Category Archives: Spirituality

Kesha la asubuhi: Karama ya uponyaji

                  *Kesha la asubuhi*

                         *Juma Tatu* 

                           *9/7/2018*

                  *Karama ya Uponyaji* ?Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa. Yakobo 5:14, 15./em>

?Uwezo wa Kristo wa kukomesha maradhi umedhihirishwa katika siku zilizopita kwa namna ya ajabu. Kabla ya wakati ambapo tulibarikiwa kwa taasisi ambamo ndani yake wagonjwa wanaweza kupata msaada kutoka katika maradhi, kwa matibabu ya uangalifu na maombi ya dhati ya imani kwa Mungu, tulishughulika kwa mafanikio na wagonjwa ambao walionekana kutokuwa na matumaini ya kupona. Leo Bwana anawaalika wanaoteseka kuwa na imani kwake. Hitaji la mwanadamu ni fursa kwa Mungu.

?Akatoka huko, akafika mpaka nchi ya kwao; wanafunzi wake wakamfuata. Na ilipokuwa sabato, alianza kufundisha katika sinagogi; wengi waliposikia wakashangaa, wakisema, Huyu ameyapata wapi haya? Na, Ni hekima gani hii aliyopewa huyu? Na, Ni nini miujiza hii mikubwa inayotendeka kwa mikono yake? Huyu si yule seremala, mwana wa Mariamu, na ndugu yao Yakobo, na Yose, na Yuda, na Simoni? Na maumbu yake hawapo hapa petu? Wakajikwaa kwake. Yesu akawaambia, Nabii hakosi heshima, isipokuwa katika nchi yake mwenyewe, na kwa jamaa zake, na nyumbani mwake. Wala hakuweza kufanya mwujiza wo wote huko, isipokuwa aliweka mikono yake juu ya wagonjwa wachache, akawaponya. Akastaajabu kwa sababu ya kutokuamini kwao. Akazunguka-zunguka katika vile vijiji, akifundisha.” (Marko 6:1-6).

?Pamoja na matibabu yetu yote yanayotolewa kwa mgonjwa, maombi sahili ya dhati yanapaswa kutolewa kwa ajili ya baraka ya uponyaji. Tunapaswa kumwelekeza mgonjwa kwa Mwokozi mwenye huruma, na uwezo wake wa kusamehe na kuponya. Kupitia katika majaliwa yake ya neema wanaweza kurejeshwa. Waelekeze wanaoumia kwa Mtetezi wao aliye katika nyua za mbinguni. Waambie kwamba Kristo ataponya wagonjwa, iwapo watatubu na kuacha kuzihalifu sheria za Mungu. Yupo Mwokozi ambaye atajidhihirisha mwenyewe katika vituo vyetu vya tiba ili kuwaokoa wale ambao watajisalimisha kwake. Wale wanye maumivu wanaweza kuungana nanyi katika maombi, huku wakikiri dhambi zao, na kupokea msamaha.-Manuscript Releases, vol. 8, uk. 267, 268.

Kamwe usibishane na pepo!

Wapendwa wasomaji wangu, za siku mbili tatu ? Haya leo ngoja niongee kidogo kuhusu pepo au mapepo. Unajua humu kwenye mitandao au hata kwenye maisha yetu tumezungukwa na mapepo wachafu. Hao au hili pepo anaweza akawa ndugu, rafiki, mfanyakazi wako, au mtu baki kabisa ambaye hana undugu wala ujamaa na wewe. 

Utakuta hili pepo kazi yake ni kuchukizwa na wengine wakiwa na furaha. Yani akiona watu wengine wana amani hata kama ni masikini kuliko yeye basi yeye roho yake inatahabika sana! Kinachofuata nikutafuta kila njia ya kufanya ile amani au furaha uliyonayo itoweke! Kama ni familia inafuraha basi atatafuta kila njia ya kuondoa furaha kwenye hiyo familia. Atagombanisha watu hata kwa kutumia watu wengine ili yeye asijulikane! Hapendi kuona watu wanaishi kwa amani na furaha kugombanisha watu ndio furaha yake yeye!

Sasa hata humu kwenye mitandao yapo haya mapepo! Kwa sisi Wakristo, Bible inatuambia "utawajua kwa matendo yao"! Yani ukiona mtu kutwa yeye nikugombanisha watu kwenye hii mitandao, kutwa kutukana watu kwakutumia sababu yoyote ile, amekalia kuvuruga familia za watu kwasababu wanafuraha? Yani muongo na umbea ndio maisha yake; mpendwa, basi jua huyo ni PEPO! Kamwe! Nasema tena Kamwe! usijibishane na Pepo! Pepo unalikemea kwa Jina la Yesu! Ukijibishana na pepo atakuambukiza mapepo yake! Hivyo njia nzuri ya kulishinda pepo ni kulikemea likafie mbali huko, hakuna jina ambalo pepo linaogopa kama jina la Mungu. Wewe kemea usimpe nafasi ya kukusogelea!

Huwa napendaga sana huu wimbo wa Rose Muhando "Nipishe nipite" haswa kwenye chorus. Huu wimbo unamkemea pepo au kwa jina lingine shetani. Huu ni mfano mzuri kabisa, kuwa pepo unalipa 'amri' nasio kuongea nalo! 

"Wewe ulimwasi Mungu, nipishe nipite 

Uliwadanganya Adamu na Eva, songea nipite 

Dunia nzima imeharibika, kwa ujanja wako 

 wewe shetani mlaaniwa, mwenyeji wa kuzimu 

Sasa nipishe nipite "Wapendwa tukemee mapepo yanayotuzunguka na kutufata fata kwa nguvu usicheke wala kulemba lemba maneno kwa pepo! Mpe amri, mwambie wewe  ulimwasi Mungu songea nipite, wewe shetani mlaaniwa mwenyeji wa kuzimu nasema sasa sogea nipite katika jina la Yesu! 

*** Kama humjui huyo kwenye picha ni mdogo wangu kipenzi Jokate Mwegelo. Missing you, love you dearly****



Kesha la asubuhi: Hata watoto wanaweza kushuhudia imani yao

                  *KESHA LA ASUBUHI*

                           JUMATANO

                           13/06/2018

          _HATA WATOTO WANAWEZA

            KUSHUHUDIA *IMANI* YAO._? *“Lakini wakuu wa makuhani na waandishi walipoyaona maajabu aliyoyafanya, na watoto waliopaza sauti zao hekaluni, wakisema, Hosana, Mwana wa Daudi! Walikasirika, wakamwambia, Wasikia hawa wasemavyo? Yesu akawaambia, Naam; hamkupata kusoma, Kwa vinywa vya watoto wachanga na wanyonyao umekamilisha sifa?” (Mathayo 21:15, 16).*

✍?Bendera ya neno la kweli inaweza kuinuliwa na wanaume na wanawake wanyenyekevu; na vijana, na hata watoto, wanaweza kuwa baraka kwa wengine, kwa kudhihirisha kile ambacho kweli hiyo imewafanyia.

✍? Mungu atawatumia mawakala dhaifu zaidi ikiwa wamejisalimisha kikamilifu Kwake. Anaweza kutenda kazi kupitia wao ili kuzifikia roho ambazo mchungaji asingeweza kuzifikia. Kuna njia kuu na vichochoro vinavyopaswa kuchunguzwa. Mkiwa na Biblia yenu mkononi mwenu, moyo wenu ukichangamka na kung’aa kwa upendo wa Mungu, mnaweza kuondoka kwenda kuwaambia wengine uzoefu wenu;

✍? mnaweza kuwajulisha kweli ambayo imeugusa moyo wenu, mkiomba kwa imani kwamba afanye jitihada zenu ziwe na mafanikio katika wokovu wao. Wasilisha nuru, nanyi mtapata nuru zaidi ili kuwasilisha. Kwa namna hiyo mnaweza kuwa watendakazi pamoja na Mungu.

✍?Mungu anatamani kwamba watoto Wake watumie juhudi zao zote, kwamba katika kutenda kazi ili kuwabariki wengine, waweze kuimarika katika nguvu ya Yesu. Mnaweza msiwe na elimu; mnaweza msifikiriwe kuwa na uwezo wa kumfanyia Mungu kazi kubwa; lakini yapo mambo mnayoweza kufanya. Mnaweza kuifanya nuru yenu iwaangazie wengine.

??‍♂```Kila mmoja anaweza kupata ufahamu wa neno la kweli, na kuwa na mvuto mwema. Hivyo nendeni mkafanye kazi, ndugu na dada zangu. Jipatieni uzoefu kwa kufanya kazi kwa ajili ya wengine. 

??‍♂Mnaweza kufanya makosa; lakini hili haliwezi kuzidi kile ambacho wale wenye maarifa zaidi, na wale walioko katika nyadhaifa za mamlaka, wamefanya tena na tena. Hamtapata mafanikio wakati wote; lakini hamwezi kamwe kujua matokeo ya juhudi duni, isiyotafuta manufaa binafsi ili kuwasaidia wale waliomo gizani. 

??‍♂Kupitia utendaji wa Roho Mtakatifu, mnaweza kuongoa roho kutoka gizani kuja kwenye kweli, na kwa kufanya hivyo roho zenu wenyewe zitajawa upendo wa Mungu.```

*MUNGU AWE NANYI MNAPOTAFAKARI*

Kesha la asubuhi: WATENDAKAZI PAMOJA NA MUNGU

                 KESHA LA ASUBUHI
              ALHAMISI- JUNE 07, 2018
  WATENDAKAZI PAMOJA NA MUNGU
“Maana sisi tu wafanyakazi pamoja na Mungu; ninyi ni shamba la Mungu, ni jengo la Mungu.” (1 Wakorintho 3:9).

▶Lazima Roho Mtakatifu awe wakala hai wa kusadikisha juu ya dhambi. Wakala huyu wa kiungu humwasilishia mzungumzaji manufaa ya kafara iliyotolewa msalabani; na kadiri neno hili la kweli linapofikishwa kwa roho zilizopo, Kristo hujitwalia, na hutenda kazi ili kubadilisha tabia yao. Yuko tayari kusaidia udhaifu wetu, kutufundisha, kutuongoza, na kutuhamasisha kwa mawazo yenye asili ya mbinguni.

▶Ni kidogo jinsi gani wawezavyo kufanya wanadamu katika kazi ya kuokoa roho, na hata hivyo ni kubwa kiasi gani wanaweza kufanya kupitia Kristo, endapo wakijazwa Roho Wake! Mwalimu mwanadamu hawezi kusoma mioyo ya wasikilizaji wake; lakini Yesu hukirimu neema ambayo kila roho huhitaji. Yeye hufahamu vipaji vya mwanadamu, udhaifu na uimara wake. 

▶Bwana anatenda kazi ndani ya moyo wa mwanadamu; na mchungaji anaweza kuwa harufu ya mauti iletayo mauti kwa roho zinazoyasikiliza maneno yake, akiwageuzia mbali na Kristo; au, kama amejiweka wakfu, mcha-Mungu, asiyejitumainia nafsi, bali humwangalia Yesu, anaweza kuwa harufu ya uzima iletayo uzima kwa roho ambazo tayari ziko chini ya nguvu ya usadikisho wa Roho Mtakatifu, na ambao katika mioyo yao Bwana anaandaa njia kwa ajili ya ujumbe ambao amempatia wakala wa kibinadamu. Kwa namna hiyo moyo wa asiyeamini huguswa, naye huitikia na kuupokea ujumbe wa neno la kweli.

▶“Sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu.” Miguso ya usadikisho iliyopandikizwa moyoni, na kuelimishwa kwa ufahamu kupitia upokeaji wa Neno, hutenda kazi katika upatanifu kamili. Kweli iliyoletwa akilini ina uwezo wa kuamsha nguvu za roho zilizokufa. Roho wa Mungu atendaye kazi moyoni hushirikiana na utendaji wa Mungu kupitia mawakala Wake wa kibinadamu. 

▶Tena na tena nimeoneshwa kwamba watu wa Mungu katika siku hizi za mwisho wasingeweza kuwa salama kwa kuwatumainia wanadamu, na kuufanya mwili kuwa tegemeo lao. Shoka imara la neno la kweli limewachimbua kutoka ulimwenguni wakiwa kama mawe yakwaruzayo yanayopaswa kuchongwa na kunyooshwa na kulainishwa kwa ajili ya jengo la mbunguni. Wanapaswa kuchongwa na manabii kwa makaripio, maonyo, nasaha, na ushauri, ili waumbwe wafanane na Kielelezo cha kiungu; hii ndiyo kazi maalumu ya Mfariji—kubadilisha moyo na tabia, ili wanadamu waifuate njia ya Bwana.

Kesha la asubuhi: KUSHIRIKIANA NA NGUVU YA MUNGU

                  KESHA LA ASUBUHI 

                          JUMATANO

                         06 June 2018

                _*KUSHIRIKIANA NA 
                 NGUVU YA MUNGU.*_? *“Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.” (Matendo 1:8).*

✍?Mungu amekusudia kutoacha chochote kisifanyike ili kumrejesha mwanadamu kutoka kwenye taabu za adui. Baada ya kupaa kwa Kristo, Roho Mtakatifu alikabidhiwa kwa mwanadamu ili awasaidie wote ambao wangependa kushirikiana Naye katika kuiumba upya na kuijenga upya tabia yake. Sehemu ya Roho Mtakatifu katika kazi hii imefasiliwa na Mwokozi wetu. Anasema, “Atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu” (Yohana 16:8). Roho Mtakatifu ni msadikishaji, na pia ni mtakasaji.

✍?Kwa vile hakuna anayeweza kutubu dhambi zake hadi pale anapokuwa amesadikishwa, ulazima wa kuungana na Roho katika kazi yetu ili kuwafikia walioanguka ni dhahiri. Vipaji vyetu vyote vya kibinadamu vitatumiwa bure isipokuwa kama tumeungana na mawakala wa mbinguni.

✍? Ni kupitia ukosefu wa maarifa ya kweli zihuishazo, na nguvu potofu ya uovu, ndiyo maana watu wamedhoofika kiasi hicho, wamezama katika vina vya1

auharibifu wa dhambi. Malaika na wanadamu hawana budi kutenda kazi kwa upatanifu ili kuifundisha kweli ya Mungu kwa wale wasioijua, ili wawekwe huru dhidi ya vifungo vya dhambi. Ni kweli pekee ndiyo iwawekayo wanadamu huru. Uhuru huu upatikanao kupitia maarifa ya neno la kweli, unapaswa kutangazwa kwa kila kiumbe.

??‍♂```Yesu Kristo, Mungu Mwenyewe, na malaika wa mbinguni wanavutiwa na kazi hii kuu na takatifu. Mwanadamu amepewa heshima iliyotukuka ya kudhihirisha tabia ya kiungu kwa kujihusisha pasipo ubinafsi katika jitihada za kumwokoa mdhambi kutoka kwenye shimo la uharibifu ambamo ametumbukia.

??‍♂ Kila mtu atakayejisalimisha ili aelimishwe na Roho Mtakatifu atatumiwa kwa ajili ya ufanikishaji wa kusudi hili lililoasisiwa na mbingu. Kristo ndiye kiongozi wa kanisa Lake, na itamtukuza zaidi pale ambapo kila kipengele cha kanisa hilo kitajihusisha katika kazi ya wokovu wa roho. Lakini watendakazi wa kibinadamu wanahitaji kuacha nafasi zaidi kwa ajili ya Roho Mtakatifu kufanya kazi, ili watumishi wafungamanishwe pamoja; na kusonga mbele katika nguvu ya kundi moja la askari. Hebu wote wakumbuke kwamba sisi tu “tumekuwa tamasha kwa dunia; kwa malaika na wanadamu.” (1 Wakorintho 4:9).```

*MUNGU AWE NANYI MNAPOJIKABIDHI KWAKE*

Kesha la asubuhi: CHUMVI YA DUNIA

                  KESHA LA ASUBUHI

                  Juma Pili 3/6/2018
  
             **CHUMVI YA DUNIA**“Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu” Mathayo 5:13

Mungu atatenda kazi pamoja na kanisa, lakini si bila ushirikiano wao. Hebu kila mmoja wenu aliyeonja Neno zuri la Mungu “nuru yenu na iangaze mbele ya watu, wapate kuyaona matendo yenu mema, wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni” (Mathayo 5:16). Yesu anasema, “Ninyi ni chumvi ya dunia; lakini chumvi ikiwa imeharibika itatiwa nini hata ikolee? Haifai tena kabisa, ila kutupwa nje na kukanyagwa na watu.” Chumvi inayookoa, yaani mvuto wa Mkristo, ni upendo wa Yesu moyoni, ni haki ya Kristo inayotawala rohoni. Ikiwa yule anayedai kuwa mtu wa dini atatunza ufanisi wa imani yake unaookoa, imempasa kuiweka haki ya Kristo mbele yake daima, na kuwa na utukufu wa Bwana kama thawabu. Ndipo uweza wa Kristo utakapofunuliwa katika maisha na tabia.

Oh, tutakapofika kwenye malango ya dhahabu, na kuingia katika mji wa Mungu, je, kuna yeyote atakayeingia pale ambaye atajutia kwamba aliyatoa maisha yake kikamilifu kwa Kristo? Hebu sasa tumpende kwa upendo ulio kamili, na kushirikiana na viumbe wa mbinguni, ili tupate kuwa watendakazi pamoja na Mungu, na kwa kufanywa washirika wa tabia ya Uungu, tuweze kumdhihirisha Kristo kwa wengine. oh, laiti tungepokea ubatizo wa Roho Mtakatifu! Laiti miale miangavu ya Jua la Haki ingeangaza katika vyumba vya mioyo yetu na akili zetu, ili kwamba kila sanamu iondolewe na kufukuzwa kutoka katika hekalu la moyo! Laiti ndimi zetu zingefunguliwa ili kuzungumzia wema wake, na kueleza juu ya uweza wake!

Kama ukiitikia kuvutwa na Kristo, 6hutashindwa kuwa na mvuto kwa mtu fulani kupitia uzuri na uweza wa neema ya Kristo. Hebu tumwangalie na kubadilishwa katika mfano wake Yeye ambaye ndani yake unakaa utimilifu wote wa Mungu kwa jinsi ya mwili, na kutambua kuwa tumekubalika katika huyo Mpendwa, “mmetimilika katika Yeye aliye kichwa cha enzi yote na mamlaka” (Wakolosai 2:10). – Bible Echo, Feb. 15, 1892.

Kesha la asubuhi: NURU YA ULIMWENGU

                   KESHA LA ASUBUHI

                 JUMAMOSI   02/05/2018

              *NURU YA ULIMWENGU? _“Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima” Mathayo 5:14_

✍?Uaminifu wetu kwa kanuni za Ukristo unatuita kwa huduma ya utendaji kwa ajili ya Mungu. Wale ambao hawatumii talanta zao katika kazi na kusudi la Mungu hawatakuwa na sehemu pamoja na Kristo katika utukufu wake. Nuru haina budi kuangaza kutoka katika kila roho iliyopokea neema ya Mungu. Roho nyingi zimo gizani, lakini wengi wanajisikia pumziko, raha na utulivu katika hali hiyo! 

✍?Maelfu wanafurahia nuru kubwa na fursa za thamani, lakini hawafanyi cho chote kwa mvuto wao au fedha yao, ili kuwaangazia wengine nuru. Hawachukui hata jukumu la kutunza roho zao wenyewe katika upendo wa Mungu, ili kwamba wasiwe mzigo kwa kanisa. 

✍?Watu wa jinsi hiyo watakuwa ni mzigo na kizuizi mbinguni. Kwa ajili ya Kristo, kwa ajili ya ile kweli, na kwa ajili yao wenyewe, wanapaswa kuamka na kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya umilele. Makao ya mbinguni yanaandaliwa kwa ajili ya wale ambao watakubaliana na masharti yaliyowekwa wazi katika Neno la Mungu.

✍?Kwa niaba ya roho zile ambazo Kristo alizifia, wale ambao wamo katika giza la makosa, wafuasi wote waaminifu wa Kristo wameamriwa kuwa nuru kwa ulimwengu. Mungu amefanya sehemu yake katika kazi hii kuu, na anangojea ushiriki wa wafuasi wake.

✍? Mpango wa wokovu umekamilika kabisa. Damu ya Yesu Kristo imetolewa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu, Neno la Mungu linazungumza na binadamu katika mashauri, makaripio, maonyo, ahadi, na kutia moyo, na ufanisi wa Roho Mtakatifu unatolewa ili kumsaidia katika juhudi zake zote. Lakini pamoja na nuru yote hiyo ulimwengu bado unaangamia gizani, ukiwa umezama katika makosa na dhambi.

??‍♂```Ni nani watakaokuwa watendakazi pamoja na Mungu, ili kuleta hizi roho katika kweli? Ni nani atakayewapelekea habari njema za wokovu? Watu ambao Mungu amewabariki kwa nuru na kweli wanapaswa kuwa wajumbe wa rehema.Utajiri wao unapaswa kutiririka kupitia katika mfereji wa kimbingu. 

??‍♂Juhudi zao za dhati hazina budi kuonekana. Imewapasa kuwa watendakazi pamoja na Mungu, wenye kujikana nafsi, wenye kujitolea, sawa na Yesu, ambaye kwa ajili yetu alikuwa maskini, ili kwamba kupitia umaskini wake, sisi tupate kuwa matajiri. – Review and Herald, Machi 1, 1887.```

*MUNGU AKUBARIKI MUWE NA SIKU NJEMA*

Kesha la asubuhi: Roho Hatimaye Aondolewa

                   *Kesha la Asubuhi*

                          *Alhamisi*

                     *Tarehe 31/5/2018*

                     *Roho Hatimaye
                          Aondolewa*??Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu; na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu; na mwenye haki na azidi kufanya haki; na mtakatifu na azidi kutakaswa. Ufunuo 22:11.

??Wakati ujumbe wa malaika wa tatu utakapofungwa, rehema haitaendelea kusihi tena kwa ajili ya wakazi wa dunia wenye hatia. Watu wa Mungu wametimiza kazi yao. Wamepokea “mvua ya masika,” “kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana” (Matendo ya Mitume 3:19), na wako tayari kwa ajili ya saa ya majaribio iliyoko mbele yao. Malaika wanaharakisha kwenda mbele na kurudi nyuma kule mbinguni. Malaika mmoja anarudi kutoka duniani na kutangaza kuwa kazi imekwisha; jaribio la mwisho limeletwa juu ya dunia, na wote waliojithibitisha wenyewe kuwa ni waaminifu kwa sheria za Mungu wamepokea “muhuri ya Mungu aliye hai” (Ufunuo 7:2).

??Kisha Yesu anaacha kazi yake ya upatanisho katika patakatifu pa mbinguni. Anainua mikono na kwa sauti kuu anasema, “Imekwisha,” na jeshi lote la malaika wanaweka chini taji zao anapotoa tangazo makini: “Mwenye kudhulumu na azidi kudhulumu: na mwenye uchafu na azidi kuwa mchafu: na mwenye haki na azidi kufanya haki: na mtakatifu na azidi kutakaswa.” (Ufunuo 22:11). Kila kesi imeamuliwa kwa ajili ya uzima au mauti. Kristo amefanya upatanisho kwa ajili ya watu wake na kufutilia mbali dhambi zao. Idadi ya watu wake imekamilishwa; “ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote” (Danieli 7:27), inakaribia kupewa kwa warithi wa wokovu, na Yesu atawale kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana.

??Anapotoka katika patakatifu, giza linawafunika wakazi wa dunia. Katika wakati ule wa kuogofya watakatifu inabidi waishi mbele za Mungu aliye mtakatifu bila kuwa na Mwombezi. Kizuizi ambacho kimekuwapo juu ya waovu kinaondolewa, na Shetani anakuwa na mamlaka kamili juu ya wale ambao hatimaye hawakutubu. Uvumilivu wa Mungu umefika mwisho. Dunia imekataa rehema yake, imedharau upendo wake, na kuikanyaga chini ya miguu yao sheria yake. Waovu wamevuka mpaka wao wa rehema; Roho wa Mungu, akiwa ameendelea kupingwa, hatimaye sasa anaondolewa. - The Great Controversy, uk. 613, 614.

Kesha la asubuhi: Muda U Karibu wa Kuondoka kwa Roho

             *KESHA LA ASUBUHI*
           JUMATANO MEI 30, 2018
      *Muda U Karibu wa Kuondoka 
                       kwa Roho*Na Roho na Bibi-arusi wasema, Njoo! Naye asikiaye na aseme, Njoo! Naye mwenye kiu na aje; na yeye atakaye, na ayatwae maji ya uzima bure. Ufunuo 22:17.

? Kipindi cha rehema hakitaendelea kwa muda mrefu zaidi. Sasa Mungu anaondoa mkono wake unaozuia kutoka katika dunia. Kwa muda mrefu amekuwa akizungumza na wanaume na wanawake kupitia katika uwakala wa Roho Mtakatifu wake; lakini hawajasikia wito huu. Sasa anazungumza na watu wake, na kwa ulimwengu, kwa hukumu zake. Muda wa hukumu hizi ni muda wa rehema kwa wale ambao bado hawajapata fursa ya kujifunza ukweli ni nini. Kwa upole Bwana atawatazama. Moyo wake wa rehema unaguswa; mkono wake bado umenyoshwa ili kuokoa. Watu wengi watapokelewa katika zizi lenye usalama ambao katika siku hizi za mwisho watausikia ukweli kwa mara ya kwanza.

? Bwana anawaita wale wanaomwamini kuwa watendakazi pamoja na yeye. Wakati maisha yangalipo, hawapaswi kujisikia kuwa kazi yao imekwisha. Je tutaruhusu ishara za mwisho wa wakati kutimizwa pasipo kuwaambia watu kuhusu kile kinachoujia ulimwengu? Je tutawaruhusu waende chini gizani bila kuwa tumewasisitizia hitaji la matayarisho ya kukutana na Bwana wao? Isipokuwa sisi wenyewe tumetenda wajibu wetu kwa wale wanaotuzunguka, siku ya Mungu itakuja juu yetu kama mwivi. Machafuko yameujaza ulimwengu, na hofu kuu iko karibu kuja juu ya wanadamu. Mwisho uko karibu sana. Sisi tunaoufahamu ukweli tunapaswa kuwa tunajitayarisha kwa ajili ya kile ambacho kiko karibu sana kuujia ulimwengu kama mshangao wa ajabu mno.

? Kama kanisa ni lazima tuweke tayari njia kwa ajili ya Bwana, chini ya uongozi wa Roho Mtakatifu. Injili inapaswa kutangazwa katika usafi wake. Kijito cha maji ya uzima kinapaswa kuongeza kina na kupanuka katika mwendo wake. Katika viwanja vya karibu na vya mbali, watu wataitwa kuacha plau-majembe ya kukokotwa na wanyama, na kutoka katika kazi za kawaida za biashara, na wataelimishwa pamoja na watu wale wenye uzoefu. Kadiri wanavyojifunza kufanya kazi kwa ufanisi, watatangaza ukweli kwa nguvu. Kupitia katika utendaji wa ajabu kabisa wa majaliwa ya Mungu, milima ya magumu itaondolewa.

? Ujumbe wenye maana sana kwa wakazi walioko juu ya dunia utasikika na kueleweka. Watu watafahamu ukweli ni nini. Mbele, na mbele zaidi, kazi itaendelea, hadi dunia yote itakapokuwa imeonywa. Na ndipo mwisho utakapokuja. -Review and Herald, Nov. 22, 1906.

*MUNGU AKUBARIKI*

Kesha la asubuhi: Bidii Katika Kutoa Onyo la Mwisho

                *KESHA LA ASUBUHI*

                  Jumanne Mei 29, 2018

        *Bidii Katika Kutoa Onyo la
                          Mwisho*_Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake. Ufunuo 18:1_

? Siku hadi siku hupita na kuwa milele, ikituleta karibu zaidi na kufungwa kwa mlango wa rehema. Sasa inatubidi kuomba kwa jinsi ambavyo kamwe hatujawahi kuomba kwa ajili ya Roho Mtakatifu kuwekwa kwa wingi zaidi juu yetu, na lazima tutafute uwezo wake unaotakasa upate kuja juu ya watendakazi, ili watu ambao wanawafanyia kazi wapate kufahamu kuwa wamekuwa pamoja na Yesu na kujifunza kutoka kwake. Tunahitaji uwezo wa kuona kwa macho ya kiroho sasa kuliko wakati wo wote uliopita, ili tupate kuona mbali, na kwamba tupate kutambua mitego na njama za adui, na kama walinzi waaminifu kutangaza hatari. Tunahitaji nguvu za kiroho ili tupate kupokea kadiri ambavyo akili ya mwanadamu inaweza kupokea, mada kuu za Ukristo, na jinsi ambavyo kanuni zake ni za kudumu.

? Watu wa Mungu wanaponyenyekesha roho mbele zake, kama mtu mmoja mmoja akitafuta Roho Mtakatifu wake kwa moyo wote, itasikika kutoka katika vinywa vya wanadamu ushuhuda kama ule unaowasilishwa katika Maandiko: “Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake” (Ufunuo 18:1). Kutakuwapo na nyuso zinazong’aa kwa upendo wa Mungu, zikisema, “damu yake Yesu, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote.” (1 Yohana 1:7). Wale walioko chini ya uwezo wa Roho Mtakatifu wa Mungu hawatakuwa washupavu wa dini, bali watulivu, imara, huru kutokana na ubadhirifu. Lakini hebu wale wote ambao wameipata nuru ya ukweli ikiwaka wazi na dhahiri katika njia zao, wawe waangalifu katika jinsi wanavyotamka amani na usalama. Mwe waangalifu ni mvuto gani mnaoweka wakati huu.

? Yesu anatamani sana kuweka majaliwa ya mbinguni kwa kipimo kikubwa juu ya watu wake. Maombi yanapanda kwenda kwa Mungu kwa ajili ya utimilizwaji wa ahadi hii; na hakuna ombi hata moja lililotolewa kwa imani linapotea. Kristo alipaa juu, aliteka mateka, akawapa wanadamu vipawa. Wakati, baada ya kupaa kwa Kristo, Roho alipokuja chini kama ilivyoahidiwa, kama upepo wenye nguvu unaokimbia haraka, akijaza sehemu yote ambapo wanafunzi walikusanyika, matokeo yake yalikuwa nini?

Maelfu waliongolewa katika siku moja. Tumefundisha, tumetegemea kuwa malaika atashuka kutoka mbinguni, kwamba dunia itaangazwa kwa utukufu wake, pale tutakapoona uvunaji wa roho sawa na ule ulioshuhudiwa katika siku ya Pentekoste. - Home Missionary, Nov. 1, 1893.

*TAFAKARI NJEMA NA MUNGU AKUBARIKI*

Kesha la asubuhi: Kufanya Kazi Kupitia Vyombo Vinyenyekevu

            *KESHA LA ASUBUHI*

             _IJUMAA MEI 25, 2018_

     *Kufanya Kazi Kupitia Vyombo
                   Vinyenyekevu*  _Kwa sababu upumbavu wa Mungu una hekima zaidi ya wanadamu, na udhaifu wa Mungu una nguvu zaidi ya wanadamu. 1 Wakorintho 1:25._

? Mungu atatembea juu ya watu wenye nafasi duni katika jamii, watu ambao hawajafikia kuwa wasiojali miale angavu ya nuru kupitia katika kutafakuri kwa muda mrefu juu ya nuru ya ukweli, na kukataa kufanya maboresho au mwendelezo wo wote ndani yake. Wengi kama hao wataonekana wakikimbia hapa na pale, wakibidishwa na Roho Mtakatifu wa Mungu kupeleka nuru ile kwa wengine. Ukweli wa neno la Mungu, ni kama moto katika mifupa yao, ukiwajaza kwa tamaa kuu ya kutaka kuwaelimisha wale wanaokaa gizani.

? Wengi, hata miongoni mwa wasomi, sasa wanatangaza maneno ya Mungu. Watoto wanahimizwa na Roho kwenda mbele na kutangaza ujumbe kutoka mbinguni. Roho amemwagwa kwa ajili ya wote watakaosikia ushawishi wake, na, huku wakiacha taratibu zote za kibinadamu, kanuni zake za lazima na njia zake za uangalifu, watatangaza ukweli kwa nguvu ya uwezo wa Roho. Makundi mengi watapokea imani na kujiunga katika majeshi ya Bwana.

? Wengi wa wale ambao wanakiri kuwa wafuasi wa Bwana kwa sasa hawajisalimisha kwa uongozi wa Roho wake, lakini wanajaribu kumfunga lijamu Roho Mtakatifu, na kumwendesha kama wapendavyo. Wote walio kama hao ni lazima waache kujitosheleza kwao, na kujisalimisha wenyewe bila kubakiza cho chote kwa Bwana, ili apate kutenda mapenzi yake mema ndani yao na kupitia kwao.

? Mapigo saba ya mwisho yako karibu kushuka juu ya wasiotii. Wengi wameacha wito wa injili uende bila kusikiwa; wamepimwa na kujaribiwa; lakini vizuizi vikuu vimeonekana kutisha mbele ya uso wao, vikizuia mwendo wao wa kusonga mbele. Kupitia katika imani, ustahimilivu, na ujasiri, wengi watavishinda vikwazo hivi na kutembea kwenda katika nuru yenye utukufu. Karibu pasipo kutambua vikwazo vimesimamishwa katika njia nyembamba; mawe ya kujikwaa yamewekwa katika njia hii; vyote hivi vitasukumwa mbali. Kinga ambayo wachungaji wa uongo wameweka kuyazunguka makundi yao ya kondoo zitakuwa kama hakuna; maelfu watapiga hatua kwenda kwenye nuru, na kufanya kazi ya kuieneza nuru hii. - Review and Herald, July 23, 1895.

              *MUNGU AKUBARIKI
                  UNAPOTAFAKARI*

Kesha la asubuhi: Kufukuza giza

                *KESHA LA ASUBUHI*              

                         JUMATANO

                          23/05/2018

                 *_KUFUKUZA GIZA_*
?_Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa Bwana umekuzukia. Maana, tazama, giza litaifunika dunia, Na giza kuu litazifunika kabila za watu; Bali Bwana atakuzukia wewe, Na utukufu wake utaonekana juu yako. Isaya 60:1, 2._

✍?Kanisa limeteuliwa kuwa njia ambayo kupitia hiyo nuru takatifu inapaswa kuangaza katika giza la kimaadili la ulimwengu huu, na miale yenye kuleta amani ya Jua la haki kuanguka juu ya mioyo ya wanadamu. 

✍?Kazi ya binafsi kwa mtu mmoja mmoja na kwa familia hufanya sehemu ya kazi ambayo inabidi ifanywe katika shamba la Bwana la mizabibu ya kimaadili. Upole, ustahimilivu, uvumilivu, upendo wa Kristo ni lazima vidhihirishwe katika kaya za dunia. 

✍?Kanisa lazima liinuke na kuangaza. Wakiwa angavu kwa Roho na nguvu ya ukweli, watu wa Mungu ni lazima waondoke na kwenda katika ulimwengu unaolala katika giza, ili kudhihirisha nuru ya utukufu wa Mungu. Mungu ametoa kwa watu uwezo bora wa akili ili utumike kwa ajili ya heshima yake, na katika kazi ya umisionari nguvu hizi za akili zinaitwa katika utendaji hai. Uboreshaji na ukuzaji wa hekima wa karama hizi za Mungu utaonekana ndani ya watumishi wake. Siku kwa siku kutakuwapo na ukuaji katika kumfahamu Kristo.

✍?Yeye aliyewahi kusema kwa jinsi ambavyo kamwe hakuna mwanadamu aliwahi kusema, aliyevaa vazi la ubinadamu, bado ni Mwalimu Mkuu. Kadiri unavyofuata katika nyayo zake, ukiwatafuta waliopotea, malaika watasogea karibu, na kupitia katika nuru ya Roho wa Mungu, ufahamu mkuu zaidi utapatikana kuhusu njia na mbinu bora za kufanikisha kazi iliyowekwa mikononi mwako. …

??‍♂```Wale ambao wangelikuwa nuru ya ulimwengu wameangaza miale dhaifu na milegevu tu. Nuru ni nini? Nuru ni uchaji Mungu, wema, ukweli, rehema, upendo; ni udhihirishaji wa ukweli katika tabia na katika maisha.

??‍♂ Injili inategemea uchaji Mungu wa waumini wake binafsi kwa ajili ya nguvu zake za kuleta maendeleo, na Mungu ametoa kinachotakiwa kupitia katika kifo cha Mwana wake mpendwa, ili kwamba kila roho iwezeshwe kikamilifu kutenda kila tendo jema. Kila roho inapaswa kuwa nuru kali inayong’aa, ikionesha sifa zake yeye aliyetuita kutoka katika gizani na kuingia katika nuru yake ya ajabu. -Review and Herald, March 24, 1891.```

*MUNGU AWE NANYI MNAPOJISOGEZA KARIBU NAE. AWABARIKI WOTE*

Kesha la asubuhi: Kusafiri Pamoja na Wamisionari

                     *Kesha la Asubuhi*
                          *Juma Nne*
     *Kusafiri Pamoja na Wamisionari??Basi hawa walipokuwa wakimfanyia Bwana ibada na kufunga, Roho Mtakatifu akasema, Nitengeeni Barnaba na Sauli kwa kazi ile niliyowaitia. Ndipo wakiisha kufunga na kuomba, wakaweka mikono yao juu yao, wakawaacha waende zao. Basi watu hao, wakiisha kupelekwa na Roho Mtakatifu wakatelemkia Seleukia, na kutoka huko wakasafiri baharini hata Kipro. Matendo ya Mitume 13:2-4.

??Ni jinsi gani tunauhitaji uwapo wa Mungu! Kwa ajili ya ubatizo wa Roho Mtakatifu, kila mtendakazi anapaswa kuwa anapumua maombi yake kwenda kwa Mungu. Makundi mbalimbali yanapaswa kukutana pamoja ili kumwita Mungu kwa ajili ya msaada maalum, kwa ajili ya hekima kutoka mbinguni, ili kwamba watu wa Mungu waweze kufahamu jinsi ya kupanga na kubuni jinsi ya kutekeleza kazi hiyo. Kwa namna ya pekee watu wanapaswa kuomba kwamba Bwana awachague mawakala wake, na kuwabatiza wamisionari kwa Roho Mtakatifu. Kwa siku kumi wanafunzi waliomba kabla baraka ya Pentekoste kuja. Ilihitajika muda kiasi kile kuwafikisha katika ufahamu wa kile kinachomaanishwa na kutoa maombi yenye kuleta matokeo yanayotarajiwa, kusogea karibu zaidi na zaidi kwa Mungu, kukiri dhambi zao, kunyenyekesha mioyo yao mbele za Mungu, na kwa imani kumtazama Yesu, na kubadilishwa kufanana na sura yake. Baraka ile ilipokuja, ilijaza mahali pote walipokuwa wamekusanyika; na huku wakiwa wamejazwa uwezo, waliondoka kwenda kufanya kazi yenye kuleta matokeo yanayotarajiwa kwa ajili ya Bwana.

??Inatupasa kuomba kwa bidii kwa ajili ya kushuka kwa Roho Mtakatifu kama vile wanafunzi walivyoomba katika siku ile ya Pentekoste. Iwapo walimhitaji [Roho yule] wakati ule, tunamhitaji zaidi leo. Giza la kimaadili, kama vile kitambaa cha maziko, linaifunika dunia. Kila aina ya mafundisho ya uongo, uasi, na madanganyo ya kishetani yanaongoza vibaya akili za wanadamu. Pasipo Roho na uwezo wa Mungu, itakuwa ni kazi bure kusumbuka kufanya kazi katika kuwasilisha ukweli. Ni lazima tuwe na Roho Mtakatifu ili apate kutuhimili katika mapambano haya; “Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho.” (Waefeso 6:12).

??Hatuwezi kuanguka maadam tunamtumainia na kumwamini Mungu. Hebu kila roho ya kwetu, wachungaji na washiriki, iseme, kama Paulo alivyosema, “Hata mimi napiga mbio vivyo hivyo, si kama asitaye; napigana ngumi vivyo hivyo, si kama apigaye hewa” (1 Wakorintho 9:26), bali kwa imani na tumaini takatifu, katika kutarajia kupata thawabu. - Home Missionary, Nov. 1, 1893.

BAADA YA KUFA NINI KINAENDELEA? By Melania Shedrack

           *BAADA YA KUFA NINI
                 KINAENDELEA?*VIFUATAVYO NI VITU VINAVYOTOKEA. I. *UKIFA HAUWEZI KUFAHAMU NENO LOLOTE* ....MHUBIRI 9:5-6,10 kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lo lote lililofanyika chini ya jua. Lo lote mkono wako utakalolipata kulifanya, ulifanye kwa nguvu zako; kwa kuwa hakuna kazi, wala shauri, wala maarifa, wala hekima, huko kuzimu uendako wewe II. *MWANADAMU ANAPOKUFA HANA TOFAUTI NA MNYAMA* ....MHUBIRI 3:19-20 Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili.Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena, ZABURI 49:12 Lakini mwanadamu hadumu katika heshima, Bali amefanana na wanyama wapoteao III. *UKIFA HAUWEZI KUJUA WATOTO WAKO WANAENDELEAJE* ..... AYUBU 14:21 Wanawe hufikilia heshima, wala yeye hajui; Kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao IV. *UKIFA HAUWEZI TENA KUMSIFU MUNGU BALI UKIWA HAI* ........  ZABURI 146:2,4 Nitamsifu Bwana muda ninaoishi, Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai. Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea V. *WALIOKUFA WOTE BADO WAMELALA MAKABURINI WATAFUFULIWA YESU ANAPORUDI MARA YA PILI* ......  1 WATHESALONIKE 4:13-18 Lakini, ndugu, hatutaki msijue habari zao waliolala mauti, msije mkahuzunika kama na wengine wasio na matumaini.Maana, ikiwa twaamini ya kwamba Yesu alikufa akafufuka, vivyo hivyo na hao waliolala katika Yesu, Mungu atawaleta pamoja naye. Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana, kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko, na sauti ya malaika mkuu, na parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi tulio hai, tuliosalia, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani; na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele. Basi, farijianeni kwa maneno hayo. Isaya 26:19 Wafu wako wataishi, maiti zangu zitafufuka; amkeni, kaimbeni, ninyi mnaokaa mavumbini, kwa maana umande wako ni kama umande wa mimea, nayo ardhi itawatoa waliokufa VI. *JE MUNGU ANAO UWEZO WA KUMRUDISHIA KILA KIUNGO AMBACHO MWANADAMU ANAKUWA NACHO WAKATI WA UHAI WAKE MF.NGOZI,NYAMA,,MIFU­­PA,,,!* .......  EZEKIELI 37:3-10 Akaniambia, Mwanadamu, je! Mifupa hii yaweza kuishi? Nami nikajibu, Ee Bwana MUNGU, wajua wewe. Akaniambia tena, Toa unabii juu ya mifupa hii, uiambie, Enyi mifupa mikavu, lisikieni neno la Bwana. Bwana MUNGU aiambia mifupa hii maneno haya; Tazama, nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi. Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi; nanyi mtajua ya kuwa mimi ndimi Bwana. asi nikatoa unabii kama nilivyoamriwa; hata nilipokuwa nikitoa unabii, palikuwa na mshindo mkuu; na tazama, tetemeko la nchi, na ile mifupa ikasogeleana, mfupa kwa mfupa mwenziwe. Nikatazama, kumbe! Kulikuwa na mishipa juu yake, nyama ikatokea juu yake, ngozi ikaifunika juu yake; lakini haikuwamo pumzi ndani yake. Ndipo akaniambia, Tabiri, utabirie upepo, mwanadamu, ukauambie upepo, Bwana MUNGU asema hivi; Njoo, kutoka pande za pepo nne, Ee pumzi, ukawapuzie hawa waliouawa, wapate kuishi. Basi nikatabiri kama alivyoniamuru; pumzi ikawaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno. VII. *HAIRUHUSIWI KUFANYA IBADA YA WAFU AU KUWAOMBEA ETI MUNGU AWABARIKI/AWASAMEHE* TORATI 18:9-11 Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au binti yake kati ya moto, wala asionekane mtu atazamaye bao, wala mtu atazamaye nyakati mbaya, wala mwenye kubashiri, wala msihiri, wala mtu alogaye kwa kupiga mafundo, wala mtu apandishaye pepo, wala mchawi, WALA MTU AWAOMBAYE WAFU VIII. *JE NI KWELI WAFU WAKIFA BAADAYE HUWATOKEA NDUGU ZAO?* ...... 2 WAKORINTHO 11:13-15 Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao. JIBU NI HAPANA -Wafu wanaowatokea watu na kuongea nao tena wanafanana kabisa na ndugu zao waliokufa hizo huwa ni roho za mashetani zinazojigeuza katika maumbile mbalimbali ya marehemu ili kuwadanganya watu kuwa hawafi huo ni udanganyifu mkubwa wa shetani *TAHADHARI:* Wafu hawaendi mbinguni wanapokufa bali huzikwa kaburini, pia hawawezi kusamehewa kama walikufa bila kuungama dhambi zao.

Kesha la asubuhi: Anakwenda Nyumba kwa Nyumba Pamoja na Watendakazi wa Injili

                   KESHA LA ASUBUHI

                              IJUMAA

                         18 MAY 2018

*Anakwenda Nyumba kwa Nyumba Pamoja na Watendakazi wa Injili* ? _Akawaita wale Thenashara, akawapa uwezo na mamlaka juu ya pepo wote na kuponya maradhi. Akawatuma wautangaze ufalme wa Mungu, na kupoza wagonjwa. Akawaambia, Msichukue kitu kwa safari yenu, fimbo, wala mkoba, wala mkate, wala fedha, wala mmoja wenu asiwe na kanzu mbili. Na nyumba yo yote mtakayoingia kaeni humo, mpaka mtoke mjini. Luka 9:1-4._

✍?Bwana anawaita watu wake kuchukua njia mbalimbali za huduma za umisionari. Wale walioko katika njia kuu na walio katika sehemu zisizofahamika vizuri katika maisha wanapaswa kusikia ujumbe wa injili. Washiriki wa kanisa wanapaswa kufanya kazi ya uinjilisti katika kaya za majirani zao ambao bado hawajapata ushahidi mkamilifu wa ukweli ulio kwa ajili ya wakati huu.

✍?Hebu wale ambao wanachukua kazi hii wafanye maisha ya Kristo kuwa somo lao la kudumu. Hebu na kwa bidii sana, wawe wanatumia kila uwezo katika huduma ya Bwana. Matokeo yenye thamani sana yatafuatia juhudi za dhati zisizo na ubinafsi. Kutoka kwa Mwalimu mkuu watendakazi watapokea elimu ya juu kabisa kuliko zote. Lakini wale ambao hawagawi nuru hii waliyoipokea siku moja watatambua kuwa wamepata hasara ya kutisha.

✍? Wengi wa watu wa Mungu inabidi watoke na machapisho kwenda katika sehemu ambazo ujumbe wa malaika wa tatu haujatangazwa. Kazi ya mwinjilisti wa vitabu ambaye moyo wake umejazwa na Roho Mtakatifu imejaa uwezekano wa ajabu wa mema. Uwasilishaji wa ukweli, katika upendo na usahili, kutoka nyumba moja hadi nyingine, unapatana na maelekezo aliyotoa Kristo kwa wanafunzi wake alipowatuma katika safari yao ya kwanza ya umisionari. Kwa nyimbo za sifa, maombi ya dhati, na uwasilishaji sahili wa ukweli katika familia moja, watu wengi watafikiwa.

✍? Mtendakazi mtakatifu atakuwapo kupeleka usadikisho kwa mioyo. “Mimi niko pamoja nanyi siku zote” (Mathayo 28:20) ndio ahadi. Kukiwapo uthibitisho wa uwapo wa kudumu wa Msaidizi wa jinsi hiyo, tunaweza kutenda kazi kwa imani na tumaini na ujasiri.

??‍♂```Ukinaifu wa huduma yetu kwa Mungu unapaswa kuvunjwa. Kila mshiriki wa kanisa anapaswa kujiingiza katika huduma fulani maalum kwa ajili ya Bwana.

??‍♂ Hebu wale ambao wamejiimarisha katika ukweli waende katika sehemu jirani, na kufanya mikutano. Hebu Neno la Mungu na lisomwe, na hebu mawazo yanayoelezwa yawe katika jinsi ambayo yataeleweka na wote bila shida. - Review and Herald, May 5, 1904```.

                   *MUNGU AKUBARIKI*

Nawatakieni Ramadhan njema!

Nawatakien Ramadhan njema kwa wasomaji wangu wote ambao ni waumini wa dini ya Kiislam. Tukumbukane kwenye dua zenu, na zaidi tuombee amani ndani ya miyoyo yetu na kwa taifa letu. Ramadan Mubarak!

Kesha la asubuhi: Ana shauku ya kuwasaidia walimu

           ? *KESHA LA ASUBUHI*?
                             Alhamisi
                          Mei 17, 2018

*ANA SHAUKU YA KUWASAIDIA WALIMU*
*_______________________________* 

? Fungu kiongozi
??
?2 Wafalme 2:15.

_*"Na hao wana wa manabii, waliokuwako Yeriko wakimkabili, walipomwona, walisema, Roho ya Eliya inakaa juu ya Elisha. Wakaja kuonana naye, wakainama kifudifudi mbele yake".*_
?➖➖➖??➖➖➖?

✅ Roho Mtakatifu alikuja katika shule ya manabii, akileta hata mawazo ya wanafunzi katika upatanifu na mapenzi ya Mungu. Kulikuwapo na muunganiko hai kati ya mbingu na shule hizi, na furaha na shukurani za mioyo yenye kupenda ilidhihirika katika nyimbo za sifa ambazo malaika walijiunga kuimba.

✅ Iwapo walimu wangelifungua mioyo yao kumpokea Roho huyu, wangelikuwa tayari kushirikiana naye katika kutenda kwa ajili ya wanafunzi wao; na pale anapopewa njia huru, atasababisha mabadiliko ya ajabu. Atafanya kazi katika kila moyo, akirekebisha ubinafsi, kuumba na kusafisha tabia, na kuleta hata mawazo kuwa mateka kwa Kristo. …

✅ Badala ya kunyamazishwa na kurudishwa nyuma, Roho Mtakatifu ingelifaa akaribishwe, na uwapo wake kuhimizwa. Wakati walimu wanapojitakasa wenyewe kupitia katika utii wa Neno, Roho Mtakatifu atawafanya kuona kidogo mambo ya mbinguni. Watakapomtafuta Mungu kwa unyenyekevu na bidii, maneno ambayo wameyazungumza kwa msisitizo thabiti yatachoma mioyoni mwao; ndipo ukweli hautafifia katika ndimi zao.

? ```Uwakala wa Roho wa Mungu hauondoi kutoka kwetu umuhimu wa kutumia akili na vipawa vyetu, bali hutufundisha jinsi ya kutumia kila uwezo kwa ajili ya utukufu wa Mungu. Akili za mwanadamu zikiwa chini ya uongozi maalum wa neema ya Mungu zinakuwa na uwezo wa kutumiwa kwa ajili ya kusudi lililo bora duniani. Kutokujua hakuongezi unyenyekevu au kumfanya mtu ye yote anayekiri kuwa mfuasi wa Kristo kuthamini zaidi mambo ya kiroho. Kweli za Neno takatifu zinaweza kufurahiwa vyema zaidi na Mkristo mwenye akili. Kristo anaweza kutukuzwa vyema zaidi na wale wanaomtumikia kwa akili. Kusudi kuu la elimu ni kutuwezesha kutumia uwezo ambao Mungu ametupatia kwa namna ile itakayowasilisha dini ya Biblia na kukuza utukufu wa Mungu.```
?? - North Pacific Union Gleaner, May 26, 1909.

*UWE NA TAFAKARI NJEMA MTOTO WA MUNGU*
_______________________________

Pastor Caleb Migombo: PUMZIKA KIDOGO / GET SOME REST

                   PUMZIKA KIDOGO

Kwanini Yesu, katikati ya siku yenye shughuli nyingi, aliwataka wanafunzi wake kuuacha umati wa watu na kwenda naye mahali pa faraga kupumzika? Alifahamu kuwa kadri walivyokuwa na kazi nyingi za kufanya ndiyo walivyohitaji kuweka muda wa kupumzika na kuwa pamoja na mwokozi wao. Kutofanya hivyo mwisho wake kungewaumizi wao wenyewe na wale wote waliokusudia kuwahudumia.

Sisi nasi leo, ni muhimu kuzingatia ukweli huu.

Mungu anajua shughuli zako na changamoto za Maisha yako ya kila siku – Iwe ni nyumbani, kazini, au Kanisani. Mungu anajua pia kuwa unahitaji hekima yake ili uweze kuwa na mtizamo sahihi wa kila shughuli na namna inavyopaswa kufanywa- na unahitaji pia nguvu kutoka kwake ili uweze kufanya kila jambo kwa usahihi. Kama hutapanga kuwa na muda wako wa kupumzika na kupata nguvu mpya (kimwili na kiroho)- upo uwezekano mbeleni wa wewe na wote uwapendao kuumia. Uchovu unaathiri kufikiri kwetu, namna tunavyowasiliana, na uwezo wetu wa kupenda wanaotunzunguka.

Yesu akawaambia, “Twendeni peke yetu mpaka mahali pa faragha mkapumzike kidogo.” Alisema hivyo kwa kuwa kulikuwa na watu wengi mno waliokuwa wanafika hapo na kuondoka hata Yesu na wanafunzi wake hawakuweza kupata nafasi ya kula chakula" Marko 6:31


                  GET SOME REST

Why, in the midst of such a busy day, did Jesus insist His disciples leave the crowds to rest and be alone with Him? He knew that the busier they were, the more they need to make time to rest and be alone with Him. If they didn’t, eventually they would hurt both themselves and those who they were seeking to help. The same is true for us

God knows the demands and responsibilities you face-at home, on the job, even in your church. But God also knows you need His wisdom to keep those things in perspective, and you need His strength to get them done rightly.

Then, because so many people were coming and going that they did not even have a chance to eat, he said to them, “Come with me by yourselves to a quiet place and get some rest.” Mark 6:31

Kesha la asubuhi: Anaongoza Utakaso wa Familia

                   *KESHA LA ASUBUHI*

                 _ALHAMISI MEI 10, 2018_

           *Anaongoza Utakaso wa Familia* _Mlee mtoto katika njia impasayo, Naye hataiacha, hata atakapokuwa mzee. Mithali 22:6._

? Ninawasihi wazazi kujiweka tayari wao wenyewe na watoto wao kujiunga na familia ya juu. Kaa tayari, kwa ajili ya Kristo, kaa tayari kukutana na Bwana wako kwa amani. Anza kufanya kazi katika familia yako kwa namna itakayoleta matokeo mema. Anza katika mzizi wa jambo lenyewe. Leteni ukweli katika nyumba zenu, ili kuwafanya kuwa watakatifu na kuwatakasa. Usiuache katika ua wa nje. Ni vipofu kiasi gani wale wanaodai kuwa Wakristo kuhusu maslahi yao wenyewe! Ni kiasi gani wanashindwa kabisa kuona kile ambacho Kristo angeliwatendea iwapo angeliruhusiwa kuingia katika nyumba zao.

? Hebu Wakristo na watende kwa bidii ili kupata taji ya uzima kama vile walimwengu wanavyotenda ili kupata manufaa ya kidunia, na kanisa la Mungu kwa hakika litasonga mbele likiwa na nguvu. Roho Mtakatifu hutoa matendo ambayo yanapatana na sheria ya Mungu. Kazi ya kuhuisha ya Roho itaonekana katika familia zenye kujitahidi ili kuonesha wema, uvumilivu, na upendo. Uwezo wenye nguvu zote uko kazini, ukiandaa akili na mioyo ipate kujisalimisha kwa uwezo unaoumba wa Roho Mtakatifu, ukiwaongoza wazazi kujitakasa wao wenyewe, ili watoto wao pia wapate kutakaswa.

? Nyumba ambayo washiriki wake ni Wakristo wapole, waungwana huweka mvuto wenye ushawishi mwingi kwa ajili ya wema. Familia zingine watazingatia matokeo yaliyopatikana na nyumba kama hizo, na watafuata mfano uliowekwa, kwa upande wao wakilinda kaya zao dhidi ya mivuto ya kishetani.

? Malaika wa Mungu mara nyingi watatembelea makazi ambayo ndani yake mapenzi ya Mungu yanatawala. Chini ya nguvu ya neema ya Mungu kaya kama hiyo inakuwa ni mahali pa kuburudisha kwa wasafiri dhaifu na wachovu. Kwa kulinda kwa uangalifu, nafsi inazuiwa kujionesha kuwa na haki. Mazoea sahihi yanatengenezwa. Kuna utambuzi makini kuhusu haki za watu wengine. Imani itendayo kazi kwa upendo na kuitakasa roho inashikilia usukani, na kuitawala kaya yote. Chini ya mvuto mtakatifu wa kaya kama hiyo, kanuni za udugu zilizowekwa katika Neno la Mungu zinatambuliwa kwa upana zaidi na kutiiwa. - Southern Watchman, Jan. 19, 1904.

     *MUNGU AKUBARIKI     UNAPOTAFAKARI*

Kesha la asubuhi: Anajibu maombi ya kutaka msaada wa Mungu

         *KESHA LA ASUBUHI*
                   JUMATANO
                    09/05/2018
*_ANAJIBU MAOMBI YA KUTAKA MSAADA WA MUNGU _* ? _Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo. Kumbukumbu 6:6, 7_.

✍?Akina baba na akina mama, nitawezaje kupata maneno ya kuelezea jukumu lenu kubwa! Kwa tabia mnayoidhihirisha mbele ya watoto mnawafundisha kumtumikia Mungu au kuitumikia nafsi. Basi toa maombi yako ya dhati kwa mbingu kwa ajili ya msaada wa Roho Mtakatifu, ili mioyo yenu ipate kutakaswa, na kwamba njia mnayoifuata iweze kumheshimu Mungu na kuwavuta watoto wenu kwa Kristo.

✍? Inapasa kuwapa wazazi hisia ya umakini na utakatifu wa kazi yao, pale wanapotambua kuwa kwa mazungumzo au matendo ya kizembe wanaweza kuwapoteza watoto wao.

✍?Wazazi wanahitaji uongozi wa Mungu na Neno lake. Wasipoyasikiliza mashauri ya Neno la Mungu, wasipofanya Biblia kuwa mshauri wao, kanuni ya maisha, watoto wao watakua wakiwa wazembe na watatembea katika njia za kutokutii na kutokuamini.

✍? Kristo aliishi maisha ya kazi na kujikana nafsi, na alikufa kifo cha aibu, ili apate kutoa mfano wa roho ambayo itawachochea na kuwatawala wafuasi wake. Kadiri ambavyo wenzi wa maisha wanajitahidi nyumbani kwao kufanana na Kristo, mvuto wa mbinguni utaenezwa katika maisha ya familia yao.

??‍♂```Katika kila nyumba ya Kikristo Mungu anapaswa kuheshimiwa kwa dhabihu za asubuhi na jioni za sifa na maombi. Kila asubuhi na jioni maombi ya dhati inabidi yapande kwa Mungu kwa ajili ya baraka na uongozi wake. 
Je Bwana wa mbingu atapita katika nyumba kama hizo na asiache baraka hata moja pale? Hapana, kwa kweli.

??‍♂ Malaika wanasikia utoaji wa sifa na maombi ya imani, na wanabeba maombi kwenda kwake yeye anayehudumu katika patakatifu kwa ajili ya watu wake, na kukiri ustahili wake kwa niaba yao. Maombi ya kweli hushikilia nguvu za Mungu na kuwapa watu ushindi. Juu ya magoti yake Mkristo anapata nguvu ya kupinga jaribu. - Review and Herald, Feb. 1, 1912.```

*MUNGU TUWEZESHE KUTAMBUA KIMBILIO LETU NI WEWE TU*