HONGERA SANA ANTON H. NGOLI

fb_img_1482025152919Hongera nyingi zikufikie mdogo wangu na Kiongozi mwenzangu wa Jukwaa La Watu Wenye Ulemavu Tanzania kwa kuhitimu masomo yako yaliyochukua miaka mitatu ukiwa chuo cha ununuzi na ugavi IPS. Najivunia sana kwa wewe kuwa mmoja kati ya vijana wengi nilikuwa nashauriana nao kipindi nipo IPS. Juhudi zako na uvumilivu wako katika kufuata ndoto yako ndio imekufikisha hapo ulipo. Kila safari ina changamoto na mafanikio, hivyo zidisha juhudi na nia katika kila step utakayo piga kuelekea katika mafanikio yako. Jamii ya watu wenye ulemavu kupitia bodi ya Jukwaa la Watu Wenye Ulemavu Tanzania ina imani na elimu yako pamoja na juhudi zako na tuna imani uta acha alama nzuri katika jukwaa kupitia utendaji wako kama Katibu Mkuu wa Jukwaa.

Mungu akupe maisha marefu yenye furaha, amani na upendo kwa watu wote.Tuendelee kutafuta Maarifa ili kupanua ufahamu wetu tulio pewa na Mungu

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!
Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Ni mimi kaka yako
P.L. Sarungi
Raisi wa Jukwaa La Watu Wenye Ulemavu Tz.

****fb_img_1477414420906-1Nami naomba nimpe pongezi zangu za dhati! Naomba ukatumie elimu uliyopata siyo tu kwa faida zako binafsi bali jamii inayo kuzunguka na taifa kwa ujumla! Hongera sana!

Leave a Reply