Nguvu iliyowekwa ndani ya mwanamke inaweza kumpa furaha na amani kila mwanaume atakaye ijua nguvu hiyo!

IFIKE MAHALA WANAUME TUWAHESHIMU WANAWAKE KWA JINSIA YAO na sio kuwapa kipaumbele kwa haja zetu za ki mwili, Mwanamke hatajwi kama kiburudisho cha Mwanaume, Mwanamke anatajwa kuwa UBAVU WA MWANAUME... Mchukulie Mwanamke kuwa sehemu ya Maisha ya kila mwanaume aliye timilifu "RIJALI" na hapo ndipo heshima ya Mwanamke itapatikana ndani ya akili yako, Mwanaume kumchukulia Mwanamke kama chombo fulani ni kujilaani mwenyewe maana NGUVU ILIYOWEKWA NDANI YA MWANAMKE INAWEZA KUMPA FURAHA NA AMANI kila mwanaume atakaye ijua nguvu hiyo. Mwanamke anazo nafasi nyingi kwa Mumewe ikiwa atapewa heshima, kutomheshimu Mwanamke ni kujishusha ki akili maana Mwanzo wa Mwanamke ni DADA na baadaye anakuwa MAMA achilia mbali hayo Mwanamke ni PAMBO LA MOYO WA MUME! Kumuacha Mwanamke akihangaika na kuteseka na watoto "FAMILIA" ukaangukia kwenye uhuni usokuwa na maana ni kujiwekea laana na mahangaiko siku zote za maisha yako, Mwanamke anapokuwa ametelekezwa MAISHA YAKE YOTE HUISHI KWA MASONONEKO na mpweke, Hakuna mtihani mgumu kwa Mwanamke kama KUOLEWA NA MWANAUME ASOJUWA SABABU YA NDOA... Hakuna Mtoto hupatikana kwa bahati mbaya maana maandalio ya mtoto yanapatikana kwa muingiliano wa ki mwili baina ya Mwanaume na Mwanamke "TENDO LA NDOA" inapofika mahala wanaume wanashindwa kutambuwa majukumu yao ya ulezi kwa watoto wao ilihali wakati wa mahitaji ya ki mwili aliweza kupambana juu ya ushawishi ni DHAMBI! Nanyi wanawake muwage mnaangalia na wanaume mnaokutana nao, Saa zingine SURA HUONGEA na muda mwingi MTU MBAYA HUJIKITA KWENYE UONGO ili kuificha tabia yake halisi.

#Elista_kasema_ila_sio_sheria ?

***Imenukuluwa kutoka Elista Realif For Heart*** 

Leave a Reply