Kulipwa kwa kazi ya campaign ya chama ni halali yako!- Alpha Igogo

Alpha Igogo
Blogger

Katika kila jambo au shughuli yoyote lazima kuna fedha zitatumika tu! Hii haijalishi ni shughuli ya chama, kanisa, msikiti, kijamii, au za kipagani lazima fedha zitahusika! Lakini sasa uingizaji na utoaji wa hizo fedha zinaweza kuwa katika mfumo uliyo rasmi (yani kuna kuwa na budget, mfumo wa malipo, na washuhudiaji) au siyo rasmi (yani hakuna accountability ya aina yoyote ile).

Tukirudi katika mada yetu kama kichwa cha habari kisemavyo, kuwa, “kulipwa kwa kazi ya campaign ya chama ni halali yako” basi ngoja tuzungumzie hilo kwa sasa. Kampeni za siasa huwa lazima chama kinajipanga kwa mikakati (strategies) ya jinsi ya kufanya campaign yenye mafanikio. Na moja ya mikakati hiyo ni jinsi ya kukusanya pesa rasmi kwaajili ya kukamilisha mikakati hiyo! Hapo ndipo utasikia kitu ‘budget ya campaign’. Pia kwa serikali ya Tanzania huwa wanakitu kinaitwa posho / ruzuku ya chama wakati wa campaign!

Hiyo budget ya campaign haitumiki tu kununulia vitendea kazi vya campaign bali pia kuwalipa wanachama / makada watakao kuwa teyari kufanya campaign hiyo kulingana na malengo ya chama chao. Ndio maana wakati wa campaign huwa wana aajiriwa watu maalum wa kufanya campaign au kikosi maalum cha nguvu kazi kwa ajili ya campaign husika kwa mfano anaweza ajiriwa Campaign Manager, au Financial Controler kwa ajili hiyo tu!

Sasa wewe kama ni mwanachama uwe mtu wa kawaida au “celebrity” kupewa fedha kwa ajili ya campaign ni kitu cha kawaida, ni swala ambalo linatambulika kisheria, na zaidi ya yote ni halali yako!

Wewe unapo acha shughuli zako za uzalishaji wa kila siku nakwenda kufanyia chama campaign nilazima chama kikupe hela za kujikimu maana utahitaji hela ya kukutoa point A to Z, utahitaji kula, utahitaji kulala kama ni nje ya mahala unapo ishi! Huwezi kuchukua pesa zako binafsi kufanyia chama campaign wakati kwanza umeacha shughuli zako za uzalishaji, pili kama una familia inamaana budget ya familia utaivuruga kwa mambo ya campaign.

Jamani, hata makanisani kuna budget ya kutembelea washiriki ambao ni wagonjwa, wajane n.k nawatu huwa wanapewa pesa za kujikimu na safari kama hizo. Hivyo si ajabu mtu kulipwa kwa shughuli ya campaign kwani hizo ndizo zile hela wenyeviti na viongozi wengine wa chama wanatumia kwa matumizi yao binafsi haswa kama hakuna mwanachama au wanachama ambao wanaweza ku-question uongozi! Kiwango / kiasi cha ulipwaji waweza tofautiana kutokana na nguvu aliyo nayo mtu huyo pamoja na makubaliano yao. Fedha zote zinazo ingia kwenye budget ya campaign ya chama lazima ziwe kwenye mfumo rasmi unao eleweka! 

Labda kama baba yako ni Mzee wa “Vijisenti” (you don’t need that kind of “petty” money)  kama sivyo kulipwa kwa kazi ya campaign ya chama ni halali yako!

Mungu ibariki Africa. Mungu ibariki Tanzania.

 

 

Leave a Reply