Muhtasari-sehemu ya 5: Kutembelea familia ya Nyagilo.

Nyagilo’s residence, Mbweni.

Namshukuru Mungu kwa kutupa nafasi ya kutembelea familia ya mdogo wangu Janeth/ familia ya Nyagilo. Mimi nilikuwa sijawahi kufika kwenye huu mji wao mpya kwani walipo maliza ujenzi na kuhamia nilikuwa sipo. Wanaishi Mbweni walihamia huko takriban miaka 2 iliyopita.

Safari yetu ilianzia nyumbani Kibada ambapo nilipata ukodaki moment na mtoto wa kaka yangu aitwae Mary, huyu ni mjukuu namba 3. Na kulia kwangu ni kijana wa dada yangu mkubwa anitwa Daniel, yeye ni mjukuu namba 2 na pia ndio mjukuu mkubwa wa kiume.

Mercy

Bidada hapo juu ndio mjukuu namba moja, na wazazi wangu hupendelea kumtambulisha hivyo kwa watu “mjukuu namba moja” 😍😍 Eeh! Niliwapiga chenga wakubwa zangu nikaleta mjukuu wa kwanza! 😅😅

Hapo juu naye ni mpwa wangu, mtoto wa pili kuzaliwa kati ya watatu. Anaitwa Evin Otieno Nyagilo, bali mie napenda kumuita “my International nephew” 😍😍

Alipewa jina la kati la baba yetu. Pia mtoto wa dada yangu Daniel naye alipewa jina la kati la baba yetu-Otieno. Mbaaraka mkubwa sana. Mary yeye alipewa hilo jina kwasababu alizaliwa siku ya Christmas 25th, December huko U.K. She’s a Christmas baby. 😍😍 Huwa napenda kumuita Kitukuu cha Queen Elizabeth, Muingereza mwenye ngozi ya Chocolate. 😜😍😍

Kwakweli, tulipokelewa vizuri sanaaaaaaa! Tulikula, tukanywa, na kusaza! Tukacheza na kufanya utalii wa mji wa Mbweni. Jamani huko watu wamejengaje sasa?! Yani ni kibabe sana.

Sisters

Hapo ni wadada wa tumbo moja, Wakwanza kwa madada ndio mama Daniel, halafu mimi-mama Mercy, halafu Janeth -mama Evin. Yani Magreth a.k.a Mrs Jacob Massawe ndio alikosekana hapo. Alikwenda Moshi kwenye harusi ya shemeji yake.

Pia Blessing pichani juu naye hakuwepo, yeye ndio mtoto wa mwisho kwa baba. Anafanya tunakuwa na idadi ya watoto 5 wakike. Mungu wetu ni mwema sana twamshukuru kwa yote.

Leave a Reply