Kesha la asubuhi: Ana shauku ya kuwasaidia walimu

           ? *KESHA LA ASUBUHI*?
                             Alhamisi
                          Mei 17, 2018

*ANA SHAUKU YA KUWASAIDIA WALIMU*
*_______________________________* 

? Fungu kiongozi
??
?2 Wafalme 2:15.

_*"Na hao wana wa manabii, waliokuwako Yeriko wakimkabili, walipomwona, walisema, Roho ya Eliya inakaa juu ya Elisha. Wakaja kuonana naye, wakainama kifudifudi mbele yake".*_
?➖➖➖??➖➖➖?

✅ Roho Mtakatifu alikuja katika shule ya manabii, akileta hata mawazo ya wanafunzi katika upatanifu na mapenzi ya Mungu. Kulikuwapo na muunganiko hai kati ya mbingu na shule hizi, na furaha na shukurani za mioyo yenye kupenda ilidhihirika katika nyimbo za sifa ambazo malaika walijiunga kuimba.

✅ Iwapo walimu wangelifungua mioyo yao kumpokea Roho huyu, wangelikuwa tayari kushirikiana naye katika kutenda kwa ajili ya wanafunzi wao; na pale anapopewa njia huru, atasababisha mabadiliko ya ajabu. Atafanya kazi katika kila moyo, akirekebisha ubinafsi, kuumba na kusafisha tabia, na kuleta hata mawazo kuwa mateka kwa Kristo. …

✅ Badala ya kunyamazishwa na kurudishwa nyuma, Roho Mtakatifu ingelifaa akaribishwe, na uwapo wake kuhimizwa. Wakati walimu wanapojitakasa wenyewe kupitia katika utii wa Neno, Roho Mtakatifu atawafanya kuona kidogo mambo ya mbinguni. Watakapomtafuta Mungu kwa unyenyekevu na bidii, maneno ambayo wameyazungumza kwa msisitizo thabiti yatachoma mioyoni mwao; ndipo ukweli hautafifia katika ndimi zao.

? ```Uwakala wa Roho wa Mungu hauondoi kutoka kwetu umuhimu wa kutumia akili na vipawa vyetu, bali hutufundisha jinsi ya kutumia kila uwezo kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Akili za mwanadamu zikiwa chini ya uongozi maalum wa neema ya Mungu zinakuwa na uwezo wa kutumiwa kwa ajili ya kusudi lililo bora duniani. Kutokujua hakuongezi unyenyekevu au kumfanya mtu ye yote anayekiri kuwa mfuasi wa Kristo kuthamini zaidi mambo ya kiroho. Kweli za Neno takatifu zinaweza kufurahiwa vyema zaidi na Mkristo mwenye akili. Kristo anaweza kutukuzwa vyema zaidi na wale wanaomtumikia kwa akili. Kusudi kuu la elimu ni kutuwezesha kutumia uwezo ambao Mungu ametupatia kwa namna ile itakayowasilisha dini ya Biblia na kukuza utukufu wa Mungu.```
?? - North Pacific Union Gleaner, May 26, 1909.

*UWE NA TAFAKARI NJEMA MTOTO WA MUNGU*
_______________________________

Leave a Reply