“Wanaume wenzangu! To spare maneno tusiongee kila kitu. Kwa wake zetu” *** Harris Kapiga

Reposted from @harriskapiga Huu ni waraka kwa Wanaume! Walio kwenye ndoa! Wasio kwenye ndoa! Na walio na wachumba!

Familia ya Harris Kapiga katika picha

Si kila kitu cha kuonge na mkeo / mchumba wako, hasa mapungufu ya wazazi wako! Walezi wako, jamaa zako wakaribu ndugu zako, Boss wako! Kazini / kwenye biashara yako! Wanaume wengi huwa tunadhani tunanogesha penzi kumbe tunaharibu.

Unaanza mama yangu bana omba omba sana, una mwambia mkeo hapo au mchumba! Dada zangu bana waongeaji sana! Wana madeni kila kona. Boss wangu bana ananionea wivu anafanya fitina nifukuzwe kazi. Sisi bana, tumezaliwa kila mtu na baba yake! Mama aliachaga shule kakimbilia kwa bwana! Bi Mkubwa bana wanamsemaga mchawi! Kuongea kila Kitu hasa mapungufu ya wazazi na jamaa zako wakaribu unaharibu mahusiano kati ya mkeo na hao unaowasema vibaya kwake!

Lazima tukubaliane kila mtu anamapungufu , hata wewe unaeongea unayo yakwako! Baada ya kuongea nakudhani unanogesha Penzi! Kumbuka mwanamke kiukweli wale sio ndugu zake! Hana feelings nao kiviile kama wewe! Sababu ni wazazi wako, na umemjaza sumu mkeo / mchumba wako, anajiweka mbali sasa! Unageuka mwanaume unataka mke apeleke watoto kwa bibi yao! Akawasalimie na wewe ulimjaza masumu Bi Mkubwa mchawi! Bi Mkubwa ana mdomo; Bi Mkubwa ni mama yako unataka uonekane mwema, umpelekee wajukuu! Mke kagoma sababu ulimjaza masumu na mapungufu ya kwenu! Mgogoro unaanza, ooo mke jeuri, hapendi mama, haendi kwa mama! Kumbe wewe ndo ulikuwa mbaya ukamharibu (mazungumzo mabaya huharibu tabia njema)

Wanaume tumeumbwa na koromeo ina maana kuna vitu tuvihifadhi pale! Nieleweke hasa mapungufu ya jamaa zako, wazazi, boss wako na ndugu wakaribu!

1Petro 3;7…… Kadhalika ninyi waume kaeni na wake zenu kwa Akili. Kwa akili ni pamoja na kuchagua mambo yakuongea kuendeleza familia kwa Amani; Mwandishi ka endelea kusema Na kumpa mke Heshima; mtu unaemheshimu huezi mwambia kila kitu utachagua vya kuongea!

Wanaume wenzangu! To spare maneno tusiongee kila kitu. Kwa wake zetu! Vingine tunaharibu! Sasa pale umejiachia umemwambia mkeo sisi tumezaliwa kila mtu na baba yake!Halafu akakufuma na sms ya mapenz! Akakasirika ukasikia! Malaya kama mama yako! Aliewazaa kila mtu na baba yake! Usirushe ngumi! Uliongea kila kitu – #regrann

Ujumbe mzuri sana! Hii tabia ipo sana hata kwa wanawake! Unakuta mwanamke anaongelea vibaya sana ndugu zake tena watumbo moja akifikiri kwamba mwanaume atamuona yeye ni watofauti sana kumbe hajui anajichimbia kaburi lake mwenyewe! Mimi huwa naamini mtu ambaye anaongelea mtu katika njia ya kutaka kumfanya yule mwingine aonekane hana thamani au ni mtu wa ovyo mara nyingi hua kuna mapungufu mengi ndani yao hivyo wanajaribu kuondoa attention kutoka kwao kwa kuamini kwa njia hiyo watu hawato ona mapungufu yao na kutokujiamini kwao. (trying to diverge attention from their weaknesses / insecurities by pointing other people weaknesses and flaws). Hivyo hiyo ni njia yao ya kujihami! Ni guilty ya kutokujiamini ndio inawasumbua. Japo wengine ni mashetani na mapepo ndio yamewajaaa.

Leave a Reply