“Nimechoka, sitakubali kuendelea kuona wanangu wakisononeka na sitakaa kimya.” *** Jacqueline Mengi

Naam! Hayo ni maneno yake mwenyewe Jacqueline Mengi aliyekua mke wa marehemu Billionaire Dr Reginald Mengi. Ujumbe huo aliandika kupitia account yake ya Tweeter na pia ku-share kwenye Insta-story yake! Kuna wengi wamemsapoti na kuhuzunika naye kitu ambacho kinaonekana kimemfariji Jacqueline hata kuandika tena ujumbe mwingine wa kushukuru leo hii kwa kutumia Insta-story yake (soma ????),

Ujumbe wa Jacqueline leo hii kwa Insta-story yake

leo hakupeleka Tweeter ?? najiuliza kwanini huu ujumbe wa shukrani haupo Tweeter leo? ?? nafikiri jibu lako halitakua na tofauti sana na lakwangu! ??

Jacqueline mpendwa, unajua kuishi na Wamarekani kumenifundisha mambo mengi sana na moja ya vitu ambacho nimejifunza na nimeamua kukitumia katika maisha yangu ya kila siku ni kua ‘kama kweli unampenda mtu kwa dhati basi lazima utamwambia ukweli mchungu’! Umwambii mtu ukweli ili kumnyanyapaa la asha! Ni ili umfungue macho na akili aone vitu kwa mapana na katika uhalisia! Wenye lugha zao wanasema “help them to see outside the box”!

Sasa mpendwa Jacqueline, mama wawili, Ooh! How I miss calling you muke ya Billionaire ?? naomba nikwambie ukweli but you have to understand it comes from a very place of nothing but PURE LOVE! Najua naweza nikawa nalugha isiyo kupendeza, unisamehe tu kwani somehow I’m taking it very personal kwa kuvaa viatu vya watoto wa marehemu Dr. Mengi na ndugu zake! Na pia hii mikasa inatokea kwenye familia nyingi za Kiafrika hivyo kwa upande mmoja au mwingine inanigusa!

Unasema umenyamaza kimya kwa mengi sana?! Ni mengi yapi hayo? Maana huku social media sisi ambao tunakufatilia hatujawahi kuona ukilalamika kuhusu jambo lolote juu ya watoto wa marehemu wala ndugu zake, hivyo kuandika ujumbe kama huu bila kuelezea japo kwa kifupi tu ili watu wajue kama wanakusapoti wanakusapoti kwa misingi hipi?! Unasema umechoka, hutokubali na hutokaa kimya?! ?? mmh! Hivi watoto wa marehemu mzee Mengi nao wakisema hayo maneno na wakaamua kuvunja ukimya wao hivi itakuaje??! Hivi utaweka sura yako wapi?!

Marehemu Dr Mengi akiwa na watoto wake Regina na Abdiel wakati wa msiba wa mke wake marehemu Mercy Mengi!

Labda nikuulize, hivi unajua watoto wa marehemu wamenyamaza kimya kwa muda gani sasa?! Toka wazazi wao walipo farakana nakutenga mpaka mauti ilipo watenganisha kama ahadi ya kiapo walichokula mbele za Mungu, na hatimaye sasa ni yatima, hao watoto umesha sikia wanaongea wapi kwenye hizi media?! Unafikiri wanamangapi mioyoni mwao ambayo yanawaumiza kimwili, kiroho, kiakili hata kisaikolojia lakini wamenyamaza nayo wanalia nayo huko ndani ya nyumba zao wakati taa zikiwa zimezimwa, madirisha yamefungwa, na pazia likiwa limeshushwa?! Na hayo yote wanavumilia kwasababu wanalinda heshima ya familia yao pamoja na Legacy ya baba yao ambayo wao wenyewe walimsaidia baba yao kuijenga!!

Marehemu Dr Mengi namke wake wa kwanza marehemu Mercy Mengi

Hivi, unajua Regina na Abdiel wanamaumivu kiasi gani ndani ya mioyo yao, kutoka kuzaliwa na kukua katika familia walioaminishwa kua inafuraha na amani mpaka wazazi kutengana, mara baba kuishi “single life” na hatimaye kuoa msichana ambaye ana umri sawa na “Mjukuu” wake?! Unataka kweli nao waseme wamechoka na ni muda sasa wa wao kuvunja ukimya?!! Jacqueline take that chip off your shoulder and learn to humble yourself!! Hao watoto wamenyamaza na mengi sana ndani ya mioyo yao, wanamaumivu makali sana only people with EXTRAORDINARY kind heart will understand maumivu yao! So, don’t play a victim card because it doesn’t give you any justice!!

***Itaendelea***

Leave a Reply