“Ndugu zangu Watanzania…….!”

#regrann  Regrann from @queenelizabethtanzania -  Ndugu zangu Watanzania, sidhani kama nitakuwa na maneno ya kuisha kuelezea shukrani zangu za hali ya juu, amani , furaha na nderemo. Kuanzia taji la Miss Kinondoni (Asante sana waandaaji na wadhamini), Miss Marcelina Dar es Salaam zone (Asante sana waandaaji na wadhamini) mpaka kufikia taji la juu kabisa la The New Miss Tanzania 2018; Dada Basilla Mwanukuzi, The Look Company, dada yetu mpendwa wa kambi, Marion Elias na wengine wote napenda kuchukua fursa hii kusema NAWAPENDA na kuwathamini SANA! Ndugu zangu watanzania kupitia mitandao ya kijamii na hata tuliobahatika kuonana mmenipa moyo sana mpaka kufikia hapa nilipo; sina cha kuwalipa; Nashukuru sana! Washiriki wenzangu wa The New Miss Tanzania 2018; ninawapenda sana na bila nyinyi mimi nisingeweza kuwa mshindi. Tushirikiane zaidi kuweza kufikisha tasnia hii mbele.

Taifa langu, wanahabari, kamati na uongozi wa kampuni ya The Look, Dada Basilla Mwanukuzi; Asanteni sana!

Asante TANZANIA! @newmisstanzania - #regrann

Leave a Reply