter Sarungi

Nchi za Africa bado zitakuwa na kazi ngumu sana ya ki utawala katika kuunganisha jamii tatu katika nchi ambazo ni Wenye Nchi, Wana siasa na Wana Nchi ili kifikia maendeleo ya kweli. Kwa bahati mbaya kumekuwepo na udanganyifu mkubwa unao fanywa na Wana siasa walio pewa wajibu wa kuunganisha na kuleta mahusiano mazuri katika jamii hizi ili ziweze kufanya Kazi kwa ushirikiano hatimaye kuleta maendeleo ya nchi.

Wana Siasa wengi wa Africa wamevuruga nchi zao kupitia mifumo wanayoiweka katika kuongoza nchi. Wana nchi wengi bado hawajui athari za mifumo mbalimbali katika kuendesha maisha yao ya kila siku. Mifumo hii huanza kuathiri maisha ya wana nchi tangu wanapo zaliwa, ukuaji wao, kuelimika kwao, uchumi wao, afya zao, uhuru wao hadi uzee wao. Mifumo hii inaweza kuamua ni kwa kiasi gani wananchi waelimike, wapate afya nzuri, waajiriwe, wajitegemee, wapate uhuru na mengine mengi yakiwemo yanayohusu siasa. Ndio maana kuna msemo unasema ukiona wafuasi ni wabovu basi jua wametengenezwa na kiongozi wao na ukitaka kujua ubovu ama ubora wa nchi basi chunguza athari zinzowapata jamii husika kutokana na mifumo ya kuendesha nchi.

Watawala wengi wa Africa wamekuwa na uturatibu wa kutengeneza jamii dhaifu na masikini katika kuhoji, kushauri, kufikiri, wasi jitambua na wasio jua wanachokitaka. Watawala wamekuwa wakitengeneza jamii hizi ili kuendeleza malengo yao ya kutwala dola kupitia mifumo. Na kwa bahati mbaya mifumo hii imeweza kuwaathiri hadi wenye nchi na kujikuta wakitumikishwa na Wana Siasa, ndio maana utakuta kuna idadi kubwa ya wanajeshi walio ishia darasa la saba na kidato cha nne kuliko wale waliofika kidato cha sita na kuendelea. Wote hawa hujikuta wakitawaliwa na wana siasa kwa maagizo hata ya kutekeleza jambo kwa mnyonge kwa maana mfumo waliofundishwa na kuapa ni wa kutii bila kuuliza.

Watawala wengi wa Africa wameweza kupitisha na kuhalalisha mifumo ya kuzalisha jamii dhaifu na Bongolala kupitia njia tatu….fb_img_14819059905521. KUDHOOFISHA ELIMU KWA JAMII
Watawala wengi wa Africa wana amini kuwa kutawala jamii iliyo elimika kupitia Elimu bora ni ngumu sana na ina waweka katika riski kubwa ya kutawala milele, hivyo hulazimika kutengeneza jamii kubwa isiyokuwa na elimu ili kudhoofisha uelewa wao na uwezo wao wa kufikiri. Watawala hawa wana vuruga mfumo wa elimu kwa makusudi na kuweka mifumo dhaifu yenye kutoa nafasi ndogo ya wana nchi wachache kupata elimu hadi ngazi za juu na hata hao wanaopata nafasi hiyo hawapati Elimu inayostahili na kumkomboa karika utegemezi.

2. KUDHOOFISHA UCHUMI WA JAMII
Ni ukweli usio pingika kuwa Uchumi imara ni nguvu nzuri kwa jamii. Jamii yenye uchumi imara inaweza kuelimika kwa gharama yoyote ile ikiwa uchumi wao ni imara. Jamii yenye uchumi imara inaweza kuamua kufuatana na maslahi yao hata inaweza kupinga mifumo dhalimu ya nchi na hata kuwapinga watwala. Kwa kuhofia vikwazo hivyo, Viongozi wengi wa Africa wamekuwa wakidhoofisha uchumi wa jamii zao ili kuwafanya wanyonge wasioweza kuhoji ubaya ama uzuri wa watawala. Viongozi wengi wamekuwa wakikusanya pesa nyingi kupitia kodi na kujilimbikizia wao pamoja na utawala wao kama alivyofanya hayati Mobutu Seseko wa Congo. wanapenda sana kuona pesa nyingi zikiwa kwao kuliko kwa wana nchi na ndio maana hata sekta binafsi zina zorota katika kuchangia maendeleo ya jamii.

3. KUDHOOFISHA UHURU WA KUTOA MAONI
Watawala wengi wa Africa hawapendi kusikia maoni tofauti na waliyo nayo wao, hawapendi kusia ukweli walio uficha, hawapendi kupingwa kwa namna yoyote ile. Hivyo watawala hawa wataingiza sheria na taratibu za kuua uhuru wa kutoa maoni kinzani. Inaaminika kuwa kuna watu hata ukiwa dhoofika ki uchumi na ki elimu lakini bado wanaweza kiwa wajasiri wa kutoa maoni yao hata kama ni ya kupinga utawala bila kujali vikwazo walivyonavyo. Hivyo ili kuto ruhusu riski hiyo, watawala huweka mifumo ya sheria za kukandamiza Uhuru wa kutoa maoni na hata Uhuru wa kujieleza kwa jamii.

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!
Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

#MyTake
Africa kama ilivyo nchi ya kisadikika, ina safari ndefu sana ya kubadili mifumo ya nchi. Mabadiko hayo huletwa na jamii iliyovuka vikwazo vitatu hapo juu yaani lazima uwe vizuri kichwani, uwe vizuri mfukoni na uwe na njia nyingi tata za kutoa maoni yako. Kinyume na hapo itakugharimu wewe na familia yako.

Asanteni sana, ngoja niendelee kutunisha mfuko wangu ili itakapo hitajika kubadili mfumo nami niwemo.

Barabara kuelekea kwenye mafanikio siku zote ipo kwenye matengenezo” – Arnold Palmer

“Barabara kuelekea kwenye mafanikio siku zote ipo kwenye matengenezo” – Arnold Palmerfb_img_1481841340954

#TBT Ninashukuru kufundishwa na tuongozwa kwa mfano naye.

Arnold Palmer alikua mmarekani mtaalamu wa Gofu ambaye historia inaeleza kuwa ni mmoja wa wachezaji bora wa Gofu. Nilishukuru sana kusajiliwa Kwenye shule yake ya gofu nilipokuwa shule. Uongozi wake ulikua muhimu sana Kwenye maendeleo yangu binafsi.  // fb_img_1481841340954“The road to success is always under construction.”— Arnold Palmer

#TBT Very grateful to have been trained and mentored by him.

Arnold Palmer was an American professional golfer who is generally regarded as one of the greatest players in the sport’s history. I was fortunate enough to be enrolled his golf academy during high school. His mentoring and coaching was instrumental to my personal development.

“Haya ni maneno yake Mwenyekiti wa Chadema Mbowe”-Lemutuz

screenshot_2016-12-15-10-43-34-1screenshot_2016-12-15-10-47-27-1screenshot_2016-12-15-10-47-59-1screenshot_2016-12-15-10-48-21-1

“Guys think before you speak” -Lemutuz

screenshot_2016-12-15-10-50-57-1

“Maisha ni kupanga na kupanga ni kuchagua”-Lemutuz

screenshot_2016-12-15-10-53-22-1 screenshot_2016-12-15-10-57-02-1screenshot_2016-12-15-10-57-09-1

Happy 70th Annivessary to UNICEF! Thank you for serving and protecting children!

screenshot_2016-12-14-10-46-15-1screenshot_2016-12-14-10-44-58-1screenshot_2016-12-14-10-45-37-1screenshot_2016-12-14-10-45-28-1screenshot_2016-12-14-10-44-04-1screenshot_2016-12-14-10-44-21-1screenshot_2016-12-14-14-48-03-1screenshot_2016-12-14-14-41-26-1screenshot_2016-12-14-14-48-26-1

“I’m so proud of you my guardian, sis and mentor” -Jokate Mwegelo

screenshot_2016-12-12-09-17-29-1screenshot_2016-12-12-09-17-20-1Nice! Congrats to her!

“Tulinde na kutetea haki za makundi mbalimbali kwenye jamii yetu”-Jokate Mwegelo

screenshot_2016-12-10-21-00-49-1screenshot_2016-12-10-20-45-20-1Asante mrembo wetu kwa kutukumbusha hili swala la kuwatetea na kuwalinda wasio na watetezi! Binafsi siyo kwamba najisifia lakini nimejikuta nikifanya hivyo bila hata ya kumjua mtu huyo najikuta nimesha vaa viatu vya muhusika na kuanza kumpigania! Sipendi watu wanao onea wenzao bila sababu ya msingi! Kama yule Muhaya  Ruge wa Clouds  FM na loser wake walivyo muonea Lady Jadee ??? Nipo very sensitive na maswala ya unyanyasaji kwa binadamu yoyote yule ……..asante sana kwa kutukumbisha!

“Wanasema eti Tanzania hatuna demokrasia lakini hawasemi wanatulinganisha na nani?”-Hoyce Temu

screenshot_2016-12-09-10-05-52-1screenshot_2016-12-09-10-01-55-1screenshot_2016-12-09-10-02-06-1????

ADUI WA TANZANIA NI WATANZANIA WENYEWE-Peter Sarungi

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

Inapotokea jambo fulani halifanyiki kwa mafanikio yaliyo tarajiwa basi wahusika hukaa na kutafakari ni kwa sababu gani jambo halijafanikiwa yaani maana yake wanatafuta mchawi ama adui aliye zuia mafanikio yao.

Tanzania yetu ni nchi yenye mipango mingi na mizuri na yenye kuvutia utekelezaji, nchi nyingi zimekuwa zikiiga mipango hii na kufanikiwa katika utekelezaji wake hata kuwa mfano kwa jamii za kimataifa. Chakushangaza ni pale unapo ambiwa kuwa chanzo cha mafanikio hayo ni mipingo iliyo buniwa na wataalaam kutoka Tanzania, maana utakuta utekelezaji wa mipango hiyo katika nchi ya Tanzania haiendani na wenzetu walio copy na kupaste kwao. Kwetu Tanzania utekelezaji umekuwa ni wa hasi na kuzalisha matokeo hasi kwa nchi.

Tumekuwa tukipata sera nyingi na nzuri lakini inapofika utekelezaji wake wanaibuka wana siasa wenye nguvu kikatiba kuliko watendaji na wanavuruga kabisa ule mpango kwa kuweka siasa katika utendaji na mwisho wa siku mambo yakiharibika wanasiasa wana ruka lawama na kuwasukumia rungu watendaji. Kila kitu katika nchi yetu kina endeshwa na siasa maji taka au siasa propaganda. Kuna haja ya wana siasa wetu kubadilika.

?????????? Hii ni shule niliyoikuta maeneo ya ndani ya Dodoma-Kibakwe katika jimbo la waziri wa TAMISEMI anaye simamia mipango na kampeni ya madawati katika shule zetu.fb_img_1481212567254Mmmmmmmh! ??????- Alpha

Habari nyepesi nyepesi ni kuwa Ivanka Trump ndio ata play the FirstLady role!

screenshot_2016-12-05-21-34-28-1Inasemekana ya kwamba Ivanka Trump ndio aka “act” as FirstLady kwenye uongozi wa baba yake. Nimeweka “….” kwasababu haiwezi ikafanywa official kwani kisheria hairuhusiwi lakini hiyo haimaanishi hawezi fanya hivyo. Yani anaweza akawa active kwenye maswala mengi kama mtoto wa Rais  napia kwenda kumuwakilisha FirstLady kwenye mikutano yote. Lakini hato lipwa mshahara wala benefits zozote kama FirstLady………….

Ivanka alikuwa very active kwenye campaign management team ya baba yake na sasa ni Adviser kwenye transition team ya baba yake ambapo hata kaka zake nao wapo. Vile vile inasadikika kuwa Ivanka Trump takuwa the most powerful First-Daughter in USA history!…….

Wiki hii walikuwa wanatafuta nyumba ya kununua karibu na WhiteHouse hapo DC. Nahilo ndilo linawapa watu imani kuwa nikweli she’s going to “act” as FirstLady sababu kwani Trump wana hotel ya kifahari hapo karibu na WhiteHouse na ina suite (chumba) specific for Ivanka Trump hivyo kama ni kumsalimia baba walikuwa na sehemu ya kulala na hata wangeweza kukaa ndani ya WhiteHouse!….. Inasemekana watoto wakiume ndio watakuwa wakiendelea kuendesha business zao………Anyway, time will tell!

Kitu ambacho sikujua kuwa Ivanka Trump na mme wake ni Wasabato kama mimi ? ? Ivanka alibatizwa kwenye Usabato baada ya kukutana na mumewe. Wakati mumewe ni Msabato wakuzaliwa. ……..You go Ivanka one day I will meet you ?? simnajua baba yangu ni President Dr. Magufuli ??

Hongera sana Rebeca Ngyumi! 2016 African Women Of The Year in Civil Society And Activism!

screenshot_2016-12-05-12-56-12-1

Hongera sana Rebeca kwa tuzo ulizopata! Wow! Wanawake Watanzania ndio watakao ubadilisha na kuondoa mfumo dume wa unyanyasji wanawake na watoto ndani ya Tanzania na Africa kwa ujumla! Umeonyesha ujasiri mkubwa sana, mfano mzuri mno kwetu sote! “Sina ambacho nitahathirika endapo serikali itasema hii sheria iendelee lakini nafikiri tunajukumu kama wana nchi kuhakikisha tunaweka mifumo mizuri ya sheria ambayo inalinda wana nchi wengine nasiyo tu sisi peke yetu”! Nimependa sana hayo maneno yako! Tatizo kubwa linalo sumbua Bara la Africa ni UBINAFSI! Tuondoe ubinafsi kuwa hilo halinihusu! Sikiliza nikwambie ee mwanamke mwenzangu; kama limemkuta mwanamke au msichana mwenzio basi hilo pia ni LAKO LINAKUHUSU SANA! Kwani laweza kutokea kwako wakati wowote ule au kwa vizazi vyako! Ngoja niseme ule msemo wa Mboni Masimba kuwa “Sauti ya mwanamke ni sauti ya jamii”!! Hivyo ondoa ubinafsi kwa faida ya taifa lako!screenshot_2016-12-05-12-55-33-1Kitu ambacho nimeshindwa kuelewa ni kwanini serikali ilikata rufaa?!! Baba yangu Dr. Magufuli hawa waliokata rufaa nao ni #JIPU tu wanahitaji kutumbuliwa kwakweli!!……….. Unajua hizi bangi za ukubwani ni shida sana, mie hapa ninakaribia kugonga 40 na ndoa bado naigopa kama gereza la Keko halafu eti watu wanapinga maamuzi ya Mahakama?! Kha! Natamani niwajue hawa watu, walikuwa Wanaume au Wanawake? Na nini haswa ilikuwa nia yao!screenshot_2016-12-04-13-19-13-1

Wanawake kwa pamoja tunaweza badilisha Africa lakini kumbuka kuwa siku zote mabadiliko huanza na wewe!!………Hongera sana Rebeca, well done! Very well deserved!!

 

Stand-up comedy ni sanaa kama zilivyo sanaa nyingine-Jokate Mwegelo

screenshot_2016-11-29-10-45-21-1screenshot_2016-11-29-10-45-14-1screenshot_2016-11-29-10-44-41-1Beautiful! Umependeza mno Jokate wetu! That dress is WOW!!…………Ulichosema ni cha kweli kabisa. Hichi kipaji siyo cha kukidharau hata kidogo kwanza lazima uwe na akili shap sana ili uweze kuwa comedian mzuri. Yani lazima uwe na uwezo wakuona na kutengeza joke papo kwa papo. Pia ni sanaa ambazo zinahitaji maandalizi na nidhamu sana kama zilivyo muziki na mpiraa n.k ili uweze kuburudisha, na kufikisha ujumbe kwa jamii katika njia ya pekee. Binafsi ni mpenzi sana wa Stand-up comedy kama hazitumii maneno makali sana…….. Asante kwa maoni yako kwa jamii na viongozi hii pia ni ajira kubwa sana kama zilivyo ajira zingine. Kuna watu kama Jimmy Fallon, Kevin Hart, Jimmy Kimmel n.k ambao ni mharufu sana au hata Jay Leno na David Letterman ambao kwa sasa wamestahafu na wamejitengenezea kipato kikubwa sana kwa kutumia commedy hapa U.S.A……..pia kuna mpaka channel ya TV hapa inaitwa Comedy Central ambayo inaonyesha commedy siku nzima. Hivyo hii ni fursa ya kutizamwa sana na serikali pia watu ambao wangependa kuwekeza kwa wasanii wa aina hii.

“As young people the future is ours but this is not the future we want for ourselves” -Getrude Clement

screenshot_2016-11-26-18-05-19-1 screenshot_2016-11-27-08-38-46-1

Hongera sana Faraja Nyalandu kwa maono mazuri ambayo yana faida kubwa sana siyo tu kwa taifa letu bali kwa dunia nzima. Sauti ya mtoto ni sauti ya dunia kwani kinacho tokea leo effects zitakuwa baraka au laana kwa watoto wa vizazi vyote. Maamuzi mabaya ya wazazi yanaleta maafa kwa watoto wa vizazi vyote. Nipale wazazi kama wewe wanapo amua kuweka interest za watoto mbele ndipo wao. Ni mpaka pale wazazi wanapo acha kuwa selfish na kujali si tu watoto wao bali pia watoto wa wazazi wengine ndipo mabadiliko yanatokea. Hongera sana. Ulifanya maamuzi mema!…….Hongera sana kwa Getrude Clement nyota njema huonekana asubuhi!

G.C at UN -“As young people the future is ours but this is not the future we want for ourselves”! Ni jukumu la wazazi kuhakikishia watoto usalama wao katika nyanja zote za maisha, kijamii, na kimazingira. Huwezi kumwambia mtoto alale bila wasi wasi wakati anaomba nyumba ina tingishika. Lazima atakuwa na hofu! Mbaya zaidi na huzuni kubwa ni pale mtoto anapo muomba mzazi wake amuhakikishie usalama wa maisha yake wakati hilo ni jukumu lakwanza la mzazi! “You may think that we are too young to know about the risks and reality of climate change but we see that in our daily lives”-G.C Wazazi amkeni, badilikeni! #ItBeginsWithYou

NIMEKUENZI FIDEL CASTRO KWA JINA LAKO-Peter Sarungi

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

Kuna watu hawawezi kupotea dunia kwa sababu ya alama walizoweka wakati wa maisha yao. Mmoja wa watu hao ni aliyakuwa muasisi mkombozi na raisi wa kwanza wa CUBA Fidel Castro.

Fidel Castro alifanya jambo ambalo lilifanywa na watu wa zamani waliokuwa na ujasiri mwingi, uthubuti mwingi, uzalendo mwingi, utu mwingi na maono ya kuifanya nchi yake ijitegemee. Hawa ni kizazi cha Kwame Nkuruma, Julius Nyerere, Nelson Mandela, Patric Lumumba, Samora Mashel na wengine wengi waliokuwa wakipambana katika kutimiza maono yao kwa nchi. Hivyo ndo vizazi vilivyokuwa na hisia za ukweli za uzalendo kwa taifa lao.fb_img_1480340327658Huyu Fidel ndio chanzo cha mimi kumwita mwanangu jina la FIDEL PETER SARUNGI nikimwenzi Jasiri wa CUBA. Historia ya Fidel ni kubwa na imebeba vitu vingi ingawa natamani kama mwanangu akirithi ujasiri, uzalendo, utu, uthubutu na uwezo wa kutawala. fb_img_1480257721064Mungu ailaze roho ya Fidel Castro mahala pema, yeye amekwisha maliza kutimiza maono yake na ameacha alama kwa jamii yake. Mungu atusaidie na sisi tutimize maono tuliyobeba.

R.I.P FIDEL CASTRO

WALEMAVU WALIOPATA FURSA WAMEJISAHAU SANA-Peter Sarungi

Peter Sarungi (kushoto), Spika wa Bunge ndugu Ndugai pamoja na viongozi wengine wa siasa,
Peter Sarungi (kushoto), Spika wa Bunge ndugu Ndugai pamoja na viongozi wengine wa siasa,

Kuna msemo wa wahenga unasema ALIYESHIBA HAMKUMBUKI MWENYE NJA. Haya maneno nilidhani yanatumika kwa watu nisio wajua tu kumbe hata watu ninao wajua na ambao tena wapo kwenye jamii nyonge ya watu wenye ulemavu. Watu wenye ulemavu sasa wamefikia Milion 4, jamii hii bado imeendelea kukumbwa na umaskini mkubwa unao sababishwa na ugumu wa mazingira wanayokutana nayo katika kutafuta maisha bora. Watu wenye ulemavu wamelia sana kuhusu changamoti zao lakini sauti zao bado hazisikiki katika vyombo vya maamuzi na mipango ya nchi, hii inatokana na uchache wa watu wenye ulemavu waliopata fursa kushindwa kutumia fursa zao katika kutetea na kushawishi vyombo vya maamuzi na vyombo vinavyotunga sera, sheria na mipango kukumbuka uwepo wa wa watu wenye ulemavu ili kusaidia utekelezaji wa sera na sheria zinazo toa fursa kwa watu wenye ulemavu. Ukweli ni kwamba ni walemavu wachache sana walioweza kupata fursa za uchumi, fursa za siasa na hata fursa za kijamii, Lakini hawa wenzetu wengi wamekuwa mabalozi wasiojali maslahi ya kundi hili na hata kufikia kujiondoa kiroho katika kundi hili ingawa ki mwili bado wana hesabika ni watu wenye ulemavu.fb_img_1480102785902

Kwa bahati mbaya jamii imetumia ulemavu wetu kama alama ya utambulisho (public figure) kiasi kwamba jamii inakutambua kwa ulemavu wako na si vingine kisha sifa zingine zinafuata na mara nyingi sifa mbaya za watu wenye ulemavu zimekuwa zikivuma kuliko sifa nzuri za jamii hii. Hili ni tatizo linalozaa utengano kwa jamii ya watu wenye ulemavu maana hawa wanaopata fursa kwa mgongo wa kundi hili wamejisahau na kujikuta wanapigania maslahi yao na matumbo yao bila kujali uwepo wa jamii ambayo imesababisha wao kupata fursa. Wenzetu badala ya kutuunganisha katika fursa, wao wameendelea kula dili na wasio husika. Badala ya kupaza sauti ya ushawishi na utetezi, wao wameendelea kukaa kimya na kuridhika kwa vinono wanavyopata. Badala ya kuanzisha miradi ya kuwezesha jamii hii wao wana anzisha miradi ya kitapeli katika jamii, wameshindwa kushawishi utekelezaji wa sera za walemavu ingawaje kila siku wapo angani kwenda mataifa ya wenzetu waliopiga hatua juu ya utekelezaji wa sheria na sera za watu wenye ulemavu, Wameshindwa kushawishi kuanzishwa kwa jumuiya ya walemavu katika vyama vyao vya siasa ingawa wao wamepata fursa kupitia jumuiya ya wanawake, wameshindwa kushawishi utekelezaji wa sheria no.9 ingawaje wamepewa utawala katika sheria na wizara ndani ya ofisi ya waziri mkuu, wamegeuza dhamana kuwa msaada, wamegeuza msaada kuwa mtaji na wametumia mtaji wa unyonge wa walemavu kuwa fursa kwao na familia zao

Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)
Peter Sarungi (Next Speaker-Baba Pilato)

#Mytake
Wewe uliyepata fursa za uchumi, siasa na utawala kupitia walemavu, jiulize, Umeifanyia nini kundi hili linaloteseka na kunyanyasika kila siku wakati linakutegemea wewe kushawishi na kutetea mabadiliko yao? Ujue Mungu anakuona vizuri sana. Usijisahau ukadhani unaishi bila ulemavu na hata ukaukataa kwa maneno na matendo, bado utaendelea kuwa kwenye kundi hili maana hakunaga uponyaji kwa uumbaji wa Mungu labda kwa usanii na maigizo.fb_img_1480102909327

UKIMYA WA HAWA NDUGU ZETU UNAUMIZA NA KUKERA KULIKO HATA KELELE ZA WAPINZANI WETU. Badilikeni..

Asanteni

**Baadhi ya maoni ya watu**screenshot_2016-11-25-13-40-52-1-1 screenshot_2016-11-25-13-40-33-1 screenshot_2016-11-25-13-41-16-1

Congratulations Faraja Nyalandu!

screenshot_2016-11-21-08-47-54-1screenshot_2016-11-21-08-48-08-1

Kindly may I offer my heartfelt congratulations to Faraja Kota Nyalandu the Founder and Executive Director of Shule Direct for a very well deserved appointed position to serve as Global Future Council For Education, Gender, and Work by the World Economic Forum! Thank you for making us proud, a good example to many young girls and boys. Wishing you the best in everything and continue to make us proud~~~~~~~~~~~ Alphascreenshot_2016-11-21-08-47-18-1

“THE MAN THAT MADE AMERICA GREAT AGAIN”

While the Greatest Country in the world celebrates (Or reluctantly celebrates) Clinton’s win, I will be mourning and celebrating the end of the GREATEST LEGACY I have seen with my own eyes, THE OBAMA LEGACY. The first black man to be President with one of the highest approval ratings ever. A man who picked an ailing economy to easily outmunavre China’s economy leaving the Chinese one in the dust. A man who killed Osama Bin Laden, a man who ensured 90% of Americans are insured, A man who brought unemployment down to 4.9%, a man who helped America get back its high status as a great Natural gas producer and accorded with cheap gas.A man that made us Black men realise if we try harder we can reach the very highest of what we were intended or created for. The Greatest man walking on Earth today. fb_img_1478659262996HUSSEIN OBAMA…THIS MAN HAS MADE AMERICA GREAT AGAIN

Source: Gondwe Goole  Facebook 

Matukio katika picha: Jokate Mwegelo

screenshot_2016-11-05-15-32-14-1 screenshot_2016-11-05-15-39-56-1 Kidoti is doing what Kidoti is supposed to do! Endelea hivyo hivyo vijana wanakuitaji Jokate wahamasishe kufata ndoto zao na mbinu za kupambana na vikwazo ndani na nje ya familia. Naamini kwa kufanya hivyo hata wewe huta amini jinsi watakavyo kubadilisha maisha yako……good job! Keep it up!screenshot_2016-11-05-15-40-56-1screenshot_2016-11-05-15-40-51-1 screenshot_2016-11-05-15-41-40-1 screenshot_2016-11-05-15-42-03-1screenshot_2016-11-05-15-38-54-1Nimependa sana huo ubunifu wa kufunika mabenchi. Sio kama zama zile unakuta benchi lina vumbi na kutu halafu wanataka ukae ??

“Kenya tatizo ni moja tu! Ukabila”- Rais JP Magufuli

fb_img_1478139802483