Hakuna ubaya kumkumbusha mtu kitu au kumpa mtu tahadhari. Tatizo ni jinsi unavyo sema na mahala unapo semea ndiyo huleta shida!

Kwanini unamkatisha mwenzio tamaa? Wewe Kama haukubaliani na ndoto za mtu mwingine, basi pale anapo amua ku share na wewe badala ya kumkatisha tamaa ni vyema ukanyamaza’  If you don’t have any positive thing to say to someone just “shut your front door!” Tujifunze kupenda kubariki wengine  nasi tutabarikiwa tena zaidi. Mtu anapo share na wewe  mawazo  yake au  mipango yake inamaana amekuamini, kama upendi aendelee kukuamini basi nyamaza! Hivyo itakuwa umetumia busara zaidi kuliko kuanza kumtolea maneno ya kukatisha tamaa kama vile; “sidhani kama utafanikiwa”, au “mh! Jitahidi mwanzo  mugumu.”

Okay, mtu kufuata  ndoto zake sio lazima afanikiwe kama wewe unavyotaka au unavyo fikiria kwani kitendo cha mtu kujaribu teyari ni mafanikio tosha! na wewe ni nani haswa mpaka ujue what the future holds of your fella?  Unajua aliye tengeneza bulb alijaribu mara ngapi kabla ya kufanikiwa? Bill Gate alishawahi kusema kuwa yeye huwa haajiri mtu ambaye hajawahi ku fail! Na hawa ni watu ambao leo hii dunia inawatazama kama baadhi ya watu ambao ni the most achievers in the world!  “Mmh! Mwanzo mugumu” oh! well, who doesn’t know that?! Nani asiejua kua katika kujaribu kufanya kitu chochote kile unaweza usifanikiwe? Why uone umuhimu wa kumguna mtu ili umwambie mwanzo mugumu? Au Wenzetu wanasema “talking / saying with attitude” hivi unajua Billoner Mr. Trump amewahi ku file bankruptcies mara ngapi? na ni nani asiye jua kuwa Rome haikujengwa ndani ya masaa 24?!

Hakuna ubaya kumkumbusha mtu kitu au kumpa mtu tahadhari. Tatizo ni jinsi unavyo sema na mahala unapo semea ndiyo huleta shida! Pia tabia ya kurudia rudia kitu kimoja kila wakati it becomes annoying! Namwishoe mtu anaanza kulichukulia hilo neno in a negative way hata kama ulilisema kwa nia nzuri. Kwanza nimegundua  ukiona mtu anakukatisha tamaa kwenye juhudi zako jua huyo mtu anatamani sana kuwa wewe ila hawezi! Hivyo kupooza maumivu  anaona akuvunje wewe nguvu ya kusonga mbele! Siku zote jaribu kuwa mbaraka kwa mwingine hata kama mambo yako unaona hayapo sawa. Kwa kufanya hivyo utajenga tabia ya kupenda maendelo ya wengine nahapo ndipo utakapo barikiwa nawewe. Be a blessing! Kataa kuwa na roho ya kichawi!

2 thoughts on “Hakuna ubaya kumkumbusha mtu kitu au kumpa mtu tahadhari. Tatizo ni jinsi unavyo sema na mahala unapo semea ndiyo huleta shida!”

Leave a Reply