Happy birthday Mercy!

Leo ni siku kazaliwa mrembo wangu! Alizaliwa siku ya JumaMosi kuu (siku moja kabla ya Pasaka). Saa tisa mchana katika hospital ya Tanzania Matertenity Service (Siku hizi inaitwa Tanzania Matertenity Hospital), chini ya uangalizi wa marehemu Dr Amood na Dr Kapesa.

Mercy!

Kalinitesa na uchungu haka, sitokaa nisahau! ?? Niliwekewa chupa mbili za maji ya uchungu ndipo kakatoka! ?? Alikuwa kanona ndani ya tumbo la mama yake na mama mwenye alikuwa na mwili mdogo. Nilikuwa napenda kula chips na kachumbari kupita maelezo! Yani ndio kilikuwa chakula changu kikuu kila usiku! Maharage yalikuwa hayapitiii, yani nikijilazimisha kula natapika bila kujijua! ?? Halafu utamsikia mama Igogo akisema “vipi? Mjukuu kakataa maharage?” ???

Namshukuru Mungu kwa zawadi ya hichi kiumbe! Nilizaa mtoto mwenye afya njema nikampa jina Mercy. Jina hili nilikuwa inspired na rafiki yangu ambaye tulisoma naye Kowak Girls Secondary school, yeye anaitwa Mercy Msofe, kwasasa anaishi Arusha. Pia anajina lingine ambalo alipewa na babu yake (baba yangu mzazi), alimpa jina la Theresia a.k.a Teddy. Nijina la marehemu shangazi yangu. Baba yangu kwao (tumbo la mama yake) walizaliwa wavulana watatu na msichana mmoja. Kwakua Mercy ndio mjukuu wa kwanza kwa wazazi wangu akaamua kumuenzi marehemu dada yake ambaye alifariki mwaka mmoja kabla ya Mercy kuzaliwa. Basi Mercy na Teddy yote ni majina yake. Na lakilugha ni Obworo! Ni nickname ya marehemu shangazi yangu, Theresia Obworo!

Mimi namuombea maisha mazuri sana yaliyojaa baraka nyingi na utukufu wa Bwana Mungu. Mwenyezi Mungu amuhepushe na pepo zote. Akalitukuze jina la Muumba wake siku zote za maisha yake. Naomba kwa imani katika jina la Yesu, Amen!

Happy birthday beautiful girl, nakupenda sana nawe wajua hivyo! ?❤

Zifuatazo ni baadhi ya salamu za kheri kutoka kwa :-

Kutoka kwa babu!

“Me & U, are 41 years older and younger than one another, that is what inspired me to wait until all has exhausted their best wishes to you on this very special day, when you have seen the 27th anniversry. As I strive to reach my 95th anniversary to come, my wishes are that you shall celebrate 68th anniversay while healthier with sound knowledge, richer in heart, wealthier in charity, and sorrounded with numerous loving family members as it is with me today, on this wonderfull good friday which filled with happiness of sharing my love with you. UWE NA SIKU MURUA SANA, AHEROI MOKALO NYAKWARA MOKUONGO. ☝️? With all my Love?From ? Babu.”

Aunt Janeth!
Kutoka kwa aunt Mage
Kutoka kwa cousin-sister Sarah

Happy birthday Mercy!

Leave a Reply