Mtangazaji Maduhu aupa mkono wa kwaheri ‘ukapela’!

Beyonce sang it well “if he liked it he should have put a ring on it”! Basi ndivyo Mtangazaji maharufu toka Morning Star Radio ajulikanaye kwa jina la Maduhu alivyo fanya, he put ring and sealed it before God on Sunday April 7th, 2019.

Ndoa hii TAKATIFU ilifungwa katika kanisa la Wasabato la Nations Of Praise liliopo ndani ya jimbo la Houston, Texas inchini Marekani siku ya Jumapili majira ya saa kumi jioni saa za Marekani.
Mnaona neno “Takatifu” hapo juu ☝️ nimeweka kwa herufi kubwa na wino mwingi eh?! Nikuwakumbusha walevi na “mashakunaku” kuwa “alicho kiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe”!! Wale walevi wasiyo na haya huyu ni mke wa mtu muogopeni! Na wale mashakunaku wenye macho juu juu kama tunguli za mchawi nawakumbusha huyu ni mume wa Sule peke yake hachangii na mtu wala hamkodishi tafuteni wenu! ?? kama nawaona mnavyo nisonya ???

Ndoa ilifungwa inchini Marekani kwasababu Bibi harusi yeye ni Mmarekani mwenye asili ya Kitanzania. Ambapo kule Tanzania anatokea maeneo ya Upareni.
Bwana na bibi harusi kwa furaha wenye nyuso za tabasamu baada ya kula kiapo kitakatifu!
Wapambe walikuwepo! Walipendeza sana.
Kwamara nyingine naomba niwapongeze sana Mr and Mrs Maduhu kwa kufunga ndoa takatifu! Wamesema wanaotaka ndoa za “mkeka” nyie fanyeni tu lakini sisi tunakwenda kula kiapo kitakatifu mbele za Mungu wetu aliye umba Mbingu na dunia! Mbarikiwe sana na nawatakieni furaha na amani isiyo na kikomo ??

**Shukrani zangu za dhati ziwaendee wadau wote waliotuma hizi picha kwenye lile group la “Harusi tunayo”. Mbarikiwe sana ??**

Leave a Reply