ULIMI UNA NGUVU YA AJABU…..! Our Tongues has enormous power….. !

Our Tongues has enormous power 

Our tongues have enormous power-both for good and for evil. Indeed, with our tongue we can build healthy relationships, and with it we can destroy people’s lives…including our own. How do you use your own tongue?

The Apostle James put it this way: “The tongue also is a fire, a world of evil among the parts of the body…with the tongue we praise our Lord and father, and with it we curse men, who have been made in God’s likeness” (James 3:6,9).

Commit your tongue to God. Beyond that, commit your whole inner being to Christ, and ask Him to cleanse you of anger and hate, and fill you instead with His love and patience.

A gentle answer turns away wrath, but harsh word stirs up anger. Proverbs 15:1

ULIMI UNA NGUVU YA AJABU

Hakuna kiungo cha mwili kilicho na nguvu ya kujenga au kubomoa mahusiano yetu kama Ulimi…Hakika ndimi zetu zina nguvu ya ajabu – ya kutenda mema au mabaya. Kwa kutumia ulimi (maneno yetu) tunaweza kutengeneza mahusiano mazuri au kuharibu maisha ya watu wengine -na kuua mahusiano yetu wenyewe. Je Unautumiaje Ulimi wako?

Yakobo katika waraka wake anauelezea Ulimi hivi: “Ulimi nao ni kiungo kidogo sana lakini hujivunia mambo makuu. Fikirini jinsi moto mdogo unavyoweza kuteketeza msitu mkubwa! Ulimi pia ni kama moto. Ulimi ni ulimwengu wa uovu kati ya viungo vyetu. Humchafua mtu nafsi nzima na kuwasha moto maisha yake yote, nao ulimi huwashwa moto wa kuzimu… Kwa kutumia ulimi tunamsifu Bwana na Baba yetu na kwa ulimi huo huo tunawalaani watu ambao wameumbwa kwa mfano wa Mungu. Katika kinywa hicho hicho hutoka sifa na laana. Ndugu zangu, haipaswi kuwa hivyo. [Yakobo 3: 5-6, 9-10]

Usalimishe Ulimi wako kwa Mungu. Zaidi ya hapo salimisha maisha yako yote na moyo wako kwa Kristo, na muombe akutakase na kukuondolea hasira, chuki, na roho ya kisasi — badala yake akujaze upendo wake na uvumilivu.

“Jawabu la upole hugeuza hasira; Bali neno liumizalo huchochea ghadhabu” [Mithali 15:1].

***Imeandikwa na Pastor Caleb Migombo***

Leave a Reply