Malezi ya watoto na changamoto zake!

Pole sana mpendwa, tunamuombea uponyaji wa haraka! …….tukio hili limenikumbusha jinsi my cousin brother alivyo “piga pasi” tumbo lake!  kaka yangu alikuwa na tabia ya kunyoosha sehemu za shati lake ambazo zimejikunja huku akiwa teyari amevaa!! Kumbe mtoto anamuangalia na siku moja akachukua pasi iliyokuwa yamoto Akanyoosha tumbo lake! It was an awful experience! He was  2.5 yrs old by then sasa hivi anakwenda miaka 30 na sidhani kama anakumbuka hilo tukio!…….Anyway, malezi ya watoto yana changamoto nyingi sana. Wewe mzazi unaweza kuwa makini lakini watu unao ishi nao wakawa ni majanga! Nikuomba Mungu tu kama una amini kuwa Mungu yupo!…..Juzi nilisimuliwa kisa cha mtoto wa cousi-sister wangu ambaye house girl alimfungia ndani ya nyumba akiwa amelala halafu yeye akaenda shule kumfata mtoto mkubwa, with a assumption kuwa “atawahi kurudi”! Too bad alipofika shule, siku hiyo walikuwa wamekwenda picnic picnic wakawa wamechelewa kurudi ikabidi dada wa kazi amsubiri! Mtoto aliye achwa nyumbani he is barely 3 yrs old!! Aliamka usingizini haoni mtu ndani ya nyumba! Mtoto kalia mpaka kachoka ma njaa juu! Mama mtu anarudi nyumbani anakutana na hayo majanga! Yani ni alimfukuza house girl siku hiyo hiyo!…..Sasa can you imagine kama moto ungewaka ndani ya nyumba na mtoto kachwa mwenyewe? Au mtoto angechezea jiko la gas ambalo wanalo hapo ndani! Hivi ingekuwaje?! . ……Malezi ya watoto yanahitaji maombi ya ziada kwani bila Mungu hatuwezi!

Leave a Reply