MATOKEO YA KELELE ZA #BringBackBenAlive NI YAPI NA YAMEISHIA WAPI?- Peter Sarungi

Peter Sarungi a.k.a The Next Speaker-Baba Pilato!

Watu wa Makabila yanayo patikana mkoa wa Mara (Kwetu Pazuri) wana desturi ya kuwa jasiri, wakweli na wenye uwezo wa kusimamia jambo analo liamini. Lakini huku jijini Dar tulipokuja kutafuta maisha, mambo yake yanaendeshwa kwa usanii, unafiki, uoga, dilli, uongo na kutafuta kicky pasipo sababu ya msingi.

Uozo huu umeingia hadi kwenye siasa kiasi kwamba huwezi kutofautisha siasa za chama tawala na zile za Upinzani yaani wote wamekuwa wafuasi wa mambo hayo ya jijini.

Wahusika Tuelezeni, kwanini mpo kimya kwa swala mlilo lianzisha? na mtuambie matokeo chanya ya #Bring_Back_Ben_Alive ?

Msianzishe kampeni katika mitandao halafu mkaziacha katikati bila kujua hatima yake, What if Ben amedhurika? Kelele zenu na ukimya wa Ghafla utakuwa umemsaidia nini Ben? Tafakari, Chukua hatua… 

Leave a Reply