“Acha Alama nzuri mioyoni mwa wale wanaostahili”***** Zamaradi Mketema

Reposted from @zamaradimketema Leo nilikutana na watu walikuwa wanajadili jambo japo katika hali ya masihara lakini nikagundua makosa makubwa ambayo huwa tunafanya sisi binaadamu

Zamaradi Mketema na binti yake Shubi Ruge Mutahaba

Watu wengi husema ukipendwa Ringa, mi nasema hapana, Ukipendwa THAMINI, na ikiwezekana mkomeshe kwa kumpenda zaidi, wenye mapenzi ya kweli ni wachache mno Duniani, Make Sure ukimpata kuwa KILEVI chake, mfanye awe ADDICTED na wewe, mzoeshe ama weka utaratibu ambao hata itokee mmekosana ashindwe kukaa siku moja mbili kakaza, sababu kuna kitu tu anakosa, kuna watu wanahisi pozi ndio Ujanja, Pozi ni ushamba!! Especially kwa mtu anaekupenda, kama wanavyosema Dawa ya Moto ni Moto kwenye mabaya basi hata mazuri ni hivyohivyo, mtu akikupenda mpende zaidi, haupotezi unawekeza, hata kesho akiwa mbali, kitakachomuumiza ni hiko, lakini kama wewe ni mtu wa headache kilasiku hakuna atachokumbuka

Beautiful Zamaradi Mketema

Na hii haiapply kwa mume/mke ama mpenzi peke yake, ila hata rafiki na watu wema tunaokutana nao, Acha Alama nzuri mioyoni mwa wale wanaostahili kiasi kesho na kesho kutwa hiyo ndio silaha yako pale mtakapokuwa mbalimbali, ukijiangalia una chochote ulichowekeza kwa wale wakupendao!!? Unahisi wewe ni kilevi chao ama headache!!? Kuna Alama umeshaweka ama ndio Upepo utakapopita umepita!? Tafakari halafu chukua hatua

Nimejisikia tu kuongea hiki, Muwe na Usiku Mwema!! – #regrann

Leave a Reply