Mwanangu mimi ….!

Unajua saa nyingine huwa siamini kama ni mwanangu ?? Mwenzenu nimekuza! Nikiangalia tulipotoka na tunapoelekea yani hakuna ninachokiona zaidi ya mkono wa Mungu ukiwa juu ya vichwa vyetu kumimina mibaraka yake.

Namshukuru Mungu sana na nitalitukuza jina lake milele. Kanipa rafiki wa milele. Tumekuwa pamoja, tumejifunza mengi pamoja, haswa kupitia makosa yangu mimi kama mama yake, yakampa somo la moja kwa moja. Mungu ni mwema sana. Nimevuka stage ya kuwa strictly mama; sasa hivi ni mama plus rafiki. Tunaongea na kuelekezana kirafiki tu! Kama malezi niliyompa kabla ya miaka 18 hayakumuingia na kumtengeneza kuwa kiumbe bora basi katika umri huu hakuna kitakacho mbadili zaidi ya kumuombea tu! Namshukuru Mungu sanaaaaaaa, mwanangu hajawai kunisumbua hata kidogo. Mungu kanibariki na mtoto msikivu, mwenye hofu ya Mungu, yani ni mtoto mwema mnoooo ndio maana saa nyingine siamini kama nimemlea mimi! ?? such a beautiful, humble, strong, smart, intelligent, classy, loyal, hard working, independent, charming young lady. I mean the list can go on and on but glory and honor all to Almighty God! ??

Leo nimejisikia kupost picha zetu haswa zahuyu mrembo wangu! ?? Kwani kunatatizo?! ?? sikuhizi nimeachana na kupost picha za watu haswa tusio na undugu, urafiki au mazoea. Ndio maana mnaniona sipost mara kwa mara. Nafanya mambo yangu mengine ambayo yananipa furaha na amani zaidi na hayo ndio nitakuwa napost humu.

??

Nimejisikia kumpost kuweka kumbukumbu ?? si blog ya mama yake jamani! ?? Ndio raha yakuwa na kitu chako mwenyewe ulicho kitengeneza wewe mwenyewe kwa utashi wa akili zako na mikono yako miwili. Hakuna atakaye kupangia nini cha kufanya labda huyo mtu ni punguani! ?? ………… Mungu azidi kumbariki sana na kumpa afya njema. ??

Leave a Reply