Category Archives: Elimu juu ya maisha

Temeke SDA Nursery and Primary School watoa shukrani kwa mama Igogo!

Mama Igogo akitazama kwa furaha picha iliyochorwa kwa taswira yake.

Wanao onekana kwenye video hapo juu ni baadhi ya wafanyakazi wa Temeke SDA Nursery and Primary School walifika nyumbani kwa mama Igogo mchana wa jana tarehe 09/27/2021, masaa ya Africa Mashariki, kwaajili ya kutoa shukrani zao za dhati kwa mchango wake wa hali na mali ambao aliutoa toka kuwaza yakwamba kanisa la Temeke SDA linahitaji kuwa na shule, kuisimamia kuanzishwa kwakwe toka elimu ya awali ya chekechea (Nursery school) mpaka kufikia kuwa na darasa la kwanza mpaka la saba.

Kuhakikisha kuna kuwa na boarding (hostel) kwa wanafunzi wanao kaa mbali haswa wanafunzi wa jinsia ya kike! Mama Igogo alikuwa full time Mkurugenzi mkuu (Director) ambaye hakuwai kulipwa mshahara hata mara moja kwa miaka 7! Alifanya kazi ya kujitolea kwa asilimia 100%! Na baada ya miaka 7 aliomba “kung’atuka” na kuwaachia vijana waikimbize. Yeye alibakia kuwa mshauri kwenye bodi ya shule. Mungu ni mwema shule ilisimama na inaendelea vizuri! Mwanangu ni mmoja wa wanafunzi wa mwanzo kabisa wa shule hii! Alianzia  Nursery hadi darasa la sita. Mungu azidi wabariki wote walimu, wanafunzi, pamoja na watu wote wanaojitoa kwaajili ya huduma hii muhimu sana kwa jamii. ????

Kwenye video ya pili ni Mama Igogo akitoa shukrani zake za dhati baada ya kupokea shukrani na zawadi ya picha kutoka kwa wafanyakazi wa Temeke SDA Nursery and Primary School. 

Na hapa, mama Igogo akitoa ufafanuzi wa zawadi ya picha iliyochorwa kutoka kwenye moja ya picha zake ambazo alipiga akiwa kwenye Makao Makuu ya Wasabato ulimwenguni yaliopo Silver Springs, Maryland/ Washington DC eneo la kumbukumbu za Ellen G. White (mmoja wa waasisi wa dhehebu la Wasabato). Mama yangu hajatembea dunia nzima, Mungu ni mwema amembariki kutembelea nchi kadhaa hapa dunia na ameona mengi; lakini safari ya kutembelea kijiji cha history ya Wasabato huko Battle Creek, Michigan na safari ya kutembelea Makao makuu ya Wasabato ulimwenguni kwakweli ni moja ya safari ambazo zimemgusa sana moyo wake na siku zote huwa anaziongelea kwa hisia sana! Namshukuru Mungu kuwa amenichagua mimi binti yake kuwa kiungo kikuu cha mbaraka huo. Si kwamba asingeweza kufika Marekani hapana! Naamini Mungu kama alimpangia kufika angefika tu bila ya mimi kuwepo kama hizo nchi zingine alizo tembelea bila mimi kuwepo! Lakini kufika sehemu kama hizo kwa urahisi na kwa furaha kupitia mwanae naamini nikitu kinampa faraja kubwa sana moyoni! ?? No mama ain’t done yet! Mungu atupe uhai utakula more good time very soon! ?????

Mzee O.O Igogo, Magreth Otieno Igogo, na mama Igogo

Hapa juu ni moja ya picha waliyopiga wakati walikuwa wamekwenda kutembelea kijiji cha historia ya Wasabato huko Battle Creek, Michigan mwaka 2014 mwezi wa 11. Picha A siku hii zipo nyingi lakini zipo kwenye Flashdisk, sijapata muda wa kuziangalia.

Kama ulipitwa na picha za mama Igogo kutembelea Washington DC basi bonyeza ???? Safari ya mama Washington DC , na Safari ya mama Washington DC

Twamshukuru Mungu kwa yote kwani ni kwa neema yake tu ndio maana haya yote yanatokea. Sifa na utukufu ni zake yeye tu milele na milele. ????

“Inawezekana mno ukiamua” ~~ Zamaradi Mketema

Reposted from @zamaradimketema – Unaweza ukawa na rafiki au jamaa unaemuamini sana au mlietengeneza Bond kubwa lakini ukaja gundua kuna mambo anafanya nyuma yako yasiyofaa dhidi yako/sio mtu mzuri ila UKASHINDWA KUJITOA KWAKE.

kwa kuogopa kumpoteza ukajikuta unajitafutisha hata sababu mwenyewe za kukataa ubaya wake alioufanya, na hata kugoma kuuona (kutafuta excuses/kuwa In Denial) kutokana na ile Bond iliyopo kati yenu.

Zamaradi Mketema, TV / Radio presenter

Na watu wa namna hii mara nyingi unakuta ni mtu ulieshare nae vingi, anakushauri ama ana siri zako nyingi sana hivyo inakutanda hofu ya kumpoteza bila kujali ule ubaya wake ambao unaweza kuwa na athari kubwa mbele.

Kwanza kabisa fahamu hakuna sababu yoyote kati ya hizo juu zinazotakiwa kukufanya ukeep mtu mbaya, kama hofu yako ni SIRI ULIZOMPA mwache ajue azimwage na kuzitangaza, hakuna jipya Chini ya jua, na ni bora kukata kuliko kumpa nafasi ya kujua mengine asiyostahili, na jiulize una uhakika gani kwamba hajamwambia hata mtu mmoja hivi hivi mkiwa mnaongea, hivyo usiendelee kuwa mtumwa wa mtu kwa kuogopa eti atatoa siri zako, mwache atoe tu, sidhani kama litakuwa jambo jipya Duniani.

Kuhusiana na swala la BOND YENU, Ukishaona mtu ni mbaya train yourself not to associate with them katika namna yoyote ile kwa kujifunza kusolve matatizo yako mwenyewe kidogo kidogo, itakuwa ngumu mwanzo lakini utaweza, itafika kipindi utaona kabisa humuhitaji tena, na usiendeshwe sana na hisia unapokumbwa na kitu, maana inaweza kutokea jambo na ukaona kabisa yeye ndio anaeliweza na huenda ni kweli lakini kumbuka ni kwakuwa tu uliamua kuamini hivyo, yes utamkumbuka lakini kumbuka tatizo ni la siku moja linapita, sasa kwanini tatizo la siku moja linalopita likufanye uendelee kumkeep mtu asiefaa milele, maana the more unavyoendelea kumshirikisha ndio the more utakavyoshindwa kujitoa kwake, usijiendekeze.

Na zaidi angalia MADHARA yanayoweza kutokea kutokana na ubaya alionao, kisha kubali kuwa huyo mtu hakufai, na hii inapaswa ianze na wewe, kumbuka HAUPOTEZI kama unaempoteza ana hasara zaidi kuliko faida, hivyo Kata, na jifunze kudeal na vitu mwenyewe, inawezekana mno UKIAMUA. – #regrann

Unapokutana na mtu mwenye mafanikio usimuombe pesa. Muulize amefanyaje kufikia hapo alipo!

“When you meet a person with means, a person that is well-off you think is successful  that you always wanted to be; don’t go there asking  for money” Hayo ni maneno yake Comedian na TV host Steve Harvey kwenye Oprah Master Class. Master Class ni show ambayo watu wengi waliofanikiwa katika nyanja mbali mbali za maisha wanaelezea mafanikio yao kwa undani zaidi toka walivyokuwa wadogo mpaka walipo fikia. Changamoto zipi walipata, vipi waliweza kuvumilia, kumudu hizo changamoto, na hata kufanikiwa bila ya kukata tamaa. Unapopata nafasi ya kukutana na mtu au watu ambao unawaangalia kama  “role mode / icon”  katika maisha yako usiwaombe pesa waombe wakuelimishe nini walifanya kufikia hapo walipo. Watu wengi wapo wepesi wa kuomba pesa kwa mtu aliyejaliwa kuwa nazo kwa ajili ya kujikimu na hiyo shida aliyonayo. Nautakuta muda mwingi shida hiyo haiishi ni kaituliza tu kwa muda. Hii yote nikwasababu wengi tunapungukiwa hekima ya kujua kuwa ni kheri mtu akupe elimu ya maisha ya nini alikifanya mpaka kufika hapo ili uone kama na wewe unaweza tumia njia hiyo kufikia malengo yako au kujikwamua kutoka sehemu moja kwenda nyingine. Au utakuta wengine tumepingukiwa hekima ya kuona mafanikio ya watu ni maovu mbele zetu nakuanza kutafuta njia ya kumuangusha bila kujua kuwa anguko lake ni maafa kwako pia. …….Hivyo tuwe waelevu kama nyoka na wenye hekima kama Solomon ili tuweze kujifunza kutoka kwa wengine haswa ambao tunaona wana tija katika maisha yetu. Pale watu wanapokukatisha tamaa wewe piga moyo konde usiwasikilize. Kwanza mimi kwa experience yangu binasfi watu wengi wenyekukatisha watu tamaa ni watu ambao hawajiamini na pia hawapendi kuonekana kuwa wao wameshindwa katika kufikia kile wakitakacho hivyo hamna la zaidi zaidi ya kupiga makelele ili uwe muoga. Wakati ukweli wanatamani wangekuwa na ujasiri kama wako. Utaona wanakuja na maneno mengi ya kejeli ikishindikana wataingilia personal attack “hajaolewa”, “mnene”, “hana nywele”, “mbeba mabox” yani ukishaona mtu anaenda kwa personal attacks jua maumivu yamemuhelemea ?? . . Nasiku hizi social media, basi watatafuta kila event au tukio lenye viongozi waende kupiga picha ili warushe kwa Facebook / Instagram basi tu ufikirie kuwa there really happy and making it, wakati rohoni wanatamani wawe na kipaji au nafasi kama yako. ?? Wanasaikolojia wanasema mara nyingi watu wanao ongelea wengine vibaya muda wote huwa kuna mambo ambayo hayopo sawa kwa upande wao sasa kwasababu hawataki watu wajue huo upande wao hauwapendezi, basi dawa inakuwa ni kugeuza attention kwa wengine! Na huo ndio ukweli! Wewe usikate tamaa na mapicha yao! Nawala usiache mashauzi yao yasio na kichwa wala miguu yakuumize au yakutoe kwenye malengo yako. Mimi nilivyoanza hii blog yangu nimetungiwa uzushi wa kila namna; ooh huyo muhuni anatafuta mwanaume, huyo FBI, huyo kada wa CCM (utafikiri walishaniona na kadi ya CCM au nimevaa gwanda la CCM ??), mara anatafuta umaaharufu, mara mkabila, mdini, yani maneno mengi mno wengine wakadiri hata kwenda kwetu kuchunguza maisha ya kwetu nakuja kuongea kwenye magroup yao. Mara kazi yake kudhalilisha watu. Eti huyo anagombania mali za wazazi wake ?? Wengine wakazunguka kuwaambia watu wasiweke picha zao kwa hii blog. Yani hayo yote walifikiri nitaacha kublog!! Lakini nipo hapa and I’m here to stay! Mimi najua ninachofanya na ninako kwenda hivyo sijali. Waliokua wanasema mimi kazi yangu ni ku copy and paste ndio hao hao wanakosa raha kwani wanatamani niwaweke humu kwa blog yangu nami hata habari nao sina ??  Ni maumuvi makali sana wanapata. Wewe songa tu, wakikwambia huwezi wambie wewe ni nani hata useme hivyo! Kitu kingine usiamini kila rafiki. Yani ukiona mtu ambaye ni rafiki yako anachukia maendeleo au mafanikio ya mwingine achana na huyo rafiki mara moja. Kwani inamaana wewe ni rafiki yake Kwasababu haujamzidi kimaendeleo lakini siku ukitaka kunyanyuka atakuwa wakwanza kukuangamiza! Niamini nimeyaona! Siku zote kuna mtu mmoja ambaye atakuelewa na ambaye atakuwa yupo teyari kukusaidia kufikia malengo yako. Mungu huwa hamtupi mja wake! Kama nipesa basi huyo mtu anaweza kusaidia, kama ni mawazo yanini ufanye ili ufanikiwe basi huyo mtu atakuwa yupo tayari kutoa ushauri. It means that person believes in you and truly cares about you! When it looks like nobody cares trust me someone is out there who really cares about you! Muda ukifika Mungu atamleta kwako. Usikate tamaa!

**Imeandikwa na Alpha Igogo** **#TBT #Sept.2017**