Pastor Caleb Migombo: PUMZIKA KIDOGO / GET SOME REST

                   PUMZIKA KIDOGO

Kwanini Yesu, katikati ya siku yenye shughuli nyingi, aliwataka wanafunzi wake kuuacha umati wa watu na kwenda naye mahali pa faraga kupumzika? Alifahamu kuwa kadri walivyokuwa na kazi nyingi za kufanya ndiyo walivyohitaji kuweka muda wa kupumzika na kuwa pamoja na mwokozi wao. Kutofanya hivyo mwisho wake kungewaumizi wao wenyewe na wale wote waliokusudia kuwahudumia.

Sisi nasi leo, ni muhimu kuzingatia ukweli huu.

Mungu anajua shughuli zako na changamoto za Maisha yako ya kila siku – Iwe ni nyumbani, kazini, au Kanisani. Mungu anajua pia kuwa unahitaji hekima yake ili uweze kuwa na mtizamo sahihi wa kila shughuli na namna inavyopaswa kufanywa- na unahitaji pia nguvu kutoka kwake ili uweze kufanya kila jambo kwa usahihi. Kama hutapanga kuwa na muda wako wa kupumzika na kupata nguvu mpya (kimwili na kiroho)- upo uwezekano mbeleni wa wewe na wote uwapendao kuumia. Uchovu unaathiri kufikiri kwetu, namna tunavyowasiliana, na uwezo wetu wa kupenda wanaotunzunguka.

Yesu akawaambia, “Twendeni peke yetu mpaka mahali pa faragha mkapumzike kidogo.” Alisema hivyo kwa kuwa kulikuwa na watu wengi mno waliokuwa wanafika hapo na kuondoka hata Yesu na wanafunzi wake hawakuweza kupata nafasi ya kula chakula" Marko 6:31


                  GET SOME REST

Why, in the midst of such a busy day, did Jesus insist His disciples leave the crowds to rest and be alone with Him? He knew that the busier they were, the more they need to make time to rest and be alone with Him. If they didn’t, eventually they would hurt both themselves and those who they were seeking to help. The same is true for us

God knows the demands and responsibilities you face-at home, on the job, even in your church. But God also knows you need His wisdom to keep those things in perspective, and you need His strength to get them done rightly.

Then, because so many people were coming and going that they did not even have a chance to eat, he said to them, “Come with me by yourselves to a quiet place and get some rest.” Mark 6:31

Leave a Reply