Hongera Mr and Mrs Uchebe

Vitu kama harusi au interview ukiona nimechelewa kuweka jua bado sijatizama nikitizama lazima niweke. Bora niwe wa mwisho kutoa pongezi au kusema lakini niseme kitu ambacho ni sahihi! Mimi siyo shabiki wa "breaking news" hivyo nablog kwa style yangu ambayo napenda nikiandika kitu naandika  from the heart na siyo ushabiki "maandazi"! Naamini ndio maana wasomaji wangu wako loyal sana kwani kunakuwa na emotional attachment.  ??? Imenibidi nicheke kwanza, mnamkumbuka Muhaya eeh? Naye amekuwa zilipendwa ?? Nani anataka kufa kwa stress maisha yenyewe mafupi haya ?? Sasa kuna siku aliniambia kuwa eti "wasomi" wengi hawana emotional attachment kwa watu au situation kwani hicho ndio kitu kikubwa wanafundishwa shuleni ???? halafu huyo huyo akimaliza kuongea na wewe anasema "I love you" ??? I wonder kumbe ndio maana maisha ya wasomi wengi wa Tanzania ni Fake kama degree zao eeh!! Ile degree ya Dr Mengi ndio yakweli  peke yake ?? ?? well,  mimi sijui kuishi a fake life sina sababu ya kunifanya niishi maisha ya uongo and I don't consider myself msomi so wakwende huko na degree zao ??........ Anyway back to Mr and Mrs Uchebe Hii harusi ya Shishi babe binti wa Donald Trump  niliona picha  nikampa hongera kwa Instagram account yake lakini nilijua lazima nikipata muda wa kuitazama nitatoa pongezi rasmi hapa kwa blog! Wenyewe  wanasemaga "better late than never"! ....... Hongera sana Mr and Mrs Uchebe, ndoa yenu idumu katika Bwana. Ukabarikiwe uzao wa tumbo lenu milele na milele!

Shilole ulipendeza sana mno! Ulikuwa kama katoto fulani hivi ambaye baba yake anapesa fulani za kumwagwa ?? tatizo sasa bibi harusi wewe ukawa unaongea utadhani MC ??  jamaniii! Najua unapenda kuongea lakini kha!  Mpaka unamwita mtu " Mbwa wewe" ? wewe kiboko ?? Halafu Mungu alivyokujalia sasa amekupa mume mpole utadhani siyo Muhaya ???  Yani huyu kaka ni muungwana sana, halafu siyo mtu wa social media muombe Mungu sana ili aendelee hivyo hivyo! Huyu Shilole atakufaa sana hakuna raha kama kuwa na mume mwenye kumjua na kumpenda Mungu na anajitahidi kukuweka wewe karibu na Mungu! Maisha bila Mungu ni ushetani mtupu asikwambie mtu! Mpende mumeo mwaya!

Nimempenda sana jinsi marafiki zako walivyokupa zawadi za kukujenga! Yale mambo ya kununuliwa dinner set na TV is sooo 70's!! Watu wanakuletea zawadi ya vyombo vya plastic?!  vyanini? kwanza vinaleta cancer ??? hizi ndio zawadi!

My JoJo!! Kanoga eeh!! CCM oyee indeed ??  Hongera sana kwa kumpa zawadi nzuri sana hakuna kama elimu haswa ya kujua jinsi ya kufanya kile kitu unacho kipenda! ........ Halafu nyie wasichana ambao mnajiita "celebrity" embu muige mfano wa kuongea kama Jokate hapo! Hakuna kitu kina boa nakuonyesha some sort of kutokuwa smart and insecure kama msichana asiyejua kuongea kwa mpangilio wa maneno ya kueleweka!!! Yani wale wasichana ambao wanaongea utadhani ndio wanaanza kuota meno!! Au utafikiri hajui kiswahili kabisa anaishia  na "aaa" nyingi zisizo na mpango!! It's just boaring kwakweli! ..........Mwisho huyo MC aliyevaa T-shirt like really!!! Huo ni utovu wa nidhamu kwakweli! Umeonyesha dharau sana kwa Mr and Mrs Uchebe!! Shame on you!! Kila vazi na mahali pake, huwezi hata siku moja ukavaaa T-shirt au ndala kwenye harusi ya mtu!! Labda kama wewe unaroho ya kichawi!! Halafu T-shirt yenyewe mbaya utafikiri umetoka mazoezini!! Kwa mara nyingine tena, hongera sana Mr and Mrs Uchebe, mbarikiwe sana.

Leave a Reply