Usiumize kichwa chako na mipango ya mtu! Fanya yako!

Nafikiri kuna ugonjwa mpya wa umeingia  nashindwa kuelewa niupe jina gani. Sijui ndio ugonjwa wa “kuwashwa washwa” in Dr. Magufuli’s voice ?? baadhi ya watu wanapenda kufatilia mambo ya watu mpaka huruma! Sikujua mambo yangu yanaumiza watu kichwa namna hiyo! Am I such a big deal?! Sikujua asanteni, na hapo ni haka ka blog tu watu hamlali ??? ee Mungu endelea kumimina hizo baraka zako, mtumishi wako nipo teyari kuzipokea Baba, mimina Baba ??  Eti mtu unaangaika kutaka kujua kwanini amehamia Houston? Jamani kwani kuna dhambi gani mie kuhamia Houston!! Oh, nasikia unataka kuhamia? Nihamie wapi tena??? Mie hapa ndio Kigoma mwisho wa reli!! Yani mnakera nyie watu!!  …….watu wangejua kuna raha sana kufanya yako wasinge angaika na maisha ya mtu! Wewe mbaba / mama mzima mwanaume loser fulani anakutumia kufatilia mambo ya Alpha halafu na wewe unajiona mjanja eti unakubali ?? hivi unalipwa kiasi gani? Maisha yangu yanakuvutia eeh!? Basi wewe endelea kutembelea hii blog majibu yako yote utayapata hapa wala usiumize kichwa kumuuliza mtu! ……..Embu acha kuumiza kichwa na mipango ya maisha ya mtu mwingine fanya yako! ??

Leave a Reply