Mhe. Anna Mghwira rasmi ndani ya Chama Cha Mapinduzi!

Mjane wa Baba wa Taifa, Mama Maria Nyerere akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira mara baada ya kutangaza kuhamia Chama cha Mapinduzi CCM katika mkutano wa tisa wa UWT uliofanyika mjini Dodoma.

Hatimaye yametimia! Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira ahamia rasmi CCM! Apokelewa kwa shamgwe na heshima zote mbele ya Mama wa Taifa mama Maria Nyerere!…….. Mimi siyo mwanachama wa chama chochote cha siasa lakini kama nikiambiwa nichague chama basi CCM kitakuwa chama changu siku zote! Yani ni kama leo hii mtu niambie nichague dini au dhehebu, jibu langu litakuwa mimi ni Mkristo wa dhehebu la Kisabato! Nitakuwa Msabato mpaka siku nakufa!  Hayo ni mawazo yangu na msimamo wangu kama yanakukwaza sorry but no sorry! …..Hivyo namtakia kheri Mhe. Anna Mghwira katika kutekeleza kazi ya ujenzi wa taifa kwa kupitia ilani ya CCM!

Makamu wa Rais Samia Suluhu Hassan akimpongeza Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira mara baada ya kuhamia rasmi katika Chama cha Mapinduzi CCM katika mkutano wa wa tisa wa UWT uliofanyika mjini Dodoma.

***picha na caption zote kwa hisani ya IssaMichuziblog***

Leave a Reply