Category Archives: Family first

Ubatizo wa mzee O.O Igogo.

Jumapili ya tarehe 06/18/2023, mida ya 12:30 asubuhi (masaa ya AfricaMashariki). Mchungaji Aketch wa kanisa la Menonite lililopo Dar es salaam, Tanzania,  jimbo la Segerea; alifanya ubatizo wa kuzaliwa upya kwa njia ya maji mengi kwenye bwawa la Golden Tulip hotel, Oysterbay. Miongoni mwa  waumini wapya hao katika Bwana, alikuwemo Mzee Otieno Olung’a Igogo ambaye ni baba yangu mzazi.


Wahitimu wa darasa la ubatizo wakielekea kwenye bwawa kwa furahq teyari kuzaliwa upya.

Juu ni Mzee O.O Igogo akibatwizwa kwa maji mengi. Hongera sana kwake, Mwenyezi Mungu azidi tembea naye kwenye safari hii ya kiroho.

Mchungaji Aketch pamoja na mama Mchungaji (mwenye nguo nyekundu) wakiwa na mtoto aliyezaliwa upya siku ya leo mzee O.O Igogo na mama Igogo.

Baadhi ya wanafamilia ya mzee O.O Igogo kutoka Segerea siku ya jana jioni waliungana na wanafamilia ya mzee O.O Igogo ya Kibada, wakapata chakula cha jioni pamoja, wakapumzika, na leo asubuhi waliamka mapema sana kwaajili ya kumsindikiza baba /Babu yao kipenzi kwenye safari yake mpya ya kiroho ambapo atabatizwa kwa maji mengi. …. Sifa na utukufu vyote twamrudishia yeye aliye umba Mbingu na nchi. Amen.

Muhtasari wa kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Mercy.

Birthday girl herself

Siku ya tarehe 02, 04, 2023 ilikuwa ni siku ya kumbukizi ya mfanano wa siku ya kuzaliwa mwanangu Mercy.

Birthday girl akiingia kwenye mgahawa

Kama video inavyo onyesha hapo juu 👆🏿 Alianza kusherekea siku moja kabla ya siku yake maaalum kuwasaili, ambayo siku hiyo ilikuwa ni Jumosi ya tarehe 04/01/2023. Sambamba na marafiki zake walikuwa pamoja chakula cha usiku katika mgahawa ujulikanao kama Tourão Brazilian Churrasqueria uliopo downtown Houston, Texas. 😍😍

Mtu na mama yake

Basi siku yenyewe ilipofika tulikuwa na muda mzuri pamoja asubuhi na jioni tukaenda tena kufanya kile twapendelea kufanya zaidi 😍😍 Kwakweli sina kingine mwaka huu zaidi ya kusema Asante Mungu wangu. Sifa na utukufu zote ni zako wewe Baba muumba wa Mningu na nchi na vyote vilivyoko. 🙏🏿🙏🏿

Asante Baba yangu. Asante Mungu wangu, Asante.

Happy 70th birthday Sir O.O Igogo!

Birthday boy himself 😍

“HAKIKA mimi👆 Unipendaye, LEO tumshukuru Mola wetu Muumba na mpaji wa UHAI, kwa kuniwezesha kuhitimu elimu maisha ya MIONGO 7🙏🏿🙏🏿Nikiwa na Afya ya mwili na akili njema siku zote. Furaha niliyo nayo moyoni ni Upendo na Heshima unayonipa kama👉🏿Baba&Babu&Best wako #001 NAKUSHUKURU SANA, SANA👏🏿” ***Sir O.O Igogo***

Naam, hapo juu hiyo ilikuwa ndio salamu yake mzee O.O Igogo siku ya leo ambapo Mwenyezi Mungu amemjalia kutimiza umri wa miaka 70. Kusema ukweli siku zote nilikuwa nikasikia ndugu na marafiki wakisema kuwa baba/mama/bibi yangu ametimiza miaka 70 au 75 basi nafurahia sana. Chaajabu hata siku moja sikuwahi kuwazia wazazi wangu kufika umri huu. 😅😅 Sio kwamba sikujua kuwa wataufikia, hapana! Nivile tu sikuwahi kuwatengenezea picha ya kufikirika wakiwa katika umri huu. Sounds weird eh! 🙈 Twamshukuru Mungu kwa kutupa afya njema ambayo imetuwezesha kushuhudia siku hii ya leo.

Mimi mwenyewe na birthday boy

Nami nilimuandikia ujumbe wakumtakia kheri kwa siku hii muhimu. …”Happy70th birthday to the most influential man in my life! I’m blessed to call you dad. You deserve all that’s beautiful and precious in life. I wish you nothing but absolute happiness, love, peace, and good health on this superb milestone. Happy birthday Jategi, love you much. Otieno Igogo”⁷

Kwakweli tunashukuru sana Mungu kwa kutupa mbaraka huu wa pekee. Tunamtakia maisha marefu yaliyojaa furaha, amani, upendo, na afya njema.

Baba, Blessing, na mama

Recap: Mzee 0.O Igogo 70th birthday 👆🏿 …… Thank you so much, Robin Thomas Edson, @pixelspro_films, for capturing all these beautiful and precious moments on our dad’s 70th year of life journey on this planet.  Ubarikiwe sana.

Masaa kadhaa kabla ya kumbukizi ya kuzaliwa kwake niliamua kuangalia na ku-share tena baadhi ya video za Mzee O.O Igogo zilizo nivutia na kunikosha moyo 😍😍 na 👆🏿 👇🏿 ni sehemu ya hizo baadhi zilizo zipenda zaidi. Haya enjoy them 😜😜

Muhtasari -sehemu ya mwisho: Jambo lililo umiza moyo wangu!

Maisha yamejaa changamoto ambazo hazikwepeki, na mbaya zaidi zinakuja bila taharifa. Mwezi wa kumi.mwaka huu dada yangu mkubwa (pichani juu) alipatwa na ajali ya kuungua moto.

Akiwa hospitalini

Nisingependa kuelezea undani wa ajali hii kwani huo ni ushuhuda wake yeye, mimi namshukuru Mungu kwa miujiza ya uponyaji wa haraka ambao kwa imani yetu haba hatukuweza kuona ukija. Hali ilikuwa mbaya sana sema ni vile tu siwezi kuweka picha zake humu kwani kama nilivyosema ni ushuda wake yeye. Alilazwa hospitali ya Tabora (Tabora ndipo makazi yao yalipo kwa sasa) kwa muda kisha akahamishiwa Muhimbili ambapo alilazwa takribani zaidi ya mwezi mmoja.

Baada ya kutoka hospitali wanandugu walikusanyika nyumbani kwao huko Yombo Vituka kwaajili ya kumshukuru Mungu kwa maajabu ya uponyaji wake aliyompatia dada yetu.

Mungu ni mwema sana na siku zote anajibu maombi yetu zaidi ya imani yetu. Tutalisifu na kulitukuza jina lake milele na milele.

Muhtasari-sehemu ya 5: Kutembelea familia ya Nyagilo.

Nyagilo’s residence, Mbweni.

Namshukuru Mungu kwa kutupa nafasi ya kutembelea familia ya mdogo wangu Janeth/ familia ya Nyagilo. Mimi nilikuwa sijawahi kufika kwenye huu mji wao mpya kwani walipo maliza ujenzi na kuhamia nilikuwa sipo. Wanaishi Mbweni walihamia huko takriban miaka 2 iliyopita.

Safari yetu ilianzia nyumbani Kibada ambapo nilipata ukodaki moment na mtoto wa kaka yangu aitwae Mary, huyu ni mjukuu namba 3. Na kulia kwangu ni kijana wa dada yangu mkubwa anitwa Daniel, yeye ni mjukuu namba 2 na pia ndio mjukuu mkubwa wa kiume.

Mercy

Bidada hapo juu ndio mjukuu namba moja, na wazazi wangu hupendelea kumtambulisha hivyo kwa watu “mjukuu namba moja” 😍😍 Eeh! Niliwapiga chenga wakubwa zangu nikaleta mjukuu wa kwanza! 😅😅

Hapo juu naye ni mpwa wangu, mtoto wa pili kuzaliwa kati ya watatu. Anaitwa Evin Otieno Nyagilo, bali mie napenda kumuita “my International nephew” 😍😍

Alipewa jina la kati la baba yetu. Pia mtoto wa dada yangu Daniel naye alipewa jina la kati la baba yetu-Otieno. Mbaaraka mkubwa sana. Mary yeye alipewa hilo jina kwasababu alizaliwa siku ya Christmas 25th, December huko U.K. She’s a Christmas baby. 😍😍 Huwa napenda kumuita Kitukuu cha Queen Elizabeth, Muingereza mwenye ngozi ya Chocolate. 😜😍😍

Kwakweli, tulipokelewa vizuri sanaaaaaaa! Tulikula, tukanywa, na kusaza! Tukacheza na kufanya utalii wa mji wa Mbweni. Jamani huko watu wamejengaje sasa?! Yani ni kibabe sana.

Sisters

Hapo ni wadada wa tumbo moja, Wakwanza kwa madada ndio mama Daniel, halafu mimi-mama Mercy, halafu Janeth -mama Evin. Yani Magreth a.k.a Mrs Jacob Massawe ndio alikosekana hapo. Alikwenda Moshi kwenye harusi ya shemeji yake.

Pia Blessing pichani juu naye hakuwepo, yeye ndio mtoto wa mwisho kwa baba. Anafanya tunakuwa na idadi ya watoto 5 wakike. Mungu wetu ni mwema sana twamshukuru kwa yote.

Muhtasari-Sehemu ya 4: Tulisherekea kumbukizi ya siku ya kuzaliwa kwao.

Twamshukuru Mungu kwa pumzi ya uhai anayotupatia kila siku ambayo ilituwezesha kuona na kusherekea siku ya kumbukizi ya kuzaliwa wapendwa wetu. Kulikuwa na birthday tatu mwezi wa Nane. Yakwanza ni ya mdogo wangu Janeth kama video inavyo onyesha hapo juu 👆🏿,

Tulikutana Johari Rotana hotel tukala, tukanywa, na kufurahi pamoja sisi kama madada na wifi yetu mke wa kaka yetu. Yani hapo katika madada aliyekosekana ni Blessing peke yake. 😍😍

Ikafuatiwa na ya mume wake Janeth, shemeji Tobby mtu kati hapo juu!

kisha ya mama yetu mkuwa Mama Sarungi. Tulifurahi sana.

Twamshukuru Mungu kwa yote. 🙏🏿❤️🙏🏿

Muhtasari -sehemu ya 3: Familia yakutana.

Baba na binti zake

July 31st, 2022 siku kadhaa baada ya mimi kufika nyumbani wanafamilia walikusanyika kwaajili ya kusalimiana na kufurahia pamoja kama familia. Zifuatazo ni baadhi ya picha na video ya siku hiyo.

Baba na wanawe

Yani hapo juu ni picha hadimu sanaaaaaaa! Kitendo cha kaka yetu mkubwa kuwepo kwenye picha ni kitendo kinachotekea kwa NADRA mno. Hapendi kupiga picha kabisa yani hata hapo tulimlazimisha kweli akaona aibu akakubali 😅😅

Mzee 0.O Igogo na kaya zake 😍
Mabinti wa marehemu mzee Cornel Awiti

Pichani juu ni mama yangu mzazi na wadogo zake wa tumbo moja. Warembo wa marehemu mzee Cornel Awiti na marehemu Valeria Awiti, hapo wamekosekana mabinti watatu tu nao ni; Felista Awiti (Mrs Joseph Musira) huyu ndio wakwanza kuzaliwa. Wapili kuzaliwa ni Mwalimu Anna Awiti (Mrs. John Obure), na Yacinta Awiti (Mrs Amos Onditi) huyu kuzaliwa ni wapili kutoka mwisho kati ya watoto 18. Mtoto wa mwisho kuzaliwa ni huyo mwenye gauni lenye maua meusi na meupe hapo juu anitwa Julia Awiti (Mrs Airo).

Wakwe nao hawakubaki nyuma 😍😍 Mmoja hakuwepo ila aliwakilishwa vyema na mkewe (dada mkubwa) mwenye gauni la blue.

wajukuu na babu yao
wadada katika ubora wetu

Twamshukuru Mungu kwa yote. 🙏🏿❤️🙏🏿

Muhtasari -sehemu ya pili: Jambo lililonifurahisha zaidi mwaka 2022 ….!

Mama na mwana 😍

Kamanilivyosema kwenye posti yangu iliyopita somahapa yakwamba mwaka 2022 ulikuwa na baraka zake nyingi sana. Basi katika kuhesabu mibaraka yangu naweza sema huu nao ni moja ya mbaraka mkuu. Ni jambo ambalo lilinifurahisha zaidi 😍😍 Ni surprise niliyo wafanyia wazazi wangu.

Tarehe 25 mwenzi wa Saba, mwaka huu wa 2022 (07/25th/2022) ilikuwa siku ya furaha sana baada ya mipango yangu ya kuwafanyia wazazi wangu haswa mama yangu safari ya kuwasalimia bila ya kuwapa taharifa kama ilivyokua huko nyuma. Nimpango ambao nilipanga na mdogo wangu aitwaye Magreth Otieno Igogo a.k.a Mrs Jacob Massawe kuwa tutamfanyia mama surprise wakati wa siku yake ya kuzaliwa ambayo ni tarehe 27th July. Bahati mbaya ratiba yangu ilibidi nifike siku mbili kabla ya birthday yake. Mimi nilichukua likizo na kuandaa safari bila kumwambia mtu yoyote nyumbani isipokuwa mdogo wangu, mume wake na mwanangu tu. Sikutaka mama ajue kabisa hivyo kuzuia wanafamilia wengine kujua hata marafiki ilikuwa muhimu sana. Nashukuru Mungu kila kitu kilikwenda vizuri kama tulivyopanga tuliomba kibali cha Mungu kwa kumkabidhi mipango yetu naye akaibariki ikatimia. 😍🙏🏿😍Safari yangu ilianzia Houston, Texas.

Nakumbuka siku nakwenda airport tulimpigia mama simu, akiwa nyumbani na baba na shangazi yetu fulani wakipiga story zao, nikaanza kumuuliza anampango gani na birthday yake?! Akawa anasema nahamu namtoko fulani amazing 😅😅 lakini ameshapanga kwenda Fun city na watoto wake wa shule (school trip). Nikamwambia kwautani nikikutumia Dola Mia ($100) uongezee kwenye hiyo trip itatosha? akasema itatosha sana. Nikamwambia basi nitakutumia tarehe 25, ambayo ndio tarehe nilikuwa najua naingia nyumbani. 😅😅😅 Basi nikamalizia kwa kumwambia wakifunga shule apange trip yeye na wadogo zake na dada zake waende kutembea Zanzibar au mbuga za wanyama, wafanye bageti halafu anijulishe. Akashukuru kweli kweli bila kujua mimi hapo naingia uwanja wa ndege teyari kwa kum-surprise! 😍😍

Sasa, ilikuhakikisha chumba changu kipo katika hali nzuri mdogo wangu alimdanganya mama kuwa ana wifi yake anakuja toka Japan na ana mtoto mdogo hivyo anaomba aandae chumba cha dada Alpha (eeh usishangae sana, nina chumba changu kwa mama yangu 😍😍) ili afikie humo kwa siku kadhaa kabla ya kwenda Moshi. 😅😅 mdogo wangu wanaishi nyuma tu na kwa mama. Basi mama naye bila shaka wala kinyongo akamkubalia pasi kujua mwenye chumba yupo njiani. 😅😅Nilipofika airport nilipokelewa na mdogo wangu pamoja na mume wake. Tukiwa njiani mdogo wangu akampigia mama simu akamdanganya kuwa amekutana na rafiki yake walikuwa wote huko kijijini Kowak (kijiji alipozaliwa mama yetu), na anasema hawezi kwenda kwake mpaka afike kumsalimia. Mama akanza kuuliza ninani? mdogo wangu alikataa kata kata kusema akamwambia ni surprise akifika hapo itabidi asikilize sauti yake ili amtambue ni nani! Mama alimbembeleza sana amwambie ni nani huyo lakini mdogo wangu alishikilia msimamo kuwa utamuona wakifika. Mama kidogo akawa kama amechukia kwani alikua anasema unakuja na mgeni mimi hata kupika sijapika hata juice ndo kwanza wanatengeneza sio vizuri na hapendi kabisa. 😅😅 mdogo wangu hakubadilisha msimamo wake mpaka tukafika nyumbani, na mengine yote yamebaki kuwa historia kama hiyo video ya tukio hilo inavyo onyesha. 😅😅

Hii ni mara ya pili sasa nafanikiwa kuwa-surprise wazazi wangu. Tarehe 07 mwezi wa tatu, mwaka 2017 kwa kushirikiana na wadogo zangu pamoja na baadhi wafanyakazi wa Utegi Technical Enterprises Ltd (kampuni anapofanyia kazi baba yetu) tulifanikiwa kum-surprise baba yetu ofisini kwake, ilikuwa siku ya birthday yake. 😍😍 Tuliwahi sana ofisini kabla yake kitu ambacho hajazoea kwani siku zote yeye ndio anakuaga wakwanza kufika. Tukaingia ofisini tukazima taa sehemu ya mapokezi ili akiwa kwa nje ajue hakuna mtu. halafu tukamwambia mlizi arudishie tu mlango asifunge na funguo, na geti arudishie bila kuweka kufuli ili akifika tu ashtuke na akasirike (just to annoy him) kuwa waliacha mlango na geti wazi jana jioni. Sasa alipofika mlangoni anakuta ipo wazi akasema ooh! Tumesha ibiwa hapa, hasira zikamshika kuwa geti halikufungwa jana jioni. Halafu mdogo wetu aitwaye Guka ndio tulimuacha nje awe ana mmonita (monitoring him) kwa kutupa taharifa kwa simu kuwa ameshafika kwa parking lot. 😅😅 Na Guka alikuwa anawasiliana na dereva kusema wapo wapi. 😅😅 Tazama video hapo chini 👇🏿😅😅

Basi, alipopita tu mapokezi kuingia eneo la secretary wote tukasema “surprise” kwa nguvu na furaha huku mmoja wetu alikuwa kwenye switch ya kwashia taa, tukaanza kuimba “happy birthday to you” 😅😅😍 alishangaaje, hasira zote zikaisha hapo hapo. 😅😅😅😅 Hakuamini kuwa watu waliweza kuwahi kazini mapema hivyo ilitu wam-surprise! Alishukuru sana na furaha nyingi mno.

unaweza itazama video yote ya surprise kwa kupitia YouTube yangu hapo chini 👇🏿

Baba na mwana 😍

Kwakweli ni furaha kufanya jambo ambalo linamfanya mtu mwingine kuwa na furaha na kujisikia vizuri kwa kujiona mwenye thamani, lakini nifuraha zaidi kufanya jambo linalowafurahisha wazazi wako. Nafurahia na najisikia vizuri pale ninapoweza kuwafanya wazazi wangu wafurahi zaidi. Ni mbaraka wa pekee. 😍😍 Counting my blessings ma’am! 😅😍

Chumba cha dada Alpha

Na story zitaendelea maana mama Igogo alikuwa haamini alichokiona. 😍😍

Surprise ya mwisho iliharibika 😅😅 tulitaka dada yetu naye am-surprise mama lakini dakika za mwisho akaamua kumwambia kua anakuja halafu hata hakutuambia kuwa kamwambia mama hivyo ikawa surprise kwetu. 😅😅🙈🙈 kwakweli hii ni the best moment for 2022.

Cecy-mama mzazi

Miaka takriban 3 iliyopita dada yangu naye alim-surprise mama big time. Alikuwa mjamzito na wakati uchungu umeanza akampigia mama kumsalimia basi wakaagana vizuri. Ndani ya masaa 2 mume wake anampigia mama simu kuwa mama Dani amejifungua mtoto wa kike na wameamua kumrithisha jina la mama. Mama akawa hataki kuamini anasema mbona mama Dani nimeongea naye muda sio mrefu? 🤣🤣🤣 akaambiwa pale anakupigia alikuwa ameshikwa na uchungu na tulikua njia kwenda hospitali. 😅😅 Na mtoto mwenyewe ndo huyo hapo 👆🏿 juu. 🤩🤩

Happy 10th birthday my twin!

Babysister 😍😍

Two digits counting has officially begun! Happy 10th birthday twin babysister! Wishing you a marvelous year and many more to come. Happy birthday mdogo wa mimi. 😘❤️

sisterhood!.😍😍

Mimi mwenyewe na pacha wangu nyumbani Kibada. 😍😍

Pachaa kama pacha! Kwaraha zetu ndani ya Serena hotel, Dar es salaam.

Blessing katika ubora wake 😍

Happy birthday beautiful we all love you. 😘❤️❤️

Muhtasari wa matukio ya mwaka 2022 -sehemu ya kwanza.

Dec 2022

Mwaka 2021 niliufunga vyema na kuufungua 2022 vizuri sana. Namshukuru Mungu kwani umekua mwaka mwema sana wenye mibaraka mingi. Changamoto katika maisha hazikosekani kwani hatuwezi kujua tu imara kiasi gani kama hatutapitishwa katika changamoto hizo.

Daughter

Wanasema dhahabu au madini yoyote ya thamani hayapatikani juu ya barabara wala kando kando ya maji! Nilazima yachimbwe chini ya ardhi na yapitishwe kwenye moto mkali ndipo yawe haya madini tunayofurahia kuyaona. Hivyo, sikuzote tukipata changamoto tusikimbilie kusema “kwanini mimi?” Bali tumwambie Mungu najua hili ni darasa unanipitisha japo somo bado sijalielewa, naomba unipe HEKIMA ya kuweza kulielewa somo hili ili nifuzu mafunzo yangu vyema. Najua maumivu ninayopitia nikwaajili ya utukufu wako na mimi ndiye uliyenichagua kuwa kielelezo cha utukufu wako.

Basi kwa kusema hayo, naomba niweke kumbukunbu ya matukio yaliyozunguka maisha yangu mwaka huu wa 2022. Tukumbushane kushukuru katika kila jambo. Sikuzote tuhesabu mibaraka yetu kwani ni mingi mno sema tunafunikwa na upofu kwa kuangalia maisha ya watu wengine na kudhani kuwa wamebarikiwa kutuzidi. Hapana! Mungu anatubari sote kwa jinsi impendavyo yeye kwa wakati wake.

Hizi ni baadhi ya picha tulipiga mwanzoni mwa Dec 2021 tulikuwa maeneo ya tunako ishi karibu na NASA Space Center, Houston, Texas

Baadhi ya picha tulizopiga kwenye Christmas party 20021 iliyofanyika Hilton hotel, Houston, Texas.

2021 THC Thanksgiving Gala
April 2nd 2022

Mwenyezi Mungu alitubariki tukafurahia kuona mwanangu ameongeza mwaka mwingine. Ilikuwa siku ya Jumosi tarehe mbili mwezi wa Nne! Na zifuatazo ni baadhi ya picha ya siku hiyo.

Mama na mwana 😍

Pumzika kwa amani ya Bwana bibi Anna NYOLWENGO!

marehemu bibi Anna Nyolwengo akiwa na mwanandugu

“Ilianza kwa ajali ya kugongwa na pikipiki, ukavunjika mfupa wa nyonga, hospitalini ulikimbizwa kupata huduma, ukiwa umenyamaza kimya bila kujitambua, siku tatu baadaye uliizinduka na kuwatambua wanao, hata kwenye simu ukaongea na Otieno, kuimarika kwako iliwaruhusu madaktari kukusudia ufanyiwe upasuaji, wa kuunganisha palipovunjika, ukiwa na uhai wako wakakuchoma nusu kaputi, nayo ikazua balaa la kupoteza fahamu hadi jioni hii umetutoka Mama yetu ANNA NYOLWENGO, dada yako Rhoda alitangulia, ukabakia nasi ukooni, leo umetutoweka kwa utashi wa Mola TUNASHUKURU ????????” …… Sir O.O Igogo

Marehemu ni mdogo wake na bibi yangu mzaa baba! Pia mimi nilipewa jina la mama yao mzazi yani bibi yake baba mzaa mama! Jina langu hilo ni ARUA japo baba yangu huwa analiandika ARWA! ?? Marehemu bibi yangu mzaa baba wao asiliyao ni Kenya, ambapo ndipo na mdogo wake alipokuwa akiishi mpaka maiti ilipo mfika.

Hii wheelchair alinunuliwa wiki iliyopita wakiwa na tegemeo kuwa angetoka hospital salama baada ya kufanyiwa upasuaji. Wao walipanga kama wanadamu lakini mapenzi ya Mungu yametimuzwa! …… Poleni wanandugu na ukoo wote wa Nyolwengo. May our beloved grandmother Anna Rest In Eternal Peace! ????

“And said, “Naked came I out of my mother’s womb, and naked shall I return thither. The Lord gave, and the Lord hath taken away; blessed be the name of the Lord.” ………. Job 1:21

Mjukuu namba moja atua Dar!

Mjukuu namba moja akiwa na mama yake

Tarehe 28 ya mwezi wa Saba, mwaka huu wa 2021 mjukuu namba moja alipanda ndege na kuanza safari ya kwenda Tanzania ?? kusalimia bibi, babu, wajomba, mashangazi, mama wadogo kwa wakubwa,

Sambamba na mama yake mjukuu namba moja akiwa katika maeneo ya kiwanja cha ndege cha George Bush Intercontinental Airport kabla ya kupita kwenye bench la watu wa usalama na kuelekea kwenye terminal waliokua wakiondokea.

kwa kupitia ukurasa wake wa Instagram na Facebook mama yake mjukuu namba moja aliandika maneno haya “Safari njema Mungu awe nawe! Salimia bibi, babu, mashangazi, wajomba, ndugu, jamaa, na marafiki! ♥” ambayo yalikuwa yakimtakia safari njema binti yake!

Mungu ni mwema sana, kwani mjukuu namba moja amefika salama Dar es salaam, Tanzania majira ya saa tano usiku (11.00pm) kwa ndege ya KLM iliyopita Amsterdam, Zanzibar, na kisha kutua Dar.

Blessing akisubiria kumpokea best ake

Ndugu wakiwa na furaha ya kumuona mpendwa wao baada ya miaka 2 yakutoonana uso kwa uso. Mungu azidi kupewa sifa. ??

Mtu na mtu wake! Mashosti! …. Bibi na mjukuu namba moja!

“Ni asubuhi njema na yenye furaha, Uzao wa Uzao wetu, atua Plot No. 10.. &1..0, Utegi Street – Kibada saa saba usiku. Tumshukuru Mungu kwa kumfikisha salama kutoka Houston,Texas.” **** Sir O.O Igogo Maneno ya babu yake mjukuu namba moja.

Haya basi, namtakia mapumziko mema. Ngoja adeke kidogo kwa bibi na babu. Nakumbuka enzi babu yangu na bibi zangu wakiwa hai, siku zote nikifika Tanzania ?? lazima niende kijiji kuwaona na kudeka kwingi. Ni mwendo wa kuchinjiwa Mbuzi na Kondoo tu! ?? Nawakumbuka sana, waendelee kupumzika kwa amani. ??

Sherehe ya maisha ya mwisho ya mama Yucabeth Atieno Chaulo!

Marehemu Mama Yucabeth Atieno Chaulo enzi ya uhai wake!

Siku ya Alhamisi ya tarehe 24, mwezi wa Sita, mwaka huu (06/24th/2021) familia ya marehemu mzee Androniko Chaulo walipatwa na msiba wa mama yetu Yucabeth Atieno Chaulo, kilichotokea mida saa mbili usiku huko Dar es salaam, Tanzania. Na amezikwa leo kwenye makaburi ya ukoo wa Chaulo yaliopo katika kijiji cha Buturi, wilaya ya Rorya mkoa wa Mara, ambako ndipo makazi ya kudumu ya ukoo wa Chaulo.

Pichani juu ni mama yangu mzazi (mwenye Tie dye) pamoja na marehemu. Mapema mwaka huu alipokwenda kutembelea makazi ya mama yangu huko Kibada, Dar es salaam.

Mama Yucabeth Atieno Chaulo ni mama mzazi wa Shemeji yangu mkubwa Mussa Chaulo a.k.a baba Danny. Shemeji Mussa amemuoa dada yangu mkubwa Elline Igogo a.k.a mama Danny takriban miaka 21 na miezi kadhaa sasa. Wamebahatika kupata watoto watatu Daniel, Chaulo, na Cecilia.

family!

Akiwa na baadhi ya watoto zake, wakwe zake, mama yangu mzazi, na mdogo wangu (mwenye darkblue), Kibada Dar es salaam.

Bahati mbaya miezi kama mitatu hivi iliyopita marehemu mama Yucabeth Atieno Chaulo alimzika mmoja wa binti zake ambaye yupo kwenye picha hii, (wapili kutoka kushoto mwa dada mwenye nguo Nyekundu, nyuma ya mama yangu naye amevaa Tie Dye)! ….. Roho zao zipumzike kwa amani ya Bwana.

Mama yetu alikua akisumbuliwa na mapafu kwa muda mrefu kidogo, alikuja Dar es salaam kwaajili ya matibabu na ndipo mauti ilipomkutia. Kwa asili yeye ni Mkenya (mzaliwa wa Kenya / mluo toka Kenya) ambaye aliolewa ujaluoni huko Buturi, na ndipo alipokua ameishi muda wote wa uhai wake.

Ibada ya kuuaga mwili , Dar es salaam

Beautiful and peaceful sendoff kwa mama yetu Yucabeth Chaulo yaliyofanyika nyumbani kwa mmoja wa watoto wake huko Mwanangati, Yombo Vituka, Dar es salaam. Kuishi maisha ya kumtukuza Mungu ni raha na amani tele! Amemaliza mwendo, tuonane asubuhi ile njema! ?? ……. Aneyeimba ni mwimbaji mashuhuri ajulikanaye kama Angela Magoti. Angela ameolewa na mjukuu wa marehemu.

“Nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, Andika, Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao.” Ufunuo 14:13

Video hizi zote ni ibada ya mazishi yake leo hii 07/01/2021 huko Buturi, Rorya.

Video hii haina uhusiano na msiba huu! Japo wimbo wao huo ndio uliokuwa ukitumbuiza wafiwa.

“Bali wewe, uwe na kiasi katika mambo yote, vumilia mabaya, fanya kazi ya mhubiri wa Injili, timiliza huduma yako. Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki kwangu umefika. Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda; Baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake.” 2Timothy 4:5-8

Bwana alitoa na Bwana ametwaa jina lake lihimidiwe milele zote. Tuonane Paradiso mama yetu! ????

Video hii haina uhusiano wowote na msiba.

Sherehe ya kipekee ya kumuaga Dorice Sassi Igogo!

Ameagwa rasmi! Siku ya Jumatano, tarehe 06/02/2021 zilisikika nderemo na vigelegele vingi sana kutoka kwa familia ya Mr. Emmanuel Agonda Sassi (marehemu) na Mrs. Magreth Cornel Awiti a..k.a Mrs Agonda, a.k.a Mrs Sassi pamoja na wanaukoo wote wa Adol Igogo. Ilikuwa ni furaha ya kumuaga rasmi binti yao kipenzi Mwalimu Dorice Sassi Igogo ambaye anakwenda kuanzisha rasmi kaya (familia) yake.

Dorice akiwa na mtarajiwa wake

Ndoa ni jambo la kheri, ndio maana wazazi hufanya sherehe ya kipekee kabisa ili kumuaga mpendwa wao, kama njia mojawapo ya kuonyesha furaha yao na shukrani kwa Mungu.

Dorice a.k.a Vumilia ni binti aliyezaliwa katika familia ya watoto (3) watatu, yeye akiwa mtoto wa pili kuzaliwa na msichana pekee.

Mtoto wa kwanza ni Yustor Sassi (Kulia), Dorice, na Joseph (kushoto). Katika picha hii inaonyesha makaka wakimlisha keki dada yao, na mama mzazi akiwa pembeni anaangalia.

Yustor akiwa nafuraha nyingi wakati wa kulishwa keki na dada yake.

Joseph naye akifurahia kulishwa keki na dada

Yustor akimpigia saluti mdogo wake, kwa heshima kubwa kama afanyavyo huko jeshini!

Tazama jinsi kaka wa bibi harusi mtarajiwa akitoa saluti kwa mdogo wake kwa furaha na ushupavu wa kijeshi.

Bibi harusi mtarajiwa akielezea historia yao, wapi walikutana na nini kiliwakutanisha.

Zawadi kwa bwanaharusi mtarajiwa

Bibi harusi mtarajiwa akiwa na Mc wa shughuli hiyo ajulikanaye kama McKatokisha

Wamazazi wa upande wa bibi harusi mtarajiwa

Yani mdogo wangu huyu kwa kuchakarika aaah! Ni Mwalimu na pia ni mjasiriamali wa nguvu. Hii keki ametengeneza mwenyewe kwa mikono yake kupitia kampuni yake ya isadoricakes and sassyjuice! Izidi barikiwa kazi ya mikono yake.

Mtarajiwa akikata keki

Akilimlisha mama mzazi kwa unyenyekevu na upendo mwingi

Akimpatia mama mzaa chema keki yake kama ishara ya upendo na ukarimu wake kwake na ukoo wa mumewe mtarajiwa.

Mama mzazi naye alipata kipande chake

Mama wazaa chema na binti yao

Wamependeza kwakweli

Haya ngoja nikusaidie kidogo kama haujui, bibi harusi mtarajiwa ni mtoto wa mama yangu mdogo. Mama yake ndio kitinda mimba kwa uzao wa bibi yangu mzaa mama. Sasa basi, kama ilivyo kwa mama yake Geoffrey Kateti (kama mnamkumbuka) ndivyo ilivyo kwa mama yake na bidada hapa. Mama yake naye alifuata nyayo za dada yake (mama yangu) akaolewa Utegi! Utegi oyeeee! ?? Tofauti na mama yake Geoffrey, mama yake Dorice ameolewa ukoo mmoja na dada yake ?? chezea ukoo wa Odol! Hivyo Dorice ni mdogo wangu pande zote; kwa baba na kwa mama.

Mapenzi ya Mungu yalitimizwa baba yangu mdogo (baba wa bibi harusi mtarajiwa) aitwae Emmanuel Agonda Sassi, alishalala usingizi wa mauti takriban miaka 4 iliyopita. Twamshukuru Mungu kwa yote.

Once again, hongera sana mdogo wangu, shemeji tunakukaribisha kwetu kwa mikono miwili. Mungu awe nanyi siku zote. Amen! ????

?@lush___makeup

? @mckatokisha

? Decor@lillies_luxe_decor

#FBF

Embu tujikumbushie mambo yalivyo kuwa siku ya kuvikana Pete ya ahadi ya ndoa /uchumba, siku ya Jumatatu ya mwezi wa kwanza tarehe kumi na mbili mwaka huu, 01/12/2021. Love is the beautiful thing.

Sherehe ya kuagwa kwa Rhoda Igogo!

Siku ya Jumapili ya tarehe 05/23/2021 ndio ilikuwa siku rasmi ya kuagwa kwa bibi Rhoda Alexander Igogo. Sherehe hiyo ilifanyika nyumbani kwa baba yake mlezi huko Segerea. Zifuatazo ni baadhi ya picha na video kutoka kwenye tukio hilo. Picha hazipo kwenye mpangilio rasmi nimeweka tu!

Bibi harusi mtarajiwa akiingia ukumbuni

Mr Victor na mkewe mtarajiwa!

Rhoda na mpambe wake bi. Oliver Chumo

Oliver

Baba mubwa wa Rhoda, mzee Charles Olung’a Igogo

Wazazi wa bwana harusi mtarajiwa, Mr and Mrs Ollal

Wanandoa wapya Mr and Mrs Isaka Alexander Igogo

Mama mdogo wa Rhoda, Mrs O.O Igogo akipungia wageni

Baba mkubwa wa Rhoda, mzee Charles Olung’a Igogo (kushoto) pamoja na baba mlezi mzee O.O Igogo

Dada wa bwanaharusi mtarajiwa Ms. Aphino Alexander Igogo, pamoja na mdogo wa bibi harusi mtarajiwa Blessing Igogo wakimkaribisha shemeji yao kwa furaha.

Rhoda na mama yake mzazi

Bwanaharusi mtarajiwa akiwa na bibi yake mzaa mama yake.

wageni waalikwa wakiwa na mwenyeji wao mzee O.O Igogo

Mc Rhevan katika ubora wake

Bibi harusi mtarajiwa number 2 akitoa ombi la mwisho.

Rhoda akitoa zawadi ya keki kwa Mkurugenzi Mkuu wa Utegi Technical Ltd, Mrs Margaret Mabada kwa niaba ya wafanyakazi wote wa Utegi ambapo Rhoda ameajiriwa.

Rhoda akicheze na wafanyakazi wenzake

Baba na binti yake wakicheza

Kwa picha zaidi bonyeza ????

https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/rhodasendoffpartyphotos/

Hongera sana Isaka na Sarah!

Mr and Mrs Isaka Alexander Olung’a Igogo

Hayawi hayawi sasa yamekuwa! Wamehalalishwa duniani na Mbinguni yakwamba wawili hawa ni mwili mmoja!

Sarah akila kiapo kitakatifu

Agano hili takatifu lilifanyika siku ya Jumosi tarehe 05 /08/2021 katika kanisa la viziwi lililopo huko Bunguruni, Dar es salaam. Tunawaombe baraka nyingi sana katika familia yao hii mpya walio ianzisha!

Bibi harusi

Bwanaharusi akihakikisha je kweli ni yeye?! Kabla ya kula kiapo, maana hukawii kubadilishiwa mke kama Jacob (Yakobo)! ? mjini mambo mengi jama! ?

Bwanaharusi amehakikisha na ameridhia! ?? Kama hujawahi sikia kisa cha Jacob (Yakobo) basi chukua Biblia yako na ufungue kitabu cha mwanzo sura 29 yote itakupa stori kamili!

Kwaufupi ni kwamba, Jacob baada ya kutumikia miaka saba kwa mzee Labani kama mahari ya kumuoa binti yake Rachel (Raheli), siku ya harusi akakuta amebadilishiwa mke anaye mpenda kwa dhati na kupewa Lea ambaye alikuwa ni dada wa Rachel (Raheli). Kwani kulingana na mila na desturi za kabila na ukoo wa mzee Labani ni kuwa mkubwa lazima aolewe kwanza ndipo mdogo anafuata. Kwa maana hiyo Jacob ilibidi atumikie miaka 7 mingine ili aweze kumpata Rachel. Kwa maana hiyo Jacob alitumikia miaka 14 kwa mzee Labani kama mahari ya kumuoa kipenzi cha roho yake! …… Sikilizeni wanawake wenzangu, kama mwanaume anakupenda basi hakuna gumu wala zito mbele ya macho yake! He will move mountains just to have you! Tena bila hiyana yoyote! Wanawake wazuri ni wengi sana lakini Mke ni mmoja tu ambaye kila mwanaume anajua hilo!

Maharusi na wapambe wao
Wasimamizi wao
Mchungaji aliye idhinisha ndoa hii

Sarah akisindikizwa na kaka yake aitwaye Alex ambaye ndiye aliyemlea toka wazazi wake wamefariki hadi leo hii anapokwenda kuanzisha nyumba yake mwenyewe. Kwa Sarah hamuoni Alex kama kaka bali ni baba yake mlezi na mke wa Alex ni mama yake mlezi, hao ndio wazazi wa Sarah.

Hapo juu ni baba mlezi wa Isaka ajulikanaye kama mzee O.O Igogo. Yeye ndio amemlea Isaka toka akiwa na miaka 5. Baba mzazi wa Isaka amefariki takribani miaka 7 iliyopita. Mzee 0tieno Igogo ni mdogo wake na marehemu mzee Alexander Igogo ambaye ndiyo Baba yake na Isaka.

Mama mlezi wa Isaka Mrs O.O Igogo akisalimia maharusi, nyuma yake ni mjukuu wake aitwaye Essy.

Mashangazi na mama wakubwa kwa wadogo upande wa bwanaharusi.

Baba mlezi akiwa na furaha nyingi usoni kwa kuongeza mtoto mwingine kwa familia.

Madada, mabinamu, na mashemeji wakiingia kwa shangwe!

Kutoka kulia, ni mdogo wa bwanaharusi aitwaye Blessing, akifuatiwa na mpwa (niece) wa bwanaharusi Essy, akifuatiwa na shemeji mkubwa Mrs. Vetto Igogo, na dada mkubwa (wapili kuzaliwa kwenye familia ya kina Isaka) Aphino Alexander Igogo (Mrs Ogoche).

Mdada mwenye nguo ya blue kutoka kushoto, huyo ndio kitinda mimba kwenye familia ya akina Isaka. Anaitwa Rhoda Alexander Igogo. Naye harusi yake ni mwishoni mwa mwezi huu. Wiki hii ni kitchen party yake.

Bibi harusi mtarajiwa Rhoda Alexander Igogo akiwa na maharusi Mr and Mrs Isaka Alexander Igogo.

Bibi harusi mtarajiwa, bi Rhoda akifurahia kaka kupata “jiko”!

Mama mlezi wa bwana harusi pamoja na baba msimamizi wa ndoa hii mzee Samuel Olung’a Igogo wakitoa nasaha zao.

Baba mlezi akitoa neno kwa niaba ya kamati!

Mama mlezi akiwa na maharusi

Maharusi wakikata keki!

Wapendwa, kwamahitaji yako ya Cake nzuri zenye ubora wake, juice fresh tamu, na Mc wa kitchen party, tafadhali husisite kumtafuta @isadoricakes_and_sassyjuice ndio habari ya taifa! ???

nnnnn

Maharusi wakifungua dancing floor kwa kucheza ziro-diatance music ?? asiye na wake akumbatie chupa ya soda! ???

Meza kuu upande wa bibi harusi

The Olung’as!

Hawa ni baba zake Isaka, wadogo kwa wakubwa. Kutoka kushoto ambaye kichwa tu ndio kimeonekana ni mzee Samuel Olung’a Igogo (baba mkubwa na msimamizi wa ndoa hii), akifuatiwa na mzee Charles Olung’a Igogo (baba mkubwa), akifuatiwa na mzee Otieno Olung’a Igogo (baba mdogo na mlezi wa Isaka), akifuatiwa na Genga Olung’a Igogo (baba mdogo)

Walianza na Mungu, wakamaliza na Mungu. Mama mdogo wa Bwanaharusi Mrs Emmanuel Agonda Sassi Igogo akitoa sala ya mwisho!

Mathayo 19:5 “akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja”!

Marko 10:9 “Basi, alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe” ….. I present to you Mr and Mrs Isaka Alexander Olung’a Igogo

Mc Rhevan mtu kati hapo

picha zote shukrani kwa Mc Rhevan studio. Ukitaka kuona picha za tukio nzima tembelea ????https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/isakaandsarahweddingphotos/

Tunawaombea kheri na baraka nyingi!

Bwana harusi mtarajiwa-Isaka akiwa kwenye pozi na bibi harusi mtarajiwa-Sarah

Kesho ndio siku yenyewe kuu, ambapo wawili hawa wataunganishwa kuwa kitu kimoja na koo mbili zitaunganishwa rasmi mbele za Mungu.

Naam, kwamara nyingine tena tunapenda kutoa pongezi nyingi sana kwa watarajiwa hawa kwa kufanya maamuzi mazito yenye busara. Mungu azidi kuwatangulia katika kila jambo ambalo limepangwa kufanyika kesho basi likapatae kibali mbele ya uso wa Bwana na lifanyike kama lilivyopangwa kwa utukufu wa Mungu.

Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa rehema na neema awazidishie ulinzi wake na mibaraka yake siku zote za maisha yao. Ndoa yao ikajae amani na furaha, naye Mungu Baba awe mgeni wao siku zote. Wakabarikiwe wao na uzao wao wote. Twaomba kwa imani katika jina la Yesu. Amen! ????

akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja!” *** Matayo 19:5

“Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe” ****Marko 10:7

Jana ilikuwa siku ya kuagwa kwa bibi harusi mtarajiwa. Bi. Sarah alifiwa na wazazi wake wote wawili akiwa mdogo. Kaka yake Alex akamlea hadi sasa anatokea kwao kwenda kwake na mumewe mtarajiwa. Ni mlemavu wa kusikia na kusema??‍♂️ Hapo anatoa shukrani zake za moyoni kwa walezi wake siku ya kuagwa, na kuwapa zawadi alizomudu kama ishara ya shukrani na kumbukumbu. Mume wake mtarajiwa naye ana historia inayotaka kufanana na yake! Hawa wawili ni kielelezo halisi na ushuda hai kwamba kazi ya Mungu haina makosa.

Mimina neema zako Bwana mimina ????

??? mnaona mama zangu na shangazi yangu aliyegoma kuzeeka pale nyuma na tabasamu kama lote wakikumbushia enzi zao?! ?? so sweet!

Wababa nao hawakubaki nyuma! ??

Picha zote shukrani kwa Mc Rhevan , mtembelee Instagram @mc_Rhevan au website yake ???? https://mc.rhevan.com/

Nyumbani kumenogaaa …….!

Jamani-Jamani! Nyumbani kumenogaaa! Kama ilivyokua kawaida yao basi wametia timu tena!?? Mashangazi kwa wajomba, mama wadogo kwa wakubwa, baba wadogo kwa wakubwa, makaka kwa madada, bila kusahau mashemeji.

Si wengine bali ni familia ya marehemu Mzee William Olung’a Igogo wa Utegi, Rorya leo wamejumuika nyumbani kwa mzee O.O Igogo huko Segerea, Dar es salaam kwa maandalizi ya ndoa ya kijana wao ambaye ni mmoja wa wajukuu wa marehemu mzee William Olung’a Igogo ajulikanaye kama Isaka Alexander Igogo itakayo fanyika siku ya Jumosi tarehe 05 /08 / 2021, Dar es salaam, Tanzania.

Pichani juu ni maharusi watarajiwa bwana Isaka na Bi. Sarah katika pozi!

Basi, nami dada mtu napenda kuwatakia ndugu zangu kila la kheri katika hatua zilizo baki katika kutengeneza historia nyingine tena ya kuanzishwa kwa familia ya Bwana Isaka na Bi Sarah! Mungu awe azidi wabariki na atembee nanyi mpaka mwisho wa jukumu hili muhimu sana la kuunganisha koo mbili kua kitu kimoja! …. Nasikitika sijaweza kushiriki nanyi lakini nipo nanyi kiroho na kifikra! …. BTW, kwa msiofahamu udugu wangu na bwana harusi mtarajiwa ni hivi; Isaka ni mdogo wangu, yeye ni mtoto wa marehemu baba yangu mkubwa Alexander Olung’a Igogo. Baba yake ni mtoto wa pili kuzaliwa kwenye tumbo la bibi yangu akifuatiwa na baba yangu. Isaka alizaliwa na ulemavu wa kusikia na kuongea (kiziwi na pia ni bubu), hivyo kutoka na changamoto hizo baba yangu alimchukua na kumleta kuishi nasi Dar es salaam toka akiwa na miaka 5! Hiyo ilikuwa kwa madhumuni ya kumsaidia aweze kukaa karibu na wataalamu wenye ubobezi wa matatizo yake pia aweze kupata elimu stahiki!. Wengi wasiotufahamu vizuri huwa wanafikiria ni mtoto wa baba yangu kwasababu amekulia kwetu toka akiwa na umri huo. Ukweli ni mtoto wa kaka yake baba.

Mbarikiwe wote!

R.I.E.P uncle Zou Fu!

As family of O.O Igogo, we mourn the tragic death of our best friend, business partner, and family friend Sir. ZOU FU QIANG (in dark-red Tshirt) that happened in China earlier today! Our prayers go out to his family, friends, and everyone who is touched by his death!

From left Mr Molnar, Mr Igogo, and late Mr Zou

Mr Zou Fu a.k.a uncle Zou, he was one of the three founders and Shareholders of the on coming giant multi-millions Usd Copper Smelter and Gold Refinery entity, IGOZOMO ( IGOGO – ZOU – MOLNAR) Minerals Company Ltd, located in Mpwapwa district in Dodoma region, Tanzania.

2019 at Saba saba grounds!

Also, he was the owner and founder of Aloe vera herbal drug (Jufeel Aloe Vera juice) for human body immune boosting ……. Great human being to say the least! Such a beautiful soul gone too soon! We will surely miss you greatly!.????

“Rafiki yangu wa KWELI KIKWELI KWELI. MAREHEMU ZOU FU QIANG.(PUMZKA SALAMA.) MY DEAREST AND TRUETH FRIEND LATE Mr. ZOU FU QIANG. (REST IN PEACE)” by longtime best friend, brother, and business partner sir O.O Igogo.

Words of sympathy from Magreth
Words of sympathy from Magreth
Words of sympathy from Janet

“Thank you so much Arwa. That is a man who made me so popular and higly respected in the Chinese Communities, He was very loyal, honest, hard working, creative, excessfully kind to me and our family. I fail to stop crying whenever I recall his helping hand to all that I have gained since knowing him in 21 years. Let all of us in the family keep on praying for his Soul to rest in peace.???” ….. shukrani za baba kwa bintie Alpha kwa kutengeneza video ya baadhi ya matukio ya hivi karibuni ambayo marehemu alishiriki nasi.

Happy birthday Nyasungu!

Happy birthday to the sweetest babysister in the entire world! Thank you for unconditional love and respect you have shown to me that guides me to navigate the joys, the challenges, and understand the responsibilities of being a big sister! Wishing you an extra special day and amazing year! Happy birthday beautiful, love you so very much! ?❤❤❤

Birthday girl herself!
Akiwa na waridi wa moyo wake!
Warombo utawaajua tu!
akiwa na dada yake!
Akiingia kwa birthday dinner yake!

Cake toka kwa wazazi!

Once again, Happy birthday Nyasungu! My mama’s last born, my grandmother namesake, the peace maker, and the charm of our family ?? We love you baby girl! ?❤