“Hivi, watu wote wanaoenda kusoma kwenye vyuo vikuu hesabu zao zote ni kuja kuajiriwa serikalini?”- Mimi Mwanakijiji

Swali la Jumapili: Nimesoma malalamiko na hata manung’uniko ya watu mbalimbali kuhusiana na kusitishwa kwa ajira serikalini hadi wakati fulani mwakani. Wapo wanaolalamika kuwa kusitisha huku kwa ajira mpya na kupanda vyeo kumesababisha watu waliohitimu vyuo na wengine kukkosa kazi na hivyo “kukaa nyumbani”. Hivi, watu wote wanaoenda kusoma kwenye vyuo vikuu hesabu zao zote ni kuja kuajiriwa serikalini? Inawezekana elimu ambayo vijana wetu wanapatiwa haiwaandai kuwa wabunifu na wavumbuzi (rejea mada yangu ya juzi) kiasi kwamba nje ya serikali au utumishi wa umma hawawezi kufanya lolote na hivyo kweli “wanakaa nyumbani”?fb_img_1477237341357

Leave a Reply