Kheri ya siku ya kuzaliwa kwa mama yangu mimi!

Leo kazaliwa mama yangu mzazi, kipenzi cha roho yangu! Kwabahati mbaya afya yake imeleta shida kidogo. Lakini pamoja na yote hayo bado twamrudishia Mungu shukrani zetu za dhati kwani anastahili sifa zote na utukufu mkuu!

kama anavyoonekana hapo kwenye hiyo video akiwa mnyonge, ni baada ya kutoka hospital. Na mzamini wa pendo lake akiwa amemletea zawadi ya saa mpya na simu. ??

“Tumefika nyumbani. Mzaliwa mpya, aliye mgonjwa tumemkuta anaendelea vyema. Kapokea zawadi za Birth Day toka kwa Baba/Babu/Mfadhili na rafiki.” …. Maneno yake mzee O.O Igogo baada ya Kufika nyumbani akitokea safari.

Wazazi wangu ni wapenzi wa saa za RADO! Hii ndio aina ya saaa toka na kuwa mpaka leo hii naona wanazivaa tu! Sijawahi kujua kwanini labda siku nidodose! ?? Sindio “upaparazi” wenyewe huo! ??

Happy birthday mama, tunakupenda sana, na tunakuombea afya njema. Birthday itarudiwa pindi mjukuu wako number moja akifika hapo kesho kutwa. Tunaamini Mungu atakuwa amesha kuponya. Amen!

Leave a Reply