Hongera sana Wema, nakutakia mafanikio zaidi ya haya!

Regrann from @wemasepetu – Napenda kuchukua nafasi hii Kumshukuru kwanza Allah Sub’hannah wata’Allah kwa kunifkisha hapa nilipo sasa… Najua ni mambo mengi sana yanafanyika kwa ubaya juu yangu ila yeye ndo amekuwa Tumaini langu kubwa… Nimshukuru Mama angu mzazi pamoja na familia yangu yote kwa ujumla kwa kusimama na mimi bega kwa bega katika kila kitu… . Nitoe n shukran zangu za dhati kabisa kwa Azam Tv kwa kutupa wasanii wote wa Tasnia ya Filamu fursa hii kubwa ya kuweza kujua nani zaidi… Hakika ni Changamoto nzuri sana na naiona inakuja kuleta mabadiliko makubwa kwenye Tasnia yetu…

Napenda kutoa Special thanks to my Love, The Woman behind The Best Actress 2018, My Tyler Perry, wanamuita Neema Ndepanya kwa kuniamini na kuniongoza vyema katika kazi… Najua upo very proud na nakuahidi kuendelea kuku make proud… We have so much to do mamy… @neema_ndepanya ….

Wema Sepetu Empire, Nawapenda sana watoto wangu… Nyinyi ni zaidi ya Ndugu sasa… Na tunaenda kufanya mapinduzi makubwa sana .. Maana sio kwa hasira nilizonazo sasahivi… . Last But Not Least…. Wema Lovers… Hizi tuzo ni zenu… Nawashukuru kwa kunipa endless support kila ninapohitaji… Bila nyinyi siwezi… Ntaendelea kuwapenda na kuwathamini mpaka siku nakata kauli…

Pia nichukue nafasi hii kuwashkuru wasanii wenzangu wote tulioshiriki kwenye tuzo hizi na kuwapa hongera maana hata kuwa nominated tu ni hatua kubwa sana… . Mwisho kabisa nawashkuru wasanii WOTE wa Tasnia ya Filamu kwa ujumla… Tutakutana mwakani tena kwenye TUZO… Inshallah…….. ?????? – #regrann
Ni bora kuchelewa kuliko kukosa kabisa! Hongera sana Wema kwa tunzo ulizoshinda. Nakutakia mafanikio mengi na makubwa zaidi ya haya!…. Nimeona ile interview umesema Naseeb a.k.a Diamond atakuwa boss wako. Hakuna ubaya wowote japo kwakweli nimesikitika! Sijasikitika kitendo cha wewe kuwa na show yako ndani ya Wasafi TV hapana! Hilo halina shida kabisa kilichonisikitisha ni kuwa Naseeb / Diamond anakwenda kuwa “boss” hapo ndipo nilipo natatizo nalo! Like why?! Ungenunua airtime ya kipindi chako kwa Wasafi TV au Radio lakini uendelee kuwa your own boss na Management yako mwenyewe?! Why are you degrading yourself my dear! Who is your advisor if any? Umeonyesha udhaifu mkubwa mno kwamba huwezi endesha maisha yako au kufanikiwa bila mkono wa Diamond!! Ona sasa wanavyo kufanyia vituko mbele ya kadamnasi dunia yote ikishuhudia!! Anyway, nimesikitika sana lakini ni mitihani ya maisha uichukulie katika positive angle though najua ni ngumu sana…… Kwa mara nyingine hongera sana. ?❤

Leave a Reply