ADD Friends Campaign – Epsd 019: Adhabu ya Vyoo vya jamii kwa Watu wenye Ulemavu.

ADD Friends Campaign - Epsd 019:  Adhabu ya Vyoo vya jamii kwa Watu wenye Ulemavu.

Na Peter Sarungi (The Next Speaker)
Haja ndogo na kubwa ni moja ya matendo ya mwili ya lazima kwa viumbe vingi akiwemo binadamu. Umuhimu wake unatokana na kazi ya mfumo wa mkojo ambayo ni kutoa taka na sumu za mwili. Kwahivyo mwili huwa hauwezi kusubiri kwa mda mrefu badala yake kuna point inalazimika kutoa uchafu huo bila kujali uko katika mazingira gani.

Jamii inayo tuzunguka imekuwa ikitupa adhabu sana katika kupata huduma hii maana vyoo wanavyo jenga ni kwaajili ya kukidhi mahitaji yao ambayo mara nyingi kwa ustaarabu mdogo walio nao wengi wanachafua na kuweka hali hatarishi kwa jamii ya watu wenye ulemavu. Lakini pia vyoo hivyo vinakosa mazingira rafiki ya miundo mbinu kwa mtumiaji mwenye ulemavu kama vile vipimo vya milango, uwepo wa ngazi, maegemeo ndani ya choo, aina ya kifaa cha choo pamoja na uwepo wa maji safi na salama.

Jamii ya namna hii inayo tuzunguka haijali usalama wa afya na utu wa mtu mwenye ulemavu na hii ndio imekuwa ni changamoto kubwa kwa mtu mwenye ulemavu pale unapo amua kutoka katika mazingira uliyopo kwenda kwenye mazingira mageni wakati unapo toka ili kushiriki shughuli za uchumi, siasa na za kijamii.
Hili ni tatizo kubwa sana kwa mtu mwenye ulemavu, ni lazima awe mchaguzi sana katika kutafuta nyumba ya kupanga, awe makini sana katika kutumia vyombo vyetu vya usafiri wa umma, awe makini katika kuchagua mahala pa kufanya starehe na kadhalika.

#ADDfriends_Campaign tumeamua kubadili fikra hii ya mateso kwa mtu mwenye ulemavu. Ungana nasi kupaza sauti ili kujenga jamii ya walemavu iliyo salama.

Itaendelea.....

Leave a Reply