HUYU ANA MOYO MKUU…..by Peter Sarungi

Na Peter Sarungi (Next Speaker)Kwa sasa ni nadra sana kupata binadamu walio umbwa na Moyo Mkuu, moyo unao weza kuhimili shida, kejeli, dharau, matusi ma vikwazo mbalimbali vyenye lengo la kulainisha Moyo. Mh. Lowasa Edward alikumbwa na kashfa akiwa CCM tena Waziri Mkuu, akasemwa na kutukanwa na viongozi, wanachama na wapenzi wa chama kikuu cha upinzani Chadema Tanzania, huku akiitwa Fisadi nchi nzima… Alikaa kimya bila kujibu.

Alipo hama CCM kwenda CDM, CCM walimuona kama msaliti ingawa kwa CDM alibadilika na kuwa Malaika. Bado aliendelea kutukanwa, kudharauliwa na hata kuombewa mabaya na viongozi, wanachama na wapenzi wa chama tawala kipindi cha uchaguzi 2015… Alikaa kimya bila kujibu.

Pamoja na yote hayo, bado ameendelea kuwa na Moyo Mkuu kwa nchi yake. Huyu namfananisha na Mh. Raila Odinga wa Kenya na Mh. Kiiza Besige wa Uganda kutokana vikwazo wanavyopitia. Mungu awatimizie haja ya mioyo yao.

Tujifunze kitu hapo, unajifunza nini?

Leave a Reply