Simulizi za maisha ya mzee Igogo kwa maneno yake mwenyewe!

MATUKIO YA LEO 19.02.2020 KWA MFADHILI:- 1. Bi Mole Akungo, mjane wa marehemu Akungo fundi magari, aliyekuwa Mwajiri wa Mkurugenzi John Orwanda. Anaumwa kisukari na kasikia tuna dawa ya Jufeel, pamoja na kukosa uwezo wa kujikimu.

2. Dada yangu wa kihindi Bi. Dirishan mlemavu wa Kibiongo aliniita kumtembelea kwake, ndiye aliyekuwa mwenye ofisi ya mtaa wa mshihiri na eneo la kurasini, nilipoanzia kampuni ya Utegi. Walinisaidia mno nilipokuwa naanza kampuni.

3. Rafiki yangu Bi. Zainabu Mbuguni, mlemavu wa macho (KIPOFU KABISAA), Aliniletea zawadi ya kazi ya mkono wake, kikapu cha ukiri, aliyoitengeneza mwenyewe kuanzia kusuka ukiri na kushona kapu hilo, ili nimpelekee mama Igogo kwendea sokoni, pia kaniletea zawadi ya miwa anazolima shambani kwake huko Kibamba.

Pichani yupo na Mwanasheria Asha Nassoro Mwanasheria wangu, na Maria Patrick Kagose, Mfadhili wangu nilitumia tiketi yake ya Bus na treni akiwa mdogo, kuijia jijini Dar, kwa upendo wa Mama yake, Dada Theresia Olung’a Igogo, aka Mama Maria.

***Imeandikwa na Sir O.O Igogo na kuleta hapa na Alpha Igogo (Blogger)***

Leave a Reply