Hongera sana Mh. Nicholaus B.William!

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli akimpongeza Mhe Nicholaus B. William aliyemuapisha kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Ikulu jijini Dar es salaam leo Oktoba 28, 2017. Kulia ni mke wa Mhe. William Bi. Foster Mbuna.
Napenda kuchukua nafasi hii kumpongeza sana Mh. Nicholaus B. William kwa kuteuliwa kwake kuwa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, na Michezo. Sijawahi kukutana nawe lakini sifa zako nyingi nilizipata kutoka kwa mdogo wangu Advocate Janeth O.O Igogo jinsi ulivyo mnyenyekevu, usiye jikwenza, mchapa kazi, na muungwana. Tabia yako ya kujiona wewe ni sawa na wengine inawavutia na kuwaacha wengi kujiuliza jinsi mlivyo lelewa. Kweli kuwa mtoto wa Rais hakubadili tabia ya mtu kwani tabia ya mtu ni mtu mwenyewe! Mimi naamini hayo yote ni matunda ya kuwa na walezi wazuri na mke mwema! Hivyo nategemea hakuna kitu kubadilika zaidi ya uongozi bora toka kwao! Hongera sana. #VijanaTunaweza

Mungu ibariki Tanzania. Mungu ibariki Africa

**Picha na caption kwa hisani ya Issa Michuzi blog. Kwa maelezo na picha zaidi bonyeza ?? (MichuziBlog-Matukio)**

Leave a Reply