“Inawezekana mno ukiamua” ~~ Zamaradi Mketema

Reposted from @zamaradimketema – Unaweza ukawa na rafiki au jamaa unaemuamini sana au mlietengeneza Bond kubwa lakini ukaja gundua kuna mambo anafanya nyuma yako yasiyofaa dhidi yako/sio mtu mzuri ila UKASHINDWA KUJITOA KWAKE.

kwa kuogopa kumpoteza ukajikuta unajitafutisha hata sababu mwenyewe za kukataa ubaya wake alioufanya, na hata kugoma kuuona (kutafuta excuses/kuwa In Denial) kutokana na ile Bond iliyopo kati yenu.

Zamaradi Mketema, TV / Radio presenter

Na watu wa namna hii mara nyingi unakuta ni mtu ulieshare nae vingi, anakushauri ama ana siri zako nyingi sana hivyo inakutanda hofu ya kumpoteza bila kujali ule ubaya wake ambao unaweza kuwa na athari kubwa mbele.

Kwanza kabisa fahamu hakuna sababu yoyote kati ya hizo juu zinazotakiwa kukufanya ukeep mtu mbaya, kama hofu yako ni SIRI ULIZOMPA mwache ajue azimwage na kuzitangaza, hakuna jipya Chini ya jua, na ni bora kukata kuliko kumpa nafasi ya kujua mengine asiyostahili, na jiulize una uhakika gani kwamba hajamwambia hata mtu mmoja hivi hivi mkiwa mnaongea, hivyo usiendelee kuwa mtumwa wa mtu kwa kuogopa eti atatoa siri zako, mwache atoe tu, sidhani kama litakuwa jambo jipya Duniani.

Kuhusiana na swala la BOND YENU, Ukishaona mtu ni mbaya train yourself not to associate with them katika namna yoyote ile kwa kujifunza kusolve matatizo yako mwenyewe kidogo kidogo, itakuwa ngumu mwanzo lakini utaweza, itafika kipindi utaona kabisa humuhitaji tena, na usiendeshwe sana na hisia unapokumbwa na kitu, maana inaweza kutokea jambo na ukaona kabisa yeye ndio anaeliweza na huenda ni kweli lakini kumbuka ni kwakuwa tu uliamua kuamini hivyo, yes utamkumbuka lakini kumbuka tatizo ni la siku moja linapita, sasa kwanini tatizo la siku moja linalopita likufanye uendelee kumkeep mtu asiefaa milele, maana the more unavyoendelea kumshirikisha ndio the more utakavyoshindwa kujitoa kwake, usijiendekeze.

Na zaidi angalia MADHARA yanayoweza kutokea kutokana na ubaya alionao, kisha kubali kuwa huyo mtu hakufai, na hii inapaswa ianze na wewe, kumbuka HAUPOTEZI kama unaempoteza ana hasara zaidi kuliko faida, hivyo Kata, na jifunze kudeal na vitu mwenyewe, inawezekana mno UKIAMUA. – #regrann

Leave a Reply