NIMECHOKA, SITAKUBALI KUENDELEA KUONA WANANGU WAKISONONEKA NA SITAKAA KIMYA.” *** JACQUELINE MENGI-2

Jacqueline mpendwa, naomba uwelewe kua hakuna anayepinga maamuzi yako ya kuolewa na marehemu mzee Mengi, nawala hakuna anaeweza kuleta ubishi kwenye hilo kwani ni maamuzi ambayo marehemu aliyaafiki na kuweka wazi akiwa katika utashi wa akili zake timamu! Hilo halina mjadala! Naamini hata watoto wa marehemu walikubaliana na hiyo hali, ndio maana kuna siku ulituwekea video mkiwa Hyatt Regency Kilimanjaro hotel mkila brunch wote kama family! Hata mimi nilikua shabiki mkubwa wa “the Billionaire family” ? Honestly, I miss those moments nikiwapost humu!

Late Dr Reginald Mengi

Sasa basi, tatizo ninalo liona hapa nikitendo cha wewe kutaka to sit on the “throne” representing the “face” of Mengi’s family tena kwa dharau na kiburi! Woman! You must have lost your mind!! Who made you the ‘Queen of the castle’ to begin with?! Kwakweli, hapo UMEKOSEA SANA TENA SANA!! Hivi unajua hakuna familia iliyo simama bila MAMA!! nafahamu ili mji wa mtu fulani usimame na kuhesabiwa lazima kuna mwanamke jembe fulani nyuma yake??! Wewe umekuta mji huo umesimama, kuna maziwa na nasali, dhahabu na lulu; hivi unafikiri viliokotwa tu bara barani?! Unafikiri vilipatikana kwa kupaka makeup masaa 24 na kuweka kucha bandia?! Kuna watu waliosota kwenye huo mji ili kuakikisha hiyo empire inasimama! Kuna watu walifunga na kuomba dua kwa Mungu ili huo mji usimame! Kuna walio lia kwa changamoto mbali mbali walizopitia! Hivyo wewe kushupaza shingo lako na kutaka kukaa kwenye ‘throne’ ni uwendawazimu uliopitiliza!!

Haiwezekani, narudia kusema tena haiwezekani kuongelea Legacy ya mzee Mengi bila kumtamka mke wake mkubwa mama Mercy Mengi! Kama kweli ulimpenda marehemu kwa dhati basi lazima uheshimu jina la huyu mama! Tunafahamu kwasasa hayupo, lakini ana wawakilishi wake ambao ni Regina na Abdiel! You have obligation to respect watoto wa mke mkubwa kwani sio tu wanamuwakilisha mama yao bali na baba yao pia. Hao watoto ni chimbuko na kiini cha Dr. Mengi’s legacy! Waheshimu!

Makaburi ya ukoo wa marehemu mzee Mengi

Jacqueline, haiwezekani kamwe ukaongelea legacy ya mzee Mengi bila kutaja ndugu zake watumbo moja! Haiwezekani! Hawa ndungu ni watu ambao marehemu aliwapenda, aliwajali, na kuwaheshimu mpaka mauti ilipo mfika! Sisi tulio bahatika kusoma kitabu chake tumeona jinsi gani marehemu alivyo ongelea mchango wa ndugu zake katika mafanikio yake toka akiwa shule ya msingi! Yeye hakuwatenga wala kuwadharau sasa inakuaje wewe unaenda kinyume?

Post ya Jacqueline leo

Mmh! Sasa wewe ulitegemea nini ulipo iwekea pingamizi familia?! Haya makaburi yapo ndani ya family property hivyo wanahaki ya kukufukuza! Hata mimi ningekufukuza! Jacqueline, ngoja nikwambie, at this point you have proven to be nothing but one of the 21st century classic “homewreckers”!! And as usual Homewreckers wanatumia watoto kama kigezo cha uhalifu wao! Hawana uchungu na kuvuruga familia za watu kwani they care less for the people who “paved” the way! Nia yao huwa ni moja tu; kuchuma na kuvuruga familia za watu!! Homewrecker huwa haonagi shida kuvunja legacy ya mtu kwani hawajui vilianzaje na hata wakijua hawajali ili mradi wamepata wanachotaka! Ndio maana ni rahisi sana kwako wewe Jacqueline kuongelea huu mtafaruku kwenye mitandao kuliko watoto wa marehemu!

Nilikua nakupenda nabado nakupenda ila kwa hili?! Gal! You are deadly wrong! Halafu, acha kabisa kutumia watoto kuichafua hii family! Hao watoto wanauwezo wa kwenda kwao na kuona hayo makaburi muda wowote ule, usitumie watoto kwa hila zako! Hizi “bongo movie” zako hazita kusaidia kabisa! Usifikiri watu hawaoni mambo unayofanya! People are paying attention and they are puzzled!!

Ushauri wangu kwako, tafuta upatanisho na watoto wa marehemu pamoja na ndugu zake wa damu! Hauwezi kukalia kiti cha mzee Mengi eti unawakilisha familia ya Mengi na ukoo wake wakati ulikuta kuna mji umesimama! Hiyo itakuwa dharau kubwa sana na kuwavunjia heshima si tu watoto wa marehemu bali ukoo wote! Learn to humble yourself!

The Mengis’

Leave a Reply