Hongera sana Waziri Angellah Jasmine Kairuki!

Naomba nichukue nafasi hii kumpongeza Waziri mpya wa Madini, Mh Angellah Jasmine Kairuki! .......Kama kumbukumbu zangu zipo sawa basi naamini wewe ndio Waziri wa KWANZA MWANAMKE aliyewahi kushika wizara hiyo nyeti! Naamini utendaji wako unatija kwa taifa letu la Tanzania ndio maana Rais Dr. John Pombe Magufuli pamoja na washauri wake wakaona ni vyema ukabidhiwe hiyo wizara. ........Nakutakia utendaji na uongozi mwema ukizidi kuweka maslahi ya taifa letu mbele. Hongera sanaaaaaa! #Mungu Ibariki Tanzania #Mungu Ibariki Africa

Leave a Reply