Category Archives: General

Jinsi nilivyo kuja Marekani!

Andrews university ndio chuo kilichonipa nafasi mimi ya kuja Marekani. Ngoja niwape story fupi ya safari yangu ya kuingia hapa.

Siku zote nilikuwa natamani kusoma /kuishi nje ya Tanzania.  Na mara nyingi nilikuwa napenda Australia, UK, na Marekani. Ilikuwa rahisi kujenga hisia zangu na maeneo hayo kwani mara nyingi nilivahatika kupata vijuzuu vinavyoonesha shule mbalimbali za nchi hizo. Basi, nikiwa katika muhula wa mwisho wa kumaliza chuo pale C.B.E siku moja nikiwa kanisani Temeke SDA, katika matangazo nikasikia wakitangaza kuwa chuo cha Andrew wanapokea wanafunzi kwa muhula wa Fall (Fall semester), na wakasema kuna vijuzuu kama kuna mtu angependa kwenda akachukue ili ujuwe jinsi ya kujiunga. Mara baada tu ya ibada, nikaenda kuchukua kijizuu. Baada ya siku kadhaa nikaenda kwenye intranet Cafe fulani ilikuwa karibu na chuo cha C.B.E. Ndio kwa mara yakwanza nafungua email akaunti yangu πŸ™ˆ Nikajaza fomu siku hiyo. Baada ya muda wa miezi kadhaa nilitumiwa barua kwa njia ya posta kuwa wamenikubali kuingia chuoni hapo kwaajili ya degree ya kwanza.  Wakati huo nilikuwa nimesha hitimu C.B.E sasa natafuta chuo cha kwenda.

Nakumbuka mmoja wa wadogo zangu (cousin sister) aitwaye Detta alikuwa akipenda kunitania kuwa “aah wewe ni wa hapa hapa tu” namwambia mie nakwenda zangu Marekani subiri utaona. Hapo sijajua kama nitachaguliwa au la! Ila yeye alikuwa anasema hivyo kwasababu dada yangu mkubwa alisoma China, kaka yangu alikuwa UK, na mdogo wangu yeye alikuwa anasoma South Africa. Hivyo akawa anasema mie nitabaki Bongo.

Ghafla, siku moja naletewa barua nikiwa job (niliajiriwa na Utegi Technical Enterprises Ltd baada ya kumaliza chuo), kuangalia ilipotoka nakuta ni Andrews University.  Nikaifungua haraka sana! Nikakuta ni barua ya kukubaliwa kujiunga na chuo ila sasa muda ulikuwa umebaki wiki 2 tu shule ianze πŸ™†πŸ½β€β™€οΈπŸ™†πŸ½β€β™€οΈ Nikachanganyikiwa maana hizo hela zinazo hitajika na muda uliobaki, dah! Yule mzee kutoka kanda maalum nitamuingiaje?! 🀣 Mtu wakwanza kumwambia alikuwa ni mama. Yeye akanipa moyo akasema hongera sana, mwambie baba haraka sana. Sasa kesho yake hasubui tumesha maliza kunywa chai tunataka kwenda kazini, mama akalipua bomu kimtindo. πŸ™†πŸ½β€β™€οΈ

Akasema “Umesha mwambia baba?”, nikajifanya kutoa macho πŸ˜… baba akauliza nini unataka kusema? Akasema (Akaniita kwa jina langu la kilugha) kaa chini “let’s talk ni nini”. Ikabidi nimwambie. Akasema sasa kwanini naogopa kusema jambo zuri kama hilo. Nikamwambie mzee nikienda siku yakwanza tu inatakiwa malipo ya awali ya nusu semester (muhula) au ada nzima. Kanijibu sasa tatizo ni nini? Kwani wewe ndio unatoa hizo pesa? Basi mzee wa watu siku hiyo akasimamisha shughuli zake zote, kuhakikisha napata documents zote zinazohitajika na kuzituma kwa njia ya fax na DHL. Chuo nao walikuwa shapu walipoamka tu wakatuma email kua sawa wanasubiria documents za DHL halafu watatuma I-20 (form maalum yakuombea viza ya shule). Mzee aliwaambia kutoka na muda watume kwa DHL halafu atawalipa hiyo pesa. Basi baada ya wiki 1-20 imefika. Nikaweka appointment ya kuomba viza. Tukaenda kwenye Viza, kumbuka nina siku tu zakuripoti shule, hivyo ticket ya ndege ilibidi nikate kabla hata ya kupata viza.
Kwenye viza si kidogo watuzingue! 🀣🀣

Basi, tumefika kwenye viza wala sikuhojiwa maswali mengi, wakasema kila kitu kipo vizuri lakini cheti changu cha form 4 ni “Fake”! πŸ™†πŸ½β€β™€οΈπŸ™†πŸ½β€β™€οΈ Wakadai tumepiga simu wizara ya elimu wamesema hizo namba sio zake. πŸ₯ΊπŸ₯Ί Wakasema kama mnaweza kwenda wizarani mkahakiki nendeni kisha mrudi hapa. Wakatupa reference namba, na jina la mtu walie ongea naye hapo wizarani. Basi, tukatoka mbio kwenda wizarani, tunafika getini tukasema jina la mtu tunayekwenda kumuona, wakampigia simu huyo mtu kumwambia kua kuna wageni hapa wanahitaji kukuona. Yule mtu akaomba aongee na baba, akasema samahani rudini ubalozini wanawasubiria kule tumesha tatua tatizo. Alikosea kusoma namba. 🀣🀣🀣 Baba akasema lakini nilimuuliza unahuwakika kuwa cheti cha binti yangu ni feki na akanijibu kuwa “100% sure”. Mzee hasira zikamshika lakini sasa atafanyaje inabidi turudi tena ubalozini. Sasa wakati baba anamaliza kuongea na yule.mtu wa wizarani, secretary wake akapiga simu muda huo huo akasema “baba mnatafutwa na ubalozi wa Marekani wamesema mwende sasa hivi”, baba akamwambia ndio tunaelekea huko, lakini hawa watu leo ndio watanijua mimi ni nani! 🀣🀣🀣 Usichezee mzee wa kutoka kanda maalum.

Basi tukafika ubalozini, tukapokelewa vizuri, yule mdada akaomba msamaha kwa usumbufu, akachukua passport yangu akasema kesho asubuhi uje uchukue na nakutakia masomo mema. Mzee Igogo sasa akaanza, “young lady I need an official oppology letter” 🀣🀣 Eti huwezi kunifedhehesha mbele za watu halafu unaomba msamaha kiholela holela namna hiyo. πŸ™ˆπŸ™ˆ Yani mie I was like just give my passport am ready to board. Nyie muendelee na drama yenu kimpango wenu. 🀣🀣 Nilipata passport asubuhi, usiku nikaondoka zangu siku hiyo hiyo.

Ilikuwa mara yangu yakwanza kutoka nje ya East Africa. Niliondoka na ndege ya British Airways, business class 😍😍 mzee Igogo sijui alifikiri nikipanda economy nitachelewa πŸ™ˆ Mwe! Nilifurahi sana. Tukafika UK, tukapelekwa hotelini kwa ajili ya kupumzika mpaka asubuhi kuanza safari ya kuelekea Chicago O’Hare International Airport. Baada ya kufika Chicago shulenilinielekeza kuchukua basi lakuelea Indiana. Waliniambia nishuke kituo cha mwisho ambapo ni Indiana Airport na hapo nitakuta gari la chuo cha Andrews likinisubiria. Nilifata maelekezo nikafika shule salama kabisa.

Nilifikia kwenye dormitories za chuo. Jamani acha tu! Unaingia kwenye dormitory ya chuo kama hotel vile. 😍 Nilikuwa na roommate mzungu kutoka Canada, alikuwa anaitwa Melissa Gonzalez. Vyumba ni self contained, mna bathroom na shower yenu kwa chumba, for a minute nikakumbuka mabafu ya C.B.E mabafu 3 watu zaidi ya 20 ni mwendo wa kusubiriana wengine wanaamua kuoga< kwenye kolido🀣🀣 Kwakweli,.Andrews ni shule nzuri sana sema gharama zake sasa! πŸ™†πŸ½β€β™€οΈπŸ™†πŸ½β€β™€οΈPasua kichwa.

Muhtasari wa kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Mercy.

Birthday girl herself

Siku ya tarehe 02, 04, 2023 ilikuwa ni siku ya kumbukizi ya mfanano wa siku ya kuzaliwa mwanangu Mercy.

Birthday girl akiingia kwenye mgahawa

Kama video inavyo onyesha hapo juu πŸ‘†πŸΏ Alianza kusherekea siku moja kabla ya siku yake maaalum kuwasaili, ambayo siku hiyo ilikuwa ni Jumosi ya tarehe 04/01/2023. Sambamba na marafiki zake walikuwa pamoja chakula cha usiku katika mgahawa ujulikanao kama TourΓ£o Brazilian Churrasqueria uliopo downtown Houston, Texas. 😍😍

Mtu na mama yake

Basi siku yenyewe ilipofika tulikuwa na muda mzuri pamoja asubuhi na jioni tukaenda tena kufanya kile twapendelea kufanya zaidi 😍😍 Kwakweli sina kingine mwaka huu zaidi ya kusema Asante Mungu wangu. Sifa na utukufu zote ni zako wewe Baba muumba wa Mningu na nchi na vyote vilivyoko. πŸ™πŸΏπŸ™πŸΏ

Asante Baba yangu. Asante Mungu wangu, Asante.

Muhtasari-Sehemu ya 4: Tulisherekea kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwao.

Twamshukuru Mungu kwa pumzi ya uhai anayotupatia kila siku ambayo ilituwezesha kuona na kusherekea siku ya kumbukizi ya kuzaliwa wapendwa wetu. Kulikuwa na birthday tatu mwezi wa Nane. Yakwanza ni ya mdogo wangu Janeth kama video inavyo onyesha hapo juu πŸ‘†πŸΏ,

Tulikutana Johari Rotana hotel tukala, tukanywa, na kufurahi pamoja sisi kama madada na wifi yetu mke wa kaka yetu. Yani hapo katika madada aliyekosekana ni Blessing peke yake. 😍😍

Ikafuatiwa na ya mume wake Janeth, shemeji Tobby mtu kati hapo juu!

kisha ya mama yetu mkuwa Mama Sarungi. Tulifurahi sana.

Twamshukuru Mungu kwa yote. πŸ™πŸΏβ€οΈπŸ™πŸΏ

Muwe na weekend njema.

Siku zote tukipata nafasi ya kuwa pamoja huwa namshukuru Mungu sana, na huwa naakikisha nampa mwanangu 100% ya my attention! 😍😍 She’s everything to me! Kutokana na ratiba yake ya shule pamoja na kazi muda mwingi huwa tunapishana. Hivyo nyakati kama hizi ni muhimu sana kwetu sote. Si kwa uwezo wetu bali ni kwa neema yake Mungu Mwenyezi. πŸ™πŸΏβ€οΈπŸ™πŸΏ

Haya nawatakieni weekend njema na Sabato njema sana kwa waaminio.

The two digits era!

Blessing

Jamani rahaaa! Mwenzenu naringaje sasa kadogo kangu kanakuwa kadada. The two digits era began just like that ma’am! 😍😍

Mwenye birthday yake katika pozi na tabasamu kama lote kufurahia miaka 10 ya uhai wenye afya na baraka tele. Sifa na utukufu twamrudishia Mungu Mwenyezi. πŸ™πŸΏβ€οΈπŸ™πŸΏ

I’m lost of words! She’s a beautiful young lady. Mungu azidi kutembea nawe mdogo wangu ukawe kiumbe kizuri umpendeze Mungu kisha mwanadamu.

Akiwa kwenye matembezi huko Turkey wakati wa summer mwaka huu. Sasa hiyo kijana inafanana na ragi ya chama pendwa ya dad yako πŸ˜…πŸ˜…

Awwih! Once again, happy 10th birthday Blessing. Love you mingi.

Muhtasari -sehemu ya pili: Jambo lililonifurahisha zaidi mwaka 2022 ….!

Mama na mwana 😍

Kamanilivyosema kwenye posti yangu iliyopita somahapa yakwamba mwaka 2022 ulikuwa na baraka zake nyingi sana. Basi katika kuhesabu mibaraka yangu naweza sema huu nao ni moja ya mbaraka mkuu. Ni jambo ambalo lilinifurahisha zaidi 😍😍 Ni surprise niliyo wafanyia wazazi wangu.

Tarehe 25 mwenzi wa Saba, mwaka huu wa 2022 (07/25th/2022) ilikuwa siku ya furaha sana baada ya mipango yangu ya kuwafanyia wazazi wangu haswa mama yangu safari ya kuwasalimia bila ya kuwapa taharifa kama ilivyokua huko nyuma. Nimpango ambao nilipanga na mdogo wangu aitwaye Magreth Otieno Igogo a.k.a Mrs Jacob Massawe kuwa tutamfanyia mama surprise wakati wa siku yake ya kuzaliwa ambayo ni tarehe 27th July. Bahati mbaya ratiba yangu ilibidi nifike siku mbili kabla ya birthday yake. Mimi nilichukua likizo na kuandaa safari bila kumwambia mtu yoyote nyumbani isipokuwa mdogo wangu, mume wake na mwanangu tu. Sikutaka mama ajue kabisa hivyo kuzuia wanafamilia wengine kujua hata marafiki ilikuwa muhimu sana. Nashukuru Mungu kila kitu kilikwenda vizuri kama tulivyopanga tuliomba kibali cha Mungu kwa kumkabidhi mipango yetu naye akaibariki ikatimia. πŸ˜πŸ™πŸΏπŸ˜Safari yangu ilianzia Houston, Texas.

Nakumbuka siku nakwenda airport tulimpigia mama simu, akiwa nyumbani na baba na shangazi yetu fulani wakipiga story zao, nikaanza kumuuliza anampango gani na birthday yake?! Akawa anasema nahamu namtoko fulani amazing πŸ˜…πŸ˜… lakini ameshapanga kwenda Fun city na watoto wake wa shule (school trip). Nikamwambia kwautani nikikutumia Dola Mia ($100) uongezee kwenye hiyo trip itatosha? akasema itatosha sana. Nikamwambia basi nitakutumia tarehe 25, ambayo ndio tarehe nilikuwa najua naingia nyumbani. πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… Basi nikamalizia kwa kumwambia wakifunga shule apange trip yeye na wadogo zake na dada zake waende kutembea Zanzibar au mbuga za wanyama, wafanye bageti halafu anijulishe. Akashukuru kweli kweli bila kujua mimi hapo naingia uwanja wa ndege teyari kwa kum-surprise! 😍😍

Sasa, ilikuhakikisha chumba changu kipo katika hali nzuri mdogo wangu alimdanganya mama kuwa ana wifi yake anakuja toka Japan na ana mtoto mdogo hivyo anaomba aandae chumba cha dada Alpha (eeh usishangae sana, nina chumba changu kwa mama yangu 😍😍) ili afikie humo kwa siku kadhaa kabla ya kwenda Moshi. πŸ˜…πŸ˜… mdogo wangu wanaishi nyuma tu na kwa mama. Basi mama naye bila shaka wala kinyongo akamkubalia pasi kujua mwenye chumba yupo njiani. πŸ˜…πŸ˜…Nilipofika airport nilipokelewa na mdogo wangu pamoja na mume wake. Tukiwa njiani mdogo wangu akampigia mama simu akamdanganya kuwa amekutana na rafiki yake walikuwa wote huko kijijini Kowak (kijiji alipozaliwa mama yetu), na anasema hawezi kwenda kwake mpaka afike kumsalimia. Mama akanza kuuliza ninani? mdogo wangu alikataa kata kata kusema akamwambia ni surprise akifika hapo itabidi asikilize sauti yake ili amtambue ni nani! Mama alimbembeleza sana amwambie ni nani huyo lakini mdogo wangu alishikilia msimamo kuwa utamuona wakifika. Mama kidogo akawa kama amechukia kwani alikua anasema unakuja na mgeni mimi hata kupika sijapika hata juice ndo kwanza wanatengeneza sio vizuri na hapendi kabisa. πŸ˜…πŸ˜… mdogo wangu hakubadilisha msimamo wake mpaka tukafika nyumbani, na mengine yote yamebaki kuwa historia kama hiyo video ya tukio hilo inavyo onyesha. πŸ˜…πŸ˜…

Hii ni mara ya pili sasa nafanikiwa kuwa-surprise wazazi wangu. Tarehe 07 mwezi wa tatu, mwaka 2017 kwa kushirikiana na wadogo zangu pamoja na baadhi wafanyakazi wa Utegi Technical Enterprises Ltd (kampuni anapofanyia kazi baba yetu) tulifanikiwa kum-surprise baba yetu ofisini kwake, ilikuwa siku ya birthday yake. 😍😍 Tuliwahi sana ofisini kabla yake kitu ambacho hajazoea kwani siku zote yeye ndio anakuaga wakwanza kufika. Tukaingia ofisini tukazima taa sehemu ya mapokezi ili akiwa kwa nje ajue hakuna mtu. halafu tukamwambia mlizi arudishie tu mlango asifunge na funguo, na geti arudishie bila kuweka kufuli ili akifika tu ashtuke na akasirike (just to annoy him) kuwa waliacha mlango na geti wazi jana jioni. Sasa alipofika mlangoni anakuta ipo wazi akasema ooh! Tumesha ibiwa hapa, hasira zikamshika kuwa geti halikufungwa jana jioni. Halafu mdogo wetu aitwaye Guka ndio tulimuacha nje awe ana mmonita (monitoring him) kwa kutupa taharifa kwa simu kuwa ameshafika kwa parking lot. πŸ˜…πŸ˜… Na Guka alikuwa anawasiliana na dereva kusema wapo wapi. πŸ˜…πŸ˜… Tazama video hapo chini πŸ‘‡πŸΏπŸ˜…πŸ˜…

Basi, alipopita tu mapokezi kuingia eneo la secretary wote tukasema “surprise” kwa nguvu na furaha huku mmoja wetu alikuwa kwenye switch ya kwashia taa, tukaanza kuimba “happy birthday to you” πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜ alishangaaje, hasira zote zikaisha hapo hapo. πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… Hakuamini kuwa watu waliweza kuwahi kazini mapema hivyo ilitu wam-surprise! Alishukuru sana na furaha nyingi mno.

unaweza itazama video yote ya surprise kwa kupitia YouTube yangu hapo chini πŸ‘‡πŸΏ

Baba na mwana 😍

Kwakweli ni furaha kufanya jambo ambalo linamfanya mtu mwingine kuwa na furaha na kujisikia vizuri kwa kujiona mwenye thamani, lakini nifuraha zaidi kufanya jambo linalowafurahisha wazazi wako. Nafurahia na najisikia vizuri pale ninapoweza kuwafanya wazazi wangu wafurahi zaidi. Ni mbaraka wa pekee. 😍😍 Counting my blessings ma’am! πŸ˜…πŸ˜

Chumba cha dada Alpha

Na story zitaendelea maana mama Igogo alikuwa haamini alichokiona. 😍😍

Surprise ya mwisho iliharibika πŸ˜…πŸ˜… tulitaka dada yetu naye am-surprise mama lakini dakika za mwisho akaamua kumwambia kua anakuja halafu hata hakutuambia kuwa kamwambia mama hivyo ikawa surprise kwetu. πŸ˜…πŸ˜…πŸ™ˆπŸ™ˆ kwakweli hii ni the best moment for 2022.

Cecy-mama mzazi

Miaka takriban 3 iliyopita dada yangu naye alim-surprise mama big time. Alikuwa mjamzito na wakati uchungu umeanza akampigia mama kumsalimia basi wakaagana vizuri. Ndani ya masaa 2 mume wake anampigia mama simu kuwa mama Dani amejifungua mtoto wa kike na wameamua kumrithisha jina la mama. Mama akawa hataki kuamini anasema mbona mama Dani nimeongea naye muda sio mrefu? 🀣🀣🀣 akaambiwa pale anakupigia alikuwa ameshikwa na uchungu na tulikua njia kwenda hospitali. πŸ˜…πŸ˜… Na mtoto mwenyewe ndo huyo hapo πŸ‘†πŸΏ juu. 🀩🀩

Muhtasari wa matukio ya mwaka 2022 -sehemu ya kwanza.

Dec 2022

Mwaka 2021 niliufunga vyema na kuufungua 2022 vizuri sana. Namshukuru Mungu kwani umekua mwaka mwema sana wenye mibaraka mingi. Changamoto katika maisha hazikosekani kwani hatuwezi kujua tu imara kiasi gani kama hatutapitishwa katika changamoto hizo.

Daughter

Wanasema dhahabu au madini yoyote ya thamani hayapatikani juu ya barabara wala kando kando ya maji! Nilazima yachimbwe chini ya ardhi na yapitishwe kwenye moto mkali ndipo yawe haya madini tunayofurahia kuyaona. Hivyo, sikuzote tukipata changamoto tusikimbilie kusema “kwanini mimi?” Bali tumwambie Mungu najua hili ni darasa unanipitisha japo somo bado sijalielewa, naomba unipe HEKIMA ya kuweza kulielewa somo hili ili nifuzu mafunzo yangu vyema. Najua maumivu ninayopitia nikwaajili ya utukufu wako na mimi ndiye uliyenichagua kuwa kielelezo cha utukufu wako.

Basi kwa kusema hayo, naomba niweke kumbukunbu ya matukio yaliyozunguka maisha yangu mwaka huu wa 2022. Tukumbushane kushukuru katika kila jambo. Sikuzote tuhesabu mibaraka yetu kwani ni mingi mno sema tunafunikwa na upofu kwa kuangalia maisha ya watu wengine na kudhani kuwa wamebarikiwa kutuzidi. Hapana! Mungu anatubari sote kwa jinsi impendavyo yeye kwa wakati wake.

Hizi ni baadhi ya picha tulipiga mwanzoni mwa Dec 2021 tulikuwa maeneo ya tunako ishi karibu na NASA Space Center, Houston, Texas

Baadhi ya picha tulizopiga kwenye Christmas party 20021 iliyofanyika Hilton hotel, Houston, Texas.

2021 THC Thanksgiving Gala
April 2nd 2022

Mwenyezi Mungu alitubariki tukafurahia kuona mwanangu ameongeza mwaka mwingine. Ilikuwa siku ya Jumosi tarehe mbili mwezi wa Nne! Na zifuatazo ni baadhi ya picha ya siku hiyo.

Mama na mwana 😍

Nitarejea ….!

Hello wapendwa wasomaji wangu, poleni kwa kutokua nanyi toka mwaka 2022 uanze. Nitarejea muda si mrefu, kuna plugins ambazo zinatakiwa ziwe updated lakini kila nikijaribu zinaleta shida kwa blog. Hivyo WordPress na Godady wanashughulikia. Yani hata hapa nafanya majaribio.
Asanteni sana kwa uvumilivu,mbarikiwe sana.

AMETIMIZA MOJA YA NDOTO ZAKE!

Mercy akiwa na Dr Kapesa

Siku ya leo tarehe 08/16/2021 majira ya mchana masaa ya Africa Mashariki, mwanangu katimiza moja ya shahuku yake kubwa au nawezasema moja ya ndoto yake!

Amekutana na mmoja wa madaktari walio nihudumia na kuhakikisha anaingia katika dunia hii akiwa salama! ?? Marehemu Dr Amood alikuwa ndio my primary Dr lakini alinikabidhi kwa Dr. Kapesa na Dr Kaisi kama mbadala wake pindi yeye anapokuwa na majukumu mengine. Siku ya kujifungua Dr Kaisi ndio aliyekuwepo zamu, Dr Amood aliitwa na alipofika Mercy alikuwa teyari kazaliwa! ??

Mungu azidi wabariki wote Dr Kapesa na Dr Kaisi! Bahatimbaya Dr Kaisi alipatwa na stroke (kiharusi) hivyo kwasasa amepumzika kufanya kazi za utabibu aliyosomea.

BTW, nilikuwa natibiwa Tanzania Maternity Service ambapo madaktari hawa wote walikuwa business partners!

Mwanangu mimi ….!

Unajua saa nyingine huwa siamini kama ni mwanangu ?? Mwenzenu nimekuza! Nikiangalia tulipotoka na tunapoelekea yani hakuna ninachokiona zaidi ya mkono wa Mungu ukiwa juu ya vichwa vyetu kumimina mibaraka yake.

Namshukuru Mungu sana na nitalitukuza jina lake milele. Kanipa rafiki wa milele. Tumekuwa pamoja, tumejifunza mengi pamoja, haswa kupitia makosa yangu mimi kama mama yake, yakampa somo la moja kwa moja. Mungu ni mwema sana. Nimevuka stage ya kuwa strictly mama; sasa hivi ni mama plus rafiki. Tunaongea na kuelekezana kirafiki tu! Kama malezi niliyompa kabla ya miaka 18 hayakumuingia na kumtengeneza kuwa kiumbe bora basi katika umri huu hakuna kitakacho mbadili zaidi ya kumuombea tu! Namshukuru Mungu sanaaaaaaa, mwanangu hajawai kunisumbua hata kidogo. Mungu kanibariki na mtoto msikivu, mwenye hofu ya Mungu, yani ni mtoto mwema mnoooo ndio maana saa nyingine siamini kama nimemlea mimi! ?? such a beautiful, humble, strong, smart, intelligent, classy, loyal, hard working, independent, charming young lady. I mean the list can go on and on but glory and honor all to Almighty God! ??

Leo nimejisikia kupost picha zetu haswa zahuyu mrembo wangu! ?? Kwani kunatatizo?! ?? sikuhizi nimeachana na kupost picha za watu haswa tusio na undugu, urafiki au mazoea. Ndio maana mnaniona sipost mara kwa mara. Nafanya mambo yangu mengine ambayo yananipa furaha na amani zaidi na hayo ndio nitakuwa napost humu.

??

Nimejisikia kumpost kuweka kumbukumbu ?? si blog ya mama yake jamani! ?? Ndio raha yakuwa na kitu chako mwenyewe ulicho kitengeneza wewe mwenyewe kwa utashi wa akili zako na mikono yako miwili. Hakuna atakaye kupangia nini cha kufanya labda huyo mtu ni punguani! ?? ………… Mungu azidi kumbariki sana na kumpa afya njema. ??

Kheri ya siku ya kuzaliwa kwetu!

Siku ya leo mika zaidi ya arobaini iliyopita nilizaliwa mrembo mimi! ?

Namshukuru Mungu kwa kunipa kibali cha kuona mwaka mwingine!

Namuomba azidi kunishika mkono katika mwaka huu kama ulivyofanya mwazo! ????

Naamini nimejiandaa kadri ya uwezo wangu katika umri huu mpya. Nimesafisha uchafu karibia wote katika kila kona ya maisha yangu! Nimefanya maamuzi ambayo mimi mwenyewe nikikaa chini nasikia furaha moyoni mwangu! Fake friends nimewapa mkono wa kwaheri! Bila chuki wala hiyana! Well! No one cries when fake friends say goodbye! Ni Xmas tuu to me! ??

Kuna mpumbavu mmoja (excuse my language) kwa muda sana alikua anazunguka kupandikiza chuki juu yangu, kapandikiza chuki kweli kweli! Lakini hakujua kua kuna Mungu, na kwa uwezo wa Mungu mwaka huu nimetuliza. Mwanzoni nimetamani sana kumpeleka kwenye vyombo vya sheria, lakini nimeamua kumpuuza! Nimemuachia Mungu atajua nini chakumfanya!

New age, New soul, New attitude! Ni mwendo wa #Kanyaga kwakwenda mbele! Nimeshaucheza huu wimbo zaidi ya mara 20 wiki hii! ?? I am truly feeling it! Yani kitu kikinikera nasitaki kukipa my attention naimba tu #Kanyaga halafu najikuta naachana nacho! ???? ….. Namshukuru Mungu kwa yote! Happy birthday to me!

Pia leo amezaliwa mrembo Dia Alex Odemba! Naye twamshukuru Mungu kwa mibaraka yake! Happy birthday to her!

Zifuatazo ni salamu kutoka kwa baadhi ya ndugu!

Happy birthday to us! ????

“Yesterday I was in that meeting as from 8 am till 4.30 pm, Chaired by Her Excellency President Samia Suluhu Hassan. Then today we were in the meeting Chaired by the Hon. Prime Minister, Majaliwa Kassim Majaliwa, as from 9.00am till at 4.30 pm. No wonder I forgot to Congratulate you timely.??‍♀️

BELATED Birth Day Greetings. Better LATE, than NEVER. It was yesterday, when you counted another additional 365 days after your last Anniversary, that makes you more healthier spritualy and emotionaly. We are proud that as we age down to our seventies, you are as well aging up to become our care taker, a daughter in America whom we shall be Visting and staying with at her place, to share the little blessings of her with abundat Love from her inner heart, as we do Love her. Arwa Nyangaji, Dani Min Rhoda Nyolwengo aka “Agali Nyogot” Take Our Late birthday Wishes, knowing that we are aging down and becoming more forgetfull. Baba & Mama.”

Kitchen party ya RHoda Igogo

Bibi harusi mtarajiwa Rhoda Alexander Igogo

Wakati tukisubiria picha kutoka kwa wataalamu waliolipwa kufanya kazi hiyo, basi tuanze na tulizonazo.

Siku ya jumapili tarehe 05 /16 /2021 ilifanyika sherehe ya kumfunda mwali (bibi harusi mtarajiwa) a.k.a Kitchen party ya Rhoda Alexander Igogo. Sherehe hii aliandaliwa na mama yake mlezi akishirikiana na ndugu na jamaa pamoja na marafiki. Ilifanyika kwenye makazi ya wazazi walezi huko Segerea ambapo bibi harusi mtarajiwa ndipo anapo ishi na ndipo atakapotokea kwenda kwa mwenza wake.

Akiingia ukumbuni mwenye nyuso ya furaha na tabasamu kama lote ndio mama mzazi wa Rhoda na Isaka, Mrs Joyce Alexander Igogo. Ni mke wa marehemu baba yangu mkubwa (wapili kuzaliwa kwenye familia yao baba, watoto bibi Rhoda Nyakanga Olwengo). Babu yangu mzaa baba (Marehemu mzee William Olung’a Igogo) alikuwa na wake watano (5) ??? usishangae sana maana marehemu babu yake baba (my great grandfather) Chief Sarungi Igogo yeye alikuwa na wake 19 ??????? welcome to our ukoo ?? …… Rhoda ndio mtoto wa mwisho kwao. Akitoka kuzaliwa Isaka ndio Rhoda anafuata. Na harusi zao zimekuwa ndani ya mwezi mmoja. Familia hii inajumla ya watoto 7 walio hai, mmoja alifariki. Grace a.k.a Anyango, Aphino a.k.a Nyawade, Kenneth (Marehemu) a.k.a Ukombozi, William a.k.a Mzee, Dr. Obadiah, Isaka, na Rhoda a.k.a Nyolwengo, na Emilia Igogo! ….. Mungu ni mwema sana.


Haya embu tufurahishe macho kwa hizi tilizonazo!

Pichani ni Dia Alex Odemba na bibi yake mama Igogo.

Dada kama dada! Huyu ni dada yake Rhoda aitwae Aphino.

Dia Alex Odemba katika ubora wake!

Mama wa isadoricakes_and_sassyjuice. Dogo langu Mwalimu mwenye ujasiriamali wake! ??

bibi harusi mtarajiwa akikata cake yake

Kwamahitaji yako ya Cake nzuri zenye ubora wake, juice fresh tamu, na Mc wa kitchen party, tafadhali husisite kumtafuta @isadoricakes_and_sassyjuice ndio habari ya taifa! ???

Kutoka kushoto ni mama yangu mzazi, akifuatiwa na mdogo wangu Vumi Sassi, anayefuata ni mdogo wake mama yangu (kitinda mimba kwa familia yao) napia ni mama yake Vumi aitwaye Magreth Cornel Awiti a.k.a Mrs Agonda Sassi, na anayefuata ni mdogo wangu kipenzi Magreth Rhoda-Nyasungu a.k.a Mrs Massawe.

?? mama zangu hao! ??

Rhoda akiingia ukumbini kwa furaha kabisa

Mama mlezi wa Rhoda

Mrs Vetto Igogo (kushoto) pamoja na Mrs Isaka Igogo (kulia). Mmemuona bibi harusi wetu wa wiki iliyopita?! ?? Miguu imeiona? Miguu halisi ya Kiafrika! Yani wana miguu ya bia kama mawifi zao! ??

Baba naye hakutaka kupitwa na matukio katika picha ?? akiwa na furaha kubwa pamoja na binti zake akitaniana na ucheshi wa hapa na pale.

Mtu na wifi zake! Mrs. Massawe kwa mbele hapo, Mrs Vetto Igogo mtu kati, na Mrs Isaka Igogo nyuma hapo.

Wifi karibu sana Utegi!

Watu wakiserebuka kwa raha zao!

Mke ya Mrombo! ??

Mwenye nguo ya njano, anayecheza kwa hisia zote, ni dada wa bibi harusi mtarajiwa, aitwaye Grace Alexander Igogo a.k.a Anyango, yeye ndio mzaliwa wa kwanza kwa familia yao. Anafurahia kusindikiza kitinda mimba kuanzisha familia yake. Pembeni yake ni mama mlezi wa Rhoda.

Mama naye hakutaka kujivunga kwani wimbo wenyewe siunausikia? ???

Haya tunamtakia Rhoda safari njema katika kuhitimisha kilele cha sherehe za kuagwa kwake na familia yake mpaka siku ya harusi. Jumapili hii ni Send-off yake na Jumapili ijayo ndio harusi. Mungu awatangulie katika kila jambo!

BTW, hii siyo mara yakwanza kwa familia yetu kuwa na harusi mbili kwa mpigo (double wedding), kaka yangu mkubwa Vetto Igogo na dada yangu Elline Igogo harusi zao zilipishana wiki tu, tuliserebuka kwa wiki mbili mfululizo! Yani tulianza na kitchen party ya dada Elline, ikafuta harusi ya kaka Vetto, ikaja Send-off party ya dada Elline kisha harusi yake. Na baada ya hapo ikafuata sherehe ya kuvunja kamati. ??? I tell you, this familia loves to partyyy! Nahiyo ni miaka ishirini na mbili (22 yrs ago) iliyopita. Na sherehe zao Ilikuwa kubwa kweli kweli hizi ni chamtoto! Mama zigi-zig catering na Dotnata Catering walipika mpaka walishangaa. ???

***Updates: picha za nyongeza***

Rhoda na binamu yake Honorable Madam Judge Dr Modesta Opiyo.

Rhoda na mama yake mzazi

Juu ni mama mkwe wake Rhoda Mrs Scola Oguna Ollal.

Mawaidha ya akina mama, shangazi, na wanawake wachanga kwenye ndoa.

Mama mdogo Mrs O.O Igogo akitoa ombi la kwanza.

Mama mdogo Mrs Agonda Sassi akitoa ombi la mwisho. Walianza na Mungu wakamaliza na Mungu. Amen!

Kwa picha zaidi bonyeza ????

https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/pendokitchenpartyphotos/

Rhoda na rafiki yake, hizi ni pre-wedding pictures

Blessing latika ubora wake

Wadada hao! ??

Kwa picha zaidi bonyeza ????

https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/rhodapresendoffphotos/

Nyumbani kumenogaaa …….!

Jamani-Jamani! Nyumbani kumenogaaa! Kama ilivyokua kawaida yao basi wametia timu tena!?? Mashangazi kwa wajomba, mama wadogo kwa wakubwa, baba wadogo kwa wakubwa, makaka kwa madada, bila kusahau mashemeji.

Si wengine bali ni familia ya marehemu Mzee William Olung’a Igogo wa Utegi, Rorya leo wamejumuika nyumbani kwa mzee O.O Igogo huko Segerea, Dar es salaam kwa maandalizi ya ndoa ya kijana wao ambaye ni mmoja wa wajukuu wa marehemu mzee William Olung’a Igogo ajulikanaye kama Isaka Alexander Igogo itakayo fanyika siku ya Jumosi tarehe 05 /08 / 2021, Dar es salaam, Tanzania.

Pichani juu ni maharusi watarajiwa bwana Isaka na Bi. Sarah katika pozi!

Basi, nami dada mtu napenda kuwatakia ndugu zangu kila la kheri katika hatua zilizo baki katika kutengeneza historia nyingine tena ya kuanzishwa kwa familia ya Bwana Isaka na Bi Sarah! Mungu awe azidi wabariki na atembee nanyi mpaka mwisho wa jukumu hili muhimu sana la kuunganisha koo mbili kua kitu kimoja! …. Nasikitika sijaweza kushiriki nanyi lakini nipo nanyi kiroho na kifikra! …. BTW, kwa msiofahamu udugu wangu na bwana harusi mtarajiwa ni hivi; Isaka ni mdogo wangu, yeye ni mtoto wa marehemu baba yangu mkubwa Alexander Olung’a Igogo. Baba yake ni mtoto wa pili kuzaliwa kwenye tumbo la bibi yangu akifuatiwa na baba yangu. Isaka alizaliwa na ulemavu wa kusikia na kuongea (kiziwi na pia ni bubu), hivyo kutoka na changamoto hizo baba yangu alimchukua na kumleta kuishi nasi Dar es salaam toka akiwa na miaka 5! Hiyo ilikuwa kwa madhumuni ya kumsaidia aweze kukaa karibu na wataalamu wenye ubobezi wa matatizo yake pia aweze kupata elimu stahiki!. Wengi wasiotufahamu vizuri huwa wanafikiria ni mtoto wa baba yangu kwasababu amekulia kwetu toka akiwa na umri huo. Ukweli ni mtoto wa kaka yake baba.

Mbarikiwe wote!

Ramadan Mubarak!

Kheri na baraka ya mfungo wa Ramadan kwa ndugu zangu, marafiki, na wafuasi wangu wote ambao ni waumini wa dini ya Uislamu. Mbarikiwe sana. ❀

Ramadan Mubarak to all my Muslim family members, friends, and fans! May it be Joyful and glorious! ❀

R.I.E.P uncle Zou Fu!

As family of O.O Igogo, we mourn the tragic death of our best friend, business partner, and family friend Sir. ZOU FU QIANG (in dark-red Tshirt) that happened in China earlier today! Our prayers go out to his family, friends, and everyone who is touched by his death!

From left Mr Molnar, Mr Igogo, and late Mr Zou

Mr Zou Fu a.k.a uncle Zou, he was one of the three founders and Shareholders of the on coming giant multi-millions Usd Copper Smelter and Gold Refinery entity, IGOZOMO ( IGOGO – ZOU – MOLNAR) Minerals Company Ltd, located in Mpwapwa district in Dodoma region, Tanzania.

2019 at Saba saba grounds!

Also, he was the owner and founder of Aloe vera herbal drug (Jufeel Aloe Vera juice) for human body immune boosting ……. Great human being to say the least! Such a beautiful soul gone too soon! We will surely miss you greatly!.????

“Rafiki yangu wa KWELI KIKWELI KWELI. MAREHEMU ZOU FU QIANG.(PUMZKA SALAMA.) MY DEAREST AND TRUETH FRIEND LATE Mr. ZOU FU QIANG. (REST IN PEACE)” by longtime best friend, brother, and business partner sir O.O Igogo.

Words of sympathy from Magreth
Words of sympathy from Magreth
Words of sympathy from Janet

“Thank you so much Arwa. That is a man who made me so popular and higly respected in the Chinese Communities, He was very loyal, honest, hard working, creative, excessfully kind to me and our family. I fail to stop crying whenever I recall his helping hand to all that I have gained since knowing him in 21 years. Let all of us in the family keep on praying for his Soul to rest in peace.???” ….. shukrani za baba kwa bintie Alpha kwa kutengeneza video ya baadhi ya matukio ya hivi karibuni ambayo marehemu alishiriki nasi.

Happy Anniversary to my parents!

Mr and Mrs Otieno Igogo @Seacliff hotel

??? Cecy anasema Otty mpaka kufa eeh, nami nasema Cecy wangu wakufa na kuzika eeeeh …. usitumie pesa aa kama fimbo kaka mambo ya pesa mpaka makubaluano hapo ndipo pesa huwa na thamani eeh ?? ??? Happy Anniversary to one of my favorite love birds! Mzidi barikiwa mpaka mshangae! ?❀

“Sometime back over four decades ago, I was visiting my old Mum in the village of Utegi, on a date same like today, 17th August.

I had a fully commited heart and desire to go out and look for the better half of me, so that we can pair and share our remaining part of the long walk to Heaven together.

Poor and young as I was, I did not have any other Choice than for that beautiful young girl I knew since 1970, whose home was in the village of Kowak.

During those days there were no telephones, nor did I have any means of transport neither did I have any money to afford bus fare to the ten kilometers distance away from my Village of Utegi. So I remained with only one means of mobility, if I had to make a suprise visit to my choice of life patners homestead, and that was walking on foot to and fro.

Ernegetical with full courage on assumption that she ought be at home, I set my feet on the ground pace after pace, at times I jogged to catch up with time, till I reached Kowak.

Counting on good luck and trust that she would not shame me, I reached the Kumbini shoping Centre of Kowak. I had look for a reliable person to send across to her home, for signaling of my presence and got one young man whom I sent over and eventualy made my mission a successful.

It was on that very same of 17th August over four decades ago when we traditionaly paired as couples to date with my better half named Cecilia.

Our beloved and Mercifull God has blessed our life together with very understanding, humble, highly deciplined and caring four daughters and a son, giving us a marvellous gift of seven grand children to date.

This is not a tell tell or a bed time story, but a true and live background of the Mzee Otieno Igogo and his Spouse Cecilia.”~~ Sir O.O Igogo

“Kijana wangu Boaz (UVCCM) na Mchumba wake walinitembelea jioni ya leo ofisini, na kutuletea Zawadi ya Kumbukizi ya siku yetu na Min Ji (mama). 17.08.2020” *** Sir O.O Igogo

Haya wenye chama chao wamewakilishwa ?? Asante Boaz na wifi yetu. Mbarikiwe sana.

Meet the Obama’s extended family members!

Let me introduce you to some amazing people whom also are apart of my family. Oh Yes! I’m related to the Obama’s, Lupita Nyongo, Raila and the the greats who originated from Uhuru Kenyatta’s land. ??

Ladies and gentlemen; its my honor to bring to you the Obama’s extended family members! Lupita Nyong’o cousin-brother, sister inlaw, nephew, and niece! The Raila Odinga’s son and daughter in-law and grandchildren! The Uhuru Kenyatta’s neighbors ?? The Duke and Duchess of Homabay County family! The Royal family of Mr and Mrs Tobby Nyagilo! The Kaganian village descendants! The Luos from great land of Kenya. Looking amazing! Bless His Holy name, the Maker of all! Mbarikiwe sana. ?❀❀

??????

Happy birthday to me!

“Bwana ni mwema sana alitupa mibaraka ya mtoto wa kike usiku wa Alfajiri ya tarehe 26/06/1977 umekuwa mibaraka kwetu, umenifanya kutembea Merikani kama Queen Mungu asingetupa wewe ni nani angenipeleka kwa Hellen G. White, ni nani angenipeleka Washington DC nikaona ikulu ya Trump, ni nani angenifikisha Califonia nikaona Los Angeles, ni nani angenifanya nikaona HOLLYWOOD, na Golden Gate, umenifikisha Chicago, Michigan, Indiana, Houston, nimeona kaburi la mama Hellen G. White (Battle creek, Michigan). Kuishi kwako Merikani Mungu kanifuta machozi nami ninaongea kati ya wanawake. Ubarikiwe 100 times ningekuwa na uwezo ningekutumia nguo ya kuvaa leo lakini endelea kutuombea siku moja nami nikubariki mwanangu. Tunakupenda sana.” I LOVE YOU MORE Mama! ?❀

Blessed beyond measure! Forever grateful ???? #LovingFarther
thank you darling daughter! ?❀

Namshukuru Mungu kwa yote! Nimeuona mwaka mwingine. Happy birthday to me!

Happy birthday Mercy!

Leo ni siku ambayo mwanangu kipenzi cha roho yangu amezaliwa. Katika kuadhimisha siku hii nimeamua kuweka kumbu kumbu ya post zote za birthday wishes ambazo Niliwahi kuandika huko Facebook. Japo nikawaida yangu kupost siku za birthday yake lakini sijui bbn kwanini nimejikuta nimewaza kama Facebook ikafutika ghalafa hizi kumbu kumbu zote zitapotea. ?‍♀️?‍♀️?‍♀️ Nilipokuwa naziandika niliandika hisia zangu halisi, niliandika vitu ambavyo sio tu vilitoka moyoni bali ninaviamini, hivyo vinabeba uzito mkubwa sana kwangu. Na nilipokua nazisoma tena leo yani mwili unanisiaimka kwa furaha na tabasamu la amani moyoni. ?? Ninawatoto wengi lakini aliyekaa tumboni mwangu na kunifanya ni experience uchungu wa kuzaa ni huyu mmoja tu! Hivyo ana Extra special place in my heart and life!

Mimi huwa nikiandika kitu chochote ambacho kinagusa hisia zangu huwa sirudii kukisoma mpaka muda upite sanaaaa! Yani huwa napenda ku-present my raw feelings! Napenda mtu apate ujumbe kwa jinsi nilivyo jisikia mara ya kwanza. Ndio maana hata kama kuna makosa ya kiherufi (spelling error) huwa naacha hivyo hivyo mpaka nitakapo jiona nipo tayari kusoma hisia zangu katika maandishi ya uhalisia wake! Haya ngoja nitiririke kama ifuatavyo ??






https://www.alphaigogo.com/ni-kwa-neema-tu/

Haya yani hapa nimesha weka kumbu kumbu sawa za toka akiwa na miaka 18 mpaka leo ??? Yani hii hata siku Mungu akinijalia wajukuu basi watakuja ona jinsi nilivyo mpenda mama yao nao itabidi wampende hivyo hivyo, sitaki utani na mwanangu mie ??

Happy birthday Mercy, mjukuu number moja, ubarikiwe sana. Nakupenda leo, nitakupenda zaidi kesho, na milele nitazidi kukupenda.

“Watenda wema wa ukweli, hutenda wema kwasababu ni hulka yao na sio malipo kutokana na mtu wanayemtendea wema alivyo”***** Faraja Nyalandu

Prince Harry and his wife Meghan Markle

Reposted from @farajanyalandu Najua kipindi hiki cha #COVID19 tunaweza kusahau uwezo wa binadamu kupambania jambo lake. Kwa sasa hivi tunapambana na hiki kirusi cha corona. Kimetukumbusha wasiwasi ndio maarifa bila kupepesa macho.Hapo nyuma niliwafurahia sana Prince Harry na Meghan wake. Waliamua jambo lao, waliamua watapendana. Mapenzi ni rahisi kuliko upendo. Upendo huwa ni parefu jamani. Lakini hawa wameweza kutuonyesha vyote: mapenzi na upendo. Lakini zaidi wametuonesha thamani ya hivyo vitu wawili. Upande mmoja namuonea huruma Harry na upande mwingine namuona ni shujaa, kati ya hawa wawili, yeye amesacrifice sana. Amejua kumtetea huyu dada. Haijalishi dada anastahili au hastahili. Watenda wema wa ukweli, hutenda wema kwasababu ni hulka yao na sio malipo kutokana na mtu wanayemtendea wema alivyo. Hata hivyo ametukumbusha uwezo wa binadamu kupambania jambo analolipenda, analoliamini na analotaka. AKIAMUA. Ukiona vinginevyo tofauti na unavyotarajia ujue ni maamuzi pia.

Tuendelee kupambana na corona. Tuendelee kutetea tunaowathamini na tunavyovithamini. GOD is still ON THE THRONE! #BeSafe – #regrann