Pumzika kwa amani ya Bwana bibi Anna NYOLWENGO!

marehemu bibi Anna Nyolwengo akiwa na mwanandugu

“Ilianza kwa ajali ya kugongwa na pikipiki, ukavunjika mfupa wa nyonga, hospitalini ulikimbizwa kupata huduma, ukiwa umenyamaza kimya bila kujitambua, siku tatu baadaye uliizinduka na kuwatambua wanao, hata kwenye simu ukaongea na Otieno, kuimarika kwako iliwaruhusu madaktari kukusudia ufanyiwe upasuaji, wa kuunganisha palipovunjika, ukiwa na uhai wako wakakuchoma nusu kaputi, nayo ikazua balaa la kupoteza fahamu hadi jioni hii umetutoka Mama yetu ANNA NYOLWENGO, dada yako Rhoda alitangulia, ukabakia nasi ukooni, leo umetutoweka kwa utashi wa Mola TUNASHUKURU ????????” …… Sir O.O Igogo

Marehemu ni mdogo wake na bibi yangu mzaa baba! Pia mimi nilipewa jina la mama yao mzazi yani bibi yake baba mzaa mama! Jina langu hilo ni ARUA japo baba yangu huwa analiandika ARWA! ?? Marehemu bibi yangu mzaa baba wao asiliyao ni Kenya, ambapo ndipo na mdogo wake alipokuwa akiishi mpaka maiti ilipo mfika.

Hii wheelchair alinunuliwa wiki iliyopita wakiwa na tegemeo kuwa angetoka hospital salama baada ya kufanyiwa upasuaji. Wao walipanga kama wanadamu lakini mapenzi ya Mungu yametimuzwa! …… Poleni wanandugu na ukoo wote wa Nyolwengo. May our beloved grandmother Anna Rest In Eternal Peace! ????

“And said, “Naked came I out of my mother’s womb, and naked shall I return thither. The Lord gave, and the Lord hath taken away; blessed be the name of the Lord.” ………. Job 1:21

Leave a Reply