Category Archives: Wedding ceremony

Sherehe ya kipekee ya kumuaga Dorice Sassi Igogo!

Ameagwa rasmi! Siku ya Jumatano, tarehe 06/02/2021 zilisikika nderemo na vigelegele vingi sana kutoka kwa familia ya Mr. Emmanuel Agonda Sassi (marehemu) na Mrs. Magreth Cornel Awiti a..k.a Mrs Agonda, a.k.a Mrs Sassi pamoja na wanaukoo wote wa Adol Igogo. Ilikuwa ni furaha ya kumuaga rasmi binti yao kipenzi Mwalimu Dorice Sassi Igogo ambaye anakwenda kuanzisha rasmi kaya (familia) yake.

Dorice akiwa na mtarajiwa wake

Ndoa ni jambo la kheri, ndio maana wazazi hufanya sherehe ya kipekee kabisa ili kumuaga mpendwa wao, kama njia mojawapo ya kuonyesha furaha yao na shukrani kwa Mungu.

Dorice a.k.a Vumilia ni binti aliyezaliwa katika familia ya watoto (3) watatu, yeye akiwa mtoto wa pili kuzaliwa na msichana pekee.

Mtoto wa kwanza ni Yustor Sassi (Kulia), Dorice, na Joseph (kushoto). Katika picha hii inaonyesha makaka wakimlisha keki dada yao, na mama mzazi akiwa pembeni anaangalia.

Yustor akiwa nafuraha nyingi wakati wa kulishwa keki na dada yake.

Joseph naye akifurahia kulishwa keki na dada

Yustor akimpigia saluti mdogo wake, kwa heshima kubwa kama afanyavyo huko jeshini!

Tazama jinsi kaka wa bibi harusi mtarajiwa akitoa saluti kwa mdogo wake kwa furaha na ushupavu wa kijeshi.

Bibi harusi mtarajiwa akielezea historia yao, wapi walikutana na nini kiliwakutanisha.

Zawadi kwa bwanaharusi mtarajiwa

Bibi harusi mtarajiwa akiwa na Mc wa shughuli hiyo ajulikanaye kama McKatokisha

Wamazazi wa upande wa bibi harusi mtarajiwa

Yani mdogo wangu huyu kwa kuchakarika aaah! Ni Mwalimu na pia ni mjasiriamali wa nguvu. Hii keki ametengeneza mwenyewe kwa mikono yake kupitia kampuni yake ya isadoricakes and sassyjuice! Izidi barikiwa kazi ya mikono yake.

Mtarajiwa akikata keki

Akilimlisha mama mzazi kwa unyenyekevu na upendo mwingi

Akimpatia mama mzaa chema keki yake kama ishara ya upendo na ukarimu wake kwake na ukoo wa mumewe mtarajiwa.

Mama mzazi naye alipata kipande chake

Mama wazaa chema na binti yao

Wamependeza kwakweli

Haya ngoja nikusaidie kidogo kama haujui, bibi harusi mtarajiwa ni mtoto wa mama yangu mdogo. Mama yake ndio kitinda mimba kwa uzao wa bibi yangu mzaa mama. Sasa basi, kama ilivyo kwa mama yake Geoffrey Kateti (kama mnamkumbuka) ndivyo ilivyo kwa mama yake na bidada hapa. Mama yake naye alifuata nyayo za dada yake (mama yangu) akaolewa Utegi! Utegi oyeeee! ?? Tofauti na mama yake Geoffrey, mama yake Dorice ameolewa ukoo mmoja na dada yake ?? chezea ukoo wa Odol! Hivyo Dorice ni mdogo wangu pande zote; kwa baba na kwa mama.

Mapenzi ya Mungu yalitimizwa baba yangu mdogo (baba wa bibi harusi mtarajiwa) aitwae Emmanuel Agonda Sassi, alishalala usingizi wa mauti takriban miaka 4 iliyopita. Twamshukuru Mungu kwa yote.

Once again, hongera sana mdogo wangu, shemeji tunakukaribisha kwetu kwa mikono miwili. Mungu awe nanyi siku zote. Amen! ????

?@lush___makeup

? @mckatokisha

? Decor@lillies_luxe_decor

#FBF

Embu tujikumbushie mambo yalivyo kuwa siku ya kuvikana Pete ya ahadi ya ndoa /uchumba, siku ya Jumatatu ya mwezi wa kwanza tarehe kumi na mbili mwaka huu, 01/12/2021. Love is the beautiful thing.

Sherehe ya kuagwa kwa Rhoda Igogo!

Siku ya Jumapili ya tarehe 05/23/2021 ndio ilikuwa siku rasmi ya kuagwa kwa bibi Rhoda Alexander Igogo. Sherehe hiyo ilifanyika nyumbani kwa baba yake mlezi huko Segerea. Zifuatazo ni baadhi ya picha na video kutoka kwenye tukio hilo. Picha hazipo kwenye mpangilio rasmi nimeweka tu!

Bibi harusi mtarajiwa akiingia ukumbuni

Mr Victor na mkewe mtarajiwa!

Rhoda na mpambe wake bi. Oliver Chumo

Oliver

Baba mubwa wa Rhoda, mzee Charles Olung’a Igogo

Wazazi wa bwana harusi mtarajiwa, Mr and Mrs Ollal

Wanandoa wapya Mr and Mrs Isaka Alexander Igogo

Mama mdogo wa Rhoda, Mrs O.O Igogo akipungia wageni

Baba mkubwa wa Rhoda, mzee Charles Olung’a Igogo (kushoto) pamoja na baba mlezi mzee O.O Igogo

Dada wa bwanaharusi mtarajiwa Ms. Aphino Alexander Igogo, pamoja na mdogo wa bibi harusi mtarajiwa Blessing Igogo wakimkaribisha shemeji yao kwa furaha.

Rhoda na mama yake mzazi

Bwanaharusi mtarajiwa akiwa na bibi yake mzaa mama yake.

wageni waalikwa wakiwa na mwenyeji wao mzee O.O Igogo

Mc Rhevan katika ubora wake

Bibi harusi mtarajiwa number 2 akitoa ombi la mwisho.

Rhoda akitoa zawadi ya keki kwa Mkurugenzi Mkuu wa Utegi Technical Ltd, Mrs Margaret Mabada kwa niaba ya wafanyakazi wote wa Utegi ambapo Rhoda ameajiriwa.

Rhoda akicheze na wafanyakazi wenzake

Baba na binti yake wakicheza

Kwa picha zaidi bonyeza ????

https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/rhodasendoffpartyphotos/

Kitchen party ya RHoda Igogo

Bibi harusi mtarajiwa Rhoda Alexander Igogo

Wakati tukisubiria picha kutoka kwa wataalamu waliolipwa kufanya kazi hiyo, basi tuanze na tulizonazo.

Siku ya jumapili tarehe 05 /16 /2021 ilifanyika sherehe ya kumfunda mwali (bibi harusi mtarajiwa) a.k.a Kitchen party ya Rhoda Alexander Igogo. Sherehe hii aliandaliwa na mama yake mlezi akishirikiana na ndugu na jamaa pamoja na marafiki. Ilifanyika kwenye makazi ya wazazi walezi huko Segerea ambapo bibi harusi mtarajiwa ndipo anapo ishi na ndipo atakapotokea kwenda kwa mwenza wake.

Akiingia ukumbuni mwenye nyuso ya furaha na tabasamu kama lote ndio mama mzazi wa Rhoda na Isaka, Mrs Joyce Alexander Igogo. Ni mke wa marehemu baba yangu mkubwa (wapili kuzaliwa kwenye familia yao baba, watoto bibi Rhoda Nyakanga Olwengo). Babu yangu mzaa baba (Marehemu mzee William Olung’a Igogo) alikuwa na wake watano (5) ??? usishangae sana maana marehemu babu yake baba (my great grandfather) Chief Sarungi Igogo yeye alikuwa na wake 19 ??????? welcome to our ukoo ?? …… Rhoda ndio mtoto wa mwisho kwao. Akitoka kuzaliwa Isaka ndio Rhoda anafuata. Na harusi zao zimekuwa ndani ya mwezi mmoja. Familia hii inajumla ya watoto 7 walio hai, mmoja alifariki. Grace a.k.a Anyango, Aphino a.k.a Nyawade, Kenneth (Marehemu) a.k.a Ukombozi, William a.k.a Mzee, Dr. Obadiah, Isaka, na Rhoda a.k.a Nyolwengo, na Emilia Igogo! ….. Mungu ni mwema sana.


Haya embu tufurahishe macho kwa hizi tilizonazo!

Pichani ni Dia Alex Odemba na bibi yake mama Igogo.

Dada kama dada! Huyu ni dada yake Rhoda aitwae Aphino.

Dia Alex Odemba katika ubora wake!

Mama wa isadoricakes_and_sassyjuice. Dogo langu Mwalimu mwenye ujasiriamali wake! ??

bibi harusi mtarajiwa akikata cake yake

Kwamahitaji yako ya Cake nzuri zenye ubora wake, juice fresh tamu, na Mc wa kitchen party, tafadhali husisite kumtafuta @isadoricakes_and_sassyjuice ndio habari ya taifa! ???

Kutoka kushoto ni mama yangu mzazi, akifuatiwa na mdogo wangu Vumi Sassi, anayefuata ni mdogo wake mama yangu (kitinda mimba kwa familia yao) napia ni mama yake Vumi aitwaye Magreth Cornel Awiti a.k.a Mrs Agonda Sassi, na anayefuata ni mdogo wangu kipenzi Magreth Rhoda-Nyasungu a.k.a Mrs Massawe.

?? mama zangu hao! ??

Rhoda akiingia ukumbini kwa furaha kabisa

Mama mlezi wa Rhoda

Mrs Vetto Igogo (kushoto) pamoja na Mrs Isaka Igogo (kulia). Mmemuona bibi harusi wetu wa wiki iliyopita?! ?? Miguu imeiona? Miguu halisi ya Kiafrika! Yani wana miguu ya bia kama mawifi zao! ??

Baba naye hakutaka kupitwa na matukio katika picha ?? akiwa na furaha kubwa pamoja na binti zake akitaniana na ucheshi wa hapa na pale.

Mtu na wifi zake! Mrs. Massawe kwa mbele hapo, Mrs Vetto Igogo mtu kati, na Mrs Isaka Igogo nyuma hapo.

Wifi karibu sana Utegi!

Watu wakiserebuka kwa raha zao!

Mke ya Mrombo! ??

Mwenye nguo ya njano, anayecheza kwa hisia zote, ni dada wa bibi harusi mtarajiwa, aitwaye Grace Alexander Igogo a.k.a Anyango, yeye ndio mzaliwa wa kwanza kwa familia yao. Anafurahia kusindikiza kitinda mimba kuanzisha familia yake. Pembeni yake ni mama mlezi wa Rhoda.

Mama naye hakutaka kujivunga kwani wimbo wenyewe siunausikia? ???

Haya tunamtakia Rhoda safari njema katika kuhitimisha kilele cha sherehe za kuagwa kwake na familia yake mpaka siku ya harusi. Jumapili hii ni Send-off yake na Jumapili ijayo ndio harusi. Mungu awatangulie katika kila jambo!

BTW, hii siyo mara yakwanza kwa familia yetu kuwa na harusi mbili kwa mpigo (double wedding), kaka yangu mkubwa Vetto Igogo na dada yangu Elline Igogo harusi zao zilipishana wiki tu, tuliserebuka kwa wiki mbili mfululizo! Yani tulianza na kitchen party ya dada Elline, ikafuta harusi ya kaka Vetto, ikaja Send-off party ya dada Elline kisha harusi yake. Na baada ya hapo ikafuata sherehe ya kuvunja kamati. ??? I tell you, this familia loves to partyyy! Nahiyo ni miaka ishirini na mbili (22 yrs ago) iliyopita. Na sherehe zao Ilikuwa kubwa kweli kweli hizi ni chamtoto! Mama zigi-zig catering na Dotnata Catering walipika mpaka walishangaa. ???

***Updates: picha za nyongeza***

Rhoda na binamu yake Honorable Madam Judge Dr Modesta Opiyo.

Rhoda na mama yake mzazi

Juu ni mama mkwe wake Rhoda Mrs Scola Oguna Ollal.

Mawaidha ya akina mama, shangazi, na wanawake wachanga kwenye ndoa.

Mama mdogo Mrs O.O Igogo akitoa ombi la kwanza.

Mama mdogo Mrs Agonda Sassi akitoa ombi la mwisho. Walianza na Mungu wakamaliza na Mungu. Amen!

Kwa picha zaidi bonyeza ????

https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/pendokitchenpartyphotos/

Rhoda na rafiki yake, hizi ni pre-wedding pictures

Blessing latika ubora wake

Wadada hao! ??

Kwa picha zaidi bonyeza ????

https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/rhodapresendoffphotos/

NYONGEZA: HARUSI YA ISAKA NA SARAH.

Video hapo juu ni muhtasari wa harusi ya Isaka na Sarah, imetengenezwa na studio za Mc Rhevan.

Mr and Mrs Jacob Massawe

Zifuatazo ni baadhi ya picha za ziada na video zilizotengenezwa na camera binafsi za wanandugu. Naziweka humu ili ziwe sehemu ya kumbukumbu. …… Hapo juu ni dada wa bwanaharusi Magreth Rhoda-Nyasungu a k.a Magreth Otieno Igogo a.k.a Mrs Massawe akiwa sambamba na laazizi wake ambaye ni Shemeji wa bwanaharusi. #Warombo #SweetMangi ??

Mama Dia a.k.a Cheusi akiwa na best ake mama Igogo

Dia Alex Odemba akideka kwa bibi yake.

Mrs. Massawe

Shemeji yake Isaka, Mr. Massawe (kushoto) akiwa na kaka zake Isaka, Mr. Albetus Ajee Chuche (mtu kati) na Mr. Guka Otieno Igogo (kulia).

Mashabiki wa Simba nao walipewa haki yao! ?

Hongera sana Isaka na Sarah!

Mr and Mrs Isaka Alexander Olung’a Igogo

Hayawi hayawi sasa yamekuwa! Wamehalalishwa duniani na Mbinguni yakwamba wawili hawa ni mwili mmoja!

Sarah akila kiapo kitakatifu

Agano hili takatifu lilifanyika siku ya Jumosi tarehe 05 /08/2021 katika kanisa la viziwi lililopo huko Bunguruni, Dar es salaam. Tunawaombe baraka nyingi sana katika familia yao hii mpya walio ianzisha!

Bibi harusi

Bwanaharusi akihakikisha je kweli ni yeye?! Kabla ya kula kiapo, maana hukawii kubadilishiwa mke kama Jacob (Yakobo)! ? mjini mambo mengi jama! ?

Bwanaharusi amehakikisha na ameridhia! ?? Kama hujawahi sikia kisa cha Jacob (Yakobo) basi chukua Biblia yako na ufungue kitabu cha mwanzo sura 29 yote itakupa stori kamili!

Kwaufupi ni kwamba, Jacob baada ya kutumikia miaka saba kwa mzee Labani kama mahari ya kumuoa binti yake Rachel (Raheli), siku ya harusi akakuta amebadilishiwa mke anaye mpenda kwa dhati na kupewa Lea ambaye alikuwa ni dada wa Rachel (Raheli). Kwani kulingana na mila na desturi za kabila na ukoo wa mzee Labani ni kuwa mkubwa lazima aolewe kwanza ndipo mdogo anafuata. Kwa maana hiyo Jacob ilibidi atumikie miaka 7 mingine ili aweze kumpata Rachel. Kwa maana hiyo Jacob alitumikia miaka 14 kwa mzee Labani kama mahari ya kumuoa kipenzi cha roho yake! …… Sikilizeni wanawake wenzangu, kama mwanaume anakupenda basi hakuna gumu wala zito mbele ya macho yake! He will move mountains just to have you! Tena bila hiyana yoyote! Wanawake wazuri ni wengi sana lakini Mke ni mmoja tu ambaye kila mwanaume anajua hilo!

Maharusi na wapambe wao
Wasimamizi wao
Mchungaji aliye idhinisha ndoa hii

Sarah akisindikizwa na kaka yake aitwaye Alex ambaye ndiye aliyemlea toka wazazi wake wamefariki hadi leo hii anapokwenda kuanzisha nyumba yake mwenyewe. Kwa Sarah hamuoni Alex kama kaka bali ni baba yake mlezi na mke wa Alex ni mama yake mlezi, hao ndio wazazi wa Sarah.

Hapo juu ni baba mlezi wa Isaka ajulikanaye kama mzee O.O Igogo. Yeye ndio amemlea Isaka toka akiwa na miaka 5. Baba mzazi wa Isaka amefariki takribani miaka 7 iliyopita. Mzee 0tieno Igogo ni mdogo wake na marehemu mzee Alexander Igogo ambaye ndiyo Baba yake na Isaka.

Mama mlezi wa Isaka Mrs O.O Igogo akisalimia maharusi, nyuma yake ni mjukuu wake aitwaye Essy.

Mashangazi na mama wakubwa kwa wadogo upande wa bwanaharusi.

Baba mlezi akiwa na furaha nyingi usoni kwa kuongeza mtoto mwingine kwa familia.

Madada, mabinamu, na mashemeji wakiingia kwa shangwe!

Kutoka kulia, ni mdogo wa bwanaharusi aitwaye Blessing, akifuatiwa na mpwa (niece) wa bwanaharusi Essy, akifuatiwa na shemeji mkubwa Mrs. Vetto Igogo, na dada mkubwa (wapili kuzaliwa kwenye familia ya kina Isaka) Aphino Alexander Igogo (Mrs Ogoche).

Mdada mwenye nguo ya blue kutoka kushoto, huyo ndio kitinda mimba kwenye familia ya akina Isaka. Anaitwa Rhoda Alexander Igogo. Naye harusi yake ni mwishoni mwa mwezi huu. Wiki hii ni kitchen party yake.

Bibi harusi mtarajiwa Rhoda Alexander Igogo akiwa na maharusi Mr and Mrs Isaka Alexander Igogo.

Bibi harusi mtarajiwa, bi Rhoda akifurahia kaka kupata “jiko”!

Mama mlezi wa bwana harusi pamoja na baba msimamizi wa ndoa hii mzee Samuel Olung’a Igogo wakitoa nasaha zao.

Baba mlezi akitoa neno kwa niaba ya kamati!

Mama mlezi akiwa na maharusi

Maharusi wakikata keki!

Wapendwa, kwamahitaji yako ya Cake nzuri zenye ubora wake, juice fresh tamu, na Mc wa kitchen party, tafadhali husisite kumtafuta @isadoricakes_and_sassyjuice ndio habari ya taifa! ???

nnnnn

Maharusi wakifungua dancing floor kwa kucheza ziro-diatance music ?? asiye na wake akumbatie chupa ya soda! ???

Meza kuu upande wa bibi harusi

The Olung’as!

Hawa ni baba zake Isaka, wadogo kwa wakubwa. Kutoka kushoto ambaye kichwa tu ndio kimeonekana ni mzee Samuel Olung’a Igogo (baba mkubwa na msimamizi wa ndoa hii), akifuatiwa na mzee Charles Olung’a Igogo (baba mkubwa), akifuatiwa na mzee Otieno Olung’a Igogo (baba mdogo na mlezi wa Isaka), akifuatiwa na Genga Olung’a Igogo (baba mdogo)

Walianza na Mungu, wakamaliza na Mungu. Mama mdogo wa Bwanaharusi Mrs Emmanuel Agonda Sassi Igogo akitoa sala ya mwisho!

Mathayo 19:5 “akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja”!

Marko 10:9 “Basi, alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe” ….. I present to you Mr and Mrs Isaka Alexander Olung’a Igogo

Mc Rhevan mtu kati hapo

picha zote shukrani kwa Mc Rhevan studio. Ukitaka kuona picha za tukio nzima tembelea ????https://RHEVANSTUDIO2021.pixieset.com/isakaandsarahweddingphotos/

Tunawaombea kheri na baraka nyingi!

Bwana harusi mtarajiwa-Isaka akiwa kwenye pozi na bibi harusi mtarajiwa-Sarah

Kesho ndio siku yenyewe kuu, ambapo wawili hawa wataunganishwa kuwa kitu kimoja na koo mbili zitaunganishwa rasmi mbele za Mungu.

Naam, kwamara nyingine tena tunapenda kutoa pongezi nyingi sana kwa watarajiwa hawa kwa kufanya maamuzi mazito yenye busara. Mungu azidi kuwatangulia katika kila jambo ambalo limepangwa kufanyika kesho basi likapatae kibali mbele ya uso wa Bwana na lifanyike kama lilivyopangwa kwa utukufu wa Mungu.

Mwenyezi Mungu mwenye wingi wa rehema na neema awazidishie ulinzi wake na mibaraka yake siku zote za maisha yao. Ndoa yao ikajae amani na furaha, naye Mungu Baba awe mgeni wao siku zote. Wakabarikiwe wao na uzao wao wote. Twaomba kwa imani katika jina la Yesu. Amen! ????

akasema, Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja!” *** Matayo 19:5

“Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe” ****Marko 10:7

Jana ilikuwa siku ya kuagwa kwa bibi harusi mtarajiwa. Bi. Sarah alifiwa na wazazi wake wote wawili akiwa mdogo. Kaka yake Alex akamlea hadi sasa anatokea kwao kwenda kwake na mumewe mtarajiwa. Ni mlemavu wa kusikia na kusema??‍♂️ Hapo anatoa shukrani zake za moyoni kwa walezi wake siku ya kuagwa, na kuwapa zawadi alizomudu kama ishara ya shukrani na kumbukumbu. Mume wake mtarajiwa naye ana historia inayotaka kufanana na yake! Hawa wawili ni kielelezo halisi na ushuda hai kwamba kazi ya Mungu haina makosa.

Mimina neema zako Bwana mimina ????

??? mnaona mama zangu na shangazi yangu aliyegoma kuzeeka pale nyuma na tabasamu kama lote wakikumbushia enzi zao?! ?? so sweet!

Wababa nao hawakubaki nyuma! ??

Picha zote shukrani kwa Mc Rhevan , mtembelee Instagram @mc_Rhevan au website yake ???? https://mc.rhevan.com/

Mr and Mrs Sande Wedding

New couple in town ? Kwanza nianze kwa kuwapongeza maharusi Ken and Christine kwa kuachana na maisha ya u-bachelor na kuamua kufunga ndoa takatifu siku ya JumaMosi tarehe 11 mwezi wa 08 mwaka 2018.   Ndoa hii takatifu ilifungwa kwenye Chaple ya Sterling Banquet Hall lililopo Houston, Texas. Ambapo ilifuatiwa na sherehe nzuri sana kwenye ukumbi huo huo. Tunawaombea neema nyingi kwenye ndoa yao, Mungu akawe kiongozi wao siku zote, ndoa yao ikajae amani na furaha nyingi sana. Wakabarikie na uzao wa tumbo lao hata kizazi cha tatu na cha nne. AMEN Kwafaida ya wasomaji wangu, bwana harusi ni rafiki yangu wa miaka mingi tuliishi wote Kalamazoo, Michigan, huwa napenda kuwaita “my Kalamazoo family members” kwani tuliishi kwa amani na upendo. Kwasasa yeye anaishi Dallas, Texas na mimi naishi Houston, Texas.  Bibi harusi yeye alikuwa akiishi Spring, Texas lakini sasa amekuwa mwana Dallas, Texas kwani huko ndiko makazi yake mapya. Gosh! Ain’t they pretty ? Wasimamizi wa kiume na bibi harusi katika pozi. Kutoka kushoto ni Sammy: yeye alikuwa ndio Bestman. Nirafiki wa bwana harusi wa miaka mingi sana toka Kalamazoo, Michigan na sasa wanaishi wote Dallas, Texas.

Anayefuata anaitwa Gittu: Yeye pia ni mmoja wa “Kalamazoo family members”. Nirafiki wa bwana harusi wa miaka mingi toka Kalamazoo na sasa wanaishi wote Dallas, Texas.

Na huyo gentleman wa mwisho anaitwa Charles Nyakure kutoka Dallas, Texas ni rafiki mwema wa bwana harusi. Naye tumemu adopte kuwa mmoja wa “Kalamazoo family members”  ?? Mmenionaa ?? mimi hapa upande wa kushoto, mwanangu upande wa kulia pamoja na Mr and Mrs Sande Dada wa bwana harusi all the way from Nairobi, Kenya akiwa na bestman-Sammy Wazazi! Kutoka kushoto ni baba mzazi wa bibi harusi. Anayefuata ni dada wa bwana harusi. Mwenye nguo ya blue ni mama mzazi wa bibi harusi, na wa mwisho ni baba mzazi wa bwana harusi. Wote wamekuja rasmi kutoka Nairobi, Kenya kwaajili ya kushuhudia tukio hili takatifu.    Picha zote kwa hisani ya Charles ?…… Thank you so much Charles be blessed!

Beautiful twin brothers marry twin sisters!

Story nzuri ya kuvutia ya maharusi mapacha ambao walioa siku moja na mabibi harusi ni mapacha! Wakaka hawa ambao ni mapacha walikutana na wadada warembo wawili ambao nao ni mapacha katika shughuli za kujitolea wakati wa tetemeko la ardhi huko Haiti! ....Mapacha hawa baada ya kupendana kwa muda siku moja wakaamua kuwavika pete ya uchumba warembo wao. Na sasa wamefunga ndoa katika kanisa moja siku hiyo hiyo!.........Matukio kama haya yanayokea sana kwa baadhi ya twins! Kuna wengine niliona hapa Marekani kwenye show ya Dr. Phil wao pamoja na kuolewa siku moja (japo wanaume tofauti) lakini kwa mara mbili wakajikuta wanapata mimba kwa wakati mmoja na uzao wao wa kwanza walikuwa mapacha! Very interesting! 
Weddings are always beautiful moments to remember but for two special couples, the big day was monumental for a number of reasons. According to WOW Amazing, Eric and Shawn Crow had no idea what they were in for when they volunteered at their local church. Apparently, the pleasure of helping others wasn’t the only gratifying thing about the experience. They also crossed paths with two very special women -Teyolla and Keyolla Loux. The Men Of Their Dreams: While volunteering at the church, Teyolla and Keyolla noticed Eric and Shawn first. Although they were instantly taken by the two handsome young men, they initially didn’t believe they had a chance because the guys were older. In fact, Teyolla and Keyolla actually lost contact with the guys for about three years as they spent most of their time volunteering all over the country. But, then fate led them all to Haiti. They all attended a special class to prepare volunteers for work after an earthquake in Haiti. After meeting again, they went on a double date and the sparks began to fly. Tying The Knot: After a whirlwind romance, Shawn popped the big question to Teyolla, but to their surprise, Eric also proposed to Keyolla. Since they all met together and the proposals took place simultaneously, they agreed it would only be befitting that they tied the knot on the same day. Remember…Love has the power to heal or kill… Always proceed with caution! In fact, the two girls – who were adopted by their foster parents Derek and Reneé Loux – even invited their birth mother to partake in the preparations for their big day. The ladies wore identical strapless gowns to marry their best friends. The couples celebrated their big day with a host of family members and friends. Congrats to Shawn and Teyolla and Eric and Keyolla 

Read more at:WhenLoveWasReal 

Hongera sana Mr and Mrs Davis Kateti!

Mr and Mrs Kateti

Hongera sana mdogo wangu Davis Kateti na wifi yangu Ester Kateti kwa kula kiapo KITAKATIFU. Mungu awaongoze katika kila jambo jema mlitendalo! Akapate kuwa ngao na kimbilio lenu wakati wote siku zote katika nyakati zote za raha na tabu! Akabariki uzao wenu hata kizazi cha tatu na cha Nne! Nyumba yenu ikawe hekalu ndogo; amani, upendo, furaha vikadumu ndani yenu! Hongereni sana wapendwa!

Continue reading Hongera sana Mr and Mrs Davis Kateti!

Thank you from Mr and Mrs A. Banduka 

We would like to thank you for all the love and support you have given us over the course of our lives and for being in the midst of this exciting and memorable adventure. We appreciate each of you and recognize your participation. We’re honored that you came to celebrate and witnessed our love and vows to each other. To each and everyone of you, you mean so much to us and we’re beyond thankful to have you in our lives. Finally, to all of those who have given us their time and helping hands with planning this wedding, WE THANK YOU. From the bottom of our hearts we could not have done this without you.

Hongera sana Gideon na Rebecca!

img-20161211-wa0003Hongera sanaaaaaa Gideon na wifi yangu Rebecca. Nawaombea kheri na baraka nyingi sana katika ndoa yenu. Mkapate kubarikiwa mzae matunda mazuri na matamu sana. Congratulations!
img-20161211-wa0002Bwana harusi Mr Gideon ni mfanyakazi wa HoleyPharm Ltd katika department ya Marketing, Advertising, and Sales kwa muda wa miaka kumi (10) sasa. Na siku ya leo masaa ya East Africa-Tanzania alikula kiapo kitakatifu cha ndoa katika kanisa takatifu la Magomeni Seventh Day Adventist pale Mwembe Chai!
img-20161211-wa0001 Maharusi pamoja na wasimamizi wao wakipata picha ya pamoja kabla ya kuelekea Kunduchi beach ambapo sherehe ya harusi hiyo ilifanyika!img-20161211-wa0004Mama Igogo, Deputy Director of HoleyPharm  akiwa teyari kwenda kuserebuka kwa furaha kabisa kwenye harusi ya mfanyakazi wake! img-20161211-wa0002-1Kwa mara nyingine tena, hongera sana kaka Gideon na wifi karibu sana ndani ya familia ya HoleyPharm. Mbarikiwe sana ❤❤