Category Archives: Mother and daughter moment

Muhtasari wa kumbukizi ya siku ya kuzaliwa Mercy.

Birthday girl herself

Siku ya tarehe 02, 04, 2023 ilikuwa ni siku ya kumbukizi ya mfanano wa siku ya kuzaliwa mwanangu Mercy.

Birthday girl akiingia kwenye mgahawa

Kama video inavyo onyesha hapo juu πŸ‘†πŸΏ Alianza kusherekea siku moja kabla ya siku yake maaalum kuwasaili, ambayo siku hiyo ilikuwa ni Jumosi ya tarehe 04/01/2023. Sambamba na marafiki zake walikuwa pamoja chakula cha usiku katika mgahawa ujulikanao kama TourΓ£o Brazilian Churrasqueria uliopo downtown Houston, Texas. 😍😍

Mtu na mama yake

Basi siku yenyewe ilipofika tulikuwa na muda mzuri pamoja asubuhi na jioni tukaenda tena kufanya kile twapendelea kufanya zaidi 😍😍 Kwakweli sina kingine mwaka huu zaidi ya kusema Asante Mungu wangu. Sifa na utukufu zote ni zako wewe Baba muumba wa Mningu na nchi na vyote vilivyoko. πŸ™πŸΏπŸ™πŸΏ

Asante Baba yangu. Asante Mungu wangu, Asante.

Muwe na weekend njema.

Siku zote tukipata nafasi ya kuwa pamoja huwa namshukuru Mungu sana, na huwa naakikisha nampa mwanangu 100% ya my attention! 😍😍 She’s everything to me! Kutokana na ratiba yake ya shule pamoja na kazi muda mwingi huwa tunapishana. Hivyo nyakati kama hizi ni muhimu sana kwetu sote. Si kwa uwezo wetu bali ni kwa neema yake Mungu Mwenyezi. πŸ™πŸΏβ€οΈπŸ™πŸΏ

Haya nawatakieni weekend njema na Sabato njema sana kwa waaminio.

Muhtasari -sehemu ya pili: Jambo lililonifurahisha zaidi mwaka 2022 ….!

Mama na mwana 😍

Kamanilivyosema kwenye posti yangu iliyopita somahapa yakwamba mwaka 2022 ulikuwa na baraka zake nyingi sana. Basi katika kuhesabu mibaraka yangu naweza sema huu nao ni moja ya mbaraka mkuu. Ni jambo ambalo lilinifurahisha zaidi 😍😍 Ni surprise niliyo wafanyia wazazi wangu.

Tarehe 25 mwenzi wa Saba, mwaka huu wa 2022 (07/25th/2022) ilikuwa siku ya furaha sana baada ya mipango yangu ya kuwafanyia wazazi wangu haswa mama yangu safari ya kuwasalimia bila ya kuwapa taharifa kama ilivyokua huko nyuma. Nimpango ambao nilipanga na mdogo wangu aitwaye Magreth Otieno Igogo a.k.a Mrs Jacob Massawe kuwa tutamfanyia mama surprise wakati wa siku yake ya kuzaliwa ambayo ni tarehe 27th July. Bahati mbaya ratiba yangu ilibidi nifike siku mbili kabla ya birthday yake. Mimi nilichukua likizo na kuandaa safari bila kumwambia mtu yoyote nyumbani isipokuwa mdogo wangu, mume wake na mwanangu tu. Sikutaka mama ajue kabisa hivyo kuzuia wanafamilia wengine kujua hata marafiki ilikuwa muhimu sana. Nashukuru Mungu kila kitu kilikwenda vizuri kama tulivyopanga tuliomba kibali cha Mungu kwa kumkabidhi mipango yetu naye akaibariki ikatimia. πŸ˜πŸ™πŸΏπŸ˜Safari yangu ilianzia Houston, Texas.

Nakumbuka siku nakwenda airport tulimpigia mama simu, akiwa nyumbani na baba na shangazi yetu fulani wakipiga story zao, nikaanza kumuuliza anampango gani na birthday yake?! Akawa anasema nahamu namtoko fulani amazing πŸ˜…πŸ˜… lakini ameshapanga kwenda Fun city na watoto wake wa shule (school trip). Nikamwambia kwautani nikikutumia Dola Mia ($100) uongezee kwenye hiyo trip itatosha? akasema itatosha sana. Nikamwambia basi nitakutumia tarehe 25, ambayo ndio tarehe nilikuwa najua naingia nyumbani. πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… Basi nikamalizia kwa kumwambia wakifunga shule apange trip yeye na wadogo zake na dada zake waende kutembea Zanzibar au mbuga za wanyama, wafanye bageti halafu anijulishe. Akashukuru kweli kweli bila kujua mimi hapo naingia uwanja wa ndege teyari kwa kum-surprise! 😍😍

Sasa, ilikuhakikisha chumba changu kipo katika hali nzuri mdogo wangu alimdanganya mama kuwa ana wifi yake anakuja toka Japan na ana mtoto mdogo hivyo anaomba aandae chumba cha dada Alpha (eeh usishangae sana, nina chumba changu kwa mama yangu 😍😍) ili afikie humo kwa siku kadhaa kabla ya kwenda Moshi. πŸ˜…πŸ˜… mdogo wangu wanaishi nyuma tu na kwa mama. Basi mama naye bila shaka wala kinyongo akamkubalia pasi kujua mwenye chumba yupo njiani. πŸ˜…πŸ˜…Nilipofika airport nilipokelewa na mdogo wangu pamoja na mume wake. Tukiwa njiani mdogo wangu akampigia mama simu akamdanganya kuwa amekutana na rafiki yake walikuwa wote huko kijijini Kowak (kijiji alipozaliwa mama yetu), na anasema hawezi kwenda kwake mpaka afike kumsalimia. Mama akanza kuuliza ninani? mdogo wangu alikataa kata kata kusema akamwambia ni surprise akifika hapo itabidi asikilize sauti yake ili amtambue ni nani! Mama alimbembeleza sana amwambie ni nani huyo lakini mdogo wangu alishikilia msimamo kuwa utamuona wakifika. Mama kidogo akawa kama amechukia kwani alikua anasema unakuja na mgeni mimi hata kupika sijapika hata juice ndo kwanza wanatengeneza sio vizuri na hapendi kabisa. πŸ˜…πŸ˜… mdogo wangu hakubadilisha msimamo wake mpaka tukafika nyumbani, na mengine yote yamebaki kuwa historia kama hiyo video ya tukio hilo inavyo onyesha. πŸ˜…πŸ˜…

Hii ni mara ya pili sasa nafanikiwa kuwa-surprise wazazi wangu. Tarehe 07 mwezi wa tatu, mwaka 2017 kwa kushirikiana na wadogo zangu pamoja na baadhi wafanyakazi wa Utegi Technical Enterprises Ltd (kampuni anapofanyia kazi baba yetu) tulifanikiwa kum-surprise baba yetu ofisini kwake, ilikuwa siku ya birthday yake. 😍😍 Tuliwahi sana ofisini kabla yake kitu ambacho hajazoea kwani siku zote yeye ndio anakuaga wakwanza kufika. Tukaingia ofisini tukazima taa sehemu ya mapokezi ili akiwa kwa nje ajue hakuna mtu. halafu tukamwambia mlizi arudishie tu mlango asifunge na funguo, na geti arudishie bila kuweka kufuli ili akifika tu ashtuke na akasirike (just to annoy him) kuwa waliacha mlango na geti wazi jana jioni. Sasa alipofika mlangoni anakuta ipo wazi akasema ooh! Tumesha ibiwa hapa, hasira zikamshika kuwa geti halikufungwa jana jioni. Halafu mdogo wetu aitwaye Guka ndio tulimuacha nje awe ana mmonita (monitoring him) kwa kutupa taharifa kwa simu kuwa ameshafika kwa parking lot. πŸ˜…πŸ˜… Na Guka alikuwa anawasiliana na dereva kusema wapo wapi. πŸ˜…πŸ˜… Tazama video hapo chini πŸ‘‡πŸΏπŸ˜…πŸ˜…

Basi, alipopita tu mapokezi kuingia eneo la secretary wote tukasema “surprise” kwa nguvu na furaha huku mmoja wetu alikuwa kwenye switch ya kwashia taa, tukaanza kuimba “happy birthday to you” πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜ alishangaaje, hasira zote zikaisha hapo hapo. πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜…πŸ˜… Hakuamini kuwa watu waliweza kuwahi kazini mapema hivyo ilitu wam-surprise! Alishukuru sana na furaha nyingi mno.

unaweza itazama video yote ya surprise kwa kupitia YouTube yangu hapo chini πŸ‘‡πŸΏ

Baba na mwana 😍

Kwakweli ni furaha kufanya jambo ambalo linamfanya mtu mwingine kuwa na furaha na kujisikia vizuri kwa kujiona mwenye thamani, lakini nifuraha zaidi kufanya jambo linalowafurahisha wazazi wako. Nafurahia na najisikia vizuri pale ninapoweza kuwafanya wazazi wangu wafurahi zaidi. Ni mbaraka wa pekee. 😍😍 Counting my blessings ma’am! πŸ˜…πŸ˜

Chumba cha dada Alpha

Na story zitaendelea maana mama Igogo alikuwa haamini alichokiona. 😍😍

Surprise ya mwisho iliharibika πŸ˜…πŸ˜… tulitaka dada yetu naye am-surprise mama lakini dakika za mwisho akaamua kumwambia kua anakuja halafu hata hakutuambia kuwa kamwambia mama hivyo ikawa surprise kwetu. πŸ˜…πŸ˜…πŸ™ˆπŸ™ˆ kwakweli hii ni the best moment for 2022.

Cecy-mama mzazi

Miaka takriban 3 iliyopita dada yangu naye alim-surprise mama big time. Alikuwa mjamzito na wakati uchungu umeanza akampigia mama kumsalimia basi wakaagana vizuri. Ndani ya masaa 2 mume wake anampigia mama simu kuwa mama Dani amejifungua mtoto wa kike na wameamua kumrithisha jina la mama. Mama akawa hataki kuamini anasema mbona mama Dani nimeongea naye muda sio mrefu? 🀣🀣🀣 akaambiwa pale anakupigia alikuwa ameshikwa na uchungu na tulikua njia kwenda hospitali. πŸ˜…πŸ˜… Na mtoto mwenyewe ndo huyo hapo πŸ‘†πŸΏ juu. 🀩🀩

Mwanangu mimi ….!

Unajua saa nyingine huwa siamini kama ni mwanangu ?? Mwenzenu nimekuza! Nikiangalia tulipotoka na tunapoelekea yani hakuna ninachokiona zaidi ya mkono wa Mungu ukiwa juu ya vichwa vyetu kumimina mibaraka yake.

Namshukuru Mungu sana na nitalitukuza jina lake milele. Kanipa rafiki wa milele. Tumekuwa pamoja, tumejifunza mengi pamoja, haswa kupitia makosa yangu mimi kama mama yake, yakampa somo la moja kwa moja. Mungu ni mwema sana. Nimevuka stage ya kuwa strictly mama; sasa hivi ni mama plus rafiki. Tunaongea na kuelekezana kirafiki tu! Kama malezi niliyompa kabla ya miaka 18 hayakumuingia na kumtengeneza kuwa kiumbe bora basi katika umri huu hakuna kitakacho mbadili zaidi ya kumuombea tu! Namshukuru Mungu sanaaaaaaa, mwanangu hajawai kunisumbua hata kidogo. Mungu kanibariki na mtoto msikivu, mwenye hofu ya Mungu, yani ni mtoto mwema mnoooo ndio maana saa nyingine siamini kama nimemlea mimi! ?? such a beautiful, humble, strong, smart, intelligent, classy, loyal, hard working, independent, charming young lady. I mean the list can go on and on but glory and honor all to Almighty God! ??

Leo nimejisikia kupost picha zetu haswa zahuyu mrembo wangu! ?? Kwani kunatatizo?! ?? sikuhizi nimeachana na kupost picha za watu haswa tusio na undugu, urafiki au mazoea. Ndio maana mnaniona sipost mara kwa mara. Nafanya mambo yangu mengine ambayo yananipa furaha na amani zaidi na hayo ndio nitakuwa napost humu.

??

Nimejisikia kumpost kuweka kumbukumbu ?? si blog ya mama yake jamani! ?? Ndio raha yakuwa na kitu chako mwenyewe ulicho kitengeneza wewe mwenyewe kwa utashi wa akili zako na mikono yako miwili. Hakuna atakaye kupangia nini cha kufanya labda huyo mtu ni punguani! ?? ………… Mungu azidi kumbariki sana na kumpa afya njema. ??

Safari ya mama Washington DC

 Siku iliyofuata, tuliamka na kupata breakfast, kisha tukaendelea na mizunguko yetu.Β     Nilitaka mama aone Washington DC yote kila jengo la office na majumba ya matajiri wa huko. Bahati mbaya au nzuri mama alikataa kutembea alidai amechoka kwasababu ya mizunguko ya jana yake. Hivyo, ikabidi tuchukue tour bus ambayo ilituonyesha sehemu zote tulizopenda kuona.Β Of course, nimuhimu kusalimiana na wapendwa wako pale unapopata nafasi. Basi hapa tutakutana na cousin yangu (mtoto wa mama yangu mkubwa, mama yake ni wapili kuzaliwa katika familia ya mama yangu) Dr. Joseph Obure yeye anafanya kazi hapo Washington DC.Β Mama na wanaeΒ Mama na kijana wake Β wakisogoa story za miaka mingi ?Β 

Mama na binti yake katika pozi ?


Siku ilyofuata, tulianza kwa kununua green tea na pumpkin bread (my all time favorite breakfast) katika cafe ya Starbucks, tuliungana na aunt yangu aitwaye Sophie au mama AnnaDΒ na baadaye kuanza safari ya kuelekea Makao Makuu duniani ya kanisa la Wasabato. Β 

Hili eneo ni kubwa sana kama utabahatika kutembelea basi panga angalau masaa azidi ya matatu ili uweze kufaidi na kujifunza kidogo. Mama yangu alifurahia sana.Β 

  

Basi safari yetu kwa siku hii ikaishia napa, tukaenda kula na kufanya mizunguko kidogo ya dakika za mwisho kwani muda wetu ulikuwa unatupa mkono.Β    
Nawatakieni maandalizi mema ya Sabato na Sabato njema kwa waumini wote wa dhehebu la Wasabato duniani ?

Mother’s Day 2018: Je, ungependa ku-share nasi hadithi / shukrani ya mama yako mpenzi?

Mother and daughter moment: Mother's Day inakuja ni jumapili ijayo, je umepanga kufanya nini au kumfanyia nini mama yako? Mimi binafsi nitakuwa Washington, DC niki enjoy kidogo na mama yangu! Kwani hii itakuwa Mother's Day ya kwanza kabisa kwa mama yangu kuwa hapa Marekani pamoja nami; hivyo nitaitumia nafasi hii vyema.Β Sasa basi tuambie kuhusu wewe. Je, ungependa kuShare nasi stori ya mama yako au kutoa shukrani zako kwa mama ukiambatanisha na picha ya mama yako? Basi wasiliana na alphaigogo.com kwa kutuma ujumbe kwa njia ya blog, Instagram DM, au Facebook nasi tutaweka ujumbe wako.Β 

**Zoezi hili linaanza rasmi leo hii mpaka JumaMosi.**
Asanteni 
Pichani ni mdogo wangu Janeth na binti yake Essy. #TBS 2017

 

Mama na mwana

Regrann from @monalisatz - Dear Mama, Najisikia mwenye bahati mno kuwa mtoto wako.Umekuwa mama bora kwangu,bibi mzuri kwa watoto wangu,rafiki yangu wa karibu, mfanyakazi mwenzangu, kila kitu kwangu. Sijui ningekuwaje bila wewe?
Mungu akutunze mama yangu.
Nakupenda kila saa,
Nakupenda kila siku.
Happy birthday Mama @natashamamvi - #regrann

Mother and daughter moment

Pretty-pretty-pretty! Such a lovely priceless moment, mama Cookie na Cookie wake! ???....... Jamani Valentine's moments unaweza ukachagua mtu yoyote umpendayeΒ  uka dedicate mwaka huu kwake! Anaweza akawa mama yako mzazi, baba, dada, mtoto wako n.k! Yoyote yule amabye yupo karibu na ndani ya roho yako! Ila kama ni mume / Mke lazima awe amehalalishwa na mamlaka husika kama serikali, kanisa, au msikitini!Β Β 

Mama Mbuna: Mungu wangu ninaye mtumikia akubariki milele yote

Wooh Mungu ni mwema mno. Ilikuwa siku kama ya leo (Alhamisi), tarehe kama ya leo (11/01/ mwaka uleeee, mnamo saa 09:30 mchana, mvua yenye utulivu ikiwa inanyesha, nikiwa pale Ocean Road Hospital, BWANA alinipatia mtoto mzuri wa kike tunayemuita Foster Mbuna Mkapa. Aliyefanya CV yangu ibadilike na kuanza kuitwa mama Foster tangu siku hiyo. Β Nakutakia baraka zote za rohoni na za mwilini unapoisherehekea siku yako hii ya kuzaliwa. Kwa imani nakutamkia neno hili kwamba "hakuna silaha yoyote itakayo inuka juu yako ambayo itafanikiwa." Mungu wangu ninaye mtumikia akubariki milele yote. HAPPY BIRTHDAY TO YOU. MUMMY LOVES YOU!!!!!!

Cookie Moses Iyobo nionee huruma mwenzio!

Jamani Cookie binti wa Moses Iyobo na aunty Ezekiel ni nini unanifanyia mwenzio! Embu nionee huruma my darling, wewe hujasikia wenzio ndoa zinavunjika hawataki kuzaa kwa uchumi huu wa Babu yako Trump na Dr. Magufuli ?? maisha magumuΒ  mwanetu ??.Β  Β 

Tatizo ni jinsi wewe ulivyo mzuri yani mpaka unanitia katika vishawishiΒ  mwanangu wee! Nitakuwa mgeni wa nani mie maisha yenyewe haya ya paycheck to paycheck, Niki miss paycheck moja tu nakuwa homelessΒ  ????????‍♂️ You are beautiful and photogenic fulani amazing kweli kweli! Mungu akulinde, ukuhepushe na manyang’au ya hii dunia! Amazing! BTW, happy belated birthday mama Cookie, Ubarikiwe sana.

Mother and daughter moment!

Mama Gabby na Gabby wake! Beautiful pic

QuoteΒ for today: You’reΒ the most beautiful thing I keep inside my heart!

Mama na mwana: Hakika wema na fadhili zako zitanifuata siku zote za maisha yangu!

Ni kwa neema tu! Nasema ni kwa neema yake Mungu kwani akili yangu haikuwai kuwaza kuwa ipo siku kama hii! Hivyo namshukuru sana Mungu kwani ni hakika wema na fadhili zake zitanifuata siku zote za maisha yangu, nami nitadumu ndani yake! Nimeweza kuona ukuu wa Mungu kwa kufanikisha uumbaji wake! Amenibariki na rafiki wa kweli ambaye upendo wetu utadumu milele na milele! Β ………Najua tunamipango mingi sana naomba Mungu azidi kutuwezesha katika kila jambo! Moja ya vitu ambavyo nasubiri kwa hamu sana ni passport ya mwanangu!! Yes! her American passport!! Ee Mwenyezi Mungu mimina baraka zako!! Yani can’t wait!! Maana tutatembe hii dunia mpaka ndege zinune Β zigome kabisa kuruka ?? ……..Anyway, namshukuru Mungu kwa mbaraka Β wa huyu mtoto! Naomba azidi kunilindia na kumuongoza katika kila jambo haswa kiroho, asikae mbali naye!

Mother and daughter moment

Thankful. Grateful. Blessed #LoveOverEverything

Wamenoga eeh! Mama na mwana, Nancy na binti yake Zuri. So pretty!

Quote for today: A daughter is just a little girl who grows to be your best friend.

 

 

Mother and daughter moment

Akothee na mama yake mzazi

?? ngoja nicheke kwanza, maana Akothee ananifurahisha sana! I think she is a sister I need ??? ……. Yani Akothee anajua how to do a “role” change! Akiwa kanisani siku ya Sabato utamjua ndo yeye anavaaga Vi-min na kukatika kwa stage ?? Yani hadi kilemba ile Luo style anafunga siku ya Sabato na sadaka anakusanya. Β Na akiwa anakula #bata ni anakula kweli kweli. Sasa kama hapa yupo na mama yake mzazi, muangalie alivyo tega masikio kwa usikivu utafikiri sio yeye. So funny! Wamependeza sana! …….Akothee I know you are my loyal reader, but I want you to be my sister please, I know my sisters love me but they don’t mind to share with you at all ?? We will drive this world crazy, I can tell ??……. Nice pic Akothee, say hello to mama!

Mother and daughter moment!

Nimependa sana hii picha ya Mwamvita Makamba na mama yake! Wamependeza sana. Ilikuwa ni sherehe ya mdogo wake Mwamvita ina itwa “bag” party mie ndo nimeona leo mwe kama kawaida yangu kama kitu nilikuwa sijui basi nawaeleza tu ukweli! Watu walipendeza sana. Nimeipenda!

Mother and daughter moment!

Beautiful Emelda Mwamanga na binti yake Gabby! So nice! Nivizuri kuwapenda watoto wetu zaidi wakiwa katika umri huu mdogo kwani inawajengea kuamini, kutambua thamani yao wakiwa wakubwa, Β na kuwa wajasiri! Mtoto yoyote yule anahitaji muongozo, na mipaka lakini pia anahitajika kuwa huru haswa kifikra! Hivyo nijukumu la mzazi kumjenga mtoto wazingira huru ya kujieleza na kutafakari ambayo yana boundaries at the same time!

Mtoto siyo mdoli jamani, mfunze mtoto maadili mema, na jinsi y kuweza kukabiliana na hali zote za maisha. Kwamfano hapo Gabby unaona amefundishwa kupika na kuchanganya vitu kwa kutumia blander hivyo hata akienda kwa watu ambao wanatumia "high tech" kitchen appliances hashangai sana. Napia anajua jinsi ya kutumia mikono yake kushika vitu! Nilishawahi kuona kwa macho yangu mtoto wa miaka nane (8yrs old) bado anatawazwa akimaliza kutumia choo ?? Yani anajisaidia haja kubwa halafu anita dada wa kazi au mama yake amsafishe! And the mother was very OK with it ?? Jamani!! Anyway, those are rich people problems, maskini kama sisi tutayawezea wapi? ??

 

Ndugu wanapokutana…….!

Pale ndugu wanapokutana ni furaha kwa kwenda mbele! ........mama akipata kumbukumbu ya picha na binti yake kwa furaha ya kuonana tena baada ya miezi kadhaa kupitia! Magreth akimpokea dada yake Elline kwa furaha sana!.......... Β kwafaida ya wasomaji wangu, Elline ni dada yetu mkubwa, mimi ndio namfuata. Yeye alikuwa anaishi Geita lakini mwezi uliopita wamehamishiwa kikazi Makao Makuu (Dodoma). Hivyo sasa ni wakazi wa Dodoma! ........Tunamshukuru Mungu kwa yote!Β 

Mother and daughter moment!

Mama na mwana wakiwa katika mazingira safi kabisa ya Kisumu International Airport, hapo nchini Kenya! Hii Airport kwa muonekano tu wa nje inaonekana ni safi zaidi ya ile ya kwetu pale Bongoland! Japo hii ipo nje ya mji wa Nairobi lakini inavutia kwa usafi sana........Ni nini haswa tatizo letu sisi Watanzania! Maana hata mazingira yatengenezwe mazuri vipi haichukui muda utashangaa jinsi yalivyo chafuliwa, na kuharibiwa! Saa nyingine tunailaumu serikali kwa mambo ambayo ni sisi wenyewe ni tatizo! Kweli aliyeturoga kafa!.........Picha hii imepigwa week na siku kadhaa sasa wakati mama Igogo alipokuwa amekwenda kwenye msiba kwa wakwe zake na binti yake!

Motherhood!

Mama na mwana! Pendeza sana mama yetu so beautiful! Β Happy belated Mother’s Day to you mama yetu we love you ? Btw, Dinnah na mimi tulisoma wote CBE Marketing major natulikuwa roommates. Β Dinnah ni ana akili usipime hata waliosoma naye UD watashuhudia! Plus msafi sana kama mimi vile ??

 

Mother and daughter moment

What a beautiful picture of Hoyce Temu and her beautiful lovely daughter Rubby! Priceless! Happy Mother’s to Hoyce Temu