Mh.Edward Lowassa: Amenifanyia siku yangu kuwa njema sana. He has made my day

Siasa ni sera na itikadi siyo chuki wala uwadui! Wenyewe wenye lugha zao wanasema 'Politics is just a game'!  Na hapo ndio mimi nasema tusilazimishane kuupenda au kucheza mchezo huu!! Acha wale wanaopenda siasa wahubiri siasa, wale wanaopenda mambo ya kumtukuza Mungu wahubiri injili ya Mungu, wambea na wadaku wote washinde Facebook na Instagram kufuatilia maisha ya watu!! Kila mtu afanye kile kitu roho napenda!! Kwani siyo wote tunaoweza cheza mchezo huu wa siasa, wengine hatujui ku-control hisia zetu kuweka siasa kwenye maswala ya msingi!! Nasisitiza mimi sio mwanasiasa! Tusipangiane maisha!!

"He has made my day" hayo ni baadhi ya maneno ya Mh. Edward Lowassa baada ya kuonana na Rais Dr. John Pombe Magufuli siku ya jana. Naona wanachama wengi wa  Chadema wana lalamika kuwa wamesalitiwa??! Nikabaki kujiuliza, wamesalitiwa?? ?? na nani tena?! Kama ni usaliti basi ulifanyika 2015 pale kiongozi wenu alipo mchukua mtu ambaye hakuwa mwanachama wenu na kumpa nafasi ya kugombea urais bila hata aibu!! Ule ndio ulikuwa usaliti!!  Eti kwanini Mh. Lowassa hakushirikisha viongozi wa chama kabla ya kwenda kumuona Rais?!! ?? What a madness!! Are these people really know what they are saying! Hivi ukiwa mwanachama wa Chadema maisha yako yote ni mali ya chama??!! ?? ....Anyway Mh. Mbowe kawaelimisheni vizuri sana katika hili.  Msikilize hapo ?? Mh. Lowassa ni raia wa Tanzania kama walivyo raia wengine, kuonana na Rais ni haki yake kimsingi!! Haitaji kibali cha mtu yoyote yule kuendesha maisha yake nje ya chama.

Kuna maisha nje ya siasa na hayo ni maisha yako wewe mwenyewe  hayamilikiwi na mtu yoyote! Una uhuru wa kujumuika, kufanya biashara, kula, kuoa, kusali na mtu mwingine yoyote yule ambaye siyo adui (mf. Mtu ambaye gaidi) wa inchi yako! Siyo ndugu zako wote ni wanasiasa au wafuasi wa chama chako sasa utavunja undugu kwasababu ya Siasa?!! Kuna watu naona wanaingiza siasa mpaka kwenye maswala ya ndoa? Jamani hivi hii ni Siasa au ushetani!! Ndoa ni agano takatifu, leo hii mnataka watu waliokula kiapo mbele za Mungu waachane kwasababu ya Siasa?!! Huyu shetani anaye waingia Watanzania niwakukemewa kwa nguvu zote!! Embu turudi nyuma kidogo, sinimekwambia kuwa wenyewe wanasemaga Siasa ni mchezo tu! Sasa hapo mastering wa hii game kwa upande wa Chadema ni Mh. Edward Lowassa na Mh. Freeman Mbowe! Kumbuka Mh. Lowassa alijiunga na Chadema kwa mkataba wa kupewa nafasi ya kugombea urais na hiyo ndio imekuwa nia na lengo lake mpaka wiki kama tatu zilizopita, msikilize ?? akiwa bado anaomba Mungu amsaidie kushinda Urais 2020

Umemsikia eeh! Wakati huo huo Mh. Mbowe ameshaona kuwa Mh. Lowassa is not a great candidate kwa 2020 hivyo target yake ni Mh. Tundu  Lissu.  Lakini kwakuwa bado anamuhitaji Mh. Lowassa kwaajili ya nguvu ya umma na kifedha inabidi aendelee kumlaghai akae ndani ya chama mpaka 2020 halafu wamfanyie ule mchezo aliomfanyia Dr. Slaa  ?? but Mh. Lowassa is too smart for that ndio maana anaanza kuwafanyia maigizo kwani ameshaona dalili za yeye kufanyiwa mchezo aliomfanyia Dr Slaa! ??? Hivi huwa wanasema eti "Karma is a........" and what goes around always huwa linarudi kinyume nyume eeh ?? I love it when politicians played themselves! Mh. Edward Lowassa amekwishaona hana tena maslahi yakudumu na Chadema sasa sibora arekebishe huku kwingine before it's too late! Nammemsikia akisema anaona miaka mingine 5-10 ya uongozi bora wa Dr Magufuli ??? should I say CCM oyee ee on behalf of CCM members or will I be morally wrong since I am a blogger I should stay neutral and keep my mouth shut ?? #IHatePolitics #HeHasMadeMyDay  Btw, swala la Mh. Lowassa kuwa ni mtu muungwana na mstarabu hata mimi niliwahi sema huko nyuma, soma ?? Mr&MrsMkapaGoldenAnniversary
NilisemagaHukoNyuma

Leave a Reply