Martin Tiho ashirikiana na Jokate kuanzisha “Sauti Ya Watu Wenye Ulemavu”!

Mr. Martin Tiho na Jokate Mwegelo

“Nikiwa na rafiki yangu Martin Tiho niliyekutana nae kwa mara ya kwanza miezi miwili nilipofanya ziara katika ofisi za New Habari Sinza jijini Dar es Salaam, alikuwa anasambaza CD za filamu aliyoigiza na kutengeneza mwenyewe. Tukabadilishana mawasiliano baada ya kununua CD yake na kuahidi kushirikiana nae. Ameanzisha kampeni yake ya “Sauti Ya Watu Wenye Ulemavu.” Na hivi karibuni tutawaletea tshirt kama njia moja wapo ya wewe kuchangia katika project yake. Nilimwalika aje tupige picha za pamoja. Picha hizi zitakuwa kwenye tshirt zake. Karibuni. Usengwile.” Jokate Mwegelo

Leave a Reply