Pastor Caleb Migombo: Tunapokuwa watoto, mawazo yetu na kufikiri kwetu vinapangiliwa kutokana na uzoefu wa maisha tunayoishi

Kwa kiasi fulani, wewe na mimi tumepangiliwa (programmed). Tunapokuwa watoto, mawazo yetu na kufikiri kwetu vinapangiliwa kutokana na uzoefu wa maisha tunayoishi. Mpangilio huo wa namna ya kufikiri na kuishi hutokea kwa kila mmoja wetu. Lakini kama vitu ambavyo vimewekwa katika ubongo wetu na kumbukumbu za vichwa vyetu ni vibaya au si vya kweli, basi matokeo yake tunaweza kupata matatizo baadaye katika Maisha.

Kwa maana hiyo basi, kufikiri kwetu na mioyo yetu vinahitaji kupangilia upya; tunahitaji kuweka vitu vipya vizuri na vya kweli pale palipokuwa vitu vibaya amabavyo vimeeota mizizi ndani yetu…Na hapo bila shaka yoyote tunapohitaji msaada wa Mungu. Katika neno lake Mungu anatupatia ukweli unaofaa kuchukua nafasi ya uongo ambao umekuwa ukiuamini sikuzote kuhusu wewe na maisha yako.

“Wewe ni wa thamani machoni pangu, na mwenye kuheshimiwa, nami nimekupenda; …” ISAYA 43:4  In a sense, you and I get programmed. When we are young, our minds are constantly being programmed by the experiences we have. This programming happens to all of us. But when the things that have been put into our memories are bad and untrue, we will have problems later in life.

In that case, we need to reprogram our mind and hearts; we need to replace the bad things that has taken root there with good and true things. And that is where God can help. In His word, He provides truths to replace the lies you have believed about yourself.

“Since You are precious and honored in my sight, …I love you”.  ISAIAH 43:4

Leave a Reply