??SOMA HII ITAKUSAIDIA SANA MDADA??JIFUNZE EWE MWANAMKE

  1. Usikimbilie kuhama na kuondoka nyumbani kwa wazazi wako kabla hujajipanga vizuri
  2. Usimsubiri mwanaume ndio uanze maisha, unaweza ukaishi maisha yako mwenyewe na ukaweka msingi mzuri utakaokusaidia huko baadae.
  3. Kaa mbali na marafiki waovu, jifunze kuheshimu kila mtu kuwa na busara na vaa mavazi ya heshima.
  4.  Usimchekee chekee kila mwanaume, kwa maana wengine sio waoaji ni chui waliojivika ngozi ya kondoo! Ni bora ukaendelea kubakii single kuliko uje kuolewa na mtu ambaye atakufanya ujute maisha yako yote hapa duniani. Omba Mungu akupe busara na ustahimilivu.
  5. Jijengee tabia ya kula kwa afya, siku zote jitahidi ule milo yote mitatu acha kula biscuit na soda, usipendelee chips na mishkaki na vyakula vya aina hiyo. Fanya mazoezi mepesi kuuweka mwili wako uendelee kuwa mzuri wa kuvutia. Wewe ni tunu kwa mume wako mtarajiwa au uliyenae.
  6. Vaa kwa heshima, watu watakujaji kulingana na jinsi tu ulovyovaa hata maongezi yao yataegemea kutokana na uvaaji wako.
  7.  Usitumie SEX kama njia ya kujihakikishia Mapenzi. Kufanya mapenzi sio tiketi ya kupendwa. Ata SEX na wewe na atakuacha kwenye mataa ya ubungo junction.
  8. ⭐Usiolewe nae kwa vile ana pesa za kutosha na ni tajiri kwa sababu karibuni tu na wewe utakua moja ya mali anazomiliki.⭐
  9. Jiongezee thamani, get a career! Usiwe mpumbavu kufikiri mwanaume ndio atasuluhisha matatizo yako yote. Jibidiishe kwa kazi zako binafsi hakuna raha juu ya kuwa na maamuzi ya kutumia kile kipato ulichokipata kwa jasho lako.
  10. Wewe ni wa muhimu mno, una thamani kubwa sana! Jipende jiheshimu, jijali. Usijali umetendwa na wangapi katika mahusiano! Usikate tamaa jiweke vizuri. Ishi maisha yako. Hayo unayopitia ni funzo tu ktk maisha.

⭐Above all, Remember this, Charm is deceitful, and beauty is vain: but a woman that fears the LORD, she shall be respected.⭐

MUNGU AWABARIKI WANAWAKE WOTE ULIMWENGUNI, ABARIKI KAZI ZA MIKONO YENU NA SIO KAZI ZA MAUNGO YENU. NINYI NI WA THAMANI MNO. FB_IMG_1457286600275-1Nawatakia weekend njema yenye mafanikio….
?????????

Hahaha! Walimu utawajua tuu ???……..Umenikosha sana na ujumbe wako haswa number 8! Hiyo kitu ndo natamani wanawake wengi wajue kuwa they should never let men treat them like  ‘property / object’ au “project” fulani!! Wanawake nao ni binadamu wanatakiwa kuheshimiwa, kufanya maamuzi binafsi, na kutimiza ndoto zao……..!!

Very proud of you #MyChildhoodFriend.    #KekoJuuForLife

#MyPrimarySchoolMate.       #LiveLongMgulaniShuleYaMsingi

#MySecondarySchoolMate.   #KowakGirlsForeverInMyHeart

Leave a Reply