Hongera sana Magreth Rhoda Nyasungu!

Napenda kuchukua fursa hii kumpongeza mdogo wangu pamoja na shemeji yangu kwa maamuzi waliyochukua ya kujulisha koo mbili kuwa wanataka tuungane na tuwe wamoja. Hongera sana mdogo wangu kwa kuvishwa rasmi pete ya uchumba na kututambulisha shemeji / mkwe wetu rasmi.  Mungu akulinde na akutangulie mpaka siku ile tutakapo shuhudia ukila kiapo kitakatifu mbele za Mungu.  Ubarikiwe sana, we love you so much. To my handsome brother inlaw pongezi nyingi kwako kwa kufuata taratibu za kimila za kabila la Waluo na Wachagga katika kumposa binti yetu / mdogo wetu Magreth. Wewe sasa ni mmoja wa familia ya Igogo kwani posa na mahali umesha kabidhi, hivyo na penda kusema karibu sana ujaluoni, na karibu sana katika familia yetu..... nimekubatiza jina la "shemeji mzungu" kwani hiyo rangi adimu kwetu ?? Kwa faida ya wasomaji wangu ambao ni wageni humu; Magreth ni mdogo wangu tumbo mmoja, yeye ndio mtoto wa mwisho kwa mama yetu. Jina lake ni Magreth alipewa jina la mke wa family friends wetu ambao wana asili ya kijerumani (Germany). Sasa basi kwakuwa wajina wake ana asili ya watu weupe ndio akapewa nick name (jina la utani) ya lugha ya kiluo "Nyasungu" tafsiri yake ni mtu mweupe au mzungu. Hiyo "Nyasungu" kwasababu ni mwanamke angekuwa mwanaume angeitwa "Jasungu"! Wanawake katika mila za Mluo akitaka kutambulishwa kwa kutumia ubini wake au mahala alipozaliwa au asili yake lazima uwanze na "Nya" na kwa wanaume ni "Ja". Kwa mfano binti kutoka Kenya tutamuita 'Nyakenya' na mwanaume 'Jakenya'. Hilo jina la Rhoda ni jina alipewa ukubwani akiwa primary  school.  Ni jina la marehemu bibi yetu mzaa baba. Yani jinsi alivyokuwa akikuwa ndivyo kila mtu alikua akishangaa jinsi anavyofanana na bibi yani mpaka kucha za miguu. Wakati ule bibi alikuwa bado yupo hai hivyo hata yeye akawa anashangaa jinsi wanavyo fanana. Basi baba akawa anasema japo nimekupa jina la rafiki yetu Magreth itabidi nikubatize jina jipya la mama yangu. Basi toka wakati huo mpaka leo watu wengi wameshazoea kumuita Rhoda unless wale aliosomanao, wafanyakazi wenzake au wanao sali wote ndio wanamuita Magreth.

Mama mzaa  chema na binti yake Kutoka kushoto ni mama mdogo (Mrs Igogo-Junior), anyefuata ni Mrs Igogo -Senior, na kulia ni dada yetu Mrs Margreth Olambo Mabada Mama mzaa chema na wadogo zake Baba mzazi, baba mzaa chema  Sir O.O Igogo  Baba mdogo wa bwana harusi mtarajiwa kafunga safari kutoka Moshi kuja kushuhudia kijana wake akiposa. Ubarikiwe sana  baba. Mashangazi kutoka upande wa bwana harusi mtarajiwa   babu na wajukuu zakeNdugu wa bibi harusi mtarajiwa
Kwa mara nyingine tena, hongera sana Magreth Rhoda Nyasungu ??

Leave a Reply